CleverKING
JF-Expert Member
- Apr 24, 2014
- 8,502
- 25,470
CRDB ni benki ya wakulima kama..... Vijijini unalikumbuka hili tangazo? Tegemea bp ni nini...trekta meli ndege na vyombo vinginevyo...bp Tanzania limited ni zaidiiii! Je unakumbuka? Vikoromboso vinavyoendelea sasa iv kwenye radio ni aibu tupu. Damn I miss my childhood!!!
Du! mkuu, umenikumbusha mbali sana.
Mimi nilipenda sana usomaji wa taarifa za habari za watangazaji wafuatao.
Mzee mwenyewe nguli David Wakati RIP ( ambae hata kanisani Mtakatifu Albano) nasikia alikuwa akipenda kusoma somo la kwanza kwenye biblia)
Charles Hillary
Julius Nyaisanga
Salim Mbonde
Ahmed Jongo
Abisai Stephen
Peter Makorongo
Mikidadi Mahmud
Sekione Kitojo
Suleyman Kumchaya
Florian Kaiza
Jacob Tesha
Bujaga Izengo Kadago
Tumbo Tamim Risasi (alikuwa anapooza kidogo kwenye usomaji wake na ndio maana alikuwa hasomi taarifa kwenye "peek time" kama saa mbili usiku)
Sarah Dumba
Halima Kihemba
Betty Mkwasa
Chini ya marehemu David Wakati, RTD ilikuwa na heshima yake kwa wakati ule na kila msikilizaji aliweza kufahamu ni mtangazaji gani angesoma taarifa ya habari ya saa saba mchana, saa mbili jioni na saa nne ya usiku.Watangazaji walikuwa wakipangwa kusoma taarifa kulingana na uzito wa taarifa hizo na uwezo wao.
Kwa kweli RTD ilikuja kupoteza watangazaji hodari na wenye uwezo mkubwa wa utangazaji katika tasnia hiyo na ni masuala ya malipo ndio yaliyoanza kuwatawanya kwenye kutafuta maslahi sehemu zingine.
kwenye mwaka 2010 Anko J aljkuwa anatangaza Abood tv. Morogoro. kwasasa sipo moro so sijajua kama bado yupo hapo au tena amehama
Levoraaa levoraaaa levoraaaa levoraaa
Kwa vijana wa zamani. Unakumbuka nini unapopitia majina haya? Je, yuko wapi kwa sasa? Unamkumbuka katika kipindi kipi kilichokufurahisha?
1. Bujaga Izengo Kadago
2. Debora Mwenda
3. Sarah Dumba
4. Julius Nyaisanga
5. Charles Hillary
6. Eshe Mhidini
7. Frolian Kaiza
8. Tumbo Risasi
9. David Wakati
10. Halima Kihemba
11. Betty Mkwasa
12. January Costantine
13. Lando Mabula
14. Ben kiko
15. Abubakary Lyongo
16. Sued Mwinyi
17. Abisai Stevin
18. Nswima Ernest
19. Malima Ndelema
20. Richard Leo
21. Ahmed Jongo
22. Christina Chokunogela
23. Shaban Kissu
24. Jacob Tesha
25. Sallim Mbonde
26. Sekion Kitojo
27. Omary Jongo
28. Abdalla Majura
Yaani unapozungumzia RTD nakaumbuka vitu vingi sana,kama vile vipindi chei chei shangazi,mama na mwana,kombora-saa 11 asubuhi. Nakumbuka vipindi vya maigizo characters wake kama Mzee Mundu,Jangala,Bi nyakomba,Mzee Jongo etc bila kusahau igizo la twende na wakati characters kama Fungafunga,Kidude etc. Reporters kama Dominic Chilambo,Ben Kiko etc . Yote tisa kulikuwa na kitu ambacho kwa sasa ni nadra sana,utasikia mtangazaji anasema "......utakuwa nami mtangazaji wako........nikiwa na fundi mitambo...."
Tumalizie na huu wimbo
"Kuleni chakula bora...chaku-ujenga mwili....."
Kama huo huukumbuki basi kumbuka huu
"Dereva..kagonga mtu....eeh..sawa hiyoooo?.......haaaata. Hiyo si-sawa dereva acha vituko"
Pamoja mkuuMkuu sio Dereva kagonga mtu!! Usahihi ni kuwa
"Dereva kalewa gongo eeh sawa hiyoooo?......