Tukumbushane maisha ya UDSM enzi hizo, wazee wa Bibo na Main Campus

Tukumbushane maisha ya UDSM enzi hizo, wazee wa Bibo na Main Campus

nipo hapa ilikuwa bumu likitoka lazima nimpeleke manzi wangu wa kichagga kula Hill Park, bumu likikata naenda kwa Bwashee pale Coet cafteria elfu 25 nakula bure semester nzima 😂😂😂
Nmekula sana ukoko udsm jameni, we acha tuu maisha haya, buku kwa siku mwezi 30k, na sikupunyuka nywele, show ilikuwa ni kali
 
Ilikuwa ikibaki wiki moja boom litoke, tulikuwa tunatoka pale njee kwenye parking ya mabibo hostel usiku tunaanza kulia
Njaaaaa njaaaa njaaaaa njaaaa
Kumbe nilikuwa najilaani nimekuja mtaani njaa imenipiga nusu kufa
Ulikuwa mtu wa makundi sana na kufuata mikumbo. Kifupi hukuwa na msimamo binafsi na ndio maana njaa inakuua huku mtaani, na iwe fundisho kwa vijana wapuuzi kama wewe, wasiojua wamekwenda kufanya nini chuo.
 
Pale sisi tulikuwa hatuangalii uandishi ni intergral tu kila sehemu ,ndi maana sizingatii uandishi .A ya Mathematics na Physics ndio zilinipeleka pale kugonga miaka yangu minne kule bondeni Coet ,wala sio Kiswahili ambacho niliginga D O-level.
Upo wapi kwa sasa, na unajishughulisha na nini?
 
Maliza kwanza chuo dogo ndio uje kunitolea shombo. Hizo ni akili za boom zinakusumbua
Unajuaje kama nina boom? Je kama sina? Huo ndio uhalisia, wengi mnajisahau na kuishi maisha yasiyo yenu, unaonekana tu kuwa ulikuwa mzee wa sosho, makundi kwa sana, clubs n.k, mkija DSM ushamba wenu wa mikoani kwenu muuache, fuateni kilichowaleta. Unaonekana hukujua kuwa baada ya chuo utakuwa peke yako.
 
Unajuaje kama nina boom? Je kama sina? Huo ndio uhalisia, wengi mnajisahau na kuishi maisha yasiyo yenu, unaonekana tu kuwa ulikuwa mzee wa sosho, makundi kwa sana, clubs n.k, mkija DSM ushamba wenu wa mikoani kwenu muuache, fuateni kilichowaleta. Unaonekana hukujua kuwa baada ya chuo utakuwa peke yako.
Unanipa tabu sana kukujibu dogo, kwani kielimu nimekuzidi mbali sana. Halafu pili wewe sio udsm member sababu ya ufaulu mdogo uliokuwa nao.
Ndio maana nakwambia maliza kwanza chuo ndio uje kunipa ushauri.
 
Unanipa tabu sana kukujibu dogo, kwani kielimu nimekuzidi mbali sana. Halafu pili wewe sio udsm member sababu ya ufaulu mdogo uliokuwa nao.
Ndio maana nakwambia maliza kwanza chuo ndio uje kunipa ushauri.
Nani kakuambia kila asiyesoma UD ana ufaulu mdogo kaka? Unakosea sana, sasa kam mpaka div 3 wapo wanaosoma UD, sasa mimi nikihitaji kwa nini nishindwe? Hoja dhaifu hiyo bro, pia hujui nasomea kozi gani na hujui kama hapo UD ipo au haipo.
 
Ni aibu huu uzi tunakumbushana mambo tuliopitia udsm members. Mtu anasoma sijui teifilo kisanji anakuja kujifanya mshauri humu
 
Ni aibu huu uzi tunakumbushana mambo tuliopitia udsm members. Mtu anasoma sijui teifilo kisanji anakuja kujifanya mshauri humu
Naomba uniambie bro, kwa nia njema tu. Ulisoma kozi gani na ni mwaka gani?
 
Haabari wadau..!
Maisha ya UDSM enzi hizo yalikuwa powa sana sijajua kwa sasa.

Tuanzie wapi ,ngoja tuanze na Boom enzi hizo lilikuwa 4000/= kwa siku ila tulivyoingia chuo ikabidi tufanye mgomo Boom liongezwe watoto wa mama hawataelewa.

Maandamano yalianzia Revo Square sijuhi kama watoto wa leo wanaijua Revo Square watu wakatolewa lecture room wajoin movement watoto wa mama wakakimbia ila watoto wa mbwa tukaingia mtaani tulivyofika Mlimani City mabomu yalipigwa kama yote vile tukapoteana.

Kipindi hicho kuna wale wajamaa ndio wakuu wa vyuo wanajiita Tripple M yaani Mkandala,Mgaya na Maboko.

Mgomo ulipoisha chuo kizima tulirudishwa nyumbani kwa mda usiojulikana,baada ya kurudishwa tena sisi waanzilishi wa mgomo tukafukuzwa ila mm nikafanya harakati sikufukuzwa.

Mwaka wa kwanza nilipata room mabibo hostel pale maisha yalikuwa powa sana wale wa mwaka wa pili na kuendelea tukawa tunawabeba yaani kitanda chembamba mnalala wawili kana mpo lupango vile ,usiombe umbebe mtu mrefu.

Mwaka wa pili inabidi huwai chuo kabla akijafunguliwa ukatafute mtu wa kukubeba (kushare naye kitanda).

Ukiwa mwaka wa kwanza ni ngumu sana kupata demu wengi wanadharau mwaka wa kwanza,ila mwaka wa pili ndio mwaka wa kupata demu inabidi uliwahi konteana jipya (first year),asikwambie mtu hapa watoto wa mwaka wa kwanza wanamegeka kiurahini sana .

Boom likiingia safari za mlimani City ,Survey ,Ambiace n.k ila boom likikata tunaanza kupiga pasi ndefu kama hatuna akili nzuri hata lectures hazipandi kipindi hiki mademu wasio na msimamo wanaanza kujiuza ili wapate pesa za kujikimu,yaani kama una demu anaweza kukusaliti boom likikata.

Kipindi cha boom likikata wahuni tunaanza kugonga RB (Rice Beens) wali maharage ambao bei yake ilikuwa 600/=Boom likikata watu wanaanza kusifia wali mahatagr wa Cafe 1 na Coet ndio mtamu.Wazee wa bibo wanapiga tu shato pori mwendo wa kutembea kwa mguu toka main campus aibu washikaji wakikuona wanajua umefua.

Kuishi mabibo ni mateso hakukuwa na Kijazi Flyover foleni mtindo mmoja usishangae kutoka bibo mpk campus ukamaliza masaa zaidi ya matatu ubungo mataa.kukosa lecture au kuchelewa test kawaida kisa foleni ya ubungo mataa.
Mie sitosahau vyoo vya hall5..nyaa nje nje nawee unaenda jazia lakoo...

Sie wengne tulikua tunakula cafeteria 1 RB mshikak m1 halaf tunaenda tena cafeteria 2 wali njegere mshikak m1...

Nilikua na madem wawil bcom na wote wanakaa hall3
 
Mimi nilisoma wakati boom ni 3000, eneo la Mlimani city kulikuwa na mapori tu, off campus hostel ilikuwa blocks za CRDB Kijitonyama.
 
Back
Top Bottom