Tukio kwenye mataa ya Mwenge: Tofauti ya Wazungu na Waafrika

Tukio kwenye mataa ya Mwenge: Tofauti ya Wazungu na Waafrika

Nilitaka kuamini storry yako Ila nilipoona CROWN Nimesita kukuamini kwa kuwa Mzungu Kama Mzungu uliyemuongelea ni vigumu kuwa na hiyo Gari. Kwanza ni Saloon/Sedan, Mzungu hutumia SUV/WAGON.

Unless ungefunguka kuwa kuwa Kuna kamzunguko kapesa kameanza kuonekana mtaani ningekuelewa.

Mengine yote umefagilia wazungu kwa mtizamo wako, na hayaendani na Story yako ya Mwenge.

Nahisi hujawahi kuishi na wazungu na kuyajua maisha yao halisi kuhusiana na fedha unawaona tu barabarani. Sasa Kama hujui hakuna mtu mchumi kama Mzungu.
Leo nimepishana na mzungu anaendesha Premio.
 
Sijui hata niseme vipi?!.

Kwa lugha nyepesi tu naweza kusema wenzetu WAZUNGU wameumbwa tofauti kabisa na sisi (ngozi nyeusi) WAAFRIKA. Sitaki kutumia maneno yanayoweza kufanya nikufuru, lakini ninachoweza kusema ni kwamba Mwenyezi Mungu aliwaumba wazungu kwa namna ya pekee sana. Kusema hivi wala sio utumwa kama wengine mnavyoweza kudhani, bali ni ile hali ya kukubali (appreciating) jamii ya watu fulani pasi na kujali dini zao, rangi zao, wala asili zao. Kukubali katika jambo jema na zuri ni busara zaidi kuliko kukataa tu hata kama ni jambo jema na lina manufaa.

Ninapozungumzia wazungu simaanishi ngozi nyeupe, hapana. Sizungumzii waraabu, sizungumzii wachina, wala sizungumzii wahindi. Nazungumzia WAZUNGU, watu wenye asili ya kutoka bara la Ulaya wenye rangi nyeupe (the white people).

Kuna Kijana anafanya kazi ya kufuta vioo vya magari katika makutano ya barabara ya kutoka Tegeta kuja Mwenge. Ni pale kwenye taa za barabarani (trafic light). Gari zinapo simama tu kwenye foleni kijana huyu humwaga povu la sabuni kwenye kioo cha mbele, kisha hutumia kifaa chake maalumu kufuta lile povu ili kuondoa vumbi. Kazi hii huifanya kwa uharaka sana na kwa ustadi wa hali ya juu. Ndani ya dakika moja na sekunde kadhaa atamwaga povu, atasafisha kioo, kisha atafuta povu na kuacha kioo cha gari yako kikiwa kisafi.

Kazi hii imekuwa ikifanywa na vijana wengi katika miji mbali mbali hapa barani Afrika.

Akishafanya hiyo kazi, wewe dereva unampatia kipande kidogo cha pesa. Kiasi cha pesa cha kumpa unapanga wewe mwenyewe. Wengi waliopata huduma ya kijana huyu walikausha kimya bila kulipia chochote na wala haikuwa kesi. Na wapo baadhi yao (wachache) walilipia shilingi 100 hadi 200 hivi.

Kuna gari aina ya CROWN iliyokuwa ikiendeshwa na Mzungu. Alionekana kama sio raia wa Uingereza basi atakuwa anatokea Wiles au maeneo ya jamii hiyo.

Kijana ni kama alijua vile. Na inaonyesha ana uzoefu wa kutosha wa malipo ya wateja anao wahudumia. Alisafisha kioo cha ile gari chap chap, kisha akasogea dirishani kwa dereva ili apate ujira wake. Yule dereva Mzungu akatoa noti ya shilingi 10,000 na kumpatia yule dogo. Daaah! Dogo alimshukuru sana kana kwamba yule Mzungu alikuwa amemfanyia kitu kikubwa sana kwenye maisha yake.

Taa ziliporuhusu ile gari ilipokuwa ikiondoka bado dogo aliendelea kumshukuru tena kwa kumpigia "saluti" yule Mzungu kuonyesha ame-appreciate kile alichofanya. Kama ilivyo utaratibu, yule Mzungu nae alijibu ile saluti ya dogo nae kwa kupiga Saluti.

