Tukio gani kwenye soka huwezi kulisahau?

Tukio gani kwenye soka huwezi kulisahau?

Timu zote zina point 86, huku City akiwa na tofauti ya Mabao 63 Man United akiwa na GD ya 55.

City akikipiga na QPR, Man United akigongana na Sunderland.

United alimaliza kwa ushindi wa goli moja, bao la Waza hivyo kufanya kuwa na point 89. City kang'ang'aniwa na QPR, mpaka dakika ya 90, City 1-2 QPR.

Kumbuka hii mechi ni muhimu kwa timu zote mbili. City anapaswa kushinda ili achukue ubingwa na QPR ashinde ili asishuke Daraja.

Sisi Mashabiki wa Manchester United, tupo tunashangalia kombe letu. Mechi imeshaisha tayari.

Zikaongezwa dakika 5 kufidia dakika zilizopotea. Asalaleeeh, dakika ya 92, Dzeko anasawazisha ubao. Sasa ni 2-2.

Bado matumaini kwetu ni makubwa mno. Droo hiyo isingesaidia. Ubingwa ni wetu sisi.

Dakika ya 93, La haula!. Aguero anafunga goli na kufanya kuwa 3-2.

Nilihuzunika mno. Hakika nilipata huzuni iliyo kuu. Mpaka na leo sitosahau. City anatawazwa kuwa bingwa kwa mara ya kwanza.

Hata hivyo QPR aliponea kushuka baada ya Bolton kutoka sare.

Mungu naomba hili jambo lifutike kwenye kumbukumbu zangu.
Goli la aguero if I'm not mistaken
 
IMG_7918.jpg


IMG_7917.jpg
 
Hilo la Muani hata yeye mwenyewe kichwani mwake haliwezi kufutika.Pia matukio kama haya hayafutiki kichwani mwangu (1) Gatuso kumkaba Ronaldo, hiyo ilikuwa AC Milan Vs Man utd
(2) Suarez kudaka mpira uliokuwa unaelekea kuwa goli, Uruguay Vs Ghana (3) World cup 2010 German Vs England Lampard anasawazisha lakini refa anakataa goli.Nadhani hiyo ndio iliwafanya waingereza wagundue goal line technology maana mpira aliopiga Lampard ulivuka mstari WA goal na kurudi ndani.
Gattuso akavua bukta yake mara baada ya dakika 90.
 
Timu zote zina point 86, huku City akiwa na tofauti ya Mabao 63 Man United akiwa na GD ya 55.

City akikipiga na QPR, Man United akigongana na Sunderland.

United alimaliza kwa ushindi wa goli moja, bao la Waza hivyo kufanya kuwa na point 89. City kang'ang'aniwa na QPR, mpaka dakika ya 90, City 1-2 QPR.

Kumbuka hii mechi ni muhimu kwa timu zote mbili. City anapaswa kushinda ili achukue ubingwa na QPR ashinde ili asishuke Daraja.

Sisi Mashabiki wa Manchester United, tupo tunashangalia kombe letu. Mechi imeshaisha tayari.

Zikaongezwa dakika 5 kufidia dakika zilizopotea. Asalaleeeh, dakika ya 92, Dzeko anasawazisha ubao. Sasa ni 2-2.

Bado matumaini kwetu ni makubwa mno. Droo hiyo isingesaidia. Ubingwa ni wetu sisi.

Dakika ya 93, La haula!. Aguero anafunga goli na kufanya kuwa 3-2.

Nilihuzunika mno. Hakika nilipata huzuni iliyo kuu. Mpaka na leo sitosahau. City anatawazwa kuwa bingwa kwa mara ya kwanza.

Hata hivyo QPR aliponea kushuka baada ya Bolton kutoka sare.

Mungu naomba hili jambo lifutike kwenye kumbukumbu zangu.
Kila nikisikia Agueroooooooooooooooooooooooooooooopp


Nasikitika sana
 
Ni mchezo wa Fainali ya kombe la dunia, takribani watu bilioni 1 duniani wanafatilia mtanange huo.

Dakika ya 3 ya nyongeza ndani ya dakika 120, ubao ukiwa unasomeka 3-3 kwa Ufaransa na Argentina.

