Tuhuma nzito ya ufisadi wa kupora ardhi mpaka sasa haijajibiwa

Tuhuma nzito ya ufisadi wa kupora ardhi mpaka sasa haijajibiwa

Mkuu ulizia wenyeji wa Kagera na hasa hasa wilaya za Muleba, Bukoba, Karagwe na kadhalika...Wenyeji wa kule migogoro ya ardhi huwa ni ya "EKIBANJA" mashamba ya ukoo yenye migomba na mibuni...hiyo ndiyo migogoro ambayo kesi zake huwa zinafika hadi makama za rufaa! mtu anaweka hadi wakili kwa kesi ya kipande kidogo cha mita 75 za mraba! Ardhi aliyomilikishwa JPM kule inafahamika kama "ORWEYA" kwa maana ya mbuga na mapoli nyingi zipo chini ya serikali za vijiji ambao hata wewe unaweza kwennda kununua kwa ajili ya kuwekeza!
Katika bandiko lako uliandika kuwa kagera hakuna migogoro ya ardhi, lakini katika utetezi ukasema iko migogoro, Rekebisha kauli yako halafu tuendelee.

Nimekwambia ya Ngoswe mwachie Ngoswe! Kama hiyo ardhi inayoitwa orweya ingekuwa inaweza kupatikana kirahisi hivyo si watu wangeenda kulima huko! Angalia pale Bigoro, wananchi walianza kulima kwa kupewa hata eka moja tu; walitoka huko vijijini wakaja kulima hapo porini - ni kwa sababu huko waliko hakuna ardhi ya kutosha. Wamelima wanakaribia kuvuna wakatolewa eti ni eneo la wafugaji. Wamerudi wapi? Huko walikokuwa wamekimbia kwa ukosefu wa ardhi! Hivi wangepewa hapo pa mheshimiwa si wangeshukuru sana. Ndugu yangu kumbuka watu wanaongezeka lakini ardhi haiongezeki kihivyo; mtu mmoja anapochukua eneo kubwa peke yake hilo ongezeko la watu litaenda wapi?
Umesema JPM alimilikishwa, sawa, ila mimi nikauziwe - kwa nini
 
Nashindwa kuamini kuwa mpaka muda huu hakuna hata mmoja wao miongoni waliotajwa aliweza kutoka hadharani kukanusha au kufafanua juu ya tuhuma hizi. Yaani hata ofisi zao zimeshindwa kuwatetea!

Swali la msingi hapa ni je, kama tuhuma ni za uongo, kwanini ichukue muda kujibu?

Tutaelewana tu mwaka huu.
Jamaa hata asipotangazwa na NEC lakini tutampigia kura za heshima kwa kutufungua mambo mengi sana watanzania
 
Mataga wanasema Magu hatakuwa rais wa kwanza kujimilikisha eneo kubwa hivyo hapa Tz, yeye anafuata nyayo za watangulizi wake. Kama Mwinyi, Mkapa na Kikwete wanamiliki maeneo hayo makubwa, kipi cha ajabu kwa Magu?!
Si nilisikia Waziri mkuu wa zamani walimnyang'anya!
 
Back
Top Bottom