Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Karibu sana. Nipo hapa.Yani wewe nilikutafutaga Sana Kumbe umewekeza huku siku hizi eeh ,.. malkia wa gosheni bado nangoja S3 [emoji23][emoji23]
Karibu sana, mkuu.Aisee, hii kitu kama naangalia series flani vile. Kongore kwako mkuu
Nilibanwa na kazi. Nimefika hatimaye.Daah jamaa ajaweka tu
Kwa kweli aendelee kidgoTivu ila kama umeruka episode hatujaona mitchelle alivyoambiwa kuhusu kifo cha mtoto wake labda nimesahau
Ebu endelea basi
@ Antonnia Bantu Lady Mother ConfessorTUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA -- 32
Na Steve, B.S.M
Taipei, Taiwan, majira ya saa kumi na mbili jioni.
Mitchelle alifuta chozi jicho lake la kushoto akishuhudia jeneza linashuka ardhini, alishindwa kuvumilia, alijikuta anahisi uchungu mkali katika moyo wake punde alipoona mwili unashushwa, aliweza kuhimili muda wote huo lakini si hapa.
Mwanamke huyo alikuwa amevalia gauni jeusi, kofia nyeusi yenye nyavu nyepesi zilizofunika robo ya uso wake, 'gloves' ndefu nyeusi mikononi na viatu vyeusi vyenye visigino virefu, nyuma yake walikuwapo wanaume wawili, wote walivalia suti nyeusi na miwani meusi, mmoja alikuwa ni bwana Taiwan na mwingine ni Yu, nywele zao wamezitengeneza vema, zinang'aa na zimelala kana kwamba zimelambwa na mbwa, wamevalia nyuso za mawe wakiwa wamesimama kama wanasesere, mbali na watu hao alikuwapo bwana mmoja aliyekuwa anahusika na shughuli za mazishi, bwana huyo alikuwa mzee mwenye asili ya Uchina, makamo yake miaka ya hamsini za mwisho ama sitini za mwanzo, alikuwa amevalia shati jeusi yenye chapa ndogo nyeupe mfukoni mwake ikisomeka FAREWELL FUNERAL SERVICES.
Baada ya mazishi kukoma, Taiwan pamoja na mwenzake, Yu, walitoka eneo hilo wakalifuata gari lililowaleta hapa, gari kubwa aina ya Alphard rangi yake nyeusi, gari hilo lilikuwa jipya likiwakawaka, hapo wakajiegamiza wakiwa wanamtazama Mitchelle kwa mbali.
Taiwan alivua miwani yake kubwa uso wake ukabaki uchi, jicho lake la kushoto lilikuwa limevilia damu na ana ngeu mbichi pembeni yake, alijisogeza kidogo apate kuegama vizuri lakini akajikuta anaugulia maumivu makali kiasi cha kubweka kama mbwa, nyonga ilimvuta akaushika mguu kama mtoto mdogo.
"Hak'ya Mungu!" Akaapia akiukunja uso, "Haya maumivu utayalipia, Mitchelle!"
Bwana Yu alimtazama kwa macho ya huruma akimshika bega kumpa pole, mbaya napo alipomshika alikuwa na maumivu pia, akabweka tena.
"Samahani, sikujua. Sasa wapi hapaumi?"
"Kila sehemu panauma."
"Ni kheri unahema, nilihofia unaweza kupoteza uhai wako kwa hasira za mwanamke yule."
"Hata mimi pia nilihofu na hilo, sikutegemea kama ningeliona jua la leo, shukrani ziende kwa yule daktari, pesa nilizomhonga zimeokoa nafsi yangu, laiti angelijua mtoto alikwishafariki muda mwingi ulopita nikawa nakula pesa yake basi leo hii ungekuwa kwenye mazishi yangu."
Alisimama akijikaza, akaupindisha mdomo wake na kusema, "lakini namsikitikia, kuniacha hai ni kosa ambalo atakuja kulijutia siku za usoni," alafu akatabasamu mwenyewe. Bado walikuwa wamesimama wakimtazama Mitchelle kwa mbali, mwanamke huyo alikuwa amesimama kaburini kwa utulivu.
