Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

KUNA MZEE HAPO KATUTUSI WA DOT COM, Mzee Mzima Busara Hakuna. Mimi Wa 94, Lakini Naweza Kuielezea RTD Nilo Ipenda Na Si TBS Ya Sasa, Namkubali Mze Masood Masood Na Zilipendwa, Napenda Zaidi Hata Sasa Kipindi Cha Kutoka Maktaba Ambacho Waga Kina Rudia Vipindi Vya Zamani. Siku Moja Walirudia Cha CLUB LAHA LEO Cha Mwaka 91, Nikasema Zamani Ilikuwa Raha. Zamani Nilimsikiaga Beni Kiko, Sijui Yu Wapi? Tumboi Lisasi, Halima Mchuka Kifo Chako Kilinipa Shida Saana! Nakumbuka Twende Na Wakati, Namkumbuka Kibuyu. Namkumbuka Bakari Msulwa Nilimfuatilia Mpaka Katika Redio Japan NHK, Anisamehe Maana Niliwaacha Ghafla Kutokana Na Majukumu Ya Hapa Na Pale. Ashedi Chelewa Na Ndelema Bado Wana Tangaza Kipindi Cha Ngoma. Masoooood Mungu Akupe Maisha Marefu, Hazina Yetu Wewe! Nina Mengi Ya Kusema Lakini RIH, RIH,RIH RTD
 
...ewaaa.....right on!!...Ms Eda Sanga...hivi huyu yuko wapi hivi sasa?.......

Kuna wakati alikuwa Tume ya Uchaguzi ya Kiravu, sasa hasikiki tena , labda amekua freelance ? Pengine Pasco aje kutusaidia
 
Kuna wakati alikuwa Tume ya Uchaguzi wakati wa Kuravu, baadaye akawa hasikiki, labda ni freelance sasa, labda Pasco aje kusaidia

Mwaka Jana Nakumbuka Alikuwa Pale Mlimani Akiwa Msimamizi Wa Mlimani Tv Na Redio. Na Mlimani Radio....... Hafikiri Atakuwa Pale
 
Duh mmenikumbusha mbali sana.nilikuwa nakipenda sana tena sana kipindi cha mama na mwana.sikumbuki jina la mtangazaji ebu nikumbusheni wajf.nilikuwa sikosi kipindi .yaani nakosa raha nisipokisikiliza .hivi yupo yule mtanganzaji?? Pia kile kipindi cha zilipendwa kila jumapili nilikipenda sana

Shangazi Debora Mwenda.
 
Mkuu TBC haikuwepo kipindi hicho.
Acha kupotosha...

Mkuu Bramo hajapotosha.
Marehemu Ally Saleh ni cousin wangu.
Alifariki wakitoka kazini na gari ya TBC kwa kugongwa na treni kwenye crossing ya Ilala Shaurimoyo.
Walikuwa watatu:-
Ally Saleh, Kwege Munthali na mwingine jina limenitoka.
 
KBC unanikumbusha kipindi cha Je huu ni uungwana? na Leonard Mambo Mbotela

Kuna mtangazaji mmoja wa KBC Bi Hadijah Ally, nadhani ni kutoka mkoa wa Mombasa. Huyu mama atakuwa mzee kwa sasa, ila ana kiswahili fasaha sana zaidi ya hata ya Watanzania.
 
pascal, hawa nao huwakumbuki? Dastan Tido Mhando, Chama omari Matata, Godfrey Mngodo, Teckla Gumbo, (Salim?- Mume wa Zamzam Maalim),Ahmed Kipozi, Julius Nyaisanga, Sango Kipozi, Abdul Omar Masudi, Mshindo Mkeyenge etc
Nawakumbuka, asante kunikumbusha Mshindo Mkenyenge ndie nilimshau, Masoud na Juliasi niliisha waweka, not sure status ya Thecla maana aliishakuwa mtu mzima sana. Tido, Chama, Mngodo, Kipozi na Sango wapo!.
Pascal
 
...ewaaa.....right on!!...Ms Eda Sanga...hivi huyu yuko wapi hivi sasa?.......
Aliajiriwa mwaka 1968 with the maiden name ya Edda Williams Ngulukulu, alikuja kuolewa na Sanga na kugeuka Edda Sanga, enzi hizi watangazaji wa habari walikuwa ni wanaume tuu, yeye ndio alikuwa mwanamke wa kwanza kutangaza habari RTD miaka ya 80's.

Alistaafu RTD na sasa ni mkurugenzi wa Mlimani Media.
Pasco.
 
Nawakumbuka, asante kunikumbusha Mshindo Mkenyenge ndie nilimshau, Masoud na Juliasi niliisha waweka, not sure status ya Thecla maana aliishakuwa mtu mzima sana. Tido, Chama, Mngodo, Kipozi na Sango wapo!.
Pascal

List imemsahau Radio DJ wa kwanza wa enzi hizo:-
Said Omar Kassongo.

Nakumbuka mitumbuizo yake na story nyiiiingi. Ama kweli wametangulia watu wa ukweli!
 