Lilikuwa tukio la kipekee sana lililo onyesha namna sisi watu weusi (waafrika) na wenzetu wazungu tulivyo tofauti. Ni tukio lililompa yule kijana FARAJA NDANI YA MOYO. Mbali na kiasi cha pesa alicholipwa na yule Mzungu lakini kwa kijana aliona thamani ya kile anachofanya (kazi yake). Thamani ya kazi ya halali inayofanywa na mikono yake. Pengine kijana yule angekuwa mwizi au kibaka akikwapua mali za watu kwenye yale makutano ya ile barabara, leo hii thamani ya kazi yake asingeiona. Na zaidi ya yote angekuwa adui mkubwa mbele ya jamii na hasa watumiaji wa ile barabara.

Ni kawaida kwa wenzetu wazungu ku-appreciate kazi ya mtu pasi na kujali ni kazi ya aina gani. Ikiwa ni kazi ya halali na unaifanya kwa ustadi basi ataiheshimu kazi yako katika kiwango kinacho stahili. Hii ni tofauti kabisa na sisi Wafrika.

Sisi waafrika ni watu ajabu sana. Mtu unafanya kazi ngumu, nzito tena inayo "RISK" maisha yako, inapofika wakati wa kukulipa anakulipa isivyostahili. Na pengine asikulipe kabisa, au akakudhulumu kwa kukulipa kidogo tofauti na ilivyopaswa. Kama huamini, mtazame Meneja au Muhasibu hapo ofisini kwako. Amepewa mamlaka ya kuwalipa mishahara yenu. Lakini swali ni Je, anawalipa kwa wakati? Na je, ikifika wakati wa malipo anawalipa tu, au anasubiri hadi usingizie mtoto au mke/mume kuugua ndio aidhinishe malipo yako?

Kwakuwa yupo kwenye mamlaka ya kukulipa basi atakulipa atakavyo yeye.

Nadhani hapo utakuwa umenielewa vizuri kile ninacho maanisha. Akiwa Muhasibu au Bosi anaye idhinisha malipo yenu kuna wakati atasubiri hadi ifike tarehe 38 ndio awalipe malipo yenu. Hatari sana.

Naomba leo niwakumbushe kitu muhimu. Ni dhambi kubwa sana mbele ya dunia na mbele ya Mungu kudhulumu jasho la anaye pigana kwa haki. Jasho la mpiganaji daima huwa halipotei bure. Mungu wetu mlezi anasema "walipeni watumishi ujira wao kama vile inavyo stahili". Tambua kuwa athari za kuchelewesha mshahara wa mfanyakazi wako zinaumiza watu wengi sana. Kuchelewa kumlipa mfanyakazi wako kunaumiza watoto wake, mke/mume wake, wazazi wake, ndugu zake na hata jamaa zake. Anapochelewa kupata malipo yake hata Mangi dukani anakosa pesa, kwani pengine huyo ni mmoja katika wateja muhimu sana pale dukani.

Ndugu yangu, ikiwa umepewa dhamana ya kulipa ujira wa mtu anayemwaga jasho lake, basi mlipe katika wakati sahihi. Na ikiwa unadaiwa, basi lipa deni lako katika wakati mliokubalina.

Mwenyezi Mungu awabariki sana.

Na Hilal Kanal
0718022322
Dar es Salaam

View attachment 1858654

Ungeenda Ulaya/Marekani ukaona waswahili wanavyo behave ungeelewa! Ni issue ya kuwa mbali na Nyumbani, na huyo ni Mzungu mmoja Kati ya mamilioni....

Pengine wewe hujawahi ona Mwafrika kafanya Hivyo, Mimi nishawahi mpaka mtu back in 2013 (50,000); baada ya kumuuliza maswali Mda mrefu!

Ulichoona Leo Hakuna sababu ya kutusema , simply umetuonea na ngozi, tembea tu sehem za San Diego, au CA kwenye slam utajua wazungu ni wenu na vichaa!

Wazungu si kitu si lolote!
 
