Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

nimerudi wadau,tusameheane...nimeandika habari yangu baada ya kusoma story mama ya huu uzi ukanifurahisha na kati ya vitu nimesuffer ni kutafuta mwendelezo kama hivi mnavyosuffer nyie[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]

ila all in all nipo hapa...

....kati ya makosa tuliyofanya(haya nilikuja gundua baada ya mchakato kuisha na kupona kabisa,kuanza kuwaza ilikuaje hadi tukafanya tukio lile),lilikua ni kuchukulia lile tukio kama kitu rahisi tu,hatukufanya uchunguzi wa kutosha labda sababu ya ile haraka ya kufanikiwa na habari za kufata mkumbo kwamba kuna watu waliofanikiwa walivyoingia humo ndani,kule Njombe kulikua na tajiri aliyeitwa Mwanzinga(marehemu kafa 2017/18 kama sijakosea) huyu ni moja ya watu wanaodaiwa kutajirika baada ya kufanikiwa kuzama humo na kutoka na mali...story kama hizi ndio zilituchanganya na kujikuta tumebamia mapango ya watu bila kujipanga...pia baadae nilikuja ambiwa kwamba ile mali haisakwi kwa makundi,yaani unatakiwa kuwa man alone,peke yako ukifanikiwa kuzama ukatoka basi umetoboa,kosa letu lilikua kwenda kikundi...tuachane na hayo

sikumbuki masaa exactly lakini siyo chini ya saa sita hivi tukawa ndio huko pango kubwa...kutembea kwenda mbele ndio ilikua mtihani sababu nje mvua ilikua inanyesha na hilo pango ndio iliku njia ya maji yanaingia halafu yanapotelea huko ndani ndani yanatokea upande wa pili wa msitu kwenye miteremko kuunda mikondo ya maji

maji yalikua mengi na yanaenda kwa kasi sana so tulikua tunatembea kwa kujishikilia pembeni kwa tahadhari sana,giza ni kubwa bila zile tochi hufanyi kitu chochote kule...ukiongea sauti kidogo tu inakua multiplied sababu ya mwangwi,lile pango linaenda linashuka chini...ni kama shimoni,umbali wa kama viwanja viwili vya mpira ndio mauzauza yakipoanza

sisi kwetu kule huwa wanasema ukisikia hofu sana ghafla kwa kitu ambacho ulianza fanya kwa ujasiri basi acha mara moja...mimi hofu ikaanza kuniingia,lbda sababu sikua na moto sana kuhusu hizi rupia kuliko wenzangu(ikumbukwe nilikua na kibarua) nilikuaga naambiwa kuhusu nywele kusimama sikuwahi experience kabla,,,mara nikahisi mapigo ya moyo yako kazi sana hofu ni kubwa na nywele zinawasha sana ndio nywele kusimama huko...kutetemeka sababu ya baridi kukazidi ,sikumwambia mtu yeyote..kwa kadri ya ramani ya mangi alisema tumefika hayo maeneo yenye masanduku,kwa maelezo yake tulitakiwa fika kwenye korongo liko ndani ya pango...kwamba kwenye korongo juu kumeunganishwa minyororo mirefuuuuu imefungwa juu kabisa imeshuka chini huko ndio imeungwa kiustadi kwenye mashanduku imara kabisa,kwa uhandisi ule hayawezi anguka leo wala kesho...ni kweli binafsi niliona sasa sijui huwa ni wenge au nini,sababu humo ni kuchafu na kuna mizizi sana huwezi confirm kuwa ni kweli ni minyororo au ni mizizi,jamaa pia alituambia kuhusu beacon,ni kweli tuliona beacon zikiwa na maelezo ya lugha hatuifahamu kwa maelezo ya mangi hizo ni code wameandikiana wao siku wakija wanazitumia kufata mali....na zile zimeandikwa katika namna ukizitumia bila kujua ndio zinakupoteza zaidi (wazungu washenzi sana)...yaani unaweza kuta mshale umeenda kusini mita 2 kumbe wanamaanisha aendee kusini ya nchi,unakuta ni songea huko au vyovyote na mali haipo hapo unapodhani wewe,ni anayeweza chukua zile mali ni lazima awe na taarifa za kutosha sanaaaa...sababu hata wao huwa wanakuja na wanarudi patupu sometimes wakikosea maelezo.

