Chaliifrancisco
JF-Expert Member
- Jan 17, 2015
- 26,021
- 79,710
Yeah dogo yupo pale Liverpool u21Hii kwangu ndio the best nakumbuka hadi matukio yaliyofanyika banda umiza siku hiyo
Pia kulikuwa na dogo muokota mipira aliyemsaidia Alexander Arnold kuonesha pasi aitupie kwa Origi.
Huyu dogo nimeingia kucheki jina lake nimekuta na taarifa zake ambazo sikuzijua.
View attachment 2633805
Dogo anaitwa Oakley Cannonier kumbe alipewa hadi na mkataba kusainiwa na Club kwa kitendo kile cha kuisaidia timu.
Hili tukio limenikumbusha fujo nyingi za mashabiki wa Barcelona siku ile.Yeah dogo yupo plae Liverpool u21
Bonge moja ya matchEnzi zile uefa inaoneshwa na Channel Ten nadhani, nikazima Tv na kwemda kulala baada ya half time. Asubuhi naambiwa Liver bingwa nikawa nabisha
Dah, mkuu umenikumbusha hiyo marathon ya 2021/2022 EPL.Sitasahau man city amegongwa mbili na Aston villa afu akashinda tatu sisi liva tulikua tunaombea agongwe tuchukue ligi
Kama kumbukumbu zangu hazijapotea...Mambo Gani hayo ya kukumbushana machungu
Na usiku huo anaalikwa dinner na roberto mancini anaporudi kwake akapitia club akakutana na kimwana funny neguesha...Mlitukota siku ile, Super Mario alitoka kuunguza sehemu ya nyumba yake akaja akatuweka goli na ushangiliaji wa aina yake
Hatari sanaHeshima kwako mkongwe mwezangu.
Fernando Redondo alimpiga tobo Henning Berg afu akaenda kutoa assist safi kwa Raul. Redondo alikuwa fundi kweli na mguu wake wa dhahabu bahati mbaya majeraha yakaharibu kipaji chake!
Hiyo ya Ufaransa kutwaa taji la Euro 2000 kuna mechi kadhaa za kukumbukwa. Nakumbuka robo fainali walikutana Ufaransa na Ureno nadhani, dakika za lala salama Ufaransa wakapata penati, Zizou akawa anaenda kupiga, Luis Figo akavua jezi na kutoka nje kabla hata Zidane hajaweka mpira kambani na akafunga kweli mechi ikaisha kwa goli la dhahabu.
Figo alivyokuja kuulizwa baadae akasema hakutarajia Zidane kama angekosa hivyo akaona atoke zake mapema😂😂
Wachambuzi wengi wa soka, wanadai michuano ya Uefa Euro 2000 iliyofanyika Ubelgiji na Uholanzi kwa pamoja ni moja kati ya michuano bora kabisa kuwahi kufanyika🫡🫡
Wale wahuni wa Barca enzi zile walikuwa siyo watu wazuri....Sir Alex alitetemeka sana!! Guardiola na Messi walimtesa sana babu wetu
Nilitoka ukumbini dk 89 ili nikirudi nikute Mechi imeisha. Naingia ukumbini Aguero anafunga goli la pili baada ya pasi ya kichaa.Timu zote zina point 86, huku City akiwa na tofauti ya Mabao 63 Man United akiwa na GD ya 55.
City akikipiga na QPR, Man United akigongana na Sunderland.
United alimaliza kwa ushindi wa goli moja, bao la Waza hivyo kufanya kuwa na point 89. City kang'ang'aniwa na QPR, mpaka dakika ya 90, City 1-2 QPR.
Kumbuka hii mechi ni muhimu kwa timu zote mbili. City anapaswa kushinda ili achukue ubingwa na QPR ashinde ili asishuke Daraja.
Sisi Mashabiki wa Manchester United, tupo tunashangalia kombe letu. Mechi imeshaisha tayari.
Zikaongezwa dakika 5 kufidia dakika zilizopotea. Asalaleeeh, dakika ya 92, Dzeko anasawazisha ubao. Sasa ni 2-2.
Bado matumaini kwetu ni makubwa mno. Droo hiyo isingesaidia. Ubingwa ni wetu sisi.
Dakika ya 93, La haula!. Aguero anafunga goli na kufanya kuwa 3-2.
Nilihuzunika mno. Hakika nilipata huzuni iliyo kuu. Mpaka na leo sitosahau. City anatawazwa kuwa bingwa kwa mara ya kwanza.
Hata hivyo QPR aliponea kushuka baada ya Bolton kutoka sare.
Mungu naomba hili jambo lifutike kwenye kumbukumbu zangu.
Marafiki zangu walionitembelea waliniaga baada ya first half. Asubuhi wananiuliza zilifika ngapi? Nilipowaambia bingwa na Liverpool mmoja akaanirushia mchanga.Miracle of Istanbul 2005
Hiyo Namba 2 ndo haitafutika akilini mwanguHilo la Muani hata yeye mwenyewe kichwani mwake haliwezi kufutika.Pia matukio kama haya hayafutiki kichwani mwangu (1) Gatuso kumkaba Ronaldo, hiyo ilikuwa AC Milan Vs Man utd
(2) Suarez kudaka mpira uliokuwa unaelekea kuwa goli, Uruguay Vs Ghana (3) World cup 2010 German Vs England Lampard anasawazisha lakini refa anakataa goli.Nadhani hiyo ndio iliwafanya waingereza wagundue goal line technology maana mpira aliopiga Lampard ulivuka mstari WA goal na kurudi ndani.
Hii ya 3 kwa 3 ndo haitasahaulikaa kamweee.1. Goli la Kibu D dhidi ya Yanga 2023
2. Simba 5 Yanga 0
3. Yanga 3 Simba 0 kipindi cha kwanza, FT Yanga 3 Simba 3