Tukiwa tunasema Kanisa Katoliki ndiyo Alama rasmi ya Ukristo Tanzania na Duniani muwe mnatuelewa tafadhali

Tukiwa tunasema Kanisa Katoliki ndiyo Alama rasmi ya Ukristo Tanzania na Duniani muwe mnatuelewa tafadhali

KANISA NI MOJA TU KATOLIKI TAKATIFU LA MITUME....Wengine wanazuga tu na Vikundi vyao!!
 
Kwanini Wakristo msiokuwa Wakatoliki mna Chuki na Roho mbaya mno? Kwani hayo Madhehebu yenu hayakutokea huko Ukatolikini?

Au kwakuwa kuna Utafiti ulifanywa na kusema Wakatoliki wengi ndiyo very Intelligent na ndiyo Intellectuals zaidi duniani?
Ni ujinga uliopitiliza kujivunia dhehebu badala ya kujivunia Yesu Kristo. Yesu hakuwa mkatoliki,Mluteli wala Muumini wa dini ya kiyahudi. Ndio maana aliingia hekaluni kufundisha na sio kufundishwa.

Yesu alikuja kufundisha "kweli"ambayo ndio Tabia ya Mungu Baba. Nini tufuate na nini tusifuate km wanadamu ili kuishinda dunia. Haya madhehebu yameundwa kwa mtazamo wa kibinadamu na si Kristo. Ndio maana mafundisho yao yanapishana. Huyu ubatizo wa maji mengi yule ubatizo wa kikombe. Huyu ubatizo wa watoto kule ubatizo wa watu wazima.Sa je tumtazame mwanadamu na mafundisho ya madhehebu au tumtazame Kristo?

Ukifanye yale ambayo Yesu kaagiza kufanya au usipofanya yale ambayo Yesu Kristo alikataza huo ndio UKristo na dhehebu au dini njema.

Biblia haijataja Katoliki,Lutheri au Anglican. Bali kila mtu analazimisha kwa kuunganishi tafsiri "dots"ili ionekane dhehebu lake ndo sahihi na la kweli.

Yesu alipoondoka aliacha kanisa( kusanyiko) la watu wanaoamini mafundisho yake au Wakristo.Wala hakuacha hizi vurugu za madhehebu ambapo kila mtu anaamini lake.
 
Ndio ukweli
Hata Papa alipotoa matamshi yenye mwelekeo wa kuunga mkono mashoga ilionekena wakristo wote ndio msimamo wao.
Hata Rwanda pale wapadre na watawa waliposhiriki mauwaji ilionekana wakristo wote wameshiriki.

Hivyo vyeo vya uaskofu, havipo kibiblia,
Huyo sheikh anatueleza Mambo yaliyo njee ya biblia
papa amesema wapi anaunga mkono mashoga na kanisa likaridhia? Mapadre wangapi na watawa walioua watu Rwanda? Mnapenda sana kujifurahisha kwa kusema uongo
 
Kanisa Katoliki ndilo kanisa halisi linaloonesha ukristo wa kwelikweli. Nimejifunza nidhamu ya hali ya juu ya mababa askofu, nidhamu ya hali ya juu kwa waumini dhidi ya viongozi wao- Alhad Mussa Salum, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Chanzo: bavicha.tz

Ukiona mpaka Muislamu anasifia Jambo tena la Kikristo jua kuwa anamaanisha na ameshajiridhisha vya Kutosha tu.

Katoliki tu ndiyo kila Kitu Ulimwenguni.
Soma historia ya Ukristo ndugu. Kanisa la Romani katoliki ni CHUKIZO mbele za Mungu. Kanisa hili ni karakana ya Shetani-ibilisi. OKOKA.
 
Kanisa Katoliki ndilo kanisa halisi linaloonesha ukristo wa kwelikweli. Nimejifunza nidhamu ya hali ya juu ya mababa askofu, nidhamu ya hali ya juu kwa waumini dhidi ya viongozi wao- Alhad Mussa Salum, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Chanzo: bavicha.tz

Ukiona mpaka Muislamu anasifia Jambo tena la Kikristo jua kuwa anamaanisha na ameshajiridhisha vya Kutosha tu.

Katoliki tu ndiyo kila Kitu Ulimwenguni.
Sasa unategemea mwislamu wa kweli anaweza kulisema vibaya Kanisa la Roma. Wote wawili ni machukizo mbele ya Bwana Yesu Kristo.
 
Ufafanuzi jana usiku nilikua naangalia TBC walikua wanaelezea kanisa fulani la RC Kibosho aise kuna michoro sijaielewa

Nimeona Mchoro una duara then ndani ya duara kuna Pembe tatu na Jicho kati kati....[emoji3064][emoji3064]Aisee..

Ngadedema!!!!!
 
Rumi ya kipagani hadi Rumi ya kidini. Shida watu hawataki kusoma biblia, pia mazoea.
 
Kwanini Wakristo msiokuwa Wakatoliki mna Chuki na Roho mbaya mno? Kwani hayo Madhehebu yenu hayakutokea huko Ukatolikini?

