Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Kweli ndugu.....siku hizi mtangazaji maarufu ni yule anayeonesha umahiri wa kuhamasisha ngono......na ndio maana akili za vijana wetu zimeelekea kwenye ngono tu.....kwa kuwa ni mambo yanayosikika mara kwa mara na kuhamasishwa na vyombo vya habari......
Ki kiukweli tunajenga taifa la vijana wavivu wanaowaza ngono na starehe pasipo kuvuja jasho....,,
Ni shida mkuu!
 
Ivi yule jamaa wa mazungumzo baada ya habari na maneno hayo alikuwaga nani maana alikuwa na maneno kuntu sana yule jamaa! Yuko wapi na anajishughulisha na nini?
Mzee Paulo Sozigwa
Namkumbuka pia Edda Sanga wa kipindi cha mama na mwana pia alikuwa mmahiri sana wa kusoma habari pamoja na mtangazaji Mwafisi kwa habari walikuwa vizuri
....viashiria vyote kilikuwa kinanikonga kile cha Majira...na jingle ya uzazi wa mpango...wameiona nyota ya kijani ya uzazi wa mpango..zindukaa🙂
 
kipindi hiki ndio hamjataja "mashairi" msomaji Athuman Khalfan saa nane nane mchana!
Halafu ijumaa mchana waumini wa dini ya kiislamu watakumbuka sauti tulivu ya mufti wao sheikh Hemed bin Jumaa bin Hemed akitoa mawaidha kwa upole na uhakika tena bila jazba....mpaka sie tusio waislamu tulikuwa tunavutiwa kusikiliza...
 
mkuu enzi hizo betri (ziliitwa mawe) zikikuwa rafiki sana kwa bajeti ya familia. kuna redio za mbao betri zikiwekwa kwenye kasha (cylinder ya plastic) na kutumika si chini ya miezi 6. kazi kubwa kuzichemsha kwenye maji na kuanika tu. ningali mdogo nilitumwa kununua mawe NATIONAL SPECIAL (za kijani) nikasahau, muuza duka kanifungashia za Burundi nikarudishwa kwa bakora. watu walitambua umuhimu wa hbr japo kulighubikwa na uhaba wa redio.
Betrii ilikuwa shida. Wakati wa redio za Memory Q, kuna mtu kazi yake ilikuwa Ku rewind kwa kutumia peni ya Bic wakati huo kwenye redio ndio alikuwa na mamlaka ya kusema. Hata akisema uongo haikuwa busara kubishana naye!!
 
Kwenye michezo alikua halima mchuka na ezekiel malongo( RIP wote)

Salamu namkumbuka Malima Ndelema. ( nakumbuka kulikua mpaka kuna klabu za salamu mojawapo ilikua Yataka Moyo salamu klabu)
Hiyo mbona juzi tu! Mwenyewe alikuwa akiitwa Abdul Masudi Jawewa(JAW).
Yaani jamani utoto bwana. Mi nakumbuka nikiwa darasa la pili nikawa naenda saa nane shule wakati wengie woote ( broethers& sisters) wanaenda asubuhi. Sasa mimi naachwa na houseboy na housegirl. sasa housegirl anaenda sokoni ananichukua nakumbuka tunapitia nyumba Fulani ( hizi zilikuwa za serekali) na yetu ilikuwa ya serekali maeneo yanaitwa uzunguni, sitataja Mkoa isiwe identified. Basi sasa ndio najua huyo housegirl alikuwa anaenda kwa BF napewa fizzes ( sidhani kama sasa zipo) ileinawekwa kwenye maji unakunywa kama juice ( note: sio kuwa nyumbani havikuwepo basi tu utoto) napewa na buiscuit nakunywa wao wana- disappear. Jamani haya mambo unaweza andika kitabu!
 
Betrii ilikuwa shida. Wakati wa redio za Memory Q, kuna mtu kazi yake ilikuwa Ku rewind kwa kutumia peni ya Bic wakati huo kwenye redio ndio alikuwa na mamlaka ya kusema. Hata akisema uongo haikuwa busara kubishana naye!!
batery za Nationa ilikuwa deal mjini,kidogo za phillips utapata...,zikizingua unazibonda bonda na kuzianika juani huku unazilinda...
 
Hivi wakuu TBC wanaweza kuwa na backup ya vitu vya zamani. ..mfano...audio clip za Jingles na signature tunes za vipindi mbalimbali. ..kipindi kama cha Bima yako, sayansi na teknolojia(hii iliimbwa na Marehemu Capt.Komba)..na nyingine kama alizotuonjesha mleta mada.

Nadhani kama wanaweza ku compile hivi vitu kwa watu wanaopenda kujikumbusha uzalendo wakajipatia kumbukumbu. Au ndio issues za copy right labda itakuwa shida.
 
Nilikuwa sikipendi... kikiisha hicho kipindi kinakuja kipindi cha ombi lako ambacho baade kilibadilishwa jina na kuwa chaguo la msikilizaji
Hapo ombi lako umenigusa!mishale ya saa tisa mchana hivi,nilikuwa navizia nyimbo za msondo hapo...
 
Nilikuwa sikipendi... kikiisha hicho kipindi kinakuja kipindi cha ombi lako ambacho baade kilibadilishwa jina na kuwa chaguo la msikilizaji
ram uko fit...,nilikuwa najaribu kukumbuka hiyo ombi lako ikawa inagoma.
 
Siyo kweli. Amin alipigwa moja kwa moja toka vita ilivyoanza, japo kulikuwa na majibizano hapo Lukaya na mahali panaitwa Luweero na Kapeeka. Wakati wote huo, Ben Kuko alikuwa ni burudani tosha kwa ripoti zilizokuwa zibawakejeli askari wa Amin, unaweza kumlinganusha na Jerry Muro lakini kwa sauti ya Hemedi Kivuyo anapokuwa anainanga timu yenu iliyofungwa!!
Mkuu nashukuru kwa kujazia, sikuthibitisha iwapo tulipigwa ndio maana nilisema inasemekana.
Ila hilo la Kivuyo na Jerry Muro umenivunja mbavu.
 
Halafu ijumaa mchana waumini wa dini ya kiislamu watakumbuka sauti tulivu ya mufti wao sheikh Hemed bin Jumaa bin Hemed akitoa mawaidha kwa upole na uhakika tena bila jazba....mpaka sie tusio waislamu tulikuwa tunavutiwa kusikiliza...
Mimi ni Mristo - ila kila ijumaa saa 8:02 alasiri nilikuwa sikosi kumsikiliza Mufti Hemed Bin Jumaa bin Hemed, ki ukweli yule mzee Pengo lake halitazibika.
 
Mkuu uko vizuri, nimejikuta nacheka tu, hiki kipindi kilikuwa siku ya jumapili saa mbili asbh, watoto wa shule fulani wanajiachia kwa nyimbo, hadithi n.k bila kusahau historia ya shule. Mwavita makamba, aliwahi kushiriki hiki kipindi wakati huo mzee makamba ni mkuu wa mkoa wa kigoma
 
Hivi dada Sara kesha tangulia??? Rip sauti yake we hakuna siku hizi wa kumuiga.
Kweli usemayo,ilikuwa sauti ya pekee.Yes alishatangulia sikumbuki vizuri kama ilikuwa ni mwishoni mwa mwaka jana au mwanzoni mwa mwaka huu akiwa mkuu wa wilaya katika moja ya wilaya kama sio mkoani mbeya basi ni mkoani iringa.
 
Back
Top Bottom