Tukubali au tukatae kwenye hii sayari ya Dunia katika nyanja ya Soka hakuna kama Pele wa Brazil

Mshambuliaji akiguswa kidogo tu penalty
Zamani haya mambo hayakwepo
 
Mpaka mastaa siku hizi wana sheria za kuwalinda na mabeki
Ndio maana mabeki hawafanyi kazi yao
 
Binafsi duniani sijaona mtu kama Messi,,na haitokuja kutokea
 

Hayo ni mawazo yako tu mkuu, na kujifanya unaujua mpira zaidi ya wengine. Kwaheri!
 
Ukitaka kujua watu wenye chuki na mfalme Messi fuatilia commets zao utajionea. Yote kwa sababu kawagalagaza wazee na vijana 😀😀
Ukiambiwa toa takwimu unabaki unabisha tu
Yaani ukitoa match za kirafiki za santos na taifa lake la brazil
Match za kimashindano za pelle amefunga mabao karibu 800
Sasa ukitoa kwa messi namna hiyo si ajabu akabaki na magoli 250
Hapo kwa mbio hamfikii pele
Sio kwa chenga
Sio kwa lolote
Ingia you tube uwalinganishe utaacha ubishi
 
Siku hizi mpira umekuja kuwa na judgemental za kipuuzi sana ukimuambia mtu flani ni mchezaji mzuri anakuuliza ana magoli mangapi?
 
Siku hizi mpira umekuja kuwa na judgemental za kipuuzi sana ukimuambia mtu flani ni mchezaji mzuri anakuuliza ana magoli mangapi?
Sio magoli tu ndugu vitu vingi alivyokuwa navyo pele kwa sasa hakuna mchezaji football anayemkaribia
 
Watu mnaweza kudhani nina miaka 70 kwa kumpamba pele hapana
Mi mwenyewe ni kijana ambaye hata 27 sina ila nilikuwa mbishi pia kuamini hakuna zaidi ya messi
Mpaka niliposhawishika kuingia YouTube kuwaangalia watu watatu wanaotajwa sana
Pele
Messi
Maradona
Kwa nilichokiona nilimweka pele namba 1
Messi 2
Maradona 3
Nikiri tu maradona hakunishawishi kabisa kati ya huyu pele na messi
 
Takwimu, takwimu, takwimu! Ili takwimu ziwe na maana Mpira wa 1956 pamoja na sheria zake, uimara wa timu pinzani na mbinu za mchezo za wakati huo basi ziwe sawasawa na za wakati huu unapotaka kumlinganisha Pele na wengine wa wakati huu. Kinyume chake unaweza kukuta Pele alishapitwa na wengi kimpira. Takwimu, takwimu, takwimu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…