Tukifanya Hivi, Kina Mwamposa na Manabii kuwa Walipa Kodi Wakubwa

Tukifanya Hivi, Kina Mwamposa na Manabii kuwa Walipa Kodi Wakubwa

Binafsi sioni sababu yakufungia hao wanaojiita mitume na manabii.

Acha wale pesa za wajinga.

Kenge anasikia mpaka masikio yatoe damu.

Watu wataacha kutoa pesa hovyo kwa manabii fake pale tu watakapoachana na akili za kushikiwa.

Tofauti na hapo namshauri Mwamposa aendelee kupiga pesa.
 
Unaweza kulifanyia hesabu kanisa katoliki kila senti ukajua inakwenda wapi na inatumika vipi tofauti na hao kina Mwaposya na wa aina hiyo.

Ipo nidhamu ya uendeshaji wa kanisa katoliki ambayo haipo katika makanisa hayo mengine.
Wakatoliki pesa zinajulikana zinaenda wapi na zinafanya nini!
Matokeo na tunayaona,ila hawa matapeli wakina mwaposa na wengineo pesa zao wanafanyia mambo yao binafsi tu kama kujenga majumba yao kuishi na mahoteli na kununua magari ya kifahari

Ova
 
Wakatoliki pesa zinajulikana zinaenda wapi na zinafanya nini!
Matokeo na tunayaona,ila hawa matapeli wakina mwaposa na wengineo pesa zao wanafanyia mambo yao binafsi tu kama kujenga majumba yao kuishi na mahoteli na kununua magari ya kifahari

Ova
Acha Ujinga wew hizo pesa unazosema unazijua za wakatoliki zinavyo tumika pia kwa wengine wanaona ni utapeli tuu. Jali Imani yako usidhihaki Imani za wengine. Ajidhaniae amesimama na aangalie asije akaanguka.
 
Kodi inatozwa kwenye mapato ya:
1. Business
3. Employment
3. Investment

Sasa tukija kwenye tafsiri business income as per Income Tax Act (ITA) unakuta akina mwamposa and co, wako nje ya wigo wa hiyo tafsiri ( out of scope)

Kodi haitozwi kwa hisia...Kodi inatozwa kwa sheria ambazo ziko challenged mpaka kwenye court of appeals kama kuna mzozo.

Sasa wakati wa utunzi na utafsiri wa sheria ya Kodi words must strictly construed and clearly stated.nje ya hapo hiyo sheria haitafanya kazi.

SASA NIAMBIENI MODALITIES YA HIYO SHERIA ITAKAAJE KIASI KWAMBA ITAMKAMATA MWAMPOSA IACHE SADAKA ZA KAWAIDA KANISANI na Msikitini

Hujui kitu wewe, hakuna mahali kwenye income tax act wamesamehe biashara zinazoendeshwa makanisani. Soma second schedule. Ni sadaka tu ndizo zimesamehewa kutozwa kodi.
Mauzo ya maji na mafuta is pure business which generates taxable income. Due to its magnitude,VAT, excise duty and income tax should be charged retrospectively.
This is happening in Tanzania because of slumberous TRA.
Katika Hali ya kawaida tunategemea sadaka inunue maji na mafuta na vigawiwe bure; if there is any consideration, then, such consideration is deemed taxable
 
Wew una uhakika kuwa kiwanda hicho hakilipi Kodi au nabwabwaja tuu maneno?
Hapa hakiongelewi kiwanda kinacho jadiliwa ni Yale maji yakisha fika kanisani baada ya kuwa yamesha lipiwa Kodi kiwandani ndipo watu wanataka waumini wakiyachukua Kodi ilipwe tena.
Ni sawa na wew muumini umeamua kupeleka vitu vyako kanisani ili vinadiwe kwajili ya kusaidia huduma halafu anatokea kibwetele fulani anataka ulipe Kodi baaada ya mnada.
Uko sahihi

Mikungu ya mavuno na vinavyonadiwa siiu za mavuno zinatakiwa kulipiwa kodi kama lengo lao ni kukomalia Mwamposya

