Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

due to world shortage,in vegetable oils,the then british labour government,emanicipated The Tanganyika Groundnut scheme,hii ilikuwa late 1940's.it was decided to grow peanuts in kongwa(dodoma) on a large extensive scale,feasibility studies ziliconclude mradi ukikamilika,tanganyika itakhidi mahitaji ya vegetable oil duniani.the project cost a COLLOSSAL £ 49 million,this was a massive project.it FAILED,and almost led to the downfall of the labour government.huu mradi it is still talked about today,sababu it was massive.had the project succeded DODOMA and tanzania in general would have greatly benefited
 
Hii Thread nikiisoma najiskia raha na kupumizisha kichwa na maskendo ya EPA etal.......Big up wachangiaji na muanzisha Thread.....
 
jamani mbona our fathers,and grandfathers waliopigana the great war,for queen and country,tumewasahau,i am sure lazima katika second world war,tulikuwa na mashujaa wazalendo,nakumbuka one or two,the late mzee barakati,the late makutika.nakumbuka nikiganda na bumbuwazi wakati marehemu mteketa akinieleza exploit zake as a signaller in varios theaters of war notably mauritius,ethiopia,south africa,burma.akiwa sudan alimuona captain mweusi for the first time,alikuwa mnubi,jitu la foot saba na ushee
 
Wazo zuri sana Field Marshall ninaomba ulikuze liwe ni kuanzisha na kutunza VIRTUAL NATIONAL PICTURES MUSEUM GALLERY ONLINE!
 
[media]http://rspringwater.com/images/EastAfrica_UhuruParadeGround_jpg.jpg[/media]


kwata la uhuru Tanganyika 1961....click to enlarge the picture!

Aaah mkulu umenikumbusha kofia za tarbushi hapo.......Kumbe zilikuwepo kwa armed forces pia....Dah si unaona historia ilikuwa imeingia vumbi kichwani mwangu sasa. Ahsante mkuu...
 

Wacha weee picha za ndege zimenikumbusha looongi....mzee akiondoka au akirudi ilikuwa tunagombania kwenda kumsindikiza au kumpokea mi na masiblings wangu....ilikuwa lazima ugomvi, hadi faza na maza wakaweka zamu...dah zamani wakulu.
 
nasema tena shukrani wakuu wa thread hii...mnakumbuka wakati wa kumaliza mgambo ile nyimbo?
kumaliza mgambo wetu ni kazi ngumu saaana!(*2)
Hata ndege wa ngani wanaruka ruka(*2)

siku hizi hata jeshi wametoa sia ajabu vijana wanakosa uzalendo....
 
...enzi hizo, East African Airways wanatesa na Dakota ilokuwa inatua mpaka Kilwa Airport!, halafu kulikuwa na DC-8, DC-9 na DC-10 ilokuwa na regular trips to London!

Unajua the sad news ni kwamba ni Nkurumah, ndiye aliyepigana sana kuiuwa EAA, na aliweza kum-recruite Njonjo akishirikiana na Makaburu wa Africa Kusini, na Muingereza Tiny Rowland,

Nkurumah, alitaka kuwe na muungano wa Afrika nzima, huku yeye akiwa rais wake wa kwanza, Mwalimu akawa a big competititor wake kwa sababu, tayari Mwalimu alikuwa na Muungano wa Tanzania, na EAA hivyo viongozI wengi wa Africa, walikuwa wako radhi kumsikiliza Mwalimu zaidi on this ishu ya muungano kuliko Nkurumah, ambaye hakuwa na any experience. Kuona hivyo Nkurumah akaanza hizo njama, ambazo baadaye zilizaa matunda ya kuvunjika kwa Jumuiya, ambako Kenya ndio waliofaidika sana na matokeo kwa sababu waliweza ku-retain mali nyingi sana za Jumuiya kuliko nchi zingine yaani sisi Tanzania na Uganda.

Mkuu Kichuguu, Ahsante kwa hizo picha kati ya hao ma-Air Hostess wa EAA, kuna mama mmoja ninaishi naye karibu sana, yaani hata leo akisema kuwa aliwahi kuwa one of hao kina mama huwa tunakufa sana na kucheka na hata yeye mwenyewe hucheka sana, lakini off course ujana na uzee ndio maisha na owte siku moja tutakuwa hivyo, kama tutafanikiwa kuishi kwa muda mrefu maana kila siku life expectency huku kwetu Africa inazidi kushuka tu, nafikiri kama sikosei mara ya mwisho ilikuwa ni miaka 37 tu! Damn it!
 
Wakuu mi nimeonelea ni vema kuwa na suala la kama kitabu/kijarida kikiwa na picha pamoja na maelezo mengine yoote kuhusiana na picha hizi kama hatujawa nacho bado. Ngoja niangalie kama itawezekana tutengeneze kitabu/kijarida kikiwa na mambo yoote haya. Nitarudi na jibu kama wanajamvi mtakubaliana na hili. Nawakilisha.....
 