Leo nimepishana na mzungu anaendesha Premio.
Wazungu wapo wa aina nyingi mkuu, nazungumzia kwa mzungu aliyemuongelea yeye. Wapo Hadi wanaoendesha bodaboda.

Soma uelewe.
 
Sijui hata niseme vipi?!.

Kwa lugha nyepesi tu naweza kusema wenzetu WAZUNGU wameumbwa tofauti kabisa na sisi (ngozi nyeusi) WAAFRIKA. Sitaki kutumia maneno yanayoweza kufanya nikufuru, lakini ninachoweza kusema ni kwamba Mwenyezi Mungu aliwaumba wazungu kwa namna ya pekee sana. Kusema hivi wala sio utumwa kama wengine mnavyoweza kudhani, bali ni ile hali ya kukubali (appreciating) jamii ya watu fulani pasi na kujali dini zao, rangi zao, wala asili zao. Kukubali katika jambo jema na zuri ni busara zaidi kuliko kukataa tu hata kama ni jambo jema na lina manufaa.

Ninapozungumzia wazungu simaanishi ngozi nyeupe, hapana. Sizungumzii waraabu, sizungumzii wachina, wala sizungumzii wahindi. Nazungumzia WAZUNGU, watu wenye asili ya kutoka bara la Ulaya wenye rangi nyeupe (the white people).

Kuna Kijana anafanya kazi ya kufuta vioo vya magari katika makutano ya barabara ya kutoka Tegeta kuja Mwenge. Ni pale kwenye taa za barabarani (trafic light). Gari zinapo simama tu kwenye foleni kijana huyu humwaga povu la sabuni kwenye kioo cha mbele, kisha hutumia kifaa chake maalumu kufuta lile povu ili kuondoa vumbi. Kazi hii huifanya kwa uharaka sana na kwa ustadi wa hali ya juu. Ndani ya dakika moja na sekunde kadhaa atamwaga povu, atasafisha kioo, kisha atafuta povu na kuacha kioo cha gari yako kikiwa kisafi.

Kazi hii imekuwa ikifanywa na vijana wengi katika miji mbali mbali hapa barani Afrika.

Akishafanya hiyo kazi, wewe dereva unampatia kipande kidogo cha pesa. Kiasi cha pesa cha kumpa unapanga wewe mwenyewe. Wengi waliopata huduma ya kijana huyu walikausha kimya bila kulipia chochote na wala haikuwa kesi. Na wapo baadhi yao (wachache) walilipia shilingi 100 hadi 200 hivi.

Kuna gari aina ya CROWN iliyokuwa ikiendeshwa na Mzungu. Alionekana kama sio raia wa Uingereza basi atakuwa anatokea Wiles au maeneo ya jamii hiyo.

Kijana ni kama alijua vile. Na inaonyesha ana uzoefu wa kutosha wa malipo ya wateja anao wahudumia. Alisafisha kioo cha ile gari chap chap, kisha akasogea dirishani kwa dereva ili apate ujira wake. Yule dereva Mzungu akatoa noti ya shilingi 10,000 na kumpatia yule dogo. Daaah! Dogo alimshukuru sana kana kwamba yule Mzungu alikuwa amemfanyia kitu kikubwa sana kwenye maisha yake.

Taa ziliporuhusu ile gari ilipokuwa ikiondoka bado dogo aliendelea kumshukuru tena kwa kumpigia "saluti" yule Mzungu kuonyesha ame-appreciate kile alichofanya. Kama ilivyo utaratibu, yule Mzungu nae alijibu ile saluti ya dogo nae kwa kupiga Saluti.

Lilikuwa tukio la kipekee sana lililo onyesha namna sisi watu weusi (waafrika) na wenzetu wazungu tulivyo tofauti. Ni tukio lililompa yule kijana FARAJA NDANI YA MOYO. Mbali na kiasi cha pesa alicholipwa na yule Mzungu lakini kwa kijana aliona thamani ya kile anachofanya (kazi yake). Thamani ya kazi ya halali inayofanywa na mikono yake. Pengine kijana yule angekuwa mwizi au kibaka akikwapua mali za watu kwenye yale makutano ya ile barabara, leo hii thamani ya kazi yake asingeiona. Na zaidi ya yote angekuwa adui mkubwa mbele ya jamii na hasa watumiaji wa ile barabara.

