Tuhuma za JWTZ kupiga raia huko Kawe: Tunaomba Waziri wa Ulinzi ajitokezee kukemea, kulaani, na kukataza jeshi kujichukulia sheria mkononi

Tuhuma za JWTZ kupiga raia huko Kawe: Tunaomba Waziri wa Ulinzi ajitokezee kukemea, kulaani, na kukataza jeshi kujichukulia sheria mkononi

Just imagine wakikuta mzee anatoka kutafuta riziki ya watoto wake wanakula ugoko.

Wakikuta bibi katoka feli kununua samaki ili akakaange auze kwa ajili ya kujipatia riziki ya kusomesha watoto na wajuu zake jamaa wanaondoka na ndoo ya samaki huku bibi akishushiwa kipigo cha mbwa mwizi.

Afu linatokea jitu kuwatetea hawa wavunja sheria.
So sad indeed
 
Na nyinyi raia wekeni utii kwa askari wenu. Kumfanyia baya askari ni kulishushia heshima jeshi. Kama kuna uonevu jeshi lina mamlaka zake, ukiripoti jambo linafanyiwa kazi.
Kwanza mwanajeshi ndie alienza ugomvi.
Pili hakuwa amevaa kijeshi hivyo kijana alijua anagombana na raia mwenzake.
Tatu jeshi alimchapa vibao kijana mbele ya watu, hivyo kupelekea kijana kuhamaki na kuamua kujihami kwa silaha iliyopelekea mauaji.

Hata hivyo tunacholaumu, ni kitendo cha jeshi kutembeza kipigo kwa watu zaidi ya mia moja (wakiwemo wakinamama ambao walikuwa wanajaribu kuwaokoa watoto wao) kwa sababu et ya kosa la mtu mmoja.

That it doesn't make sense.
 
nyie wapumbavu hamjui hata maana ya jeshi, Monduli pale duka bovu walivunjaga mpaka vinyumba vya wamasai baada ya kumpiga mwanajeshi na sime. Huko tena wameua? Vijana wa Dsm ni washamba sana na wapumbavu. Lazima aliyeua apatikane na bado mtapigwa sana mpaka mshike adabu. Heshimu wanajeshi hivyo visiasa vyenu uchwara kafanyieni huko vijiweni kwenu.
Muuaji ni mtu mmoja, na tayari alikuwa ashakamatwa. Raia wanaopigwa hawakumuua mtu , wala kuwepo eneo la tukio, na wengine hata taarifa ya huyo mwanajeshi kuuwawa walikuwa hawana.

Hivyo hapakuwa sababu ya kuwapiga wasiohusika wala kufahamu kilichotokea. Pia na wewe hauna haki ya kutukana watu waliopigwa wakati wakitoka kwenye mishughuliko yao ya kujitafutia riziki zao bila kujua wala kufahamu kilichotokea eneo hilo.
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Ndugu wanaJF wenzangu, nafikiri wengi wetu hapa JF tumesikia, tumesoma na wengine kuona kile kinachosemekana kufanywa na jeshi letu, ambalo tumelipa jina la "Jeshi la Wananchi wa Tanzania.

Jeshi hilo tulilipa jina hilo kwa kuamini kwamba, jeshi hilo limeundwa kwa ajili ya kumlinda, na kumpigania mwananchi wa Tanzania.

Lakini pia liliundwa kwa ajili ya kuilinda mipaka ya Tanzania, pamoja na viongozi wa Tanzania akiwemo raisi wa nchi (ambae ni amiri jeshi wao mkuu) mawaziri, wakuu wa mikoa na viongozi wengine mbali mbali. Hilo ndio lilikuwa lengo la kuundwa kwa jeshi hilo, lkn pia kupewa jina hilo (JWTZ)

Sasa inashangaza sana jeshi ambalo lingewalinda na kuwapigania wananchi, ndio linageuka kuwa jeshi la kuwapiga hovyo wananchi, kuwatesa wananchi na hata wengine kuwauwa wananchi bila sababu za msingi.