Makanisa mengi huuza vitu kwa bei tishio siku za mavuno huvuna mamilioni hizo za Mwamposya nu ndogo

Unakuta mbuzi mmoja siku ya mavuno ananunuliwa miiioni tano

TRA waende huko pia kama ni hivyo
 
Wakatoliki pesa zinajulikana zinaenda wapi na zinafanya nini!
Tueleze huwa pesa za katoliki zinaenda wapi kufanya nini sababu shule zao hata wakatoliki.wa kawaida hawawezi kupeleka watoto huko kusoma

Hospitali zao bei mbaya

Tueleze wewe wakipata hizo pesa huwa wanapeleka wapi kusaidia nani wa kipato kipi cha juu au cha chini?
 
Hujui kitu wewe, hakuna mahali kwenye income tax act wamesamehe biashara zinazoendeshwa makanisani. Soma second schedule. Ni sadaka tu ndizo zimesamehewa kutozwa kodi.
Mauzo ya maji na mafuta is pure business which generates taxable income. Due to its magnitude,VAT, excise duty and income tax should be charged retrospectively.
This is happening in Tanzania because of slumberous TRA.
Ukisoma huelewi, biashara yeyote lazma ikidhi tafsiri ya biashara kwa mujibu wa ITA.
Wewe ndiye unayeiita biashara kile kinachofanywa na mwamposa , ila haijakidhi matakwa ya ITA as per business definition.

Sasa biashara za kanisa zozote zinacharjiwa Kodi, mfano mashule, frem za biashara
Ila sio sadaka, michango ya kuchangia huduma kama kwenye jumuiya na mwamposa.
 
Kwa Kanisa Katoliki,je yule ambae hajatoa kabisa atanyimwa komunio? Na kwa Mwamposa yule ambae hajatoa hiyo 5,000 atapewa maji hata kama anayahitaji?
Mkuu kwani ni lazima kila dhehebu lifuate sheria za Wakatoliki?
 
Ukisoma huelewi, biashara yeyote lazma ikidhi tafsiri ya biashara kwa mujibu wa ITA.
Wewe ndiye unayeiita biashara kile kinachofanywa na mwamposa , ila haijakidhi matakwa ya ITA as per business definition.

Sasa biashara za kanisa zozote zinacharjiwa Kodi, mfano mashule, frem za biashara
Ila sio sadaka, michango ya kuchangia huduma kama kwenye jumuiya na mwamposa.

Rudia kusoma ulichokiandika, edit ili ueleweke.
Sijaelewa kitu.
 
Ukisoma huelewi, biashara yeyote lazma ikidhi tafsiri ya biashara kwa mujibu wa ITA.
Wewe ndiye unayeiita biashara kile kinachofanywa na mwamposa , ila haijakidhi matakwa ya ITA as per business definition.

Sasa biashara za kanisa zozote zinacharjiwa Kodi, mfano mashule, frem za biashara
Ila sio sadaka, michango ya kuchangia huduma kama kwenye jumuiya na mwamposa.

Ukisoma na kukaririshwa ITA bila kuelewa au kupata tafsri sahihi, you will end up arguing like you do
 
MWAMPOSA ANAUZA MAJI MENGI SANA ZAIDI YA KIWANDA CHA MAJI LAKINI HALIPI KODI VIVYO HIVYO NA MAFUTA
Mi nawashangaa sn, hivi maji ni yake? Maana ni ya kampuni yyt Ile,na yanauzwa bei ileile ambayo tunanunua kwenye hayo makampuni,ss hapo kauza vipi? Maana anachofanya ni kuchukua kule kuyaombea na watu wanachukua Kwa bei ileile!
Au unaenda na maji yako yanaombewa!
Angekuwa na kiwanda hapo kwelii
 
Mi nawashangaa sn, hivi maji ni yake? Maana ni ya kampuni yyt Ile,na yanauzwa bei ileile ambayo tunanunua kwenye hayo makampuni,ss hapo kauza vipi? Maana anachofanya ni kuchukuakule kuyaomvea na watu wanamchukua Kwa bei ileile!
Au unaenda na maji yako yanaomvewa!
Angekuwa na kuwanda hapo kwelii

Kama maji ni ya kampuni nyingine na yanauza bei ile ile hapo ni case nyingine
 
Kenya wametupita mbali sana kielimu. Wana maono kuliko sisi, angalia walivyopasua vichwa mpaka KANU ikaanguka.
 
