Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Mkandara,
Nipo likizo ya kuandika ila nimeona niulizie zaidi juu ya hili.
Pana wakati nilikutana na aliyekuwa waziri huko Ghana wakati wa Jerry Rawlings. Huyu jamaa aitwaye Yaw, alianza kunipa story za Nyerere na Muungano wetu. Akasema kuwa "Muungano wenu ulikuwa umepangwa na Waingereza pamoja na USA - CIA". Lengo la huu Muungano ilikuwa ni kuwazuia Warusi wasijenge BASE yao hapo Zenji wakati huo wao USA walikuwa na base yao Kenya. Hivyo, badala ya KWENDA Zenji na kupigana, wao wakaona dawa ni KUIUNGA Zenji Tanganyika na kuunda Tanzania na JKN awe BOSS na hapo Warusi walie tu.
Anyway, sijui hili lina ukweli kiasi gani. Maana hata Uganda kama ni hivyo basi angelisema TUUNGANE. Inawezekana kuwa watu wanaungaunga kamba na kusema ilikuwa hivi ingawa ukweli uko vingine. Ila ukisoma hapo juu maelezo yako, unaona kuwa "KUNA KAMUUNGO katika matukio."
NA labda ndiyo maana Muungano hadi leo unautata. Walifanya Muungano kwa jambo jingine kabisa ila leo mambo yanafumuka. Bila ya kujali malengo yao, nafikiri Muungano unasaidia sana sisi Watanzania tusiingie sana kwenye ukabila. Muungano ukafa, Wachaga watakuwa na hali mbaya maana wanashambuliwa hata kwa Mtoto wa Kikwete kuowa dada yao.
MUUNGANO UDUMU.

Sikonge,

Alikuwa ni Peter Enahoro au Ralph Uwechue wakiwa New African au Africa Now waliandika makala moja miaka ya 80 iliyokuwa ikisema "100 days that made Tanzania"!

Hii stori ya CIA na Warusi si ya kuzusha ni ya kweli na nafikiri nyaraka za CIA ambazo zilikuwa classified, zimefunguliwa na zinatamka wazi ni jinsi gani walisukuma Tanganyika au Kenya waungane na Zanzibar.

Sasa kwa mkao wa Pan-Africanism na One Afrika, nafikiri hii ilikuwa opportunity nzuri kwa Mwalimu katika zile njozi zake za Afrika moja. Labda ushawishi wa Marekani kwa Karume, ulimrahisishia kazi Nyerere ambaye aliona opportunity ya kuonyesha umma na dunia kuwa Afrika moja inawezekana.

Kuna haja kubwa sana ya kupata hizo de-classified nyaraka za CIA na ziwekwe hadharani ili tuachane na udanganyifu wa wanasiasa wetu na tuamue kwa mazingira ya sasa kama tunataka muungano au la!
 
attachment.php
Former AU5.jpg
 
161ge9f.jpg

Kwenye Picha: Salim, Graca,Mama Maria, Butiku,Jumbe,Mwalimu na Samora.
jumbe.gif

Jumbe
 
Nakumbuka sana somo letu la siasa shule ya msingi...eti siku hizi wanaliita 'uraia' sijui....
 
mkuu kichuguu,

hapo msaaada, najua kuna mwalimu, mkapa lakini huyu wa pembeni amefanana na pinda ila sijui ni nani mkuu weka msaaada!

hahaaaaaaaaaaaaa, yaani zama hizo pinda alikuwemo naye? Au ndio duniani wawiliwawili, kumbe mshikaji tangu ujanani alikuwa serious
 
Thread hii inatuliza sana ubongo kama ile ya Icadon ya walinzi wa viongozi. Ni watu kama "Mwiba" ndio wanaojaribu kuvuruga mtiririko huu muhimu wa kihistoria. Kumbe hati ya Muungano wetu ilifikishwa hadi BUNGENI? Zanzibar wakati huo hawakuwa na Baraza la Wawakilishi hadi 1980.
 
karume hawezi kuwepo kwenye picha hizo kwa sababu sio yeye wala Afro - Shiraz waliopindua nchi isipokuwa hawa wajomba ktk picha ambao walikuwa watu wa abrahaman babu na chama cha Umma party. baada ya mapinduzi tu propaganda zilipigwa kuwa hawa jama ni Makomunist na kuwa sasa Zanzibar imechukuliwa na utawala wa kidhalimu wa Kikomunist..