nimeongea kuhusu mangi(huyu bwana kumbe yeye alikua keshawahi kuja fanya jaribio ila hakuweza mwenyewe ndio maana akaamua kutafuta kampani)

sasa ndio akatuambia tukiwa hapo kwamba...huko chini kushuka lazima watu washushwe kwa kamba(tulibeba kwa urefu wanaotosha sana,kama marufu kule njombe zinaitwa TANTAN) nani anashuka ikawa sasa wajitolee wawili akiwemo mangi mbeba maono...alikua pamoja na usungilo,mobu na mwaikambo wawashikilie kamba na mimi nikawa tu pending nimewashikia vitu pamoja na kucheki cheki usalama tu...wakajifunga kikomando tayari kushuka,kushuka kwenyewe hujui unashuka wapi...unafata tu mizizi maana huwezi jua kama ni ndio mnyororo au nini kisa msongamano wa taka.

jamaa wakaanza kushuka chini...kimya kikatawala pale sababu ya hofu tu.

dakika kama tano za kushuka kwa tahadhari ndio ikatokea shida,kikweli huwa sijui ni nini hasa kilitikea sababu mimi ni ghafla sana nikaona mwanga mkali mno,mkali saaaana kama radi kutoka kule shimoni ni kama zikanipoteza fahamu kwa muda,mwanga uliambatana na sauti za kilio kule chini as if mtu kakamatwa ghafla na mnyama mkali,nadhani alikua usungilo sababu baadaye mangi alifanikiwa kutoka(nitasema baadae tulikutana vipi)

nilichoweza kufanya haraka kwa muda ule ilikua ni kulala chini haraka sana,kule chini sauti jamaa ilikua inazidi kupungua ikimaanisha keshazidiwa nguvu...sikujua chochote kuhusu wenzangu washika kamba pale juu sababu kila mtu nadhani alianza kujitetea kivyake..

nikaanza kukimbia nikiwa na ule upofu wa kupigwa na mwanga mkali ghafla ukiwa gizani....kimbia bila mwelekeo,nikajigonga vibaya kichwani kwenye sehemu ya juu ya pango,na kilichoniokoa ni kwamba nilikua naelekea mbele zaidi ambako ni jirani kutoka nje kuliko kule tulikotoka...wenzangu hapo sijui wameelekea wapi...ile kujigonga ikanimaliza nguvu kabisa nikajikuta nimelala hapo hapo damu zinanitoka(ile fact ya damu nadhani ndio inaaply hapa) ghafla mbele yangu,ule upande niliowaacha jamaa sasa nikaona bonge ya nyoka ila siyo wa kumeza,mkubwa kwa hawa nyoka tumewazoea ila siyo chatu..kujivutavuta nadhani nikamkanyaga ndio akanigonga,akili hapa ndio zikaja baada ya kujua kifo ndio kimefika,chap nikatoa kiatu nikafungua kamba za viatu vyote viwili,nikafunga juu ya goti na chini ya goti sababu alinigonga kwenye hii nyama ya nyuma ya mguu...nikajikamua kamua kizushi nikawa napambana sasa kuelekea nje ,ambacho sikujua(labda ni mungu tu) kwamba kumbe tulikua nje kabisa hata ya msitu ambako sasa ni karibu na barabara kabisa watu ambako watu wanapita..tena karibia na kijijini...cha mwisho nakumbuka niliweza fanya ni kupiga kelele ya mwito kule njombe inaitwa ngoro....nikapiga za vilio kama mara tano hivi pumzi ikakata sikuelewa kilichofata baada ya hapo aiseee...hadi siku nazinduka nikiwa hospitali ya kibena....mguu ukiwa na hali mbaya sana umeharibika lakini pia ngozi yangu karibia mwili mzima ikiwa na upele fulani wa kuwasha sana...

nikaanza matibabu huku nikiwa sijui nimefikaje,sijui kuhusu jamaa zangu na hapo nimetulia sijauliza mtu yoyote sababu hakuna hata aliyeniuliza kulikoni

nitarudi sasa na habari ya matibabu yang na kuujua ukweli kuhusu vifo vya jamaa zangu na yule mwengine aliyegeuka mwehu...kisha mtazamo wangu kuhusu hizi mali za wachawi wazungu...