Au kwakuwa kuna Utafiti ulifanywa na kusema Wakatoliki wengi ndiyo very Intelligent na ndiyo Intellectuals zaidi duniani?
Bwana Yesu Kristo kamwe hakuanzisha dini/Kanisa na wala hakuacha dini/Kanisa lolote hapa Duniani; bali, alileta habari njema ya WOKOVU kwa watu wote. Uroma katoliki/ Upapa umeanzishwa miaka 500 baada ya Bwana Yesu Kristo pamoja na mitume wake wote kuwa walikwisha ondoka Duniani. Ni dhehebu lililoanzishwa na waitaliano kwa maslahi ya kisiasa na kiuchumi ya waitaliano, baadaye wajerumani (Lutherani), waingereza (Anglikani) wakaiga. Romani katoliki haina uhusiano wowote na Kanisa/Ukristo wa karne ya kwanza wala mitume wa Bwana Yesu Kristo. Wanajibambika tu.
 
Uislamu na ukatoliki unaendana kwa kiasi flani
Wote ni Wapinga Kristo; tofauti yao ni kuwa waislamu wanampinga waziwazi kuwa siyo Mungu; wakatoliki wanampinga kwa kumwabudu kinyume na Mafundisho yake (ibada za sanamu, wafu, kuruhusu dhambi Kanisani, nk.). Ila tunawaombea ili wachukue hatua ya KUOKOKA kwani kila mtu atavuna alichopanda.
 
Hivi nyie katoliki mnasshindwaje kushawishi haki na time huru vinginevyo ni hovyo tu
 
Nilifurahi kuisikia radio moja maarufu iliyopo iringa inayofanya vizuri mikoa ya nyanda za juu kusini, ikielezea namna ambavyo ustaadhi mmoja alivyoshiriki kuwahamasisha jirani zake ambao walikuwa ni wakristo kufunga ndoa badala ya kukaa kiuasherati. Hilo nililiona ni Jambo jema ambalo nadhani kila mwenye kumjua Mungu angelipenda. Hivyo tusisite kubainisha yaliyo mema ili tujichumie thawabu
 
Hosea 4:6 Uzi unaburudisha sana huu.

Jinsi WAKRISTO wanavyoendelea KULIWA na MADHEHEBU ambayo si MITUME wala KRISTO aliyeyaanzisha.

NOTE: Kila mtu anakwambia dhehebu lake ni la kweli, MUULIZE, JINA LA DHEHEBU LAKE LIMETAJWA WAPI KATIKA BIBLIA?

Hapo ndiyo kigugumizi na kumezeshwa MATANGO MWITU kunapo anzia.
 
Wote ni Wapinga Kristo; tofauti yao ni kuwa waislamu wanampinga waziwazi kuwa siyo Mungu; wakatoliki wanampinga kwa kumwabudu kinyume na Mafundisho yake (ibada za sanamu, wafu, kuruhusu dhambi Kanisani, nk.). Ila tunawaombea ili wachukue hatua ya KUOKOKA kwani kila mtu atavuna alichopanda.
VYEMELO Mkuu. Acha utundu.
 
Biblia hpi na mstali hupi?
Kwani Biblia Takatifu ni Neno Pekee la Mwenyezi?!
Mbona Biblia Takatifu Inajishuhudia yenyewe!!
[emoji116][emoji116]
YN. 20:30 Basi kuna ishara nyingine nyingi alizozifanya Yesu mbele ya wanafunzi wake, zisizoandikwa katika kitabu hiki.

YN. 21:25 Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa.

Hapa ndipo kanisa Katoliki tunamshukuru Mungu sana.
Kanisa linaamini kwenye
1.Maandiko Matakatifu
2.Mapokeo Matakatifu
3.Mamlaka


Ninyi mmeng'ang'ania kipande kimoja kweli mtafika kweli naona kwa mbali mnaishia njiani[emoji2301][emoji24][emoji24]

Kuhusu Vyeo mbona Yesu Mwenyewe Amekaimisha Mamlaka yake kwa Kanisa?!
[emoji116][emoji116]
MT. 16:18-19 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda. Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lo lote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni; na lo lote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni.
 
Ya MUSA na Ya FIRAUNI yanastaajabiwa wakati gani!?!!

Wakati ule ambao tunazidi KUTOA tulichonacho kama SADAKA tukiwaaneemesha MASHEHE, MAPADRI, MAASKOFU, WACHUNGAJI NA WAINJILISTI huku sisi tukizidi kuwa maskini wa kutupwa kila kuitwapo leo.

Wakati tukiwanunulia MAGARI na KUWASOMESHA wao huku watoto wakishindwa kumudu hata gharama ya kununua RIMU PAPER 1 kwenye shule za KAYUMBA.
 
unawasema hawahawa Roma empire ndugu zake na Paulo....au unazungumzia wakatoriki gani... kama hawa wazee wa vatican ngoja tuyaache tu kama yalivyo....
 
Back
Top Bottom