Yes tunajua kwamba kila binadamu ana mapungufu yake, hivyo wapo wananchi wanaofanya makosa, au mambo mabaya kwa jeshi letu. Lakini kuna sheria na mahakama ambavyo vinaweza kutumika kuwaadhifu wale wanaofanya mambo mabaya kwa jeshi letu, na sio jeshi hilo kukimbilia tu kujichukulia sheria mkononi mpaka kupelekea maafa kama yaliotokea Kawe na kwengineko.

Malalamiko ya wananchi au raia dhidi ya jeshi hayakuanza leo, ila cha kushangaza badala ya kumalizwa kwa njia ya amani, ndio yanazidi kuongezeka kwa njia za kuchochewa na jeshi hilo hilo lililopewa dhamana ya kutulinda.

Kwa kilichotokea juzi huko Kawe, nafikiri viongozi wengi wa kiserikali wanalifahamu, lkn kwa vile pengine sio wahusika wakuu wa maswala ya kiusalama ndio maana hawahitaji kuliingilia swala hili.

Hivyo sisi wananchi tunamuomba waziri husika wa ulinzi mama yetu Stergomena Tax, pamoja na waziri wa mambo ya ndani brother Masauni waingilie kati swala hili kwa kuonya, kulaani na kutolea maelezo swala husika.

Msingoje mpaka raisi aje kulizungumzia mwenyewe, na wakati nyinyi kama mawaziri mmepewa dhamana ya kutulinda.

Kwa niaba ya wananchi wanyonge, ni mimi mpigania haki zao Mr Dudumizi wa somewhere in Kawe.
mnaua luten kanali mchekewe?lazima mpate doso mbebe dunia.
 
mnaua luten kanali mchekewe?lazima mpate doso mbebe dunia.
Soma hapo chini, maana naona baadhi yenu hamjajua kwanini nimeandika hii thread.

Sitetei mauaji yaliofanywa na kijana. Nnachotetea ni ile ya kupiga watu hovyo bila sababu, huku wakifahamu kwamba wengi hao hawakuwa eneo la tukio.
Kiongozi kauwawa na mtu mmoja, lkn waliopigwa na kujeruhiwa ni zaidi ya watu mia moja, ambao hawakuwa eneo la tukio, na wala hawakuwa wanafahamu kilichotokea.
 
Mkuu yalikukuta nini?
Hapana mkuu, yalimkuta baba yangu mdogo (umri miaka 55) aliekuwa anatokea kwake Tabata kuelekea Kawe kumtizama mdogo wake (bamdogo) ambae ni mgonjwa.

Sasa angalia umri wa huyo baba yangu mdogo aliepigwa, tena haishi hapo Kawe na pia hakuwa anafahamu hata kilichotokea siku hiyo.
 
Kuna shida kwa wanajeshi wetu. Uwezo wao wa kuwaza na kung'amua mambo ni Mdogo sana na pia ni washamba. Hao raia wanaopigwa na surubishwa ndio waliomuua huyo mkuu wao ?? Hii ndio Shida ya kuchukua form four failure. Uwezo mdogo wa kufikiri kuanzia kwa Ma luetenants. Kulikuwa na shida gani kama angempisha huyo dogo au kumpotezea tu akaendelea na safari.
 
Kuna shida kwa wanajeshi wetu. Uwezo wao wa kuwaza na kung'amua mambo ni Mdogo sana na pia ni washamba. Hao raia wanaopigwa na surubishwa ndio waliomuua huyo mkuu wao ?? Hii ndio Shida ya kuchukua form four failure. Uwezo mdogo wa kufikiri kuanzia kwa Ma luetenants. Kulikuwa na shida gani kama angempisha huyo dogo au kumpotezea tu akaendelea na safari.
Mkuu ulichoandika hapa kinaonesha kuwa wewe ni mtu muungwa san, unaweza kuishi vizuri na watu mbali mbali tena kwa amani.

Naunga mkono hoja yako.
 
Mkuu raraa reree thank you so much mkuu.

Lakin ikikupendeza na wewe tia neno kidogo katika mada. Nina imani wewe ni muungwa na mwenye upendo kwa watu.

