Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

1.SIku ya matangazo ya mpira (sauti ya Charles Hillary) , utasikia "...na mafundi mitambo kwenye OB van ;David Namaloye ,Ali Said Tunku, Fundi Ali Kengele.."
2.Mabingwa wa salamu Wajadi Fundi wa Mahuta Shimoni , Dula One wa makorora Tanga
3.Taarifa ya Habari asubuhi na Jacob Tesha
4.Kipindi cha Malenga wetu /mashairi kichizi kila siku saa nane mchana


Dah ilikuwa raha sana
 
Daah Enzi za kununua kadi na kutuma salamu redioni!! Unawapaisha wadau wako wote. Nyakati zimekwenda wapi??
 
Nakumbuka tangazo la dawa ya meno Aha..linda meno yako kwa saa ishirini na nne aha aha
Pia nikitoka shulen saa kumi nafungua redio ya baba panasonic nyeusi ina mshale flani ukiiwasha unapoint upande mwingne nakutana na kipindi cha harakati na ile jingle daah namiss sana mambo ya enzi zile
Hiyo jingle ninayo mkuu kama unaihitaji nitafute kwenye whatsapp +255 752 22 06 49 nikutumie
 
1. Hisia na muziki: yaani hapo inatengenezwa story nzuri kupitia nyimbo za wakati huo kilikua kinarushwa saa tatu na nusu usiku, siku nimeisahu
2.ATC Hewani: ratiba za usafiri wa anga kupitia shirika letu la ndege la ATC
 
Kipindi cha Lugha Ya Kiswahili nilipenda sana wimbo(jingle) yake
"Tanzania Bara na Visiwani....ya Taifa hili lugha...." Nimesahau unavyoendelea.

Pia kipindi cha rushwa. Wimbo wake
"Wito nautoa kwa taifa zima, tuchukie rushwa kwani ni adui...."

Pia Mahoka na Pwagu na Pwaguzi.

Mchezo Wa redio nilikuwa nampenda mwigizaji mmoja akiitwa Matuga.
.

Matuga alikuwa na sauti safi iliyoyulia, walikuwepo kina havijawa, mzee jongo, maua, kuna yule dada alikuwa anacheza nafasi mbili ktk mchezo mmoja, sauti ya kihindi na sauti ya kawaida jina limenitoka, alikuwa mkorofi kwenye mchezo wa mkataa pema pabaya panamwita.

Television zilivyoingia, mnakumbuka tamthilia ya Tausi miaka ya tisini katikatika hapo, unakuta mtaani kuna nyumba moja tu ndio wanativii manajazana kwenye nyumba ya watu kuangalia tamthilia ya Tausi
 
Mpendu na Shaban Kisu

Angalieni Mpendu.....
Shabani Kisu sio wa siku nyingi kivileee, ni D
Nakumbuka kipindi cha cheichei shangazi na uugua pole ule wimbo wakufungulia kipindi nilikuwa na upenda sana ingawa nilikuwa mdogo.

Chei chei shangazi, cheichei shangazi, shangazi chei shangazi, cheichei shangazi
Uje tena shangazi, uje tena shangazi......chei shangazi, uje tena shangazi........
 
Mchezo wa mzee Jangala ikidhaminiwa na pombe aina ya chibuku, nakumbuka nyimbo, idara yetu ya uhamiaji nalo jukumu kubwa saanaaaa kuwakaribishaa kuwasafirishaa na kulinda mipaka yetu[emoji441][emoji443][emoji443][emoji445][emoji445]

Watoto wasafi moyonii ni nyoota za macho ya wazaziiiiii[emoji445][emoji445][emoji445][emoji443][emoji443][emoji441]

Shamba aaanii shambaani shambaani mazaoo boora shambaani, haya twendenii shaambanii wananchi tukaalimeee [emoji443] [emoji444] [emoji446] [emoji447]

Wanawakee wa Tanzania wazuuuriii saaaanaaa, wanawakeeee tanzaniaa maendeleo tanzaniaaaa[emoji445][emoji443][emoji441][emoji443][emoji445]

Kuleni chakula boora cha kuujenga muili naku.... Pa kulala pawe boraa[emoji443][emoji445][emoji441]

Wakati umewadia wa salam za wagonjwa hosipitalinii leo tunawapa poleee, ajuaye bwana Mungu kwa mfu kuwa mzima mgonjwa kuwa salamaa leo tunawapa polee[emoji445][emoji445][emoji443][emoji445][emoji445][emoji441]

Wananchiiiii tujifunzeni ushirikaaaaa wananchi tujifunzeni ushirikaaaaa [emoji441][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445]

Jamani vitaa imetangazwaa jamaaa wananchi wote tuwe imara, vijijini na mjini msisite kuwasema walanguzi[emoji445][emoji445][emoji445]


Matangazo sasa
1. Tumaa vifurushiii barua na pesa vitu mbalimbali vifike harakaaa tena kwa uhakikaaa, itumie sasaa shirika la posta na simu tanzaaaaniaaa ndio tegemeo letuu.