Uko sahihi

Mikungu ya mavuno na vinavyonadiwa siiu za mavuno zinatakiwa kulipiwa kodi kama lengo lao ni kukomalia Mwamposya

Makanisa mengi huuza vitu kwa bei tishio siku za mavuno huvuna mamilioni hizo za Mwamposya nu ndogo

Unakuta mbuzi mmoja siku ya mavuno ananunuliwa miiioni tano

TRA waende huko pia kama ni hivyo
Wacheni kupotosha ili kumlinda huyo jamaa yenu.

Makanisa hufanya harambee kwa kuuza vitu kwa lengo la kupata pesa zitakazotumika kwa shughuli fulani hapo kanisani, kama ujenzi, ukarabati wa jengo, hakuna harambee inayofanywa bila sababu.

Kwa mantiki hiyo, sasa hebu tuambie, Mwamposa akiuza maji na mafuta, hizo pesa huwa anazipeleka wapi?na kufanyia kitu gani?
 
Sacraments ni tofauti na huo utapeli wa wachungaji feki, huuziwi sacrament kanisani unainunua kwa kutoa sadaka mbalimbali. Mapadre wanaishi kwa sadaka zetu za kila misa.

Padre akitaka kununua laptop au kifaa chochote anayo haki ya kuwaambia waumini na wakamnunulia ndio maisha ya useja hayo.

Tofauti na haya makanisa yanayotumia ujinga na ufukara wa waumini katika kutajirisha wachache.

Ni kanisa katoliki lina nidhamu ya uendeshaji na usimamiaji wa kila kinachofanyika huwezi kulinganisha na hayo makanisa ambayo ni mali za watu binafsi.
Rozali,misalaba,mvinyo vinagawiwa bure?
 
YEHODAYA hebu ngoja kidogo, viwanda vya maji vinalipa kodi kama kawaida na yeye ananunua huko.
Lakini kifuatacho naye anauza nasikia yale maji ya elfu moja anauza elfu 5 mpaka 10. That's where tunasema faida hiyo iwe taxed.
Tupo pamoja mkuu? Hata maduka yetu ya mtaani faida yao ya kuuza maji inatozwa kodi.
Achana na habari za kusikia mkuu,Fanya utafiti upate ukweli maji pale yanauzwa shs 1000 tu,zingine ni stori zisizo na ukweli
 
Nashindwa kuelewa kwanini TRA wanashindwa kuiga kwa Ruto wa Kenya na kuongeza mapato kutoka katika wimbi hili la mitume na manabii walioanzisha biashara ya Maji, chumvi, vitambaa nk wakiviita vya upako na kupata fedha nyingi sana kama biashara isiyo kodi wala cost of production. Msome Rais Ruto alivyoamua.

"Nimeongea na watendaji wa serikali yangu kuhusu baadhi ya wahubiri kucheza na imani za wakenya. Kuanzia sasa yule anataka kuuza maji asajiliwe na mamlaka ya maji, yule anataka kuuza mafuta asajiliwe na food and drugs authority, na yule anataka kuuza mbegu asajiliwe wizara ya kilimo. Watambulike kama wafanyabiashara, na serikali ijue wanauza ngapi kwa siku na walipe kodi. Huku kwa kanisa wabaki wanaoeneza neno la Mungu, sio wafanyabiashara. Hatuwezi kuruhusu imani za wakenya kuchezewa na wakora wachache, wanaotaka kujitajirisha kupitia shida za waumini wetu" William Samoei Ruto, Rais wa Kenya.
Naunga mkono hoja
P
 
Back
Top Bottom