nra2303
JF-Expert Member
- Jul 28, 2015
- 2,975
- 2,547
Alafu wasanii wa sasa hata ngoma moja hawajui kupiga wkt kila nyezo wanayo!Aliitwa Morris Nyunyusa.Nasikia alikuwa kipofu anapiga ngoma 12
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Alafu wasanii wa sasa hata ngoma moja hawajui kupiga wkt kila nyezo wanayo!Aliitwa Morris Nyunyusa.Nasikia alikuwa kipofu anapiga ngoma 12
HAPA UMENIPELEKA MOJA KWA MOJA IDHAA YA BIADHARA YA REDIO TANZANIA. [emoji122] [emoji122] [emoji122] [emoji122]Mchezo wa mzee Jangala ikidhaminiwa na pombe aina ya chibuku, nakumbuka nyimbo, idara yetu ya uhamiaji nalo jukumu kubwa saanaaaa kuwakaribishaa kuwasafirishaa na kulinda mipaka yetu[emoji441][emoji443][emoji443][emoji445][emoji445]
Watoto wasafi moyonii ni nyoota za macho ya wazaziiiiii[emoji445][emoji445][emoji445][emoji443][emoji443][emoji441]
Shamba aaanii shambaani shambaani mazaoo boora shambaani, haya twendenii shaambanii wananchi tukaalimeee [emoji443] [emoji444] [emoji446] [emoji447]
Wanawakee wa Tanzania wazuuuriii saaaanaaa, wanawakeeee tanzaniaa maendeleo tanzaniaaaa[emoji445][emoji443][emoji441][emoji443][emoji445]
Kuleni chakula boora cha kuujenga muili naku.... Pa kulala pawe boraa[emoji443][emoji445][emoji441]
Wakati umewadia wa salam za wagonjwa hosipitalinii leo tunawapa poleee, ajuaye bwana Mungu kwa mfu kuwa mzima mgonjwa kuwa salamaa leo tunawapa polee[emoji445][emoji445][emoji443][emoji445][emoji445][emoji441]
Wananchiiiii tujifunzeni ushirikaaaaa wananchi tujifunzeni ushirikaaaaa [emoji441][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445]
Jamani vitaa imetangazwaa jamaaa wananchi wote tuwe imara, vijijini na mjini msisite kuwasema walanguzi[emoji445][emoji445][emoji445]
Matangazo sasa
1. Tumaa vifurushiii barua na pesa vitu mbalimbali vifike harakaaa tena kwa uhakikaaa, itumie sasaa shirika la posta na simu tanzaaaaniaaa ndio tegemeo letuu.
2. Hebu jitokezeee jioneshe simamaa mbelee za watuuu
3. Tairi general kutoka arushaaa tanzaaaaniaaa
4. Revolaaa revolaaaaa revolaaaaaa revolaaaaaaaa
5. Wee acha kula mali ya umma wee acha kujitafuna tafuna weeeee, wachaaaaaaaaa
6. Tumia chibuku ndio pombe bora, radha ya chibuku hujulikana, sifa moja na nyinginezo ni kulinda hadhi ya mnywaji
7. Komoooooaaaaa aaa komooooaaaa komoaaaa
8. Benki ya akiba ya posta ndio yako, benki ya akiba ya posta ni kwa watanzaniaaa woooote wakubwa kwa wadogo... Wananchi unaweza kufungua akaunti ya kawaaida, akaunti ya muda na akaunti ya muda maaalum.. Usingoje kesho ooo fungua akaunti yako leooo
Watangazaji hahaha Mama Deborah, Dominic Chilambo
Nimejikuta napata sweet memories tu
matangazo ya vifo tuu, kutwa mara saba.Wakuu hebu tukumbushane enzi zile za Radio Tanzania, enzi ambazo Radio ndio ilikuwa kila kitu katika suala zima la kupata habari. Tukumbushane watangazaji mahiri wa enzi zile, vipindi vizuri pamoja na vituko mbalimbali ambavyo huwezi kuvisahau enzi za RTD.