Ndani ya dakika 3 za nyongeza, zikiwa zimebaki sekunde 16 mtanange uishe ili waende penati, huku Leo Messi akijaribu bahati yake ya mwisho ya kutwaa kombe la dunia, ghafla mpira mrefu wa kushtukiza unapigwa kuelekea lango la Argentina.

Kolo Muani, mshambuliaji wa Ufaransa anaupokea mpira ule huku akiwa amebaki yeye na kipa Emiliano Martinez na akijua kabisa akifanikiwa kuweka mpira ule nyavuni anaipa nchi yake goli la 4 na pengine la ushindi.

Kolo Muani anaucha ule mpira unadunda kisha akipiga shuti kati ambalo kipa Martinez anafanikiwa kuzuia na mguu wake na kuinyima Ufaransa nafasi ya ushindi.

Sekunde chache baadae refa anamaliza mpira. Wanaenda mikwaju ya penati na Argentina wanaenda kutwaa ndoo ya dunia mara baada ya kufanya hivyo mara ya mwisho pale Mexico mwaka 1986.

Hili tukio siwezi kulisahau maana lilibadilisha muelekeo mzima wa mechi, na tukio hili linatajwa kama moja ya save bora kuwahi kufanywa na kipa katika historia ya mashindano ya kombe la dunia.

Wewe ni tukio lipi huwezi kulisahau?

View attachment 2633541
Huyo mjinga ule mpira angempa Mbappe historia isingekuwa hivi ilivyo leo
 
Timu zote zina point 86, huku City akiwa na tofauti ya Mabao 63 Man United akiwa na GD ya 55.

City akikipiga na QPR, Man United akigongana na Sunderland.

United alimaliza kwa ushindi wa goli moja, bao la Waza hivyo kufanya kuwa na point 89. City kang'ang'aniwa na QPR, mpaka dakika ya 90, City 1-2 QPR.

Kumbuka hii mechi ni muhimu kwa timu zote mbili. City anapaswa kushinda ili achukue ubingwa na QPR ashinde ili asishuke Daraja.

Sisi Mashabiki wa Manchester United, tupo tunashangalia kombe letu. Mechi imeshaisha tayari.

Zikaongezwa dakika 5 kufidia dakika zilizopotea. Asalaleeeh, dakika ya 92, Dzeko anasawazisha ubao. Sasa ni 2-2.

Bado matumaini kwetu ni makubwa mno. Droo hiyo isingesaidia. Ubingwa ni wetu sisi.

Dakika ya 93, La haula!. Aguero anafunga goli na kufanya kuwa 3-2.

Nilihuzunika mno. Hakika nilipata huzuni iliyo kuu. Mpaka na leo sitosahau. City anatawazwa kuwa bingwa kwa mara ya kwanza.

Hata hivyo QPR aliponea kushuka baada ya Bolton kutoka sare.

Mungu naomba hili jambo lifutike kwenye kumbukumbu zangu.
Nilikuwa mwanza hii, kama mshabiki wa Man Utd iliniuma pia!!

Mbaya zaidi mashabiki wa City wakawa wanajisifu kuwa wameshinda ubingwa katika fergie time🤔

Ferguson nae akaanza kuwaita "the noise neighbours"
 
Nilikuwa mwanza hii, kama mshabiki wa Man Utd iliniuma pia!!

Mbaya zaidi mashabiki wa City wakawa wanajisifu kuwa wameshinda ubingwa katika fergie time🤔

Ferguson nae akaanza kuwaita "the noise neighbours"
Miye nilikuwa Kagera,na ndiyo hapo uhamiaji wa kimakundi wa Mashariki wa Arsenal kwenda Mancity ulipoanza Kwa kasi
 
Mechi ya madrid na barcelona santiago benabeu....aise dinho alipiga mpira hatari siku hiyo balaa tupu mpaka mashabiki wa madrid wakampigia makofi. Jamaa alikuwa nyoko.

Fa cup semi finl arsenal vs man utd ryan giggs anawachambua mabeki wa arsenal hatari mno.

Mnchester vs real madrid hatari redondo anapiga backheel matata anampita sijui alikuwa henningburg u huku delima anapiga magoli tuu. Beckhama nae akakiwasha.

Trezequet anafunga golden goal dhidi ya toldo fina ya uero 2000. Hatari.

Aisee mpira bwana bonge la burudani.
 
Back
Top Bottom