Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

Tukumbuke Zamani: Historia ya Taifa letu katika picha

lakini inasemekana alikula fedha yetu ya EPA toka kwa Jeetu na ndio maana harusi ilikuwa ya kukata na shoka tayari kwa urais!!!
Tatizo la kuwa crony wa mtu ndio hilo, wahusika hawajakana shutuma na pengine huko mahakamani ndiko vitatolewa vielelezo kuthibitisha ulaji wa hizo pesa za EPA kwani aliyewatuhumu inasemekana anaushahidi!! At that point these will not be allegations any more!! Remember wametuhumiwa na boss wa makachero!!

POLE SANA kwa kukwazwa.

- "Lakini inasemekana & pengine huko mahakamani", ahsante kwa more great thinking mr. Great Thinker I mean talking about kukwazika naamini kila mtu ana macho hapa ya kuona nani ana matatizo ya kukwazika, pole sana mkuu Mr. Great Thinker!

- Keep on coming soon nitakupatia exactly what you want,watu wengine hivi kwa nini huwa hamjionei huruma, I mean wewe mwenyewe Mungu nisaidie kujikweza kweza tu ahhgrrr! maneno mengi hoja hamna tizama hoja zako zilivyo pumba,

"
kwani aliyewatuhumu inasemekana anaushahidi!! At that point these will not be allegations any more!!"

- Nasikia kutapika mkuu!


Respect.


FMEs!
 
nakushukuru sana mtoa hii mada nimekupa na thanks kabisa umenikuna ipasavyo
be blessed
 
nakushukuru sana mtoa hii mada nimekupa na thanks kabisa umenikuna ipasavyo
be blessed
Ukizingatia wewe ni mwanamama na aliyetuma hii thread ni mwanume, tafuta lugha nzuri ya kutumia, shemeji hasije kuchinja mtu.
 
Ukizingatia wewe ni mwanamama na aliyetuma hii thread ni mwanume, tafuta lugha nzuri ya kutumia, shemeji hasije kuchinja mtu.

hahaha umeanza kufukua fukua mwisho na shemeji aone
hii ni lugha tu inapanuka Kaitaba
 
..kesi ya uhaini iliamuliwa na Jaji Kiongozi Nassoro Mzavas[r.i.p].

..kulikuwa na vifungo tofauti, lakini cha juu kabisa ilikuwa maisha. pia wapo washitakiwa walioachiwa huru.

..kesi ile ilitusisimua sana tuliokuwa tukiifuatilia. upande wa utetezi ulikuwa na mawakili machachari sana kama Murtaza Lakha, Hussein Muccadam, Tarimo,...

..nadhani wengi tulikuwa tunastaajabu jinsi mawakili hao walivyokuwa wakiwahoji mashahidi wa serikali. kwetu sisi ilionekana kama wanaihoji serikali yenyewe!! kwangu mimi ilikuwa ni kitendo cha ajabu kwelikweli.

..upande wa mashtaka nao ulikuwa haujachacha. nadhani mwendesha mashtaka mkuu alikuwa William Sekule, akisaidiwa na wengine kama Mwanyika[ ag wa sasa].

..kwa mtizamo wangu upande wa mashtaka ukiongozwa na William Sekule made very strong closing arguments na hilo lilisaidia ktk kushinda kesi.

..washitakiwa ninaowakumbuka ni: Thomas Lugakingira, Hatibu Gandhi/Hatty McGhee, Suleiman Kamando, Badru Rwechungura Kajaja, Deutrich Mbogoro, vijana wawili wa familia ya Hans Pope. wengine walikuwa Banyikwa[if not mistaken walikuwa mtu na mkewe], na Ngaiza.

..Hans Pope alikuwa ni afisa wa Polisi ambaye alitekwa nyara na majeshi ya Amini na kuuwawa Uganda. mwili wake nadhani ulipatikana baada ya majeshi yetu kuingia Uganda. vijana wake ndiyo hao walioshtakiwa kwa uhaini.

..washitakiwa wa Uhaini waliachiwa huru wakati Raisi Mwinyi anaondoka madarakani.




..Uncle Tom Lugakingira, pamoja na Hatibu Gandhi, walitoroka toka rumande[ukonga au keko]. walitorokea Kenya, na nadhani walipitia mpaka wa horohoro[sina uhakika].

..Uncle Tom alikuwa na pesa hivyo moja kwa moja akakimbilia UK. Hatibu Gandhi aliendelea kuzubaa Kenya, akaja kuwa exchanged na wahaini[ochuka,...] wa Kenya waliotorokea Tanzania.

..ni kipindi hicho hicho Moi alipinduliwa na askari wa jeshi la anga. kiongozi wao alikuwa ni Mjaluo. tuliofuatilia redio kenya tulijuwa it was over for Moi, lakini baadaye tukasikia tangazo toka kwa Maj.Gen.Joseph Mulinge kwamba jaribio limezimwa.



