Tukio gani kwenye soka huwezi kulisahau?

Tukio gani kwenye soka huwezi kulisahau?

Hii kwangu ndio the best nakumbuka hadi matukio yaliyofanyika banda umiza siku hiyo

Pia kulikuwa na dogo muokota mipira aliyemsaidia Alexander Arnold kuonesha pasi aitupie kwa Origi.

Huyu dogo nimeingia kucheki jina lake nimekuta na taarifa zake ambazo sikuzijua.

View attachment 2633805

Dogo anaitwa Oakley Cannonier kumbe alipewa hadi na mkataba kusainiwa na Club kwa kitendo kile cha kuisaidia timu.
Yeah dogo yupo pale Liverpool u21
 
Mambo Gani hayo ya kukumbushana machungu
Kama kumbukumbu zangu hazijapotea...

Alianza balloteli x2,
Beki wenu jonny evans alikula umeme,
Akaja aguero x2,akafuata DZEKO,akamaliza silva..

halafu refa alikua mark clattenburg,mlikua old trafford..
babu fergie na msaidizi wake mike phelan,walimaliza mabox ya BIG G
 
Kuna match ujerumani na Italy World Cup 2006......kocha wa ujerumani alikuwa anaandika wapiga penalties dk ya 118 asee nilichokiona kilikuwa ni ukatili wa kibinadamu asee match ilikuwa 0-0
Nimeenda toilet narudi dah nakuta Italy 2-0Germany


Kocha akatafuta kikaratasi🤣🤣
 
Sitaisahau fainali ya Uefa second leg round of 16...Kati ya Barcelona na Psg pale Le parc Des Princes......ufaransa,

1st leg Barca akifa 4-0 Camp Nou!...2016-2017

Aisee ile Comeback ya Barca chini ya mwamvuli wa MSN pale France 6-1... Na kupita Kwa aggregate ya 6-5.....

Ni Moja ya game yangu bora kabisa ya Uefa kupata kuishuhudia.... Unbelievable!

Hadi ikapewa jina la kispaniola/french....." la remontada" means " (The Comeback)".... Aisee....

Ulipigwa mpira mwingi mnoooo!.... Pira biriani....pira ugali... Pira ukoko.....nomaaa!
 
Mlitukota siku ile, Super Mario alitoka kuunguza sehemu ya nyumba yake akaja akatuweka goli na ushangiliaji wa aina yake
Na usiku huo anaalikwa dinner na roberto mancini anaporudi kwake akapitia club akakutana na kimwana funny neguesha...
Balaa,mikosi,nuksi vilianza kumwandama super mario tangu alivyokutana na jini lile
 
Heshima kwako mkongwe mwezangu.

Fernando Redondo alimpiga tobo Henning Berg afu akaenda kutoa assist safi kwa Raul. Redondo alikuwa fundi kweli na mguu wake wa dhahabu bahati mbaya majeraha yakaharibu kipaji chake!


Hiyo ya Ufaransa kutwaa taji la Euro 2000 kuna mechi kadhaa za kukumbukwa. Nakumbuka robo fainali walikutana Ufaransa na Ureno nadhani, dakika za lala salama Ufaransa wakapata penati, Zizou akawa anaenda kupiga, Luis Figo akavua jezi na kutoka nje kabla hata Zidane hajaweka mpira kambani na akafunga kweli mechi ikaisha kwa goli la dhahabu.

Figo alivyokuja kuulizwa baadae akasema hakutarajia Zidane kama angekosa hivyo akaona atoke zake mapema😂😂

Wachambuzi wengi wa soka, wanadai michuano ya Uefa Euro 2000 iliyofanyika Ubelgiji na Uholanzi kwa pamoja ni moja kati ya michuano bora kabisa kuwahi kufanyika🫡🫡
Hatari sana
 
Man city 3-2 QPR: 2012, aguerooooooooo

Man city 3-2 Aston villa ;2022
6 minutes of rescue from super Gundo & Rodri.
 
