Tuhuma za JWTZ kupiga raia huko Kawe: Tunaomba Waziri wa Ulinzi ajitokezee kukemea, kulaani, na kukataza jeshi kujichukulia sheria mkononi

Wewe umefurahia nini yeye kupoteza maisha?
Mkuu sifurahii, na pia kulikuwa na sababu ya mauaji. Sio kwamba dogo alitoka huko akaja tu kumvamia na kumuua.

Kulikuwa na sababu iliyopelekea dogo kuu. Lkn pia kuna sheria na mahakama ambavyo vipo kwa ajili ya kuendesha kesi za namna hiyo na baadae kutoa hukumu.

Wewe unahalalisha watu wasiohusika na ambao hawakuwepo hata eneo la tukio kuvamiwa na kupigwa hovyo, et kwa sababu ofisa wao ameuliwa na mtu wasiomfahamu!!
 
Siyo kaushamba,hawa ni washamba kabisa, nakumbuka miaka ya nyuma pale Mwenge kwenye magorofa waliyokuwa wanakaa hawa washamba walikuwa wanaweka mapazia ya viroba. Hawa walitakiwa wakae porini tu kwenye makambi yao.
Nimecheka sana 🤣🤣🤣
 
Walivyo wapumbavu wanasubiri habari hii ichapishwe Instagram, Facebook, na twitter ndio wajitokeze TANZANIA kuna upumbavu mwingi sana
 
Hakuna kiongozi yoyote anaweza kuwakemea ama kuwachukulia hatua yoyote hao wanajeshi, maana viongozi hawa wako madarakani kwa wizi ww kura, na hisani ya jeshi ndio inawafanya waendelee kukaa madarakani. Ingekuwa ni viongozi walioko madarakani kwa kura halali wangeweza kukemea, ama hata kuchukua hatua.

Hao wanajeshi tutawaona wa maana kama watapindua serekali hii isiyo na uhalali wa umma, na kuhakikisha tunapata katiba mpya na serekali halali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…