Tukio kwenye mataa ya Mwenge: Tofauti ya Wazungu na Waafrika

Ngoja siku upewe huduma ya kuzibuliwa mtaro bila majadiliano wala maelewano then rudi hapa uhadithie tena, sawa eeh.., tena umpigie na saluti kabisa..., mtumwa mkubwa wewe
 
Mkuu, mbona wazungu ni wengi wanaendesha gari za kawaida. kuna mzungu ana drive subaru yupo kenya na ana pesa. Hapa jirani yangu kuna wazungu wanapanda boda boda. Na wengine wana NOAH.

Ukimsoma mleta mada vizuri utamuelewa
Hazungumzii (toleo)brand ya Gari,anazungumzia(type) aina ya Gari...Ni kweli Ni nadra Sana mzungu aendeshe salon cars in Africa Tena ya kijapan
 
Hazungumzii (toleo)brand ya Gari,anazungumzia(type) aina ya Gari...Ni kweli Ni nadra Sana mzungu aendeshe salon cars in Africa Tena ya kijapan
Nimemuelewa vizuri sana mkuu, ndio maana nikampa mifano hiyo. Mfano subaru ni salon na kuna wazungu wanaendesha
 
Yaani huna kazi ya kufanya kwa kuandika gazeti zima ndani yake utopolo mtupu mpaka umefikia kujidharau Uafrika wako!! Mbona mimi nishatoa zaidi ya pesa hizo?!!
 
hyo tabia ya kunimwagia mimaji michafu kwenye kioo uwa inanikera vibaya mno.Kiukweli sitak kabisa.
 
Dogo akafunga biashara akaenda kuvuta bangi na ponbe hela yote
 
Samahani aisee saa nyingine nakuta notifications zaidi za 150 kuu kama muda hauniruhusu inakuwa ngumu kuziona zote hivyo inabidi nitafute muda ambao wakati mwingine sina ili nizipitie zote.

Asee we jamaa mbona nakuita kwenye mauzi yetu umemute?[emoji848][emoji848][emoji848]
 

Nashukuru sana ndugu yangu kwa elimu nzuri uliyowasilisha jukwani kulingana na ushuhuda na uzoefu wako ulionao.

Binafsi nimejifunza mambo mazuri kadhaa kutoka kwako leo hii. Sababu hata nami pia kwa namna moja au nyingine nimeshakuwa mhanga kwa vipindi tofauti hasa kuonyesha shukrani kwa jambo unalotendewa. Inaweza ikawa huduma.

Kupitia pia uzoefu wangu nilionao katika maisha yangu ya kila siku hapa duniani, ni kweli ndugu zangu kidogo tunakuwa na roho za ubinafsi sana hasa katika kutoa aidha shukrani au motisha kwa wenzetu wanaotusadia. Ndio maana kuna mgawanyiko wa kazi, sababu hakuna mtu ambaye ana uwezo wa kufanya kila kitu peke yako. Ukiweza hiki mwenzako ataweza kile, hiki hukifahamu mwenzako anakifahamu. Ndio kusudi pekee la Mwenyezi Mungu watu kuishi kwa kusaidiana na kutegemeana haijalishi wewe ni mtu wa aina gani kulingana na mtizamo wako.

Kitu kingine cha kujifunza ni kuanza kuwajenga watoto wetu toka kwenye msingi, namna ya kukubali kazi ya mtu mwingine pia iendane sambamba na utoaji wa dhati unaougusa moyo. Mfano mdogo tu na wengi wenu mtakuwa mashaidi katika hili, “mara nyingi tulipokuwa watoto inapofika siku ya kushiriki nyumba za Ibada, ni kawaida sana kwa mzazi kumpatia mwanae vijisenti kwa ajili ya kwenda kumtolea Mwenyezi Mungu sadaka”, tabia ambayo inajijenga na kukua ndani ya mtoto kuwa vijisenti ndio hufaa kwa kumtolea Mwenyezi Mungu.