Hee humu naona sasa wa miaka ile tunaanza kufahamiana, Dot com wakae kimya kabisaa! Enzi hizo RTD ilikuwa na watangazaji bwana, unapata raha hata kuisikiliza redio yako ya Taifa. Siyo sasa hivi yamejaa ma-mburula tu!! Jamani wapi BUJAGA IZENGO KADAGO? CHRISTINA CHOKUNOGELA (Binti alikuwaga na sauti tamu huyo enzi zile, nikatokea kumpenda kupita maelezo, mpaka home wakaniozesha kwake kila wakisikia sauti yake tu wanalipuka mkeo anatangaza!!). Jamani haya mamburula ya TBC hebu yajifunze kwa hawa watangulizi! PASCAL saidia hivi viumbe mkuu!

Ya, mama huyu(kwa sasa ni mama) ni mtangazaji mahiri sauti imetulia, akisoma habari anatulia vituo kwa vituo. Jambo ambalo silipendi ni huu mfumo wa usomaji wa TBC ambapo wameondoa ule wa mwanzo wa kutaja eneo halafu habari yake inafuata na kuadapt ile ya habari kusomwa tu ndani yake ndo unajua tukio hili lilitokea Shinyanga. Zamani ilikuwa hivi
 
Aliajiriwa mwaka 1968 with the maiden name ya Edda Williams Ngulukulu, alikuja kuolewa na Sanga na kugeuka Edda Sanga, enzi hizi watangazaji wa habari walikuwa ni wanaume tuu, yeye ndio alikuwa mwanamke wa kwanza kutangaza habari RTD miaka ya 80's.

Alistaafu RTD na sasa ni mkurugenzi wa Mlimani Media.
Pasco.

Vipi na BALANDINA HIZZA??
Mara ya mwisho nilisikia yuko Tanga, mtu mzima sana.... bado yupo?
 
Ya, mama huyu(kwa sasa ni mama) ni mtangazaji mahiri sauti imetulia, akisoma habari anatulia vituo kwa vituo. Jambo ambalo silipendi ni huu mfumo wa usomaji wa TBC ambapo wameondoa ule wa mwanzo wa kutaja eneo halafu habari yake inafuata na kuadapt ile ya habari kusomwa tu ndani yake ndo unajua tukio hili lilitokea Shinyanga. Zamani ilikuwa hivi

Zamani ilikuwa hivi: Shinyanga, Watu wanne wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa kuchovhea ugomvi.....na maelezo mengine mengi ndani yake yakifafanua habari hiyo. Siku hizi: Watu wanne wanashiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kuchochea ugomvi.........na mengine baadae utaambiwa, tukio hilo limetokea jana Shinyanga..... Sasa hii format siyo nzuri. Lakini jambo ambalo.pia siyo zuri ni kuondoa ngoma zile za mzee Morris wakati wa Taarifa ya habari TBC Taifa, badala yake wameweka Tone ambayo hata siipendi
 
Pascal Mayalla ni jina tuu, lakini wako Pascal Mayalla wengi.
Mimi ni yule Pascal Mayalla aliyekuwa RTD, pia namfahamu Pascal Mayalla fulani alikuwa JWTZ, yupo mwingine alisoma Urusi, kuna mwingine alisoma India, kuna mmoja aliishi US pale Maryland na mpaka leo mke wake yuko kule, kuna Pascal Mayalla aliyekuwa mtangazaji wa Kitimoto, yuko yule aliyekuwa TBC akifanya program za CCM, yuko Pascal Mayalla fulani ni mshauri wa siasa wa ubalozi wa Uingereza nchini, kuna Pascal Mayalla fulani ni mwandishi wa habari wa kujitegemea, kuna Pascal Mayalla fulani alisoma sheria kwa miaka 4 pale UDSM, hadi kuna Pasco wa jf, naye nasikia pia sometimes akichanganywa na Pascal Mayalla, hivyo inategemea huyo unayemfahamu wewe ni yupi!, unaweza ukawa unamfahamu yule Pasco wa jf, ukifikiri ndiye Pascal Mayalla Mtangazaji, kumbe ni watu wawili tofauti!.
Pasco.

Binafsi nilitambulishwa kwako na Anko wangu (John Kayuza) ambaye alikuwa Mwalimu wako pale TSJ, Ilala Shariff Shamba. Kipindi hicho nakumbuka hata Nadhir Mayoka naye alikuwa hapo Chuo. Pasco, maandiko yako "nayakubali"na mchango wako ndani ya JF, ni mkubwa sana na bado unahitajika......

 
Acha uongo kama wewe ukiwa unaisikiliza hii redio 24/7 huwezi kuandika ushuzi kama huo uliouandika...
nidhamu ndo msingi wa TBC.
Na Still kuna watu kama Acheli Shilewa, Masoud Masoud, Aloisia Maneno, Al anisa Shida Masamba na wengine weengi wanafanya vizuri still.
Pia kuna chipukizi kwa mfano Betty Tesha Mwinuka anafanya vizuuri mno kiasi kwamba hutachoka kumsikiliza akiwa anatangaza...
Njoo na uharo sasa...maana huo ushuzi haujabamba
....................Asheri Stanley Chilewa.................
 
Back
Top Bottom