Jamaa walidumu muda wa mwezi mmoja tu kabla ya Nyerere kuwaingiza mkenge, akawavuta viongozi wa Umma party bara ati kuwapa security, akamfukuza Okello na kumachika Karume kama alivyofanya Uganda kumweka Bina Issa baada ya kundolewa kwa Idd Amin huku azma yake kubwa ni kumrudisha Obotte..
Kwa hiyo kulikuwa na mapinduzi ya aina mbili kwanza yale ya kuwaondoa Hizbu kisha kuwaondoa Umma Party ktk picha.

Mkuu Bob,

Haya maneno yako ni mazito sana na yanaongeza nguvu sana katika kujaribu kupata picha kamili ya wapi matatizo ya muungano wetu yalipoanzia, mpaka kutufikisha hapa tulipo.

Ahsante Mkuu.
 
hivi huyu sokoine,amepata kila aina ya wasifa,was he that effective,au by virtual of his life being cut short in mitigating curcumstances,ndiyo iliyomuelevate to a cult status.
Nimesoma somewhere in the capitalist press,kwamba KAMBONA was the good president that tanzania never had. i take this to mean had kambona become a president in the roaring 60's or 70's tanzania could not have been in the rot it currently finds itself in - hii argument does it really hold water au
 
Mwenyezi Mungu azidi kuziweka roho ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere & Moringe Sokoine Mahali pema peponi. Amina.....

Asanteni mliotuwekea picha hizi kutuliwaza, i feel like crying!
 
nani kakwambia kama Nyerere hakulimbikiza mali ,kama unaijua sababu ya Mkapa kufungua genge la biashala ikulu ,usingesema hayo ?
Kifo cha Nyerere kinajulikana ni ni baada ya kufa Jamal ambae ndie aliekuwa anahifazi feza ya Nyerere kwa jina lake,ghafla Jamal alipofariki Nyerere akafunga safari hadi kwa mke wa Jamali na kuulizia ela yake ,mke wa Jamali akamjibu Bana haikuacha kitu kwa jina lako ,hapo ndipo ugonjwa ulipoanza kumtambalia Mwalim na kumuondoa duniani.

Light travels faster than sound. This is why some people appear bright until you hear them speak.

Mwiba,hio signature yako really sums it all up soo nicely......
 
attachment.php

_________________

mwalimu (rip)baba wa taifa hili, na mkewe mama maria

wakuu wote jamii forums, heshima mbele!

Katika hiki kipindi cha mapumziko nimeona sio vibaya tukijikumbusha historia yetu ya taifa katika picha, ninawaomba wakuu wote wenye picha interesting kisiasa kwa taifa letu, tuziweke hapa ili tujikumbushe na kuelemishana kidogo kuhusu taifa letu lilikotoka, unajua wananchi wasiojua walikotoka hawawezi kujua wanakokwenda.

Ahsante wakuu.
cheki pete hilo wakati huwo mwalimu alikuwa na kaufisadi.
 
hivi huyu sokoine,amepata kila aina ya wasifa,was he that effective,au by virtual of his life being cut short in mitigating curcumstances,ndiyo iliyomuelevate to a cult status.
Nimesoma somewhere in the capitalist press,kwamba KAMBONA was the good president that tanzania never had. i take this to mean had kambona become a president in the roaring 60's or 70's tanzania could not have been in the rot it currently finds itself in - hii argument does it really hold water au
Son of A,
Don't believe everything you read in the capitalist press. Wakianza kukusifia ujue kuna kitu hapo. Mwalimu aliwadisappoint by going east. Jiulize ni kwa nini walimwuua Lumumba na kumjenga Mobutu?
 
9rn8fp.jpg

241w874.jpg

Derek Bryson

Picha ya juu hapo ni Idi Amin alikuwa akitowa hotuba na kuna kitu kilimchekesha mwalimu pale...Labda mzee Malecela anaweza kutuambia ni kiti gani mwalimu alikuwa akisema hapo wakati wa hotuba ya hasimu wake mkuu....Kwasababu hata sura yake inaonuesha kama kicheko flani hivi cha kiubezaji...
 
Kichuguu, Jasusi, FMES, Rev. Kishoka, Son of Alaska,

..hii thread nimeipitia na kila kumbukumbu tunayoletewa ni ya WANASIASA tu.

..kulikuwa na thread nyingine ambapo member walijaribu ku-list idols/mashujaa wao, basi huko nako kulijaa wanasiasa.

..hivi katika jamii yetu hakuna watu wengine wa kuwaenzi zaidi ya wanasiasa? hakuna madaktari, ma-injinia, bankers, wachumi, industrialists, wanasheria, mathematicians,physicists,biologists,...ambao tunaweza kuwaenzi kwa utumishi na michango yao?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom