Zamazamani
JF-Expert Member
- Jun 13, 2008
- 1,869
- 787
Aliitwa Morris Nyunyusa.Nasikia alikuwa kipofu anapiga ngoma 12Mzee mundu nae msimsahau katika michezo ya kuigiza!
Yule aliyepiga ngoma ya taarifa ya habari aliitwa nani?
What a talent!! Angekuwa ulaya angekuwa tajiri sana na kuingia kwenye vitabu vya kumbukumbu.Aliitwa Morris Nyunyusa.Nasikia alikuwa kipofu anapiga ngoma 12
Hiyo jingle ninayo mkuu kama unaihitaji nitafute kwenye whatsapp +255 752 22 06 49 nikutumieNakumbuka tangazo la dawa ya meno Aha..linda meno yako kwa saa ishirini na nne aha aha
Pia nikitoka shulen saa kumi nafungua redio ya baba panasonic nyeusi ina mshale flani ukiiwasha unapoint upande mwingne nakutana na kipindi cha harakati na ile jingle daah namiss sana mambo ya enzi zile
Kipindi cha Lugha Ya Kiswahili nilipenda sana wimbo(jingle) yake
"Tanzania Bara na Visiwani....ya Taifa hili lugha...." Nimesahau unavyoendelea.
Pia kipindi cha rushwa. Wimbo wake
"Wito nautoa kwa taifa zima, tuchukie rushwa kwani ni adui...."
Pia Mahoka na Pwagu na Pwaguzi.
Mchezo Wa redio nilikuwa nampenda mwigizaji mmoja akiitwa Matuga.
.
Mpendu na Shaban Kisu
Nakumbuka kipindi cha cheichei shangazi na uugua pole ule wimbo wakufungulia kipindi nilikuwa na upenda sana ingawa nilikuwa mdogo.
Wako wapi hawa jamaa??
Hongera zake mkuuSina hakika kwa Angalieni Mpendu lkn Shabani Kisu yupo, ni mkuu wa wilaya gani sijui though Kisu sio wa siku mingi kivile....
salute mkuu [emoji2]Mchezo wa mzee Jangala ikidhaminiwa na pombe aina ya chibuku, nakumbuka nyimbo, idara yetu ya uhamiaji nalo jukumu kubwa saanaaaa kuwakaribishaa kuwasafirishaa na kulinda mipaka yetu[emoji441][emoji443][emoji443][emoji445][emoji445]
Watoto wasafi moyonii ni nyoota za macho ya wazaziiiiii[emoji445][emoji445][emoji445][emoji443][emoji443][emoji441]
Shamba aaanii shambaani shambaani mazaoo boora shambaani, haya twendenii shaambanii wananchi tukaalimeee [emoji443] [emoji444] [emoji446] [emoji447]
Wanawakee wa Tanzania wazuuuriii saaaanaaa, wanawakeeee tanzaniaa maendeleo tanzaniaaaa[emoji445][emoji443][emoji441][emoji443][emoji445]
Kuleni chakula boora cha kuujenga muili naku.... Pa kulala pawe boraa[emoji443][emoji445][emoji441]
Wakati umewadia wa salam za wagonjwa hosipitalinii leo tunawapa poleee, ajuaye bwana Mungu kwa mfu kuwa mzima mgonjwa kuwa salamaa leo tunawapa polee[emoji445][emoji445][emoji443][emoji445][emoji445][emoji441]
Wananchiiiii tujifunzeni ushirikaaaaa wananchi tujifunzeni ushirikaaaaa [emoji441][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445]
Jamani vitaa imetangazwaa jamaaa wananchi wote tuwe imara, vijijini na mjini msisite kuwasema walanguzi[emoji445][emoji445][emoji445]
Matangazo sasa
1. Tumaa vifurushiii barua na pesa vitu mbalimbali vifike harakaaa tena kwa uhakikaaa, itumie sasaa shirika la posta na simu tanzaaaaniaaa ndio tegemeo letuu.
2. Hebu jitokezeee jioneshe simamaa mbelee za watuuu
3. Tairi general kutoka arushaaa tanzaaaaniaaa
4. Revolaaa revolaaaaa revolaaaaaa revolaaaaaaaa
5. Wee acha kula mali ya umma wee acha kujitafuna tafuna weeeee, wachaaaaaaaaa
6. Tumia chibuku ndio pombe bora, radha ya chibuku hujulikana, sifa moja na nyinginezo ni kulinda hadhi ya mnywaji
7. Komoooooaaaaa aaa komooooaaaa komoaaaa
8. Benki ya akiba ya posta ndio yako, benki ya akiba ya posta ni kwa watanzaniaaa woooote wakubwa kwa wadogo... Wananchi unaweza kufungua akaunti ya kawaaida, akaunti ya muda na akaunti ya muda maaalum.. Usingoje kesho ooo fungua akaunti yako leooo
Watangazaji hahaha Mama Deborah, Dominic Chilambo
Nimejikuta napata sweet memories tu
Nicheki nikutumie hiyo Nidhamu ya kazi ni msingi .......0758 393 393Dah Mengi
Usomaji wa taarifa wa habari ulikuwa wa makini. Sisi tukiwa wadogo tulikuwa tunabashiri wasomaji.
Na hii ndio Taarifa ya Habari isomwayo na ...... David Wakati, SS. Nkamba/ Juma nGondae/ jamani we
Kipindi cha klabu raha leo Shooooooow!
Salamu kwa wagonjwa!
Mchana mwema
Kipindi cha wafanyakazi jamani- Wimbo wa Msondo-n Nidhamu ya kazi ni msingi wa mafanikio.......( mwenye clip hiyo aiweke)
Pwagu na Pwaguzi
Mchezo wa Redio jamani wanaact kama vile unawaona!! Wasanii hao wangekuwepo leo wangepata hela sana!
Yule Mzee alikuwa anaitwa Moris Nyunyusa, inadaiwa alikuwa anapiga ngoma 10, cha kishangaza alikuwa mlemavu wa kutokuona.Mzee mundu nae msimsahau katika michezo ya kuigiza!
Yule aliyepiga ngoma ya taarifa ya habari aliitwa nani?
Hahaaa..vijembe viiingi
Kwakweli zamani kila kitu kilikua kwenye mpangilio..
Kumekucha jama kumekuchaaaaa na jogoo vijijini wanawika hata na jua mbinguni kinatoka Wazalendo amkeni tufanye kazi saaasaaa[emoji323] [emoji323] [emoji323] [emoji122] [emoji122] [emoji122] kweli nyakati zinasonga mbele.[emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120]Wazungu wanasema "Old is Gold" tulikua pembeni ya babu zetu tukifatisha wasoma habari.
Na kuna kale kamwimbo ukikasikia tu unajua mida wa kuamka kwenda shule...daah kalikia kanakata stim zooote.
HIVI TAUSI ILIONYESHWA KITUO CHA K.B.C TV?Matuga alikuwa na sauti safi iliyoyulia, walikuwepo kina havijawa, mzee jongo, maua, kuna yule dada alikuwa anacheza nafasi mbili ktk mchezo mmoja, sauti ya kihindi na sauti ya kawaida jina limenitoka, alikuwa mkorofi kwenye mchezo wa mkataa pema pabaya panamwita.
Television zilivyoingia, mnakumbuka tamthilia ya Tausi miaka ya tisini katikatika hapo, unakuta mtaani kuna nyumba moja tu ndio wanativii manajazana kwenye nyumba ya watu kuangalia tamthilia ya Tausi