Karibuni...
Umesahau idhaa ya biadhara special kwa vijana wa enzi hizo. Na idhaa ya taifa na kipindi cha mkulima wa kisasa special kwa wazeeKipindi cha club raha leo show na kile cha "noon spin" external service kila siku saa 6 mchana , walikuwa wanasikiliza mabrazamen na msisita duh. Kazi kweli
radio csssete maarufu enzi hizo ilikuwa ni memory Q!!Nakumbuka nilikua sifaham maana ya kipindi cha "club raha leo shoooow" kikinikera kweli kikianza! Na hakuna station nyingine kubadilisha labda tuweke cassete ya UB40! Time hizo baba awe hajarudi home lkn, akirudi hatuna tena access na radio! Those were days
Upo sahihi,idhaa ya biashara ilikuwa ni special kwa mashirika ya umma - kabla mtangazaji hajaanza mambo yake alikuwa anatuomba tuburudike kwa Muziki.Umesahau idhaa ya biadhara special kwa vijana wa enzi hizo. Na idhaa ya taifa na kipindi cha mkulima wa kisasa special kwa wazee
yaaani we acha tu mtoa thread kanikymbusha Zama!!
Tupo tunaondoa STRESS!!Aisee mpaka mie najiona dogo dah
Kipindi cha club raha leo show na kile cha "noon spin" external service kila siku saa 6 mchana , walikuwa wanasikiliza mabrazamen na msisita duh. Kazi kweli
UNCLE J (R.P.I)Upo sahihi,idhaa ya biashara ilikuwa ni special kwa mashirika ya umma - kabla mtangazaji hajaanza mambo yake alikuwa anatuomba tuburudike kwa Muziki.
Unakumbuka kipindi cha Muziki na BP cha uncle J Nyaisanga, kila jumatano saa 1:15 jioni, hapo ndio tulikuwa tunapata vitu vipya kabisa toka majuu?
Nchi ilikuwa katika ubora wake!! amani kibaooo!!Hotuba za baba wa taifa baadaya mazungumzo baadaya habari
UNAKUMBUKA KIPINDI CHA AFRICA JOURNAL? Habari za wiki nzima za Africa hasa O.A.U.Nilipenda External Service sana nikiwa likizo nilikuwa namsikiliza Eda Sanga akituma salam na miziki ya akina Michael Jackson, Cool and the Gang, Bonny M halafu habari toka wapigania uhuru waliokuwa wanatumia External kwenye propaganda zao. Hapo uzalendo ulitujaa tunataja kanuni, imani bila kukosea nukta. We baba wee. Yako wapi sasa. Radio nyingi lakini hakuna chochote watoto watajua.
Elimu ya watu wazima, Kilimo chetu, umoja wa mataifa week hiii.
Walikuwa wananikera na ile miziki yao ya makabila SIPATI PICHA!Heri yako wewe ulikuwa na option ya cassette, sisi ilikuwa only Radio basi, nakumbuka kitu kikubwa brand ya "National Panasonic". Iwapo hupendi kipindi/ program fulani option ilikuwa ni kuchagua KBC Nairobi, na huko KBC ulikuwa unaombea usikutane na ile miziki yao ya "kanindo"
Nadhani betty Chalamila ndo baadae aliolewa na kujiita betty Mkwasa.kwao ni mafinga Iringa maeneo ya KINYANAMBO!!
- Jamani external service na Legandary Edda Sanga, ilikuwa burudani
- Watangazaji wa kike na sauti murua, thank God wengine bado wapo: Alacia Maneno, Christine Chokunegela, Betty Chalamila n.k
- Julius Nyaisanga (RIP) wakati anaripoti sherehe mbalimbali utapenda
- Misakato
- Mazungumzo baada ya habari