Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

I felt sorry for him kuna mgombea ububge mmoja sijui nani alitishia kumtoa kws mandata km angeandika hbr zake ndio akajiua. Nilikuwa napenda sana aliyvyokuwa anaongea

Ni kweli mkuu, huyu alikuwa ni mmoja wa favourites wangu hasa eneo la maziwa makuu ambapo nilikuwa nikimsikiliza tangu early 90s.

Aliwakilisha BBC kwa miaka 10 mfululizo, hivyo alikuwa ni mmoja wa experts kwenye eneo hili.
 
Kuna dada mmoja Regina Malekwa sasa Regina Mziwanda alikuwa anaendesha kipindi cha phone ins pale radio Tumaini in early 90s.

Nafikiri sasa yupo BBC.

Alikuwa anafurahisha kwa uhodari wake wa kuongoza zile phones ins za masuala mbalimbali has ya siasa.
 
Ni bonge la mdada love her kwa kweli. Kuna watu na vipaji sio saaa naona watu wanaongea pumba tu wengi wamevamia au tuseme wanalazimisha fani. Wengine wapenfa sifa wanaonga vitu havina ht ladha. Maadili yanashuka viwango.
 
Kulikuwa na watangazaji mahiri kama kina Bujaga Izengo Kadago,Omar Jongo,Ahmed Jongo,Nadhir Mayoka,Rashid Idd Mchata,Edda Sanga,Salah Dumba,Bett Chalamila,Sunday Shomari,Omar Liongo,Abdalah Majura na wengine wengi tu

daah Abdala Majura!!!!
 
asante sana , tafadhali naomba unitumie kale ka wimbo kabla ya kipindi cha michezo kuanza
 
Mi nakumbuka nilikua ndo mtoto so kutumwa mara dukani mara kanunue mkaa mara nenda kwa flan.... Pia wakubwa walikua wananichukua natoka nao ili wapate gia ya kwenda kuonana na wapenzi wao [emoji28] [emoji28] [emoji28] eti mzazi asiwafikirie vibaya mi mdogo Naenda nao hahahaa hahahahahaah
Umenipeleka mbali mdogo wangu. Mimi siku hizo tunatoka Seko, tukifika nyumbani siku za j. pili utapewa escort hiyo halafu mkirudi wanapelekwa chemba, hivi mliona nini? Sisemi zaidi inawezekana mdogo wangu akawa humu akaniumbua. We tulipigwa kwenda disko za mchana na hali ni saa nane mpaka 12. Mkirudi mhahesabiwa jua limetua ziwani au la lakini we acha tu.Huo urithi wanetu wameukoasa. Wacha waukose viboko vya wakati huo we! Walitusaidia maana mtu kusikia kijijini mtu kapata mimba inabidi atoroshwe apelekwe mbali. Sasa hivi maisha ndivyo yalivyo.
 
kuna ule wimbo wa issa matona kamasikosei hongera mwanangu eeh hongera,mida ya saa saba hapo njaa ishanikong'oli kinoma mama alikuwa anakipenda sana hicho kipindi
 
1 Taarifa ya habari na ile ngoma ya yule mzee asiyeona na ngoma kumi
2. Wakati wa kazi. "ujuzi niliupata hapa hapa kazini"
3. Hii ni kwaresimaa.
4. Lala salama.
5. Vipindi vya masomo ya shule za msingi tukikaa darasa zima watoto 40 na kusikiliza mwalimu wa redio. Wengine hata hiyo redio ilikuwa haisikiki vizuri lakini ilikuwa lazima mhu!
6. Kipindi cha wagonjwa. (Ajuaye bwana Mungu kwa mzima kuwa mfu, mgonjwa kuwa salaaaama leo tunatoa pole).
7. Mchezo wa Redio (Mkataa pema pabaya panamwita) Sikosi hapo. watu mnakaa kana kwamba mnawaona akina Jangala na wenzie na yule mwenye sauti kubwa na yule mama aliyekuwa na roho mbaya. Mtu unamchukia mtu hata bila kuona sura yake.
8. Mpiraa. Nakumbuka Yanga ilikuwa inacheza na Simba 74 tulipiga teke redio ya baba mimi na kaka yangu. Tulikula mkong'oto.
9. Hotuba za Mwalimu. Kila wakisema anaongea na wazee wa Dar ujue kuna kitu. Hapo hatutoki kama tupo likizo, wazee wote wa jirani wanakuja kwetu ili wasililize hotuba. Shuleni boarding kulikuwa na redio moja inazunguka kila bweni kila week.
10. Mchana na usiku mwema na miziki yake!! We acha akina Mbaraka Mwinshehe, Juma ******, Marijani Rajab, Western Jazz, Ndala Kasheba, Polisi Jazz, JKT, Tankat Almasi, Taarab nk. Samahani nimeandika mengi lakini ni kama therapy kutoa haya ya sasa kichwani. Big up mtoa mada.
Hivi niliweka matangazo ya vifo? Wote kimya maana ndo simu za vijijini. Sikuwahi ona simu mpaka nilipoenda mjini ofisini nimeenda kwa shughuli zangu za kishule nikiwa darasa la 7. We kuona watu wanaongea unafikiri wanaongea na jini.
 
Mi Nakumbuka ubovu wa radio kipindi kile maana usikivu kama uko mikoani ulikuwa mbovu sana.
 
Kuna tangazo la bia ya "tusker" wanakuambia " baada ya kazi burudika na tuskerrrrrrr" nkamwambia baba niletee hiyo tusker niburudike akacheka sana ila kaniletea Pepsi cola
 
Dah Mengi
Usomaji wa taarifa wa habari ulikuwa wa makini. Sisi tukiwa wadogo tulikuwa tunabashiri wasomaji.
Na hii ndio Taarifa ya Habari isomwayo na ...... David Wakati, SS. Nkamba/ Juma nGondae/ jamani we
Kipindi cha klabu raha leo Shooooooow!
Salamu kwa wagonjwa!
Mchana mwema
Kipindi cha wafanyakazi jamani- Wimbo wa Msondo-n Nidhamu ya kazi ni msingi wa mafanikio.......( mwenye clip hiyo aiweke)
Pwagu na Pwaguzi
Mchezo wa Redio jamani wanaact kama vile unawaona!! Wasanii hao wangekuwepo leo wangepata hela sana!
Teh na Jpili Mama na mwana
Na kale kawimbo kao
 
Dah Mengi
Usomaji wa taarifa wa habari ulikuwa wa makini. Sisi tukiwa wadogo tulikuwa tunabashiri wasomaji.
Na hii ndio Taarifa ya Habari isomwayo na ...... David Wakati, SS. Nkamba/ Juma nGondae/ jamani we
Kipindi cha klabu raha leo Shooooooow!
Salamu kwa wagonjwa!
Mchana mwema
Kipindi cha wafanyakazi jamani- Wimbo wa Msondo-n Nidhamu ya kazi ni msingi wa mafanikio.......( mwenye clip hiyo aiweke)
Pwagu na Pwaguzi
Mchezo wa Redio jamani wanaact kama vile unawaona!! Wasanii hao wangekuwepo leo wangepata hela sana!
 
Back
Top Bottom