Tujihoji: Kwa nini hayati Julius Nyerere alitaka taifa letu liwe na Viongozi kama hayati Mkapa na hayati Magufuli na Sio Lowassa au Jakaya?

Tujihoji: Kwa nini hayati Julius Nyerere alitaka taifa letu liwe na Viongozi kama hayati Mkapa na hayati Magufuli na Sio Lowassa au Jakaya?

ndege zinatumika mpaka sasa na wananchi wote (hata wapinzani wanapiga selfii nazo!), uwanja huo pia ungetumika na watu wote. Hospitali nayo wanatibiwa watu wote. Tofauti ya hizo skendo nyingine walikula wahusika peke yao mwananchi hakuambulia kitu. Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Between two evils choose none!
Kwa ujinga wake wa kutaka kufanya mambo kwa haraka haraka bila hata research amesababisha madeni makubwa
 
Kwa ujinga wake wa kutaka kufanya mambo kwa haraka haraka bila hata research amesababisha madeni makubwa
Ni kweli, ila mimi kama 'devil's advocate' au wakili wa shetani (ni mtu ambaye huuchukua upande wa kinyume katika mjadala au majadiliano, mara nyingi akipinga maoni au mtazamo uliopo. Kazi ya mwakilishi huyu ni kuleta changamoto kwa dhana zilizopo, kuchochea mawazo ya kina au kupima nguvu ya hoja kwa kutoa maoni yanayopingana. Mara nyingi, jukumu hili linachukuliwa kwa lengo la kusaidia katika uchambuzi wa kina wa dhana au kutambua udhaifu wowote katika hoja au ushahidi uliowasilishwa. Ni muhimu kutambua kwamba kuwa "mwakilishi wa shetani" haimaanishi kwamba mtu huyo anasaidia uovu au shetani kwa kweli, bali wanatekeleza jukumu la kuleta mjadala wa kina na tathmini ya maoni tofauti.)

ndiyo hatukatai alikua na mapungufu mengi sana, ila katika mapungufu yake alionyesha nia thabiti ya mwananchi wa chini kabisa kufaidika na rasilimali za nchi ndo maana hata kama alijenga vitu bila kufata utaratibu bado faida yake ingebaki kwa mwananchi wa chini ndo kama hizo ndege, bwawa la umeme, kiwanja, hospitali ya rufaa na mengineyo. Hata kama yalikua nyumbani kwao bado wananchi wote wangevitumia kama ilivoyo hizo reli nk. Tofauti na wengine waliofanya kinyume na kujifaidisha wao pekee yao bila mtu wa chini kuambuli kitu.

Pale Congo Kinshasa, kulikua na mtu anaitwa Mobutu Sese Seko, alikuwa katili balaa na alifuja mali za Congo kisawasawa alitafuna hadi mfupa. Wananchi walio wengi walitamani aondoke, alipopinduliwa miaka ya 90s na Laurent Kabila watu walifurahi lakini baadae walikuja kusema haya "Mobutu aliiba na umma (fork) na baadhi ya makombo yalituangukia sisi walala hoi a.k.a wana wa nchi lakini huyu Kabila anaiba na kijiko, anakomba chote hakuna hata tunachopata sisi wasakatonge!"

Ndo maana narudia kusema 'between two evils choose none" kati ya maovu mawili usichague lolote.

A beggar doesn't choose!
 
Kama Nyerere angelikuwepo wakati wa utawala wa Magufuli wasingeelewana kabisa.
Kwa sababu Nyerere alikua muumini wa Utawala Bora,utawala wa kufuata kaitiba,kuheshimu sheria,miiko ya uongozi,kanuni na taratibu.
Kwa bahati mbaya kabisa Magufuli alikua kinyume kabisa na uongozi unaoheshimu katiba,sheria,miongozo,kanuni na taratibu.
Alikua ni kiongozi anaeendesha nchi hovyohovyo.
Kujenga mabarabara,madaraja,majengo kwa kuumiza watu ni aina ya uongozi uliopingwa na Dunia nzima.
Adolf Hitler,Makaburu wa kusini,jean Bokassa na wengine kama hao walijenga vizuri sana nchi zao lakni walipingwa na Dunia nzima na mmoja wapo aliewapinga watawala wa namna hiyo ni mwalimu Nyerere.
Nyerere aliheshimu Mahakama,bunge ,mabaraza ya madiwani,serikali za mitaa, washauri,wazee,Viongozi wa dini na wataalam,lakini Magufuli yeye alijiheshimu yeye peke yake.
Hakuheshimu Mahakama,bunge,mabaraza ya madiwani,wazee,Viongozi wa dini,washauri na wataalam..

Katika maisha mtu mmoja kukiuka miongozo walioiweka watangulizi wake bila kufuata utaratibu huyo ni mtu wa hovyo kabisa.
Mfano kama unaona sheria Fulani inachelewesha maendeleao,basi fuata taratibu zilezile zilizoiweka sheria hiyo kuiondoa,mfano,tumia bunge kuondoa sheria inayochelewesha maendeleo,sio kuliruka bunge na kujiamlia wewe mwenyewe kufanya jambo Fulani.
Kama jambo Liko mahakamani basi iachie Mahakama ilimalize kisheria.

Na Kuna vitu vingije kwa asili yake havibadilishwi ni kwenda navyo kwa utaratibu huohuo.

Mfano haki ya msingi ya mtu kusikilizwa huwezi ukaifuta lakini Magufuli alikua kinyume na haki hiyo.

Haiwezekani wagombea wote wa ubunge wa vyama vya upinzani wakawa hawajui ama wanakosea kujaza Fomu za ubunge na udiwani.hii imetokea katika utawala wa Magufuli TU hapa Duniani.
Na utashangaa ndani ya wagombea hao Kuna wanasheria wa miaka mingi na wengine wakiwa wabunge wa miaka mingi.

Kiongozi ni yule anaeongoza kwa kufuata matakwa ya anaowaongoza sio kwa matakwa yake.na sauti za anaowaongoza ni kupitia kwa wawakilishi wao yaani wabunge,madiwani,serikali za mitaa na n.k.

Sasa mtu anaamka tu asubuhi anasema kajengeni uwanja wa ndege wa kimataifa chato,nao wanaenda kujenga.
Je mpango huo ulipitishwa na bunge?

Kiongozi asieheshimu katiba na sheria sidhani kama Nyerere angemkubali.
Kama Nyerere aliwapinga wazanzibar kwa kujiunga na OIC peke Yao kwa kutofuata sheria,sijui Magufuli angemshawishi Nini Nyerere kwa kukanyaga katiba.
Hii ni sawa na Mchj au Padri ambaye hataki maongozi ya Mungu na maneno yake BIBLIA, anajitungia mambo yake na kuamua kufanya apendavyo.
 
Back
Top Bottom