Hivyo neno lako litaweza kubadilisha mawazo ya watu mbali mbali, ambao humu wamekimbilia kuandika lawama bila kujua chanzo na sababu ya kuandika thread hii.
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Ndugu wanaJF wenzangu, nafikiri wengi wetu hapa JF tumesikia, tumesoma na wengine kuona kile kinachosemekana kufanywa na jeshi letu, ambalo tumelipa jina la "Jeshi la Wananchi wa Tanzania.

Jeshi hilo tulilipa jina hilo kwa kuamini kwamba, jeshi hilo limeundwa kwa ajili ya kumlinda, na kumpigania mwananchi wa Tanzania.

Lakini pia liliundwa kwa ajili ya kuilinda mipaka ya Tanzania, pamoja na viongozi wa Tanzania akiwemo raisi wa nchi (ambae ni amiri jeshi wao mkuu) mawaziri, wakuu wa mikoa na viongozi wengine mbali mbali. Hilo ndio lilikuwa lengo la kuundwa kwa jeshi hilo, lkn pia kupewa jina hilo (JWTZ)

Sasa inashangaza sana jeshi ambalo lingewalinda na kuwapigania wananchi, ndio linageuka kuwa jeshi la kuwapiga hovyo wananchi, kuwatesa wananchi na hata wengine kuwauwa wananchi bila sababu za msingi.

Yes tunajua kwamba kila binadamu ana mapungufu yake, hivyo wapo wananchi wanaofanya makosa, au mambo mabaya kwa jeshi letu. Lakini kuna sheria na mahakama ambavyo vinaweza kutumika kuwaadhifu wale wanaofanya mambo mabaya kwa jeshi letu, na sio jeshi hilo kukimbilia tu kujichukulia sheria mkononi mpaka kupelekea maafa kama yaliotokea Kawe na kwengineko.

Malalamiko ya wananchi au raia dhidi ya jeshi hayakuanza leo, ila cha kushangaza badala ya kumalizwa kwa njia ya amani, ndio yanazidi kuongezeka kwa njia za kuchochewa na jeshi hilo hilo lililopewa dhamana ya kutulinda.

Kwa kilichotokea juzi huko Kawe, nafikiri viongozi wengi wa kiserikali wanalifahamu, lkn kwa vile pengine sio wahusika wakuu wa maswala ya kiusalama ndio maana hawahitaji kuliingilia swala hili.

Hivyo sisi wananchi tunamuomba waziri husika wa ulinzi mama yetu Stergomena Tax, pamoja na waziri wa mambo ya ndani brother Masauni waingilie kati swala hili kwa kuonya, kulaani na kutolea maelezo swala husika.

Msingoje mpaka raisi aje kulizungumzia mwenyewe, na wakati nyinyi kama mawaziri mmepewa dhamana ya kutulinda.

Kwa niaba ya wananchi wanyonge, ni mimi mpigania haki zao Mr Dudumizi wa somewhere in Kawe.
Jeshi lolote iwe jwtz, polisi, uhamiaji nk hawaruhusiwi kuvunja sheria.

Kuchukua sheria mkononi ni moja ya kosa la kuvunja sheria. Hivyo wahusika wote wwaliopiga raia washuulikiwewa sheria.

Na uyo alieua askari akamatwe na kufikishwa mahakamani akajibu sababu ya mauaji.

Kwishney!
 
Jeshi lolote iwe jwtz, polisi, uhamiaji nk hawaruhusiwi kuvunja sheria.

Kuchukua sheria mkononi ni moja ya kosa la kuvunja sheria. Hivyo wahusika wote wwaliopiga raia washuulikiwewa sheria.

Na uyo alieua askari akamatwe na kufikishwa mahakamani akajibu sababu ya mauaji.

Kwishney!
Hakuna mtu mwenye akili anaekubaliana na matukio yote mawili. Kuua mtu au kupiga raia.

Kwa vile mtuhumiwa alikuwa ameshakamatwa na polisi, hivyo hapakuwa sababu ya wanajeshi kuingia mtaani kupiga watu wasiokuwa na hatia hovyo.
 
Back
Top Bottom