Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Tatizo unasikiliza watu...
Hao watu ndio wanakwambia sema hivi...nia na madhumuni yenu nikupotosha Uma na kuficha maovu kwakutetea Matumbo yenu
Kwa hiyo braza kaka, nimefatilia sana hoja zako lakini sijaelewa exactly ulikua unataka kufikisha nini kwa sisi hadhira, yaani Clouds wamlipe Noorah au Clouds wafungwe kwa ajali ya Noorah au point yako ni nini hasa hebu ongea na mimi nakusikiliza.WEWE hizo Habari za Sandra anzisha Uzi wako.Mimi najuana na Noorah naemwongelea hapa....
Mnajadiri mje mpoteze vipi ukweli huu.....
Vaeni Utu Vueni Viatu
Mkuu, hivi mnapata faida gani kuchonganisha watu au kupotosha ukweli. Unadhani unaweza wachafua Clouds kwa stori za 2005? Ameshindwa Shigongo mtaweza nyie? endeleeni. Hakuna msanii aliyelalamika hajalipwa hela za show.Yaani umeona comment imetaja mbuyuni kesho utasema ulikuwepo eneo la tukio...Halafu Fanya utafiti ...usipende kutumika ndugu yangu.
hatari sana hiiSIKUMBUKI KAMA AJALI YA NOORAH ILIKUWA NA UHUSIANO NA FIESTA
NOORAH hakupata ajali akiwa kazini alipata ajali akiwa na demu wake (sandra)
nakumbuka gari ilikuwa rav 4 huyo demu wa noorah alikuwa anasoma uganda (Kenya ndio sahihi nimesahihishwa) na alikuja tanzania bila kwao kujua
lengo lilikuwa kumuona bwana ake akiperfom sasa baada ya noorah kumaliza show yake wakawa wanarudi wote wamelewa na wako speed ulitokea ubishani
maana noorah alikuwa anataka kumrudisha yule demu kwao(oysterbay) na yule demu hataki kurudi kwao maana nyumban kwao walikuwa wanajua yupo shule Kenya
katika mabishano huku gari ikiwa speed yule demu aliisukuma gear kwenye parking
kama ujuavyo gari za zaman hazikuwa na sensor za kutema gear ya packin gari inapokuwa speed kali basi ilifanya tairi zote nne kufunga ghafla na gari ilibingirita mara nane
noorah hakufunga mkanda alitupwa nje ya gari na akapata ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu alikuwa anamkumbuka huyo demu tu...
na siyo kwamba alijipeleka hospital noorah alitoka eneo la ajali akiwa hajitambui kabisa alikuja kupata fahamu akiwa hospital
alikaa sana muhimbili hadi alipokuja kupona na kuendelea na mziki pamoja na masomo (IFM)
hawa jamaa fiesta wana mapungufu yao ila sometimes mnazidisha kuwaonea
umaarufu mkuuAiseeeee Jamaa alikuwa anakula MADEMU wa OYSTERBAY 😳😳😳😳.
fake id hizi mkuu unaweza kuta anaesimulia ni mzazi, ndugu, rafiki au mkeo kabisaJF usipoangalia, kuna siku utakuta mtu usomjua anasimulia historia yako tena kwa usahihi kabisa.,! [emoji23]
Jf kiboko ya magonjwa yote sugu na inarudisha nguvu za kiume.!!😂😂fake id hizi mkuu unaweza kuta anaesimulia ni mzazi, ndugu, rafiki au mkeo kabisa
Mkuu tupe side yako ya stori? Maana naanza kukuamini unajua mengi zaid ya haya yanayosemwa. Wenzako wamefunguka, wewe maliza Mkuu.Mpuuzi ashaleta Wasafi huku.....
Nakwafukra zenu mtaendelea kutumika ila mwisho mtamwagwa.....
Oneni aibu kutumika kufumba ukweli uliowazi ....