..Commandoo aliyeuawa alikuwa akijulikana kama Mussa Tamimu. maofisa usalama walijaribu kumkamata maeneo ya mwananyamala lakini akawaponyoka. baadaye walimkimbiza akarukia pickup iliyobeba bia na kuanza kuwarushia maofisa usalama. baada ya hapo alipigwa risasi na kufariki.


NB:

..FMES amemchanganya Cpt.Tamimu na jambazi sugu aliyekuwa akiijulikana kwa nickname Nyau. jina lake lilikuwa Hamisi .... "nyau."

..Nyau pamoja na majambazi wenzake 19 walitoroka gerezani Ukonga. sina uhakika walitoroka vipi. serikali ilifanya shake up kubwa sana Magereza ambapo Mkuu wao alipoteza kazi.

..baada ya hapo vitendo vya ujambazi na hali ya wasiwasi ilitawala jiji zima la DSM na vitongoji vyake. road blocks zilikuwepo kila mahali, na msako mkubwa ulifanyika.

..ujambazi ulitokana na matokeo ya vita vya Kagera. maisha yalikuwa magumu sana, na kulikuwa na askari wengi, haswa mgambo, waliorudi nyumbani na kuwa-released toka jeshini.

Nakumbuka nikiwa darasa la sita mwishoni mwa miaka ya 80 ndipo nilipoanza kusoma vitabu vya hadithi vya kina Willy Gamba na kadhalika. Lakini mojawapo ya vitabu vya ''true stories'' nilivyosoma kilikuwa ni hicho kinachohusu kesi ya uhaini. Nilikuwa bado mdogo kiumri na kielimu pia kuweza kupambanua mwenendo mzima wa kesi hiyo.

Natamani nikipate kitabu leo hii nikisome upya!
 
Daaaaaaaaaaaaa nimekumbuka mbali kweli kweli..........
 
Well heshima sana wakulu wote hapa, naona sasa ni wakati wa kurudia tena tulipoachia, thaanks!

Es!<input id="post_form_id" name="post_form_id" value="731930ea840057dfab9ef37b022ae6c9" autocomplete="off" type="hidden"><table><tbody><tr><td width="100%" align="center">
</td><td valign="middle">
</td></tr></tbody></table>


- Mwalimu @ Rome,Italy.

Mkuu sauti ya umeme huonekani siku hizi tuna miss sana michango yako kulikoni ?.
 
Yaani huoni kama hizi picha ni nuksi tupu ,hata ukitazama kwa kina utaona haziendani na hii Jamii forum inabidi ulete tambala lile lililokuwa linatumika na zile senema za bure akina Omo na Fakcho ,si mnazikumbuka ,wakituletea filamu kwenye viwanja vya mpira.
hawa ndio waliokuwa wakihimiza siasa za ujamaa na kujitegemea ,hebu angalia Madini ya Shinyanga yalianza kuchimbwa lini ,ni wakati huo huo wa siasa zao.

Kama kukumbukwa basi tukumbusheni mengi na ya kukumbuka sio picha hizi ambazo sasa zinaelekea kurithishana makampuni . Vizazi vya hawa ndivyo hivi hivi vinavyofanya biashala Ikulu ,watu hawa na siasa zao ni walemavu wa kuendeleza wananchi walio wengi ,hawa ni watu wa kusemwa na kupingwa kila kukicha ,mambo ya kuwakumbuka wayapeleke kwenye Chama chao ambacho kilitangaza kushika hatamu za Dola ,hivi wamejimilikisha kila kitu kwa faida ya nani kama sio yao yenye maslahi binafsi ila sasa tunaona akina Butiku wameanza kukana na kukanwa hii ni dalili mbaya sana.

Mwananchi anaekumbuka watu hawa bila ya shaka yeyote akiyapima maisha yake leo hii ataona ukweli kuwa hawa mnaoonyesha mapicha yao ndio walioidumaza Tanzania.

Tanzania ilipata uhuru ikiwa bado Bikira ,tofauti na akina Zimbwambwe,na wengineo ,hawa wangekuwa na uelewa maana ya kugombea Uhuru leo hii tungekuwepo mbali na maisha ya kutafutana na mlo wa siku.

Kila kukicha wanasifiwa kuwa Tanzania ni kisiwa cha Amani ,kumbe amani yenyewe ni moto unaowaka kwenye majivu ,wameitafuna Tanzania miaka 44 sasa yameanza kubaki mashimo ,wakati hao mnaowatazama wamishakufa na walio hai wanakimbiza vijisenti wanahama nchi na wengine ndio hao wanaenda kufia Ulaya na hazina na mahesabu yake hayajulikani yamepotea potea vipi ,wanasema eti fedha na mahesabu yapo katika hali ya kutatanisha toka Balali yupo hapa mpaka amepata ugonjwa mpaka wengine wanasema hajakufa na wengine amekufa ,mwisho serikali ya hawa mnaoonyesha picha zao ,haijui wafanye nini ? Hao ni CCM na waliopo ni CCM mnawakumbuka kwa misingi ipi ya uongozi na ufundishaji upi wa Uongozi tunao uona leo hii ,mwizi kusafishwa tena bungeni ,kama si aibu ni kitu gani kwao ?

