Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Pia kulikuwa na kipindi cha MISAKATO kila Jumamnosi saa 3 asubuhi, kulikuwa na nyimbo mpya za wiki. Watayarishaji na waongozaji wa kipindi walikuwa wanapokezana Uncle J Nyaisanga, Michael Katembo, na Henry Michael Libuda. Walikuwa pia ni watayarishaji na waongzaji wa kile kipindi cha Club Raha Leo. wote hao ni marehemu, miaka inakwenda loh.

Vv
Maiko Katembo alikuwa na kipindi chake pia cha mkoa kwa mkoa. Alikuwa na mbwembwe nyingi ili wasikilizaji wampende maana alijua ngoma za makabila hazina wapenzi sana!!Ama kweli siku zimesonga mbele!!!
 
kipindi hiki ndio hamjataja "mashairi" msomaji Athuman Khalfan saa nane nane mchana!

Nilikuwa sikipendi... kikiisha hicho kipindi kinakuja kipindi cha ombi lako ambacho baade kilibadilishwa jina na kuwa chaguo la msikilizaji
 
Bila kusahau wakati wa Taarifa ya Habari saa saba Mchana Taarifa ya Kiongozi kuachishwa Kazi kwa Manufaa ya Umma hilo Lilieleweka Vizuri sana Na Watumishi kuwa Na Maadili na Nidhamu
 
Malenga wetu, du sikuwahi kukipenda hichi kipindi lakini ajabu nilikuwa napenda sana kusoma mashairi kwenye gazeti la uhuru walikuwa wanatabia ya kujibizana ana kama taarabu ya sasa.
 
  • Jamani external service na Legandary Edda Sanga, ilikuwa burudani

  • Watangazaji wa kike na sauti murua, thank God wengine bado wapo: Alacia Maneno, Christine Chokunegela, Betty Chalamila n.k

  • Julius Nyaisanga (RIP) wakati anaripoti sherehe mbalimbali utapenda
  • Misakato
  • Mazungumzo baada ya habari
Betty Chalamila sasa ni DC Betty Mkwasa,sambamba na Halima Kiemba, Shaaban Kisu nk. Ni wengi
Ninatizama dirishani ohoo, naona ni mvua inanyesha oho hakuna kilichobakia oho ila ni huzuni na uchungu ehe, mwingine ni Asha usifate mambo ya dunia asha wewe kumbuka wemaaa Tabora jazz. Tulikuwa tunakacha Math siku nyingine na physics ili kusikia vigongo hivyo. Mhu.

[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji2] [emoji1] [emoji1] [emoji1]

wanafuta hawa mods ni yule wa Moro Juma ****** najua watafuta tena. Yule mzee aliyeimba "Njoo tucheze rumba rumba michangani aaaaaa rumba michanganiii" Hivi hakuwa mwanzilishi wa Cuban marimba kweli??? Wa moro. Jina wanalibana sababu ni sawa na wale alosema baba J. kuwa walifukuzwa. Weka singular badala ya wingi.
 
Nakumbuka kipindi cha kuripoti matukio,kilikua ni usiku kama sikosei ilikuwa saa 3 usiku,kuna Mwandishi mmoja alikuwa akiitwa Tumbo Risasi,nilikuwa namkubali sana
 
Nilikua napenda vipindi vyote kasoro malenga wetu kina mzee Andanenga. Nilivyovipenda zaidi ni mama na mwana, hisio sijui pitio la muziki, club raha leo show, pagu na pwaguzi, mazungumzo baada ya habari. Yule dada alikua akitunga hadithi kwa kutumia nyimbo ka ustadi mkubwa sana. Nakumbuka zaidi kipindi cha "ukulima wa kisasa". Kutokana na utoto nilikua sisikii vizuri baadhi ya maneno nikawa naimba "mwananchi mkulima alikakayoo, mwananchi mkulima alikakayooo..". Siku moja mamangu mdogo akaniskia naimba akacheka hadi machozi, ndo kuniambia ni "mwananchi mkulima wa kisasa yooo..
 
Duh....wee mkali..... umeukumbuka hadi wimbo wa sakina?
Nimesoma maneno tu sauti ikaja....Big up...you made my morning
nimefurahi zaidi kama nawe bado unakumbuka hizo vitu....enzi hizo ndo nimetoka kupima mkono kama ukipitia utosini unaweza kugusa sikio ili nijihakikishie kuanza std one.
 
