Tukio la Mtanzania kufariki Ethiopia: Kama kungekuwa na ubalozi wa Zanzibar huko labda ingesaidia

Tukio la Mtanzania kufariki Ethiopia: Kama kungekuwa na ubalozi wa Zanzibar huko labda ingesaidia

Miaka ya nyuma sana alifariki mtoto wa general wa jeshi hapa SA ubalozi ulitoa hela na vitu vyote baada ya kujua ni mtoto wa Mkuu na mambo mengi walisimamia wao...
General wa jeshi ni Mtumishi wa Umma Serikali inapaswa kugharamia mazishi yake, Mke wake na Watoto wa 4.
 
Kabla Muungano Zanzibar ilikua ina uwezo kuliko Oman Muungano umekuja kusimamisha Au kuua kabisa maendeleo ya Zanzibar
Sawa, Zanzibar ijitoe katika Muungano basi irudi kwenye maeneleo kuliko Oman.

Unaelewa kusema kabla ya Muungano Zanzibar ilikuwa na uwezo kuliko Oman hakuna maana sana, kwa sababu miaka hiyo Ghana ilikuwa na uwezo kuliko Singapore.

Na Ghana imedoroa na kupitwa na Singapore bila Muungano na Tanganyika!
 
Shida yako umeingiza uzanzibari kwenye suala la msiba. Hautuambii nani aliwapa taarifa ya msiba. Unakimbilia kuulaumu ubalozi kuwa ulikuwa unakudanganya na kuwapiga danadana kuwa hawana fungu la kuhudumia matukio kama haya badala ya kuhoji kwa nini serikali haitengi fungu kwa ajili ya dharura kama hizi. Wewe una mbunge wako, mweleze yaliyokupata ili akaibane serikali suala hili. Wao kama walipa taarifa na kuwasaidia mawasiliano na hospitali na shirika la ndege na kutoa makabrasha ya kuwawezesha kumchukua marehemu kutoka Ethiopia kuja nyumbani walimaliza wajibu wao. Ukiona ubalozi unachangia ni watumishi wanachangishana baada ya kuguswa na tukio. Sitashangaa kama mliwatukana kiasi cha kuwavunja moyo wa kuchangishana maana walijua mtasema kuwa ni fedha walizokuwa wanaficha.

Unazungumzia kusafirishwa marehemu kwa Cargo kama vile ni hiyana ya ubalozi wakati maiti zote zinasafirishwa kama cargo.

Wajibu wa kulipa gharama za hospitali na usafirishaji ni za kwenu wanafamilia kama vile inavyokuwa kwa mtanzania ambae ndugu yake amefariki Muhimbili na anataka amsafirishe akamzike Bukoba.

Poleni sana kwa msiba lakini mnatakiwa kuwa waungwana hata katika wakati mgumu kama huo.

Amandla...
Kumbe wengi humu hatujui haki zetu za kiraia.
Ndo. maana Raisi Kenyata(The Senior) aliwahi kumwambia Mwlm Nyerere ''Wewe unatawala maiti,'' Mimi natawala watu walio hai''
 
Huyu Mtanzania alikuwa safarini peke yake, Ethiopia haikuwa destination yake , alishushwa kwa dharura ya kuumwa ghafla na umauti ukamfika huko.Sisi hatuna familia wala jamaa kule.
Kama balozi yupo ,unadhani nanai awajibike kutowa msaada?
kama hawalipi gharama zote , hata kuchangia sehemu ya Gharama ubalozi hauwezi ?
aise kumbe ukiwa abiria wa ndege ya shirika Fulani ukipata shida, hata ukifa utakuwa umevunja mkataba, unappteza kila kitu"valueless"nauli uliolipa inakoma Mara Moja, bima ambayo ni incorporated kwenye nauli haina cha kumsaidia mwathirika. Shirika haliathiriki, Bima ni ya nini?
 