Fainal kati ya Simba na Stella 1993, nilikuwa safarini kwenye Bus walikuwa wakitangaza huo mpira Sasa nipo na yangu nikasikia gooooal shangwe zikarindima uwanjani, Bus zima wako kimya Mimi na kikofia changu Cha Simba nikaruka juu nikshangilia mara nasikia "Uzalendo umetushinda" niliumia saana nilipogundua ni wanayanga wanawashangilia Stella, naapa, ninaapa kwa hicho kitendo sitowasamehe yanga na niliichukia ile timu hata nikiwa nje ya nchi wanacheza siendi kuangalia nilikwenda siku moja tu kwa kulazimishwa sikuishangilia japo walishinda
 
Timu zote zina point 86, huku City akiwa na tofauti ya Mabao 63 Man United akiwa na GD ya 55.

City akikipiga na QPR, Man United akigongana na Sunderland.

United alimaliza kwa ushindi wa goli moja, bao la Waza hivyo kufanya kuwa na point 89. City kang'ang'aniwa na QPR, mpaka dakika ya 90, City 1-2 QPR.

Kumbuka hii mechi ni muhimu kwa timu zote mbili. City anapaswa kushinda ili achukue ubingwa na QPR ashinde ili asishuke Daraja.

Sisi Mashabiki wa Manchester United, tupo tunashangalia kombe letu. Mechi imeshaisha tayari.

Zikaongezwa dakika 5 kufidia dakika zilizopotea. Asalaleeeh, dakika ya 92, Dzeko anasawazisha ubao. Sasa ni 2-2.

Bado matumaini kwetu ni makubwa mno. Droo hiyo isingesaidia. Ubingwa ni wetu sisi.

Dakika ya 93, La haula!. Aguero anafunga goli na kufanya kuwa 3-2.

Nilihuzunika mno. Hakika nilipata huzuni iliyo kuu. Mpaka na leo sitosahau. City anatawazwa kuwa bingwa kwa mara ya kwanza.

Hata hivyo QPR aliponea kushuka baada ya Bolton kutoka sare.

Mungu naomba hili jambo lifutike kwenye kumbukumbu zangu.
Nilitoka ukumbini dk 89 ili nikirudi nikute Mechi imeisha. Naingia ukumbini Aguero anafunga goli la pili baada ya pasi ya kichaa.
 
1999
Dakika 88 Bayern Munich 1-0 Man United. Full time 1-2 magoli ya Teddy Sherringham na Olle. Nililala SAA 12 asubuhi.
 
Goli la mapema baada ya Yanga kufunga hata hawajamaliza kushangilia ulipigwa mpira na chenga za maudhi likaingia goli.

Hii nayo ikae kwenye rekodi
 
Hilo la Muani hata yeye mwenyewe kichwani mwake haliwezi kufutika.Pia matukio kama haya hayafutiki kichwani mwangu (1) Gatuso kumkaba Ronaldo, hiyo ilikuwa AC Milan Vs Man utd
(2) Suarez kudaka mpira uliokuwa unaelekea kuwa goli, Uruguay Vs Ghana (3) World cup 2010 German Vs England Lampard anasawazisha lakini refa anakataa goli.Nadhani hiyo ndio iliwafanya waingereza wagundue goal line technology maana mpira aliopiga Lampard ulivuka mstari WA goal na kurudi ndani.
Hiyo Namba 2 ndo haitafutika akilini mwangu
 
1. Goli la Kibu D dhidi ya Yanga 2023
2. Simba 5 Yanga 0
3. Yanga 3 Simba 0 kipindi cha kwanza, FT Yanga 3 Simba 3
Hii ya 3 kwa 3 ndo haitasahaulikaa kamweee.
 
Waarabu kuwaziba mdomo gongowazi kabla hawajamaliza kushangilia goli la Mayele jana hapo mjini Lupaso.
 
Back
Top Bottom