Halafu mnaleta mapicha ya maiti eti tukumbuke ? hivi mkisikia kulogwa ,jamani si ndio huku ? baada ya kuzungumza mambu ya maana na maisha haya ambayo yanayokwenda na kupanda kwa kasi ya Kikwete ,mnaleta picha sasa niwaulize hivi mnafaidika na kitu gani na picha hizo wakati mpo kwenye ziki za kimaisha ? Au ndio mnajiliwaza ? Sasa kujiliwaza mngetafuta angalau mapicha mazuri yanayoburudisha moyo lakini si picha za waliotuzamisha ,mpo ?
Upinzani hauwezi kwenda mbele kwa kutazama picha za watawala au Chama cha walioko madarakani au waliokufa.
Tuna msemo wa kiswahili usemao samaki akioza mmoja ndio wameoza wote.CCM wameoza wote waliokufa na hawa waliokuwepo hai ndio usiseme ni harufu mbaya tupu.

Mkuu comment yako nimeikubali kinoma huu ndio ukweli tukubali tukatae
 
we lazima uliwahi kufika IRINGA , Maana unanikumbusha enzi za Railway IRINGA. Kama inavyoonekana hapo juu.

Mabasi haya Yamenikumbusha enzi zile tunasoma bure. Unatoka mtwara unaenda sekondari ihungo bukoba, unapewa government warranty unasafiri bure mabasi ya kamata na TRC, train. kweli pale ndo tulikuwa tunajenga umoja na uzalendo pamoja na JKT. Hongera Nyerere na Chadema mnaotaka kurudisha hadhi ya elimu na kujenga utaifa, umoja na uzalendo
 
Mabasi haya Yamenikumbusha enzi zile tunasoma bure. Unatoka mtwara unaenda sekondari ihungo bukoba, unapewa government warranty unasafiri bure mabasi ya kamata na TRC, train. kweli pale ndo tulikuwa tunajenga umoja na uzalendo pamoja na JKT. Hongera Nyerere na Chadema mnaotaka kurudisha hadhi ya elimu na kujenga utaifa, umoja na uzalendo
slaa kaiweka vizuri sana hiyo
 
An undated file photo shows Tanzanian Prime Minister Edward Lowassa in Dar es Salaam. Lowassa told parliament 07 February 2008 he had tendered his resignation to the president after being implicated in a corruption scandal over an energy deal.


FMEs!
Did he tender resignation in his own will or forced to tender resignation to safe guard interest of himself, ruling party and the president who chose him to the post
 
This was the man! Angelikuwepo hai huyu leo tungekuwa industrialized. Kule kuvaa vitenge vya urafiki na kukosa sabuni kulikuwa ndio njia sahihi ya kutufundisha kutumia akili zetu kutafuta maendeleo. Bahati mbaya ndiyo hivyo tena. A winning formula was lost by the loss of this tough man

yeah this is the man of action i appreciate for what he did
 
huyo CHILUBA amewahi kufanya kazi kwenye mashamba ya mkonge tanzania kama administrater,huyu jamaa ana pair nyingi za viatu kuliko hata Imelda Marcos

how are you sure?????
Chiluba was the President of Zambia, so you preferred him to have seven pairs only??? please be fair to F. Chiluba
 
Thread hii ni muhimu sana within this next 7-days kwa sababu historia ni kutazama tulikotoka na kulinganisha na tulipo ili tuweze kujua tunakokwenda.

Hivyo kumbukumbu hii ya picha muhimu kama hizi, inaweza kusaidia kusalvage baadhi ya kura kwa symphathy ya those good old days, otherwise 'la kuvunda....
 
236030766_b687e2ae94.jpg

1149440697_0cc710ae3c.jpg


Mkuu, huyu mzee alikuwa mtata kweli nafikiri hakuna mtu aliyemfikia katika kujifanya mwafrika mzungu, maji yake aliyokuwa anakunywa yalikuwa imported toka kwa mama UK.
Sijui siku hizi yuko vipi? Mtoto wake kaolewa na Kheri Mark Bomani nafikiri enzi hizo asingeweza kukubali
 
3392715596_3170f3a26c.jpg



Hii inatumkumbusha
1. Kulikuwa na nchi kama nchi na serikali, na amani na raisi mwenye mamlaka kamili. Nchi ya somalia ilikuwa na heshima
2. John Samwel Cigiyemisi Malecela alipokuwa na akili timamu na kufanya mambo ya heshima chini ya Mwl nyerere kabla akili haijabadilika na kuwa corrupt chini ya Raisi mwinyi na heshima yake kuporomoka
 
Back
Top Bottom