Tuhuma za ufisadi zinazodaiwa kumpelekea Dkt. Ryoba kubwaga manyanga

Na nyie mlikuwa wapi? Kwa nini hamkufichuwa ufisadi huo hapo kabla ili kuonyesha kweli Ni wazalendo wa nchi hii. Ukianza kuweka mambo hadharani wakati huu wa uchunguzi huoni kwamba Kuna kitu unakitengeneza ambacho kimsingi kinaweza kuathiri uchunguzi wenyewe? Ninajaribu kuwaza tu.
 
Tatizo hatusomi habari na tunarukia tu kishabiki Magu hakuwa Mungu kuwa ajue kila kinachofanywa katika taasisi za umma hata ungekuwa wewe usingeweza ndio maana ya kuwa na wasaidizi na hapo kama umesoma vizuri kuna kampuni ipo kuanzia 1999 hadi leo, hakuna mtu peke yake ambaye anaweza kumaliza tatizo la rushwa duniani,hata huko kwa wenzetu ambako kila kitu kipo kimfumo bado tatizo la rushwa lipo, rushwa ipo kuanziakale sawa na biashara ya ukahaba, kinachofanyika ni juhudi za pamoja za kupunguza rushwa, Magu amefanya yake wacha apumzike ni raisi bora kabisa kutokea hapa Tanzania,upende usipende ndivyo hivyo, mnaojaribu kumchafua mnajidanganya bure kama akina february Marope na genge lake.
 
Mtoto wako anaumwa ETI baba yy hajui kama mwanae anaumwa? Wamezidia kete tu hapo
Ndo ushangae. Huyu Rioba anayajua yote haya na bila shaka ndo kamtuma mleta Uzi aje kumsafisha hapa. Hatudanganyiki,tunawajua CCM wote ni majizi hakuna cha Rioba ni msafi hapa.
 
TBCCM.
Wenyewe kwa wenyewe aina madhara.
 
Macbook Pro 16" Laptop- Apple bei ya mtandaoni kwa sasa ni TZS 8,058,197.00. Kwenye orodha ya TBC ni TZS12 milioni na ushee! Na hiyo bei ya mwaka jana.
Mmezidi majungu. yaani, bei ya biashara hizi za ku tender mnataka ifanane na ya mtaani? Hamjui risk ya hizi biashara?
 
Kwa ufisadi huu mnaachiaje nchi kwa kura? Mnaachiaje nchi iwe na tume huru na katiba mpya?
 
Hii sasa ndio ulikua JF. Shukrani sana mleta mada
 
Mimi sio mtaalamu kivile, ila kutokana na uzoefu kiasi wa kuhusika na masuala ya media nachelea kusema mtoa taarifa una information lakini kuna kitu unakificha aidha kwa kutokujua au kutokuelewa umesema vifaa vineletwa na vimewekwa stoo kutokana na kukosa wataalamu wa kufanya training na istallation, nimejaribu kupitia orodha tajwa hapo juu karibu asilimia 80% mpaka 85% (ya ninavyojijua mimi) vinaweza kutumika bila ya ujuzi wa ziada wala training ya ziada kwa mtu ambaye anafanya kazi kwenye media.

na hizo asilimia 10% mpaka 15% ya vifaa vilivyobaki, nina uhakika graduate wa telecommunication Engineering anaweza kuvifanyiwa installayion bila kuhitaji upekee huo unaosema.(na TBC wataalamu hawa wanao!)

hivyo kama vifaa vimetunzwa kwa ajili ya taratibu zingine za kiofisi ni bora useme, ila kuniambia kisa training na Installation nakataa, hakuna kifaa cha ajabu hapo asilimia 90% ni vya kawaida sana
 
Ayoub Rioba Chaha ni mtu safi kbs huyu jamaa hajui rushwa na sio mrushwa kabisa. Hana hata chembe ya ufisadi. Rioba tatizo lake kubwa hapo TBC ni kuleta aina ya uongozi ambao ulipaswa kupandikizwa taratibu. Aliingia na kuona baadhi ya watu hawafai kuwepo TBC na kujaza timu yake. Mtu ambaye ni muadilifu kama Rioba alitakiwa kuwa sehemu tofauti na hapo TBC ni dude moja kubwa sana. Wengine tulijua hawezi kudumu ama kukaa na watu wachafu na wezi. Kuna mkasa wa Suzan Mungy ambaye alifanya kitu tofauti na maagizo ya MD Rioba alichokifanya majibu yake aliyapata na yupo hapo alipo. Ayoub hapo anapigwa vita sana tena sana. Kwa hili nami namlaumu kwa uzembe wake inakuwaje unaongoza taasisi kubwa hivi nyaraka za zabuni ama malipo zinapita bila ya yeye kusitisha huo mchakato! Hapa anatakiwa kuwajibika kwa kufanyakazi kizembe. Endapo serikali inaweza kufanya uchunguzi wa kina huyu Rioba mimi nipo tayari hata kwenda kuapa popote sio Fisadi na wala hana tabia hizo. Ayoub hana siri ukijidai unampa siri ya dili ukae ukijua kuna siku ataitema mbele ya watu. RIOBA UNAWAJIBIKA KWA KUFANYAKAZI KIMAZOEA. ILA KAPU LA UFISADI HAUWEZI KULIBEBA HAUNA TABIA HIYO. Pole walikukosa Kasulu kwenye ajali ya gari watakupata kwa uongo wao huu.
 
Ni kweli Rioba sio fisadi. Hawa wa chini yake ndio tatizo. Na naamini akiwachukulia hatua mapema ingekuwa vyema kuliko yeye kukimbilia kujiudhuru.
 
Ni kweli Rioba sio fisadi. Hawa wa chini yake ndio tatizo. Na naamini akiwachukulia hatua mapema ingekuwa vyema kuliko yeye kukimbilia kujiudhuru.
Shida yake kubwa hana uwezo wa kuhimili hasira na jazba.
 
Mkuu angalia style ya uandishi wako isiendane na unavyoongea. Watakudaka mapema.
Punguza upumbavu, wamdake kwa kuweka fact and evidence kwa walipa kodi?

Huyu anastahili zawadi na siyo vitisho, hivi ni vitisho unaleta.
 

JEMO INVESTMENT & GENERAL ENTERPRISES LTD

mimi nikiona tu kampuni imesajiriwa kwa jina linaloishia na "investment and general interprises au general supplier" najua ni kampuni ya kupiga deal za kimchongo-mchongo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…