Ni kawaida kwa wenzetu wazungu ku-appreciate kazi ya mtu pasi na kujali ni kazi ya aina gani. Ikiwa ni kazi ya halali na unaifanya kwa ustadi basi ataiheshimu kazi yako katika kiwango kinacho stahili. Hii ni tofauti kabisa na sisi Wafrika.

Sisi waafrika ni watu ajabu sana. Mtu unafanya kazi ngumu, nzito tena inayo "RISK" maisha yako, inapofika wakati wa kukulipa anakulipa isivyostahili. Na pengine asikulipe kabisa, au akakudhulumu kwa kukulipa kidogo tofauti na ilivyopaswa. Kama huamini, mtazame Meneja au Muhasibu hapo ofisini kwako. Amepewa mamlaka ya kuwalipa mishahara yenu. Lakini swali ni Je, anawalipa kwa wakati? Na je, ikifika wakati wa malipo anawalipa tu, au anasubiri hadi usingizie mtoto au mke/mume kuugua ndio aidhinishe malipo yako?

Kwakuwa yupo kwenye mamlaka ya kukulipa basi atakulipa atakavyo yeye.

Nadhani hapo utakuwa umenielewa vizuri kile ninacho maanisha. Akiwa Muhasibu au Bosi anaye idhinisha malipo yenu kuna wakati atasubiri hadi ifike tarehe 38 ndio awalipe malipo yenu. Hatari sana.

Naomba leo niwakumbushe kitu muhimu. Ni dhambi kubwa sana mbele ya dunia na mbele ya Mungu kudhulumu jasho la anaye pigana kwa haki. Jasho la mpiganaji daima huwa halipotei bure. Mungu wetu mlezi anasema "walipeni watumishi ujira wao kama vile inavyo stahili". Tambua kuwa athari za kuchelewesha mshahara wa mfanyakazi wako zinaumiza watu wengi sana. Kuchelewa kumlipa mfanyakazi wako kunaumiza watoto wake, mke/mume wake, wazazi wake, ndugu zake na hata jamaa zake. Anapochelewa kupata malipo yake hata Mangi dukani anakosa pesa, kwani pengine huyo ni mmoja katika wateja muhimu sana pale dukani.

Ndugu yangu, ikiwa umepewa dhamana ya kulipa ujira wa mtu anayemwaga jasho lake, basi mlipe katika wakati sahihi. Na ikiwa unadaiwa, basi lipa deni lako katika wakati mliokubalina.

Mwenyezi Mungu awabariki sana.

Na Hilal Kanal
0718022322
Dar es Salaam

View attachment 1858654
Hapa kuna mambo mengi mzee. Umefanya haraka kufikia hitimisho la tukio hili. Kwanza unapaswa kufahamu tunatofautiana sana kitamaduni. Hii inakwenda mbali hadi kwenye masuala ya upendo na kujitoa. Sisi hatuna utamaduni wa tips, wala hatusaidiani kwa kulipana. Ndiyo maana unaona ukifa hapo ulipo unaweza kuzikwa na hao waliokuzunguka hata kama ndugu zako hawajulikani. Unaweza kuuguzwa na watu usiowajua... n.k. Uzunguni unaweza kufa ndani kwako ,nzi tu ndiyo itawajulisha kuwa kuna mzoga.

Hoja yangu ni kuwa sisi tuna namna tofauti ya kuonyesha upendo na huruma, tofauti na wenzetu. Ninaowalaumu ni wale ambao unakaa kimya, unaoshewa kisha hutoi kitu. Mimi ninadhani kama hutaki msimamishe mara moja. Na hata yeye kijana ajue kuwa binadamu tunatofautiana. Mwingine asingependa kuoshewa kioo chake hivyo maana hata hujui ubora wa sababuni , maji n.k. Kwa ninavyowafahamu wazungu, hiyo staili ya dogo hawaendani nayo kabisa. Ni kinyume na tamaduni zao. Wao utamamaduni wao ni wa uwazi na makubaliano.Baadhi ya wazungu, hata offer hotelini hakubali kama hajaamua ama kama inatoka mazingira ya kutatanisha. Wakati hapa kwetu mtu akikupa offer hujiulizi mara mbili. So, usishangae siku dogo akachapwa makofi na haohao wazungu unaowasifia hapa.

