Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

Shetani hanaga rafiki mkuu.
Shetani hana nafasi kwangu,dunia ni pana sana ndugu hata vitabu vitakatifu watu wanachanganyikiwa wakiona Nuhu alizini na bintiye,Rutu naye ilikua mipango yake yeye aliyeweka sheria,baya ama zuri si chaguo letu kamwe hatma huamua nimejifunza sana haya katika maisha usinyooshe kidole kwa mtu bila kujua Mungu anafanya lipi kwake
 
sawa mkuu kila la kheri..
Amin mkuu,nimeshare ili watu wengine wapate kujifunza jambo ama kuongeza ufahamu hakika pote nilipotembea kila aliejua anawaelewa hawa viumbe amebaki kushangaa ama kubisha na wanaojua hubaki kuamini kwa kushuhudia..Ila tukazie kuwa hawana mamlaka yoyote kwa mwanadamu na ukiwaelewa hawawezi kukusumbua hata kidogo imani ya mwanadamu kwa Mungu ni muhimu sana kuliko dini.
 
Mm nilikuwa natumia siku za kawaida,sikujua hyo nyingine,Shukran sana mkuu[emoji120][emoji120]
Siku hizi wadada kila mtu miski ndo habari ya mjini naona! hiyo asili yake tangu kale ni special kwa siku ya mwisho ya kuoga kutoka kwenye period.....inakata harufu na mabaki yote..
shukran zaidi pia mkuu karibu tena..
 
Kwakweli nimempenda mumewe hana shida hapa labda nae ustadh.

Ha hahahahaha ati ustaadh, hapana nimejifunza mwenyewe tu yangu mdogo na naendelea kuzifanyia kazi. Unajiskia raha na salama kama kila wakati mdomo wako utakuwa wenye kuleta dhikr na duaa..... Kila unachofanya tanguliza na duaa kutoka unapoamka mpk unapolala ivo ndivo tulivousiwa na Mtume wetu SAW. Dunia ina mengi hii tunoyaona na tusoyaona
 
Kweli unafeli wewe, hivi vistory vya keyboard vinakuogopesha!! Pole
Tunatofautiana aiseh,, binafsi mimi naogopa hizi issue za majini, ushirikina na huyu mdudu wa kuitwa nyoka.

Hizi ni kama story lakini zina uhalisia, na kama mtu hujawahi ku experience mambo kama hayo toka utotoni lazima uwe na wenge,,

Halafu hofu na emotion zinakua kubwa pale unasoma ila baada ya muda zinaondoka mfano sasa hivi naona nipo fiti kabisa
 
Mimi swala langu ilikuwa ni jini mahaba, nilikaa nalo kama miaka mitatu' ingawa mwaka wa kwanza nilikuwa nikijua ni ndoto za kawaida. Nime reply hapa maana na mimi niliogea dawa siku saba hili tatizo nikaondokana nalo ingawa nilipata vitisho vya kuogofya kidogo kabla ya kuagwa.
Wengine tukisimulia haya wanadhani ni utani au uongo, kumbe kuna watu tumekutana na vimbwanga vya hawa jamaa. Ile dawa nilikatisha kwa ujinga wangu mwenyewe maana imani yangu ilikuwa nusu nusu. Nusu niwe chizi kwa maneno ya wazazi na wanafunzi wenzangu chuoni.

Isingekuwa yule shekhe kuingila kati na kunichukua kwa visomo na kusimamiwa dawa (nyingine) nimalizie huko viziwani Z'bar, sasa tungekuwa tunaongea mengine.

Dhahabu naichukia, sitakuja kuivaa maana inaniletea kumbukumbu mbaya sana maishani mwangu ingawa nishaizoea hii hali.
 