mnisamehe kwa mpangilio mbovu,naandika haraka sana niendane na muda kupambania kombe watoto wapate chochote kitu...


nitakuja....
wilaya ya makete, kata ya matamba, kuna poli pale katika shule ya sekondali ITAMBA linaitwa kisulike, kuna mzungu alikuwa mbishi aliingia na farasi hakutoka mpaka leo

ilo poli ukingia utoki unabaki humo humo ,kuna siku bange zetu zikatutuma tuingie humo ,si unajua watoto wa dar tunaosoma mkoa, tunakua viburi
 
wilaya ya makete, kata ya matamba, kuna poli pale katika shule ya sekondali ITAMBA linaitwa kisulike, kuna mzungu alikuwa mbishi aliingia na farasi hakutoka mpaka leo

ilo poli ukingia utoki unabaki humo humo ,kuna siku bange zetu zikatutuma tuingie humo ,si unajua watoto wa dar tunaosoma mkoa, tunakua viburi
twende kazi
 
mimi miweke hapa hapa habari yangu kuhusu machimbo haya na actually siyo machimbo ni harakati za kusaka mali alizoacha mjerumani wakati wanaondoka kutuachia nchi

kuna kitu tunafumbwa sana tunafichwa ukweli,wakoloni walipanga kila kilichotokea kwenye makoloni yao na hata yanayotokea sasa yalipangwa na wanajua nini kitafatia baada hata ya miaka kumi kuhusu nchi hizi masikini za afrika

kwamba walijipanga kuondoka ni KWELI,na uhuru hatukupigania,ni wao walipanga sasa watatutawala kwa namna nyingine ili waende wakajenge nchi zao huku wakiendelea kututawala kwa mbali na kuchuma mali zao...viongozi wote wanaokuwa madarakani ni vibaraka wao,hakuna hata mmoja mzalendo wa kweli na nchi yake

nina ushuhuda wa kusema haya,moja kati ya makubaliano yao ilikua ni kuacha mali zao salama na jukumu la serikali ni kuzilinda na kuwaruhusu wakija zichukua hata baada ya miaka mia,haya yapo kimkataba na kila raisi anayeingia madarakani anaambiwa hizi siri....na waliacha mali kweli za kutosha

story yangu sasa inabase kwenye hizi mali,hapa ni madini waliyoacha kwenye misitu ya nyumbanitu huko njombe,safari ya kuzifata hizo mali zilifanya nipoteze ndugu zangu watatu na mimi kunusurika chupu chupu ila kubaki na ulemavu...sitasahau hii safari ya machozi,jasho na damu.

ngoja nikaoge nakuja...

Pole sn mkuu
 
We jamaa nadhani you're still narrow minded person. Wenzako tunasimulia ishu ambazo zimetusumbua kipindi fulani maishani ili mjifunze we unaleta kilichoujaza moyo wako! Kwani sijasema huko juu yule mzee mwenye ndevu (jini alikuwa anataka nini?)
Umejawa na mawazo potofu, mawazo maovu. Omba Mungu ayabadirishe mawazo yako, jikite kwenye kusoma positive issues something that will help you to be positive minded person na sio kuwa wicked as how you're right now.
Mkuu hapa jf watu ndio walivyo..hamaanishi alichoandika anafurahisha genge tu.
 
Pale nilipo kaa (kuwangoja washkaji) usingizi ulinipitia nililalaa mpaka nilipo amshwa na makelele ya washkaji.

Sijui nilitumia muda gani kwenye usingizi ule ila nilipo angalia saa ilikua ni saa 6 mchana.

Nilipo amka nilikutana na kijua kikali utadhani niko Sudan, yani mpaka nguo nilizo vaa zilishaanza kunyauka.

Chakwanza niliwauliza kuhusu yule mmalawi, nikaambiwa bado wako camp wanaendelea kungoja mvua iishe waanze kazi.

Nilipo wauliza vipi kama mvua imeisha huko walikotoka, wakaniambia mvua imenyamaza sasa hivi baada ya kuvuka lile korongo.