"Kesho ni siku ya kutajirika, kesho ni siku ya neema juu ya neema!" Taiwan alisema kisha akaendelea kutabasamu, kwa muda kidogo aliyasahau maumivu yake pale alipowaza pesa, pesa nono atakazozipata si muda mrefu, hata mate yalimjaa mdomoni.
"Unadhani tutafanikiwa?" Yu akauliza, papohapo Taiwan akamtazama kwa macho ya hasira, akamwambia, "Kama huniamini unaweza ukajitoa hivi sasa, bado muda unao."
Yu akanyamaza, mwenzake akaendelea kumtazama kwa macho ya maulizo, ikambidi aongee, "sawa, nimekuelewa!" Taiwan akaurejesha mgongo wake kwenye gari kisha akamwambia, "Kila kitu kipo tayari, hata asubuhi ya leo nimetoka kuwasiliana na wale jamaa nao wako tayari, sasa wewe jukumu lako ni moja tu, kazi yako ni moja na nyepesi ..."
"Ipi hiyo?" Yu akauliza kwa hamu, Taiwan akamshika mkono, "tulia, haina haraka."
Baada ya kuhiji vyakutosha, Mitchelle aliungana na wakina Taiwan tayari kwaajili ya kuondoka. Yu alishika usukani, nyuma ya gari wakiketi Taiwan na Mitchelle, gari ilikuwa kimya sana kiasi kwamba ungeisikia namna AC inavyopuliza, hakuna aliyemwongelesha mwenzake, Mitchelle alikuwa yu mbali kimawazo ingali hawa wengine walikuwa wanaigiza kana kwamba hamna mtu hapa karibu, walitazama mbele kwa nyuso za malaika asokuwa na kosa.
Baada ya muda mfupi, wakawa wamefikia kwenye nyumba fulani iliyojitenga, ukubwa wake ghorofa mbili, imepakana na bahari kwa ukaribu sana, mwonekano wake ni maridadi sana, humo gari likazama chini mpaka eneo maalum la kujiegesha, hapo wakashuka na kuendea mlango wakaingia kisha wakaelekea upande wa kushoto, huko kulikuwapo na mlango uliofanania na wa lifti, pembeni yake palikuwapo na kifaa chenye tarakimu kadhaa.
Mitchelle alibonyeza baadhi ya tarakimu na mara mlango ukafunguka, wakazama ndani. Walinyooka na korido wakapishana na milango miwili, mlango wa tatu ndo' wakaingia, humo palikuwa mithili ya maabara ama hospitali ndogo, walikutana na bwana mmoja aliyevalia koti jeupe, mzee aliyekula chumvi, kichwa chake cheupe na kibaraza chake kinang'aa.
Alimsalimia Mitchelle kwa adabu kubwa alafu akampatia muhtasari wa leo wa afya ya mhusika wake.
"Maendeleo ni mazuri, hali yake si haba, leo hii mapigo yake ya moyo yametengemaa."
Waliongozana na Mitchelle kufuata pazia kubwa la kijani, wakalisogeza na kutazamana na mwili uliolala kitandani. Mwili huo ulikuwa umejazwa mabomba sehemu kadha wa kadha, ulifunikwa sehemu za siri huku kwengine kukiwa wazi, kichwa cha mwili huu kilikuwa cheupe pe, mabega yake mapana, kifua chake kipana, uso wake unafanania na wa Mitchelle lakini umekomaa kiume kwa kushupaza fuvu za mashavu.
Mwili huo ulikuwa umetulia tuli, kama isingekuwa kupanuka na kusinyaa kwa kifua kwasababu ya kuhema basi tungedhani amekwishakufa, mashine ya kunakili mienendo ya mapigo ya moyo ilikuwa inaita kwa milio yake, kwasababu ya ukimya wa hapa mashine hiyo ikawa inasikika vema.