Huyu Mtanzania alikuwa safarini peke yake, Ethiopia haikuwa destination yake , alishushwa kwa dharura ya kuumwa ghafla na umauti ukamfika huko.Sisi hatuna familia wala jamaa kule.
Kama balozi yupo ,unadhani nanai awajibike kutowa msaada?
kama hawalipi gharama zote , hata kuchangia sehemu ya Gharama ubalozi hauwezi ?
Na ndo maana ikawa dharura na sio kwamba inatokea kila wkt l, hivyo walipaswa kwl kusaidia hiyo familia
 
Kilicho nifanya nilalamike ni kule kuona kuwa katika DHARURA isiyotazamiwa, ni lazima Balozi awajibike kwa raia wake.
Kwa tukio Hili napoteza imani na Jamuhuri Ya Tanzania na Balozi zake zote , ni kama vijiwe vya maskan.
Wezetu
Balozi wa South Africka alimsafirisha kijana wa miaka 15 aliekuja TZ kwa Baba yake aliyekuja kwa hiari yake na ridhaa ya mama yake ili asomee huku shule, baada ya mama mzazi kubadili mawazo kule cape Town na kuenda Home affairs na ku complain kutaka mwanae arudi South. Ubalozi ulimchukua kwa amri wakisaidiwa na Polisi TZ na kumsafirisha na kumfanyia shopping binti yule kabla ya kuondoka.
Huko ndio kujali raia. Yule mama hakuakiwa kuchangia chcochocte.
Hii nchi Imefubaa Mno, tumebobea kwenye siasa za maji taka na kujifanya wajuaji sana.
Ndomana Kenya tayari wana Katiba mpya sisi bado Bla bla kwa kuwa sisi Maiti
Mwakajana kuna kijana aliowa kule na kupata mtoto
Mwaka jana
 
Ni vitu ambavyo vinawezekana sema kwa Nchi zetu ikiwepo hela ya dharula wahusika hawataweza kupata kutokana na ubinafsi uliokuwepo...
Hela ya dharula unafikiri ubalozi mmoja unaweza kuhitaji kiasi gani kwa mwaka?

Unaelewa hiyo hela ya dharula inatokana na kodi ya wananchi na imepangiwa mambo mengi sana?

Unaelewa kwamba hizo balozi tayari zina madeni ya kulipa kodi za nyumba na mishahara ya watu?

Kwa nini Watanzania wengi tunapenda kuivika serikali mzigo wa matatizo yetu wenyewe?

Unajua GDP per capita ya Mtanzania mmoja wa kawaida kwa wastani ni kiasi gani na gharama za kusafirisha maiti ni kiasi gani?
 
Na ndo maana ikawa dharura na sio kwamba inatokea kila wkt l, hivyo walipaswa kwl kusaidia hiyo familia
Kifo ni kitu ambacho kila mtu anajua atafariki, sasa kinakuwaje dharula?

Kila mtu aliye nje akifa tukisema ni dharula serikali ilmsaidie, itaweza kusaidia?

Ikisaidia wengine na kuacha wengine, hapo si ndiyo mwanzo wa malalamiko ya kwamba watu fulani wanapendelewa?

Hakuna logic ya serikali kulipia nauli ya maiti kutoka nje, hili ni jambo lenye gharama kubwa sana na mara nyingine watu ambao si wasafiri hawajui kwamba nauli ya maiti ina gharama mara nyingi sana kuzidi nauli ya mtu hai.

Watu wajiwekee akiba, wakate bima, wachangishane rambirambi, wasaidiane, serikali labda itasaidia ku coordinate mambo na kufuatilia lakini kuipa serikali mzigo wa gharama hizi ni jambo lisilowezekana kwa bajeti hafifu za balozi zetu hizi.
 
Ngoja yaje kukuta, siku utaukumbuka huu uzi.
Haya masuala yanajadilika kiuchumi, habari ya ngoja yakukute hazina tija.

Kama ubalozi hauna bajeti hauna bajeti tu.

Na hapa tunaelimishana kwamba ubalozi hauna wajibu wa kurudisha maiti ili waliofikiri huu ni wajibu wa ubalozi wajiandae kabisa yasiwakute.
 
Nimeyasema haya nikiwa na Uchungu mkubwa wa kuona kuwa MUUNGANO WETU umekuwa kikwazo kwa raia wa Zanzibar .HILI NALO NI MOJA YA CHANGAMOTO ZA MUUNGANO kwenye mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa. We are not treted equaly.
Na kweli.

Kumbe mada yako imeegemea kwenye agenda maalum na siyo tukio la msiba lililotokea.
Unautumia msiba wa ndugu yako kusimamia ajenda ambayo tayari unayo kichwani.
 
Wengi watashangazwa na na mada ya hapo juu.