Kw akifupi , ninakiri na ninakuelewa unachotuambia na kutuonya. Lakini, mfano huu mmoja na namna ulivyoiwasilisha kuna mapungufu kidogo.
 
Mi huwa nawapa hata buku...but kinachonikera ni ile hali ya gari anaiona imetoka carwash imepigwa polish...yeye anakuja kumwagia mimaji michafu yenye povu kiooo daaah[emoji1751][emoji1751]

Hapo huwa nakereka kweli japo sitaongea na hela nampa[emoji848]
sasa hiyo screen ya gari itaoshwa mara ngapi wajameni? Mataa ya- fire ipigwe maji ya foma sabuni....magomeni junc. ....ivoivo Ioshwe !!... Hiyooo!! Morocco ipigwe maji...ok! Kuleee mataa ya reagent estate ivoivo!! Bado mwenge....kawe....ivoooo!! Wanajaza mipovu povu ya misabuni tyuuuuu!!!! Ndo maana rangi za Gari zina chujuka haraka.na kuchakaa. Kisa tu umfurahishe mtu...gari lazima ioshwe bila chemikali ya sabuni. Then inapigwa polish yake maalum kwa wakt maalum.na mtu maalum!!
Siyo kusafisha gari kihorera na njaanjaa zao tuuu!!
Then mnawalipa!! ...Mweee!!...wenye uelewa na magari yao wanamwambia achaaa...but anamlipa bure hela ni bora zaidi...
.lkn pia kusafisha screen ya gari ikiwa ya moto ni kosa...kwa wajuvi km mie gari kisheria inamwagiwa maji ikishapoa engine siyo hovyo hovyo tu! Popote Njiani.. ndo maana migari yenu ina mabaka mibaka.. . Unamwagia gari ya moto kunako mataa engine iko on!! Hee....mimaji jua kaliii yanateremkia chini kunako engine! Tena mivuke mnaiona kabisaaa Sometimes ile mifereji ya screen inazibaga kwa sababu mbali mbali. Sanasana majani ya miti. Sasa jiulize hilo povu la sabuni yenye kemikali lita churuzikia wapi? Na huko chini litasababisha nini hujui....
Wafokee tu waache km umewahurumia na una pesa wape tu kiasi chako....gari yako ni ya aina gani kwani!! Nikwambie kiwango cha uharibifu unachopata bila kujua...Tunza gari yako ikutunze wewe... Hizo huruma zako ni unaingia hasara maradufu tena usiyo ijua.... Af unalalamika vyuma vimebana?... haya yangu ni hayo
..
 
Wazungu wapo wa aina nyingi mkuu, nazungumzia kwa mzungu aliyemuongelea yeye. Wapo Hadi wanaoendesha bodaboda.

Soma uelewe.
lkn kumbuka zeruzeru siyo mzungu??
Mvaa wigi siyo mzungu pia!
Unajua watu wa mikoani mnajichanganya sana...
Hata wale watoto wa Remmy ongala ni weupe Peee! Hadi tako. ...Utawajua kwa meno yao...
 
Kwanza mleta mada kwa kuangalia haraka haraka hana gari huyu.....au ndo muosha magari mwenyewe!!!
Kwa sababu si kila aliyeko na mkoko barabarani ana hela waulize matrafiki uone.......
Mawazo tupu....huko barabarani.
Trafiki hakamati gari za raia hovyo hovyo saaana atamkuta na kiberiti..kuni au viji ndizi yeye anaangalia daladala...kirkuu!! Boda boda.bajaji...Magari ya mchanga tuuu!

Sasa hao wafuta vioo waende huko...lkn ujue wenyewe hao madreva wa vyombo hivi makauzu kinoma.....atakwambia zunguka kwa konda......ukienda kwa konda mlango umefungwa anakusanya nauli unarudi kwa dreva mataa yanaruhusu.....gari hiyoooooooo.....
......
 
Back
Top Bottom