Mitchelle aliutazama mwili ule kwa macho ya kujali, akaushika kwa mikono yake mpaka pale aliporidhika, akajikuta anadondosha chozi, hakukaa hapo muda mrefu akaongozana na daktari kwenda nje ya kijichumba hiki, wakapata kuteta baadhi ya mambo.
"Zile kazi zote ulizon'tumia nimezipata, taratibu naziingiza kwenye mfumo wa bwana huyu, nadhani zitakapokamilika ataweza kunyanyuka kitandani na kuwa mtu kamili ... Hata kama sio kamili lakini atakuwa sasa binadamu mbele ya macho ya watu," daktari alijipambanua, Mitchelle akatikisa kichwa kumwitikia kisha akamuuliza, "mpaka sasa mradi huo umefikia asilimia ngapi kukamilika?"
"Asilimia arobaini," daktari akajibu na kuongeza, "nadhani unafahamu, huyu mwanao ni hybrid, mfumo wake wa mwili si sawa na wewe, pia si sawa na mimi, yu katikati, namna mwili wake unavyojijenga ni taratibu sana lakini punde utakapokomaa basi yawezekana ukawa bora zaidi kuliko mimi na wewe."
"Na kwanini ni wa baridi sana?" Mitchelle akauliza, "nimemshika nikahisi baridi la ajabu. Huwa anakuwa hivyo?"
"Ndio," Daktari akajibu, "mwili wake ni wa baridi, lakini leo alikuwa wa baridi zaidi sababu alitoka kwenye jokofu si muda mrefu, nilibaini kufanya hivyo humsaidia kwenye 'recovery' ya upesi ya misuli na tishu zake za mwili."
"Kuna chochote unahitaji, Dr. Gates?" Mitchelle alisimama akauliza, hapa Dokta akatabasamu kwa mbali kisha akasema, "Ninachohitaji zaidi ni nyaraka toka kwenye chanzo, zile nyaraka hunisaidia zaidi kufanya kazi yangu, kama isingalikuwa kukawia kwa nyaraka hizo basi ningeweza kuokoa hata uhai wa Kiellin. Hayo mengine nashukuru maana natimiziwa ndani ya wakati."
Mitchelle akamuahidi Dr. Gates kwamba mradi wake utakapokamilika kama vile alivyopanga basi atamlipa kiasi kikubwa sana cha pesa kiasi kwamba hata akiacha kazi hatokuwa masikini kamwe, yeye mpaka uzao wake wa tatu, dokta akashukuru sana kisha wakaagana.
Mitchelle alienda sehemu ya kupumzika, hoteli kubwa yenye hadhi ya nyota tano, huko akajiandikisha kwa kutumia kitambulisho bandia, kitambulisho kilekile akitumiacho sehemu zingine, akajipatia chumba kikubwa chenye kila kitu anachokihitaji mtu mwenye pesa zake, hapo akatulia tuli, aliona hapa ni patulivu zaidi ya kule kwenye jengo lake kubwa, alitaka kuwa mwenyewe apate kuyapanga mambo yake kwa ufasaha, mambo ya pesa kubwa.
Akiwa ametulia katika kitanda kikubwa chenye hadhi iliyojitosheleza, mara simu yake ikaita, kutazama ni namba tupu pasipo na jina, alipoikagua namba hiyo vema akaigundua ni ya nani, akaipokea akisema, "Fenty."
Mtu wa upande wa pili akampokea kwa kumpatia taarifa,
"Hakuna taarifa ya siri tena."
"Unamaanisha nini?" Mitchelle akauliza upesi, bwana yule kwenye simu akamwambia aingie kwenye 'inbox' ya email yake, ataelewa anachomwambia, upesi Mitchelle akaingia kwenye inbox yake na huko akakutana na 'links' mbili alizozibofya zikampeleka moja kwa moja kwenye 'audio' fulani ya kuskiliza, audio hiyo ikampa sauti ya yale yaliyokuwa yanaendelea ndani ya makazi ya Hilda, Richie pamoja na Jamal, lakini hakuskiza sana, aliyaacha mambo haya ili apate kufanya kusudi lililomleta hapa, atakapolimaliza hilo, basi yatafuatia mengine.