Taratibu fuatilia

Tare 21/04/2021 siku ya juma tano, Dada yangu Fatma Said alifariki dunia Nchini Ethiopia akitokea Dubai kuja Zanzibar (Tanzania).
Akiwa ndani ya ndege 'Fly Dubai' aliumwa ghafla na kuilazimisha ndege hiyo kutua kwa dharura nchini Ethiopia ikiwa nio kiwanja cha karibu kwa walipokuwa.

Tukio hili la kumshusha pale ni sehemu ya taibu za ndege inapotiokea dharura. Mgonwa alipelekwa Hospitali na Kufarikiduni muda mchache baada ya kufika hospitali.

Yamkini serikali ya Ethiopia iliarifu ofisi ya Kibalozi ya TANZANIA kwa hatua stahiki.

Wana familia nao tulipopata habari tuliwasiliana na Balozi ili kujua hatua gani zifanywe ili Mwili wa marehemu urejeshwe Nyumbani kwa mazishi. Balozi wa Tanzania alianza kutudanganya na kutupiga danadana eti akidai kuwa hana FUND za kugharamia matukio ya aina hii.

Hatimae ilitubidi wanafamilia tulipishwe Gharama za Hospitali, Kusafirisha mwili na kila kilichohusu kusafirishwa kwa mwili husika.

Mwili ulifika jana tarehe 27/04/2021 kwa ndege ya Cargo ya Ethiopia Air Line.

Nilianza kujiuliza NINI FAIDA YA KUWA NA BALOZI NCHINI ETHIOPIA? Lakini mara nikakumbuka kuwa kama Zanzibar ingelikuwa na Ubalozi wake kule tungelipata matokeo tofauti?

Ilishawahi kutokea wanafunzi wa Tanzania walioko nje nchi fulani(siitaji) walipungukiwa na Masurufu ya matumizi, Wale wa Zanzibar wakatumiwa na SMZ fedha za kujikimu na wale wa Bara wakalazimika kurudi au familia zao kutuma fedha.

Nimeyasema haya nikiwa na Uchungu mkubwa wa kuona kuwa MUUNGANO WETU umekuwa kikwazo kwa raia wa Zanzibar .HILI NALO NI MOJA YA CHANGAMOTO ZA MUUNGANO kwenye mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa. We are not treted equaly.

Namuoba Waziri wa mambo ya nje Ahusike na tukio hili la Ethiopia kwani Ubalozi wa TZ haukusaidia lolote kifedha katika jambo hi la Marehemu.

Isije ikatumwa Invoice ya kuonesha kuwa Ubalozi ulitumia fedha,itakuwa ni Upigaji wa fedha za serikali.

Nawakilisha.

Asikwambie mtu wazanzibar wana hutu sana ,ukiona mzanzibar ana roho mbaya basi huyo mzanzibar wa magomeni au ilala.

Wabara wana umimi sana ,sasa serikali inashindwa vipi kugharamikia tukio kama hilo? JMT hawana funds za dharura?
 
Ubalozi wa Zanzibar au Ubalozi wa Tanzania?

Shina la malalamiko mkuu ni kuona wazanzibari wanatengwa au?

Poleni sana kwa msiba wa sista aisee
Pole saana dada yangu yaani viongozi wa Bara, are too selfish ,hili tukio la wanafunzi wa kitanzania kutelekezwa wenye asili ya bara nalikumbuka saana ....wewe kama hujali raia waliokuweka hapo ,you will remain useless leader forever ........
 
In the famous words of President John Fitzgerald Kennedy of The United States of America.

""Ask not what your country can do for you, ask what you can do for your country."
 
Tanzania NI MOJA.
Zanzibar na tanga nyika tulishazizika.

Kwng mm naona mtoa post ameleta ubaguzi wa wazi wazi.

Kusema kama ingekuwa ubalozi wa Zanzibar wangesaidiwa.
Maana wanasaidiwa sn na SMZ kuliko na serikali ya Tanzania.

Amesahau kama Zanzibar ni ndani ya Tanzania...
 
Kifo ni kitu ambacho kila mtu anajua atafariki, sasa kinakuwaje dharula?

Kila mtu aliye nje akifa tukisema ni dharula serikali ilmsaidie, itaweza kusaidia?

Ikisaidia wengine na kuacha wengine, hapo si ndiyo mwanzo wa malalamiko ya kwamba watu fulani wanapendelewa?

