Tujulishane mabasi yanayotuhudumia Tanzania na ubora wa huduma wanazotoa

Jamani naulizia kama kuna gari inafanya route mwanza to nairobi tafadhali
Kutokana na korona route hiyo haipo
Ukitaka kusafiri route hiyo panda basi za Zakaria au Batco kutoka mwanza hadi sirari nauli ni 10000 tu, ukifika boder unavuka upande wa kenya isebania pale kuna basi za nairobi kupitia kisiii nauli pale ni kama 1200 ksh, au 240000 tshs
Nb
Hakikisha unafika sirari kabla ya saa nne asubuhi , upande wa kenya hawasafiri tena usiku kwa hiyo basi za nairobi mwisho saa tano asubuhi
Ikitokea umechelewa basi za asubuhi , unaweza kupanda hiace za kericho , pale kuna seven seaters toyota wish , kwenda nairobi hizi ni 1500 kshs kutoka kericho, ilaa itabidi roho uishike mkononi maana jamaa wanatembea 140 km/h plus
 
Ahsante kwa ufafanuzi
 
Scandinavia ni moja ya gari nilienjoy Sana kusafiri nayo kipindi nasoma.
Ni moja ya gari ulikuwa na huduma nzuri na za kipekee,na waliwajali wateja wait Sana. Najiuliza Sana ni kipi kilisababisha wakapotea kibiashara
Nasikia kilichosababisha ni kutokulipa kodi
 

What was the motive behind this?
 
Nasikia kilichosababisha ni kutokulipa kodi
Kuna wanasiasa waliingiza mabasi yao mle kwa kutumia jina la kampuni, nasikia yakawa yanakunywa mafuta kwa jina la Scandinavia bila kulipa, deni likawa kubwa sana baada ya kuona hali ni mbaya wakayachomoa na kuweka majina mangine na kumwachia Scandinavia deni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…