Tukirudi kwa wenzetu. Swala la utoaji huendana sambamba na kuguswa kutoka moyoni, na hiyo tabia hufundishwa tangu wanapokuwa watoto wadogo. Sisi wengi wetu mafunzo tunayoyapata ni ya kibinafsi binafsi tu kutoka kwa wengi wa wazazi/ walezi wetu. Mzazi/ mlezi atampatia mtoto chungwa then atamuambia maliza kula ndio urudi kucheza na wenzako, ufute na mdogo wasikuone. Hivyo unaweza kuona unalea mtoto wa aina gani.

Hivyo matendo mengi ya watu ya ajabu tunayokutana nayo kila siku ni dhahiri yanaweza kuwa na uhusiano wa matunda ya malezi aliyoyapata mtu tangu akiwa mdogo.

Tujifunze kukubali kazi za wenzetu sababu hata ungekuwa ni wewe ungetamani kutendewa wema.

Asanteni wadau.
 
Me sikupi ht Mia ukanunue bangi na gundi na cocaine..sana Sana km utaforce utaambulia tusi taa zikiruhusu
Suala la matumizi ya pesa utakayompa sio jukumu lako, kama unayo mpe ila usitafute sababu ya kujikosha mkuu
 
Yaani huna kazi ya kufanya kwa kuandika gazeti zima ndani yake utopolo mtupu mpaka umefikia kujidharau Uafrika wako!! Mbona mimi nishatoa zaidi ya pesa hizo?!!
Una ubongo mdogo usioweza hata kufikiri.
 
Hapa Duniani hautakiwi kumdharau mtu, Mungu akikupa unafuu usiwaone wengine wazembe au wasiojituma, hata yule anayefanya kazi ya ovyo kumbuka nae ana watu wanamtegemea.

Kama alivyosema mtoa mada, japo kuwa wazungu wana madhambi ya kumchukiza Mungu na wanadamu ila tukiwaweke kwenye mizani na watu wa jamii nyingine ni ukweli usiopingika wao wana nafuu. Ukifanya kazi na mzungu kama ukifanya kwa usahihi na kwa uaminifu, hakika utalipwa vizuri na mchango wako kuthaminiwa ila kwa jamii nyingine kama wachina, waarabu, wahindi na wengineo ni shida si kidogo, ukiwahi sana kazini ni tatizo na ukichelewa ni shida sio kidogo.

kuna nguvu kubwa katika kutoa, hii ni siri ambayo watu wengi hawaitambui, unapomsaidia mhitaji kweli kiimani ina nguvu, pengine huyo mzungu alimpa hela huyo kijana sio kwa sababu ya huduma bali aliona njaa kali ambayo ilionekana waziwazi hadi usoni kwa kijana huyo. Ukiwa na uwezo wa kusaidia, wewe saidia bila kuona uchungu wa msaada uliotoa hakika Mungu asipokulipa wewe atakilipa kizazi chako.

Mwisho namalizia wazungu licha ya ufirauni wao ila wamestaarabika kuliko jamii nyingine husasani wakina sie, utasikia mtu anasema wazungu walitupeleka utumwani, swali langu ni wazungu gani walikuja kuwakamata watu weusi kama sio tulichuuzana wenyewe kwa wenyewe. Watu weusi sie tumejaa unafiki, ubinafsi, uzindaki uliopitiliza.
 
Niwe mkweli tu akimwagia maji huwa nawasha wipers haraka na kufuta mwenyewe huku nikimsisitiza aache. I guess I'm a typical Tanzanian.
Same here yaani

Tena akiwa mbishi namsindikiza na honi kabisa!!!!
 
Ulijiridhisha kuwa hakuwa mmatumbi aliyepaka cha congo ❓❔🤣🤣🤣🤣 maana umeelezwa kuwa mzungu hawezi kokota sedan bali SUV
 
Kuna mwanamke attention yake ni pesa
Appreciation kama ni hiyo pesa basi kuna two sides kwenye coin. Kampa kwa sababu ya appreciation au kampa kwa sababu hakua na chenji
 
Nisiwe mnafki mie hapana. Wacha nionekane nina roho mbaya. Ila watu wa njiani mazoea sitaki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…