Yani kumbe mvua inaanzia kwenye korongo kwenda matandani, ila kulimaliza korongo mvua hakuna.

Tulitembea mpaka kijijini, hakuna alie jua kua mimi nina dhahabu mbeleni.

Tuliingia kijijini saa 2 usiku, hapo tukalala.
Ila kwakua tulisha fika kijijini, kila mtu aliendelea kimpango wake.

Pale kijijini kila mtu anaham ya kujua kulikoni huko porini.
Nakumbuka nilitulia kwenye kiosk cha jamaa flani hivi, kila mtu alikua ananiuliza kuhusiana na porini.

Usiku kucha nilikesha kwenye kile kiosk cha jamaa nikila Royal gin (hii ni pombe kali sana) mpaka kuna kucha.

Kwakua nilikua na pesa ya kutosha niliyo chukua kwenye lile duka la marehem, hivyo ilikua mwendo wa kujimiminia pombe.

Kuna dem alinitamani nika lale kwake, lakini nilikataa kwa kuhofea asiniibie dhahabu yangu.

Migodini wanawake ndio wanaongoza kutuibia wachimbaji.

Kilicho fanyika nikumpa pombe mpaka dem akakimbia.

Asubuhi, sikutaka kulemba, na pombe zangu kichwani, nikakamata piki piki mpaka Montepuez.

Montepuez, hapa ndio kuna soko la madini yote.

Nikaingia kwa msirilanka nikapima dhahabu.

Dhahabu ilikua na uzito wa gram 112, kila gram kwa kipindi kile ilikua 2000 miticais sawa na laki moja shilingi kwa wakati huo.

Nikachukua 224,000 miticais, hapo akili yote inamuaza mama Abuu (Shemeji yenu)

Nakumbuka nilinunua piki piki na mazaga mengine kama nguo.

Nikatuma kama 60,000 miticais (sawa na Milioni tatu kipindi hicho) kwa mama yangu Tanzania, maisha yakaendelea.

MWISHO.

Naahidi kuwahabarishine matukio mbali mbali yanayo / yatayo tokea hapa mgodini nilipo.

Kumbuka kwa sasa naishi Tete, Muatiz, ila kwa hizi mvua zilizo anza kunyesha, nategemea kurudi Cabo del Gado wilaya ya Montepuez, nikatafute Ruby.

Hapa nangoja hii kazi iishe, nione kama nitaokoa chochote kinisogeze kwenye Ruby.
Ahsanteni na kwaherini.
kila lenye kheri baharia
 
Basi siku ya sita sikuoga ile dawa na nilishadharau, natoka seminar room (kwa mliosoma au mnaopafahamu Udsm ukishamaliza vimbweta vya hapa chini ya UDLS ili nivuke barabara kwenda hall 1) nikamuona yule mzee mbele yangu kama mita 30 hivi amesimama akiniangalia. Aisee nilitimuwa mbio kurudi SR nikawa napishana na wenzangu wanaorudi hostel, wengi waliniona kama nimechanganyikiwa, kufika SR niliyokuwa ninajisomea nikaingia na kujikausha huku nikitetwa. Rafiki zangu ambao niliwaacha wakanishangaa vipi mbona umerudi na ulisema hujisikii kusoma leo? Nikawaambia nawasubiri mmalize twende wote. Nikawa nasali kimoyo moyo na kunuia yale maneno aliyotuambiaga shekhe. Nilirudi SR kwasababu kuna room mate wangu wawili kwahiyo wakati wakutoka tutaongozana pamoja kwa moja mpaka room. Nikampigia simu mzee na kumweleza, pia nikampigia na shekhe. Shekhe akaniambia nisiogope kwasababu ameshadhibitiwa yule hawezi kunifanya chochote hata nikimwona tena niseme tu yale maneno na kesho niende kwake.
Nikampigia simu mdogo wangu kama kuna kitu kimemtokea, akanijibu hakuna chochote na anafurahia kesho yake anamalizia Ile dawa. Nikamwambia mi sijaoga Ile dawa na nimemuona yule mzee akiniangalia kwahiyo aombe ili lisije linamtokea huko nyumbani maana yeye ndiye aliileta Ile pete ingawa mawazo ya kuiuza nilitoa mimi.
Jimena
 