Akiwa anayafanya hayo, akaona ni vema aendelee kujiburudisha na kahawa aipendayo, muda huu hakutaka kubaki nyuma, alimwambia Jennifer amwandalie kahawa hiyo ili aendelee kuinywa atakapokuwapo safarini.
Alijimiminia unga wa kahawa kwenye kikombe kisha akajichanganyia na maji moto na sukari kwa mbali, akanywa fundo moja, akahisi mwili mwake umetetemeka kwa raha, hakika alihisi unafuu mkubwa, hamu tamu isiyoelezeka, sasa akaamini yuko tayari kwa kazi.
*****
Taipei, Taiwan, majira ya asubuhi ya saa mbili, masaa kumi na mbili kabla ya mnada mkubwa kufanyika.
Bwana Yu alikuwa pembezoni mwa jiji la Taipei akiwa ameegamia gari dogo jeusi kandokando ya barabara ndogo, hapo alikuwa anangoja jambo.
Bwana huyo alikuwa amevalia jeans nyembamba na buti kubwa la ngozi, usoni amevalia miwani kubwa ya jua mdomoni akitafuna 'bubblegum', mikono ameeka mfukoni akitazama huku na kule barabarani.
Kidogo akaliona gari fulani likiwa linakuja kwa mbali, rangi yake ya maziwa, modeli yake ni van, linakuja kwa kasi kufuata uelekeo wake, si punde gari hilo likasimama kwa upande wa pili, Bwana Yu akavuka barabara kulifuata gari hilo, Yu akazama ndani humo akawakuta watu watatu walioketi.
Watu hao walikuwa wamevalia nguo nyeusi, wote wamebana nywele zao nyuma, na kama ukiwatazama kwa harakaharaka utawaona wamefanana nyuso, tofauti zilikuwa za mbali sana kama vile sharubu changa ama upana na wembamba wa nyuso.
Baada ya Yu kuingia ndani ya gari hilo, mlango ukafungwa na mazungumzo yakaanza, hayakuwa marefu, la hasha, yalikuwa ni namna gani ya kuwezesha utekaji wa gari litakalobeba mzigo wa thamani ya mabilioni kabla ya kufika katika uwanja wa mnada, kazi ya Bwana Yu ikawa ni kusema ruti zote zitakazotumika kupitishia gari hilo, na baada ya kusema sasa kazi ikaachwa kwa genge hilo nao kusema juu ya mipango yao, kazi ilipokwisha, ndani ya dakika sita tu za maongezi, Bwana Yu akashuka toka kwenye gari akiwa na kila kitu kichwani kwake.
Alipofika kwenye gari akampigia simu Taiwan na kumweleza yaliyojiri, kisha akamalizia kwa kusema,
"Nadhani kazi yangu imeshakwisha."
"Hapana, Yu," Taiwan akamkatiza, "kazi yako itaisha usiku wa leo hii, uwe tajiri ama uwe maiti."
***
Thank you leadermoe naona chimbo jipya. Nakaribia Antonnia unaitwa huku dear.@Antonnia, Bantu Lady Mother Confessor
Hiyo episode ameruka. SteveMollelTivu ila kama umeruka episode hatujaona mitchelle alivyoambiwa kuhusu kifo cha mtoto wake labda nimesahau
Ebu endelea basi
Shukrani kipenzi Ngoja nitulie nisome!
Asante dearrr ngoja nitulie nianze kuisoma vizuri!!@ Antonnia Bantu Lady Mother Confessor
Iko moto sanaAsante dearrr ngoja nitulie nianze kuisoma vizuri!!
Ebu ngoja akujeHiyo episode ameruka. SteveMollel
Weee kumbe??? Nilikua naiona tu naipita naanza kuifatilia rasmi wabheja sanaa!!Iko moto sana
Wabheja korumba mayoWeee kumbe??? Nilikua naiona tu naipita naanza kuifatilia rasmi wabheja sanaa!!