Hakuna logic ya serikali kulipia nauli ya maiti kutoka nje, hili ni jambo lenye gharama kubwa sana na mara nyingine watu ambao si wasafiri hawajui kwamba nauli ya maiti ina gharama mara nyingi sana kuzidi nauli ya mtu hai.

Watu wajiwekee akiba, wakate bima, wachangishane rambirambi, wasaidiane, serikali labda itasaidia ku coordinate mambo na kufuatilia lakini kuipa serikali mzigo wa gharama hizi ni jambo lisilowezekana kwa bajeti hafifu za balozi zetu hizi.
Anyway sote tutakufa tuu uzuri tukifa hatujui yanayoendelea
 
Wengi watashangazwa na na mada ya hapo juu.

Taratibu fuatilia

Tare 21/04/2021 siku ya juma tano, Dada yangu Fatma Said alifariki dunia Nchini Ethiopia akitokea Dubai kuja Zanzibar (Tanzania).
Akiwa ndani ya ndege 'Fly Dubai' aliumwa ghafla na kuilazimisha ndege hiyo kutua kwa dharura nchini Ethiopia ikiwa nio kiwanja cha karibu kwa walipokuwa.

Tukio hili la kumshusha pale ni sehemu ya taibu za ndege inapotiokea dharura. Mgonwa alipelekwa Hospitali na Kufarikiduni muda mchache baada ya kufika hospitali.

Yamkini serikali ya Ethiopia iliarifu ofisi ya Kibalozi ya TANZANIA kwa hatua stahiki.

Wana familia nao tulipopata habari tuliwasiliana na Balozi ili kujua hatua gani zifanywe ili Mwili wa marehemu urejeshwe Nyumbani kwa mazishi. Balozi wa Tanzania alianza kutudanganya na kutupiga danadana eti akidai kuwa hana FUND za kugharamia matukio ya aina hii.

Hatimae ilitubidi wanafamilia tulipishwe Gharama za Hospitali, Kusafirisha mwili na kila kilichohusu kusafirishwa kwa mwili husika.

Mwili ulifika jana tarehe 27/04/2021 kwa ndege ya Cargo ya Ethiopia Air Line.

Nilianza kujiuliza NINI FAIDA YA KUWA NA BALOZI NCHINI ETHIOPIA? Lakini mara nikakumbuka kuwa kama Zanzibar ingelikuwa na Ubalozi wake kule tungelipata matokeo tofauti?

Ilishawahi kutokea wanafunzi wa Tanzania walioko nje nchi fulani(siitaji) walipungukiwa na Masurufu ya matumizi, Wale wa Zanzibar wakatumiwa na SMZ fedha za kujikimu na wale wa Bara wakalazimika kurudi au familia zao kutuma fedha.

Nimeyasema haya nikiwa na Uchungu mkubwa wa kuona kuwa MUUNGANO WETU umekuwa kikwazo kwa raia wa Zanzibar .HILI NALO NI MOJA YA CHANGAMOTO ZA MUUNGANO kwenye mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa. We are not treted equaly.

Namuoba Waziri wa mambo ya nje Ahusike na tukio hili la Ethiopia kwani Ubalozi wa TZ haukusaidia lolote kifedha katika jambo hi la Marehemu.

Isije ikatumwa Invoice ya kuonesha kuwa Ubalozi ulitumia fedha,itakuwa ni Upigaji wa fedha za serikali.

Nawakilisha.

Ni makosa makubwa kuandika message/post ukiwa na emotions, kwa sababu you will end up kuonyesha ujinga wako.
 
Mwaka jana Nchiya Oman Illeta Ndege Kuchukua raia wake wote waliokwama kwa sababu ya Corona na kuwarudisha Oman Free of charge.
Hii ndio kujali kwa nchi na raia wake.
Tiizii bola kunakucha na kunakuchwa ndio maahana hata kile kimbunga kikaonà chaja kumaliza tu nguvu zake bure kwa walking deads wa Tz kikahamja kiingie mitini
 
Mwaka jana Nchiya Oman Illeta Ndege Kuchukua raia wake wote waliokwama kwa sababu ya Corona na kuwarudisha Oman Free of charge.
Hii ndio kujali kwa nchi na raia wake.
Tiizii bola kunakucha na kunakuchwa ndio maahana hata kile kimbunga kikaonà chaja kumaliza tu nguvu zake bure kwa walking deads wa Tz kikahamja kiingie mitini
 
Back
Top Bottom