SIKU yakiwasibu sijui nini mtajibu
Huyo Iddy Mwanaharamu ni mtu ambaye uwa anaandika habari zake kutoka kwa chanzo husika kwa kufanya nacho mahojiano, ameshaandika mengi tu kuhusu wasanii ukiacha hayo mambo ya Noorahmimi na wewe nani anatumika 😂😂
wewe umecopy habari fake kutoka kwa mamluki wenzako umekuja kupaste hapa
ila ukasahau kufuta pale mwisho palipoandikwa na iddy mwanaharamu maana inaonekana huyo ndio aliandika hii habari
asante mzee muanzisha thread atakuwa kwa sasa anachungulia tu, hili ndio tatizo la kuwa na data kidogo
basi safari hii alichemsha maana hii ajali iko well known... ilipatikana barabaran tu na jamaa alikuwa yupo na private car na demu wakeHuyo Iddy Mwanaharamu ni mtu ambaye uwa anaandika habari zake kutoka kwa chanzo husika kwa kufanya nacho mahojiano, ameshaandika mengi tu kuhusu wasanii ukiacha hayo mambo ya Noorah
Usichanganye mambo, jaribu kuafatilia mambo kwa umakini kabla ya kukurupuka. Straight Music na Summer Jam/Fiesta ni vitu tofauti.Wewe jamaa Muongo sana. Baba Stylz hakupata ajali kipindi cha fiesta. Ninachojua alipata ajali pale mbuyuni Oysterbay akiwa anatokea Bilicanas. Na sababu ya ajali yalikuwa mabishano yake na mpenzi wake. Mpenzi wake alikuwa anataka waende maisha club huku noorah akitaka waende nyumbani. Kilichotokea yule dada akaweka gear kwenye "P" galfa, gari walokuwa wanatumia ilikuwa auto. Wakapata ajali na akakimbizwa Muhimbili. Baada ya kuzinduka akawa anakumbuka wimbo mmoja tu wa Hawa Mademu Vipi. Akapewa mida wa kupumzika ili akili ikae sawa. Kipindi hicho alikuwa anakaa Makumbusho. Kutokana na kuumwa akahamia kule kwa Ali Maua jirani na akina Roy producer.
Kwanza umedanganya haikuwa Fiesta kipindi hicho bali ilikuwa inaitwa Straight Music Klimax full shangwe. Wadhamini waki wa sigara ya SM.
Noorah hakuwa kwenye orodha ya wasanii hata Mr Nice hakuwepo. Aliyekuwa kwenye orodha kwa upande wa bongo fleva ni Albert Mangwea ‘Cow Boy’, Joh Makini ‘Mwamba wa Kaskazini’, Mr.Blue ‘Kabaizer’ Prof Jizey na maswahiba wawili AY na Mwana FA.
Hayo maelezo anayatoa kwa Noorah, basi yeye ndio anakosa kwa kumpatia maelezo ya uongobasi safari hii alichemsha maana hii ajali iko well known... ilipatikana barabaran tu na jamaa alikuwa yupo na private car na demu wake
sasa sioni fiesta hapo inaingiaje mkuu ndio kitu mleta mada alichoshindwa kuthibitisha maana anasema jamaa alipata ajali kazini
Unaweza kuthibitisha kwamba hayo maelezo kayatoa kwa Noorah?Hayo maelezo anayatoa kwa Noorah, basi yeye ndio anakosa kwa kumpatia maelezo ya uongo
Jina lipo nenda kamtafute Huyo Iddy Mwanaharamu then atakujibu yote ambayo una shaka nayo.Unaweza kuthibitisha kwamba hayo maelezo kayatoa kwa Noorah?
hapana ukumbuke habari haijaletwa direct na the so called iddy mwanaharamu...Hayo maelezo anayatoa kwa Noorah, basi yeye ndio anakosa kwa kumpatia maelezo ya uongo
alafu wanamuongelea iddy mwanaharamu na habari humu imeletwa na mtu mwingine....Unaweza kuthibitisha kwamba hayo maelezo kayatoa kwa Noorah?
Hakuna alicho edit kama ni makosa basi ni ya huyo mwandishi na chanzo chake, maana mimi binafsi nilisoma andiko la muhusika mwenyewe(iddy Mwanaharamu).hapana ukumbuke habari haijaletwa direct na the so called iddy mwanaharamu...
ukute huyu aliyeleta kapindisha ukweli kwa kuedit..
noorah hawezi kuongea uongo kama huo... na kama ingekuwa hivyo basi asingepanda jukwaa la fiesta 2016 kule mkoani kwao anapokaa sasa