Nilishawahi fanya hawakuwahi kurudi hadi nilipowahitaji mwenyewe,na mke wangu hajui kuhusu hawa na mara chache mwanzo wakati wanadondoka waliniomba nisiwe nawaita sababu mke wangu anaumia, baada ndio wakapata njia asihisi chochote au maumivu yoyote mara nyingi huwa wanaweza zungumza bila kuwa ndani yake kuja kwao hadi niite kuhitaji ushauri au kujadili jambo tofauti na hapo hawawezi kuja hata nikikaa mwaka bila kuhitaji kuwasiliana nao maana mara nyingi huwa wapo bize na shughuli za himaya yao mara nyingi huwa wanavamiwa na wenzao kuuwawa na majini wabaya, pia huwa napenda kuwajaribu mara kadhaa kwenda nao kwenye nyumba za ibada za kilokole na za kwetu rc kupima lengo lao kuomba Mungu kunipa muongozo,sijawahi ona tofauti kwenye maombi au nikishiriki nao vitabu vitakatifu pia kama nilivyokwambia mimi ni mtu wa namna gani sijawahi kuacha kumshirikisha Mungu kunipa busara katika hili kama naenda kinyume nae katika miaka yote hii sizani kama ameniacha kunipa maono kama ilivyo katika shari na kheri anavyonipa,Pia walaji wa mbuzi katoliki [emoji3][emoji3] hawajawahi kusema haifai kwao au inawasumbua sana sana kuna mmoja wao nae anaipenda sana kuila mama watoto akiandaa
Mh majini kwa walokole! (Labda kwa walokole feki)
Jini mpenda kitimoto!
Kwa mujibu wa biblia all demons are agents of Satan.
Kwakukaa nao miaka yote hiyo hukuwahi kuwauliza wanatokea wapi?
 
usijali kabisa...
kiuhalisia mkuu elimu iliyopokelewa imeingiliwa pia na uzushi na uongo mwingi sana....na wengi katika washirikina wamepenyeza mikono yao katika hilo....na nikuhakikishie hicho ulichokisema ukifuatilia wala sio dua ni uchawi na ushirikina....utakuta unaambiwa utaje jina la jini fulani mara elfu moja ewe fulani njoo au ukapewa ubani uwashe kwenye chumba kitupu kabisa mara uwashe mishumaa myekundu tena muda maalum usiku wa manane na mengineyo ya ajabu ajabu.....hizi si dua bali ni uchawi na ushirikina na wanaofanya wameshajua wao aakhirah hawana fungu lolote bali majanga yao yanawafaidisha duniani tu na mwisho wao huwa mbaya sana...
ni hivyo mkuu..
Asante Sana mkuu
 
Kwanza walikua wageni hawajawahi kushirikiana na wanadamu,walikuja kunisaidia tatizo la mke wangu liliisha baada ya kusumbuka sana kwa wataalamu mbali mbali na watu wa dini bila mafanikio,baada ya tatizo kuisha tukawa kama marafiki tu wanapenda kula vyakula ambavyo ni vya kawaida soda,biskuit,wali,ugali nk hawajawahi kuhitaji manukato wala kuhitaji chochote niwape,pia huwa nakauli kwao hii ndio inayofanya watu washangae utofauti huo kwani wakifanya jambo sijaliafiki nnauwezo wa kuwakosoa na wakaomba radhi na wao pia nikiwakosea huwa nawaomba radhi nimewafundisha vitu vingi pesa za huku hii sh hii na hii ni hii,kutumia simu kucheza games nk na upandaji wao mwanzo ilikua tabu kwa mke wangu maana atadondoka anachoka sana baadae wakafanyaje ila imekua tu nikiita kwa jina tu anakuja bila kudondoka au kuonyesha dalili yoyote hata tuwe kwa watu wengi mtu hawezi jua kwa wakati huo siongei na mke wangu yanafikirisha sana,sisi christian wao islamic hawajawahi kumzuia ibada mke wangu yoyote sana sana wao huwa wananikumbusha sana asiache ibada wana kipindi chao cha toba kila kikifika huwa hawafanyi lolote

Sent from my Infinix X573S using JamiiForums mobile app
Exciting mkuu, sasa hua unawaona physically au ni sauti Tu? Na kama ni physically hua wanakuja katika maumbo gani? Ngoma inogile
 
Hii sehemu ni kwa bibi yangu mzaa mama, panaitwa kisiba ni volcanic dam. Kabla hujafika kisiba kama kilomita moja kuna majengo ya zamani yalijengwa kwa mawe ambayo ilikua ngome ya wajerumani.
Hizo habari za kusema kuna mali chini kabisa kwenye maji hapo kisiba inasemekana ni kweli na inasemekana kuna wazungu walienda kuzichukua lakini walifia huko huko chini ya maji bila kutoka na chochote na ni Mara nyingi wazungu wamekua wakienda na kuweka kambi hapo.
Lazima pana mali. Nasikia wapo wazungu waliojaribu lakini walifanikiwa kuibua bunduki zikiwa bado mpya kwenye makaratasi. Pale pana mali. Ila nina wasiwasi wale wanaopiga kambi pale wanaweza wakawa wamekuja wamejidhatiti wametoa au ni chain ya waliohifadhi. Waliohifadhi hizi mali zote nasikia wanatunza kwenye vitabu jinsi ya kupafikia na namna unavyotakiwa kufanya ili kuzichukua salama
 
Back
Top Bottom