2. Hebu jitokezeee jioneshe simamaa mbelee za watuuu

3. Tairi general kutoka arushaaa tanzaaaaniaaa

4. Revolaaa revolaaaaa revolaaaaaa revolaaaaaaaa

5. Wee acha kula mali ya umma wee acha kujitafuna tafuna weeeee, wachaaaaaaaaa

6. Tumia chibuku ndio pombe bora, radha ya chibuku hujulikana, sifa moja na nyinginezo ni kulinda hadhi ya mnywaji

7. Komoooooaaaaa aaa komooooaaaa komoaaaa

8. Benki ya akiba ya posta ndio yako, benki ya akiba ya posta ni kwa watanzaniaaa woooote wakubwa kwa wadogo... Wananchi unaweza kufungua akaunti ya kawaaida, akaunti ya muda na akaunti ya muda maaalum.. Usingoje kesho ooo fungua akaunti yako leooo

Watangazaji hahaha Mama Deborah, Dominic Chilambo
Nimejikuta napata sweet memories tu
salute mkuu [emoji2]
MAMA NA MWANA ..DEBORA MWENDA
 
Dah Mengi
Usomaji wa taarifa wa habari ulikuwa wa makini. Sisi tukiwa wadogo tulikuwa tunabashiri wasomaji.
Na hii ndio Taarifa ya Habari isomwayo na ...... David Wakati, SS. Nkamba/ Juma nGondae/ jamani we
Kipindi cha klabu raha leo Shooooooow!
Salamu kwa wagonjwa!
Mchana mwema
Kipindi cha wafanyakazi jamani- Wimbo wa Msondo-n Nidhamu ya kazi ni msingi wa mafanikio.......( mwenye clip hiyo aiweke)
Pwagu na Pwaguzi
Mchezo wa Redio jamani wanaact kama vile unawaona!! Wasanii hao wangekuwepo leo wangepata hela sana!
Nicheki nikutumie hiyo Nidhamu ya kazi ni msingi .......0758 393 393
 
Namkumbuka msomaji wa taarifa ya habari ya R.T.D Barnabas Mluge.Nakumbuka vipindi vya misakato, ,mambo mpwito mpwito,club raha leo show,mazungumzo baada ya habari,Usiku wa dansi,Watangazaji Christine Chakunogela,Jacob Tesha,Mickdad Mahamdu Mruma, naikumbuka pia idhaa ya biashara ya redio Tannzania na n.k n.k!!!!!!!
 
Nakumbuka kipindi cha maneeeeno hayoooo asubuhi na mapema nikiwahi kwenda shule ya msingi janjajanja.
 
Kwenye michezo alikua halima mchuka na ezekiel malongo( RIP wote)

Salamu namkumbuka Malima Ndelema. ( nakumbuka kulikua mpaka kuna klabu za salamu mojawapo ilikua Yataka Moyo salamu klabu)
 
Ukifika umefika utoke uende wapii RTD ( hilo lilikua tangazo lao ah ah ah kitambo)
 
Wazungu wanasema "Old is Gold" tulikua pembeni ya babu zetu tukifatisha wasoma habari.

Na kuna kale kamwimbo ukikasikia tu unajua mida wa kuamka kwenda shule...daah kalikia kanakata stim zooote.
Kumekucha jama kumekuchaaaaa na jogoo vijijini wanawika hata na jua mbinguni kinatoka Wazalendo amkeni tufanye kazi saaasaaa[emoji323] [emoji323] [emoji323] [emoji122] [emoji122] [emoji122] kweli nyakati zinasonga mbele.[emoji120] [emoji120] [emoji120] [emoji120]
 
Matuga alikuwa na sauti safi iliyoyulia, walikuwepo kina havijawa, mzee jongo, maua, kuna yule dada alikuwa anacheza nafasi mbili ktk mchezo mmoja, sauti ya kihindi na sauti ya kawaida jina limenitoka, alikuwa mkorofi kwenye mchezo wa mkataa pema pabaya panamwita.

Television zilivyoingia, mnakumbuka tamthilia ya Tausi miaka ya tisini katikatika hapo, unakuta mtaani kuna nyumba moja tu ndio wanativii manajazana kwenye nyumba ya watu kuangalia tamthilia ya Tausi
HIVI TAUSI ILIONYESHWA KITUO CHA K.B.C TV?
 
Back
Top Bottom