Tukio hili la leo si la kupuuzia, Mhusika awekwe kiuzuizini, alipe faini ya milioni 2 na kifungo kisichopungua miaka 2

Timu za majeshi huwa HAZINA NIDHAMU michezoni tutarajie kuona ujinga zaidi ya huu. Halafu mbona kocha aliepigwa kajiangusha KISANII SANA. mwanaume kangumi hako tuu. Kwanza kapigwa ka ngumi halafu karudi nyuma vizuri tuu. Kapiga magoti halafu kalaaaalllaaaaa. BUMBAFU WOTE.
 
Matumizi
Matumizi mabaya ya neno kizuizini
 
Mambo ya mpira serikali (police) haingilii, ndo kanuni za Fifa hizo
 
Mimi mwenyewe sioni kama aliweza kumpata ila kosa la kurusha ngumi tu tayari anastahili adhabu.
Adhabu za TFF zinaambatana na pesa. Hapo atalimwa faini ya shilingi laki tano na kufungiwa mechi tatu au zaidi.

Hiyo ni hasara kwa klabu yake, watakapocheza mechi yoyote itabidi mapato yao ya mlangoni yapunguzwe kwa shilingi laki tano. Na uongozi makini wa timu ya mpira unatakiwa umkate mshahara wake kufidia hiyo pesa watakayolipishwa na TFF kama faini.
 
Ikifika kama milioni 3 itapendeza zaidi. Wakipigwa adhabu yenye maumivu watajipanga wawaondoe wahuni kama hao wasiendelee nao katika ligi kuu.
 
Hiyo Ngumi hakukusudia impate huyo kocha. Ni bahati mbaya kocha alisogezea uso Ngumi.
 
Huyu mvuta bangi hata kama atafumbiwa macho, bado anastahili kabisa kufungiwa maisha kujishughulisha na mchezo wa soka kwa zile ngazi rasmi.
 
Umeandika sana ila masuala ya michezo hayapelekwi polisi kama ulivyotushawishi hapo..ndiyo imeisha hiyo..ugulieni tu maumivu ya kushuka daraja.
Ni kufungiwa maisha kama wakina Manara yule jamaa jinga kabisa mimi nilikua nataka Kigoma Timu ipande na Mbeya City ishuke kwa sababu ya sheria mbovu ya TFF kushindanisha madaraja mawili tofauti yaani hizi za kina Mbeya City zinafanya vibaya ila hazishuki kwa sababu ya kijisheria cha play off cha tff...
 
Umeandika sana ila masuala ya michezo hayapelekwi polisi kama ulivyotushawishi hapo..ndiyo imeisha hiyo..ugulieni tu maumivu ya kushuka daraja.
Duuuu! Hata jinai ikitokea michezoni haiendi polisi?
 
Mbeya mmetuangusha, mnapigwaje na watu wanaoaminika kuwa washamba kuliko mtu yeyote Tanzania?
Acha dharau dogo unafikili kigoma anatoka mzembe jaribu uone kitakachokukuta, haya mambo ni temper za mchezo kigoma tungekuwa washamba tusingekuwa tunatoa vipaji Bora vya mpira na Sanaa. Jifunze heshima au tukuadabishe kama mama yako hakukulea vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…