nitakua naandika kwa vituo tuvumiliane...nilishawahi andika thread ndefu saaana kipindi fulani simu ikazimaga ghafla kila kitu kikapotea

plan yetu kuingia mwezi wa 12 ilikua sababu ile ni miezi ya kula mavuno kwa wakazi wa Njombe wanajua huu ni msimu wa mvua na watu wengi ndio huwa wanaenda kutambika huko malori kwa magari ya kifahari...hata hao kuku huwa wengi na habari ni kwamba hata mali ndio inakua nyingi,inasemekana huwa inakuja mali na kupotea na ishara ni hao kuku kuwa wengi na kupungua

tulikua watano,1.mimi ,2.mobu (marehemu) ,huyu alikua mkinga alikua ana mishe za kupasua mbao kwa msumeno wa mkono shimoni(waliokaa njombe wanajua hii style ya kupasua mbao) 3.usungilo (marehemu) naye alikua na mishe za kupasua mbao,kwao ni bulongwa makete huko 4.mangi(alitoka mzima) huyu tulifanikiwa kutoka naye ila baada ya kutoka alikaa kama wiki moja akaanza onesha dalili za kuwa kichaa,na akawa kichaa kweli akaondokaga pale njombe hadi leo sijui habari zake (mungu amrehemu huko aliko) 5.mwaikambo (marehemu) jamaa wa mbeya alikua naye kaja kuhangaika na maisha tu Njombe.

Nirudi kwangu mimi kwanza kidogo,by then mimi nilikua mwajiriwa kiwanda cha chai,ajira siyo ya kitaalamu lakini kipato cha kuweza kuwanyanyasa hao jamaa zangu wote kiuchumi...wanangu sana,tunakutana kijiweni tunawa washkaji haswaa...kwenye hii safari mimi ndio nilikua master planer,sababu labda ya kuwa na kauli...mangi ndio alikua kama mwenye maono yote na alikua na njaa sana na hii mali...kwahiyo kupona kwangu mimi ilikua sababu sikua mstari wa mbele kuingia ndani kabisa ya pango kwenye hayo masanduku..

usiku tar 22/12 tukiwa na kila kitu cha kuingia kufungua masanduku tukaenda mdandu...fika tukiwa tushapiga mitungi yetu wanangu wako mbele mbele tukaingilia upande mwingine kabisa wa msitu ambako hata hakuna watu...hakuna kibaya hapo,tunakata majani kwa mapanga na miti midogo kupata njia...tumetembea zaidi ya masaa mawili msituni ili kuja unganisha na njia ya kule wanakoingilia watalii...na sababu tayari tulikua ndani hatukuonekana na wale wazee kule nje pamoja na walinzi wa msitu


wazee...mule ndani ni giza totoro,tochi zetu za mawe zile za kuitwa KURUNZI.,,,betri tatu tatu,tukafika tukaipata ile sasa njia ya ndani kabisa kwenda mapangoni...humu mchana kunatisha saanaaa,sasa imagine usiku inakuaje,hakuna story hapo na kama ni kuitana ni kwa sauti za chini sana,hofu ilikua kubwa na mvua sasa ikawa imeanza kupiga...baridi ni kali sana msituni

tumeendaaaa tukafika sasa kwenye mlango wa pango hapo ndio visa vilipoanzia...kule ndani usiku wanyama ndio wanakua active sababu ya ratiba labda za utalii so usiku pango ndio zinakua na fujo...tukaanza liingia pango bila uoga,mwendo kama wa dakika 30 hivi...huko ni kusikia tu sauti za wadudu na wanyama wadogo..tukamaliza hiyo zone ya zile pango za kitalii sasa tukawa kwenye mwisho ambako watu huwaga hawaruhusiwi kusogea zaidi ya hapo kwa imani kwamba watapotea hawatorudi.

na ndio habari ya vifo vya ndugu zangu watatu,kichaa cha mangi na ulemavu wangu inaanzia hapa...

ulemavu wangu wala usiwape wazo...ni kwamba niliumwa na nyoka huko nikafanikiwa kwa kudra za mungu tu kuokolewa kwa kukatwa mguu wa kushoto..

nitarudi..

Pole sana mkuu
 
Back
Top Bottom