Your correct. Nakumbuka nilivyunja mlango wa redio upande wa kuwekea kanda......niliweka kanda, kumbe haijakaa vizuri mie nikang'ang'aniza kufunga mlango, kutahamaki mlango umevunjika, kipigo nilichokipata kutoka kwa mother sitakaa nisahau
dah!Aisee ile milango kumbe tulivunja wengi!Nami nilikuwa naforce kanda ya Chaka chaka mlango ulipovunjika mdingi akanipa kisago.
 
Dada Sango upo wapi nakukumbuka Dom wakati mmehamishiwa kule na mmeo. Sauti ya Sango na Ahamed ilikuwa inakosha jamani. Dada Sango kama upo humu ni PM tujuzane ya zama zile.
Dada Sango Kipozi, wakati huo akiitwa Sango Othman Tuwa, alikuwa shule ni kwetu Muhimbili Mwaka 1975, kwenye kipindi cha watoto, Mimi ndio nilikuwa staa niliyesoma historia ya shule na kujibu maswalu Mengine. Nilkuwa std.VI
 
Kusema za ukweli siku hizi hakuna watangazaji bali kuna waropokaji na wapiga domo huko studio.......baada ya kuelimika kupitia vyombo vya habari jamii ndio kwanza inahiribiwa........hakuna kipindi chenye manufaa kwenye jamii zaidi ya kuitangaza zinaa na matendo ya ngono.......
Matukio ya wasanii kufanya ngono ndio yanayopewa kipaumbele kuliko matukio mengi ya msingi yanayozinguka jamii zetu.....

Mtangazaji ukimuona mtaani mpaka unashindwa kumtofautisha na watumiaji wa mihadarati kwa jinsi alivyo na muonekano mbaya.....
Kweli mkuu,uwezekano wa madogo wa leo kuelimika kupitia vyombo vya habari ni mdogo,nakumbuka wakati ule kulikuwa na vipindi maalum vya masomo kwa shule za msingi muda wa asubuhi,kama hukwenda shule siku hiyo ukizama humo unapata faida,siku hizi tunasikiliza JAHAZI.
 
Dada Sango Kipozi, wakati huo akiitwa Sango Othman Tuwa, alikuwa shule ni kwetu Muhimbili Mwaka 1975, kwenye kipindi cha watoto, Mimi ndio nilikuwa staa niliyesoma historia ya shule na kujibu maswalu Mengine. Nilkuwa std.VI
Mbona raha, mimi dada Sango nimekutana naye nikiwa nafanya kazi shirika la kigenin na yeye yupo RTD Dodoma pamoja na mme wake. Jamani sauti zao mpaka kesho zinasika. Dada Sango kumbuka ofisi opposit na manispaa ya Dom enzi zile niikuwa mdogo wako sisemi zaidi. Ukienda moja kwa moja unafika kwako na ofisi ya RTD Dom.
 
Kweli mkuu,uwezekano wa madogo wa leo kuelimika kupitia vyombo vya habari ni mdogo,nakumbuka wakati ule kulikuwa na vipindi maalum vya masomo kwa shule za msingi muda wa asubuhi,kama hukwenda shule siku hiyo ukizama humo unapata faida,siku hizi tunasikiliza JAHAZI.

Kweli ndugu.....siku hizi mtangazaji maarufu ni yule anayeonesha umahiri wa kuhamasisha ngono......na ndio maana akili za vijana wetu zimeelekea kwenye ngono tu.....kwa kuwa ni mambo yanayosikika mara kwa mara na kuhamasishwa na vyombo vya habari......
Ki kiukweli tunajenga taifa la vijana wavivu wanaowaza ngono na starehe pasipo kuvuja jasho....,,
 
Jamani, sina uhakika naweza kukosolewa, maana enzi hizo sikuwa na access ama control ya radio - kila kitu kuhusu radio kilikuwa chini ya mzee,

Inasemekana jamaa (Ben Kiko) alikuwa reporter kwenye vita ya Kagera (alikuwa uwanja wa mapambano/ mstari wa mbele), bahati mbaya jeshi letu lilipata dhahama kwamba tulikuwa tunashambuliwa adui - jamaa alisikika akisema "ndg zangu tunashambuliwa hapa, tunapigwa jamani......" na maneno kama hayo. Kuona hivyo jamaa aliondolewa front na kurudishwa Tabora.
Siyo kweli. Amin alipigwa moja kwa moja toka vita ilivyoanza, japo kulikuwa na majibizano hapo Lukaya na mahali panaitwa Luweero na Kapeeka. Wakati wote huo, Ben Kuko alikuwa ni burudani tosha kwa ripoti zilizokuwa zibawakejeli askari wa Amin, unaweza kumlinganusha na Jerry Muro lakini kwa sauti ya Hemedi Kivuyo anapokuwa anainanga timu yenu iliyofungwa!!
 
Back
Top Bottom