Mkuu Mwanzage,

Maneno mzito sana, binafsi nitakutafuta week end unajua mashughuli sasa hivi, lakini tutazungumza zaidi.
 
Mkuu Mwanzage,

Maneno mzito sana, binafsi nitakutafuta week end unajua mashughuli sasa hivi, lakini tutazungumza zaidi.

Haina shida mkuu nitakuwepo around......Najua mashuguli ya kilimwengu haya yanatupeleka spidi
 
huyu mwingereza,TINY ROWLAND,amezivuruga sana serikali za africa,ametumia sana mali za LONRHO kuziyumbisha nchi za kiafrika,in fact this man was almost a behind the scenes president of many african countries,coup de tat nyingi africa,his name cropped up.HATA nyerere,tough as he was,amewahi kuwa cornered na TINY.in one of his speeches,nyerere amewahi kusema 'aka kaTINY kana mambo makubwa kuliko jina lake'
 

Sasa hizi hati ndio tunataka tuzione. Ili tuegemeze Muungano wetu kutokana na hati hizi. Vinginevyo inakuwa ni usanii tu.
 


Mkuu, pongezi kwa nukuu yako lakini naomba kuchangia kidooogo kwenye baadhi ya data zako. Hiyo picha ya Coastal Union ni ya mwishoni mwa mwaka 1975 ama mwanzoni mwa mwaka 1976 na ndio maana wamo pia Saidi Jacky, Mwihaji Ally, Mohamed Kampira na Salim Omar ambaye alianza kuichezea Coastal Union mwaka 1975 akiwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza pale Usagara Sec School.

Hiyo picha ya Yanga ilipigwa mwanzoni mwa mwaka 1974 Yanga ilipokwenda Brazili na Simba kwenda Poland na ziliporudi zikaenda moja kwa moja Mwanza kushiriki michuano ya klabu bingwa ya Tanzania ambapo zilifanikiwa kufika fainal kwenye uwanja wa Nyamagana na Yanga kuilaza Simba 2-1 wafungaji wakiwa Sunday Manara na marehemu Gibson Sembuli.
Katika kikosi hicho cha Yanga kilichokwenda Brazil Tenga alikuwa hajajiunga na Yanga kwa sababu yeye alijiunga mwaka 1974 mwishoni akiwa pamoja na Muhaji Mukhi, Juma Matokeo, Patrick Nyaga, Juma Shabaan na Jellah Mtagwa wote wakitokea Morogoro baada ya michuano ya Taifa Cup ya mwaka huo.
Pia Sunday Manara alikwenda Austria mwanzoni mwa mwaka 1976.

Timu ya Yanga ilicheza na timu ya Enugu Rangers International mwezi May mwaka 1975 ukiwa ni mchezo wa pili wa raundi ya pili wa kombe la klabu bingwa Afrika baada ya kutoka sare ya 1-1 wiki mbili kabla huko Nigeria. Yanga ilitakiwa kutoa draw tu ya kutofungana isonge mbele lakini dakika za mwanzo tu za kipindi cha kwanza wakapigwa kimoja kilichokaa hadi mwisho wa mchezo na kuacha umati mkubwa wa watanzania ukibubujikwa na machozi. naunga mkono mchangiaji mmoja kuwa huu ulikuwa miongoni mwa michezo ya kusisimua sana iliyopatwa kuchezwa Uwanja wa taifa.

naomba kuwakilisha.
 


...Hiyo ya Pili yenye bawa la nyuma la juu ilikuwa ni Vickers 10 ama VC 10 miongoni mwa ndege zilizotamba sana miaka ya 60 na 70 mwanzoni!
 

Hii picha imenipa huzuni sana...hayo maneno ya Mwalimu Nyerere yalikuwa na nguvu sana.
Maneno haya kwa kiasi kikubwa yanatoka katika sala maarufu sana ya Mt. Francis wa Asizi (1182 - 1226). Hii sala inabeba ndani yake ambacho haswa Biblia inasema kuhusu kuwa Mkristu.


PRAYER OF SAINT FRANCIS
Lord, make me an instrument of your peace,
Where there is hatred, let me sow love;
where there is injury, pardon;
where there is doubt, faith;
where there is despair, hope;
where there is darkness, light;
where there is sadness, joy;
O Divine Master, grant that I may not so much seek to be consoled as to console;
to be understood as to understand;
to be loved as to love.

For it is in giving that we receive;
it is in pardoning that we are pardoned;
and it is in dying that we are born to eternal life.
 

Samahani Labda nakurudisha nyuma sana. Je si kunatofauti kubwa sana kati ya kuwa na wataalamu na kuwatumia wataalamu hao? Tatizo kubwa kwa TZ ni kutojali na kutumia wataalamu wetu. Mbona wakienda kwenye mashirika ya njee they do wonders?
 
Heshima mbele kwa FMES kwa kuanzisha hii thread. Kwa kweli inaburudisha na inatukumbusha mbali na pia inatufundisha mengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…