Tujulishane mabasi yanayotuhudumia Tanzania na ubora wa huduma wanazotoa

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Huu ni uzi maalum wa kujulishana ubora wa huduma wa mabasi yanayotuhudumia nchini kwetu Tanzania na nje ya mipaka yake.

1. SCANDINAVIA EXPRESS (Kielelezo/mfano wa kampuni Bora kabisa ya usafirishaji abiria, vifurushu na pesa Tanzania)


Kampuni ya mabasi ya Scandinavia Express ni kampuni pekee ya kitanzania iliyowahi kutokea kwa kuwa na huduma za uhakika na za viwango vya hali ya juu kabisa kulinganisha na huduma zinazotolewa na kampuni za sasa. Kampuni hii ilijijengea jina kubwa na sifa nzuri ndani na nje ya nchi kwa huduma bora walizokuwa wakizitoa kwa abiria wake na pia kuliletea sifa taifa la Tanzania kwa kujulikana kuwa na mabasi ambayo ni quality na high class.

Kampuni ya Scandinavia ilianzishwa zaiidi ya miaka thelathini na tano (35) iliyopita ikiwa na mabasi machache tu aina ya LEYLAND na ilipofika mwaka 1982 kwa mara ya kwanza Scandinavia walinunua basi lao la kwanza la kisasa kutoka kampuni ya SCANIA TANZANIA COACHES aina ya SCANIA ambalo kutokana na ubora wake na uzuri wake kwa kipindi hicho waliamua kulitumia kwa safari yao mpya waliyoianzisha ya Dar es salaam hadi Iringa.


BASI LA KWANZA LA KISASA KUNUNULIWA NA SCANDINAVIA 1982

Kadiri mahitaji ya usafiri yalivyokuwa yakiongezeka ndipo michirizi ya rangi ya BLUU,KIJIVU na NYEKUNDU ikaanza kuonekana katika mabasi mengi zaidi yaliyokuwa yakisafirisha abiria karibia kila kona ya Tanzania.
Ilipofika mwaka 2001 kampuni ya Scandinavia walianzisha safari yao ya kwanza kabisa kutoka nje ya nchi kwa safari ya Dare es salaam hadi Nairobi nchini Kenya,ambapo mafanikio ya ruti hiyo yalipelekea kuzaliwa kwa ruti nyingine kati ya Nairobi hadi Mombasa na Mombasa hadi Dar es salaam. Katika mwaka wa 2002 kampuni ya Scandinavia walipanua wigo wa huduma zao kwa kuanza ruti mpya ndani ya Afrika mashariki kwa safari za Dare es salaam hadi Kampala nchini Uganda.
Ilipofika mwaka 2003 kampuni ya Scandinavia ilipanua wigo zaidi kwa kuanza kwenda katika mji mkuu wa nchi ya Zambia Lusaka.

Wakati huo wote kampuni ya Scandinavia ilikuwa chini ya mkurugenzi na mwanzilishi wake MR.MUHAMED ABDULLAH.


Kampuni ya Scandinavia ilianza kutumia mabasi ya kisasa mwaka 1982 na kuanzia hapo walikuwa wakiongeza mabasi kadili ya mahitaji ya kampuni na abiria pia na kufikia jumla ya mbasi 100 ambayo yalikuwa yakitoa huduma za usafiri ndani na nje ya nchi na mengi ya mabasi hayo yalikuwa ni ya kisasa yaliyonunuliwa kutoka kiwanda cha SCANIA na MARCOPOLO kilichopo nchini BRAZILI.

2. SHABIBY LINE


Hii ni kampuni nyingine yenye fleet za uhakika.
Mabasi mazuri na ya starehe, yakiwa na viti vya kulala, tv, usb, viti vya kusogea na Kuna baadhi ya magari viti vyake ni two by one.
Mabasi haya yanaenda sehemu mbalimbali za nchi, na unaweza kukata ticket zake mtandaoni kwenye website yao
www.shabiby.co.tz

0654 777 773

3. Sauli Luxury Bus

Hii ni kampuni ambayo haina miaka mingi sana ikihudumu kwenye njia ya Dar- Mbeya/ Tunduma/ Kyela.
Tanzania nzima hii gari inajulikana kwa kumwaga Moto iwapo barabarani.
Magari yake ya Scania na Mercedes Benz yamekuwa ni mwiba mchungu sana kwa washindani wake ambao wengi hutumia mijigari ya Kichina.
Waweza kuwapigia simu kwa booking ya Safari yako 0742 967 151

Kilimanjaro Express
Hii ni miongoni mwa kampuni kongwe za usafirishaji nchini. Imekuwa ikihudumia njia ya Dar Moshi Arusha, Dar Mbeya Tunduma etc.
Wana fleet za uhakika na nyingi, huduma nzuri. Waweza kuwasiliana nao kwa namba 0752 400 026

DAR LUX

Hii ni miongoni mwa kampuni zilizoingia sokoni kwa nguvu na kishindo kikubwa wakiwa na jengo zuri sana la kukaa abiria, huduma za kimtandao ikiwa ni pamoja na kukata ticket mtandaoni.
Hii ndio kampuni pekee iliyowahi kuwapeleka madereva wake China ili wakajifunze namna ya kuyamudu mabasi yao.

PHOENIX LUXURY BUS

Hii ni kampuni mpya kabisa ambayo imekuja na mabasi ya Kihindi aina ya BharatBenz ambayo Tanzania hayapo kabisa.
Kampuni hii kwa sasa inatoa huduma zake kwa njia ya Dar Mwanza.


DAR EXPRESS
Hii ni kampuni nyingine kongwe, Mfalme wa njia ya Dar Arusha, Nairobi, Rombo.
Kwa DAR ES SALAAM ofisi zao zinapatikana Shekilango.
 
Hakika scandnavia haijawahi kutokea. wale wa kanda ya ziwa tulizunguka nairobi na kampala
 
Naona mzee unaipromote Shabiby line kwa kutumia medani za juu kabisa za kufanya matangazo. Hiyo Kampuni ya Scandinavia umeitumia kama kiini macho tu.

All in all, Shabiby line kama zilivyo kampuni nyingine makini, nao wanajitahidi kwa kiwango chao.
 
Ungetwambia scandnavia ilipotelea wapi maana hata kusikika hakuna
 
Hizo Basi zote na mipicha yake hakuna hata moja itakayorushusiwa kutembea njia za Tanroad bila kipeperushi Cha abnormal pamoja na bendera nyekundu mbili , mbele na nyuma, ikilazimishwa kumaliza safari saa 12 jioni na kuanza safari saa 12 asubuhi.

Na siyo project ya pesa ndogo
 
Kwanini mkuu...sbb ni nini zisiruhusiwe

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Kwahiyo ndo umemaliza hivyo,
 
Scandinavia ni moja ya gari nilienjoy Sana kusafiri nayo kipindi nasoma.
Ni moja ya gari ulikuwa na huduma nzuri na za kipekee,na waliwajali wateja wait Sana. Najiuliza Sana ni kipi kilisababisha wakapotea kibiashara
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…