Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huyu Odong yupo wapi?Waanzilishi wa kunji David Silinde, Odong Oduar, Stephen Owawa.
Acha masihara ww, kweli??Vya pale Law vilikuwa poa Sana.Kule hall 3 maji yakikata kulikuwa na choo cha shimo,mh! Humo unamkuta sister do anakata gogo live maana vingine havikuwa na milango
nipo hapa ilikuwa bumu likitoka lazima nimpeleke manzi wangu wa kichagga kula Hill Park, bumu likikata naenda kwa Bwashee pale Coet cafteria elfu 25 nakula bure semester nzima 😂😂😂Tuliokuwa tunakula Hill Park tujuane
Nmekula sana ukoko udsm jameni, we acha tuu maisha haya, buku kwa siku mwezi 30k, na sikupunyuka nywele, show ilikuwa ni kalinipo hapa ilikuwa bumu likitoka lazima nimpeleke manzi wangu wa kichagga kula Hill Park, bumu likikata naenda kwa Bwashee pale Coet cafteria elfu 25 nakula bure semester nzima 😂😂😂
pole sanaPale sisi tulikuwa hatuangalii uandishi ni intergral tu kila sehemu ,ndi maana sizingatii uandishi .A ya Mathematics na Physics ndio zilinipeleka pale kugonga miaka yangu minne kule bondeni Coet ,wala sio Kiswahili ambacho niliginga D O-level.
Ukoko tena 😂😂😂😂😂wakati watu tulikuwa tunawapa wapishi rushwa 30k unakula semista nzimaNmekula sana ukoko udsm jameni, we acha tuu maisha haya, buku kwa siku mwezi 30k, na sikupunyuka nywele, show ilikuwa ni kali
Ulikuwa mtu wa makundi sana na kufuata mikumbo. Kifupi hukuwa na msimamo binafsi na ndio maana njaa inakuua huku mtaani, na iwe fundisho kwa vijana wapuuzi kama wewe, wasiojua wamekwenda kufanya nini chuo.Ilikuwa ikibaki wiki moja boom litoke, tulikuwa tunatoka pale njee kwenye parking ya mabibo hostel usiku tunaanza kulia
Njaaaaa njaaaa njaaaaa njaaaa
Kumbe nilikuwa najilaani nimekuja mtaani njaa imenipiga nusu kufa
Upo wapi kwa sasa, na unajishughulisha na nini?Pale sisi tulikuwa hatuangalii uandishi ni intergral tu kila sehemu ,ndi maana sizingatii uandishi .A ya Mathematics na Physics ndio zilinipeleka pale kugonga miaka yangu minne kule bondeni Coet ,wala sio Kiswahili ambacho niliginga D O-level.
Maliza kwanza chuo dogo ndio uje kunitolea shombo. Hizo ni akili za boom zinakusumbuaUlikuwa mtu wa makundi sana na kufuata mikumbo. Kifupi hukuwa na msimamo binafsi na ndio maana njaa inakuua huku mtaani, na iwe fundisho kwa vijana wapuuzi kama wewe, wasiojua wamekwenda kufanya nini chuo.
Unajuaje kama nina boom? Je kama sina? Huo ndio uhalisia, wengi mnajisahau na kuishi maisha yasiyo yenu, unaonekana tu kuwa ulikuwa mzee wa sosho, makundi kwa sana, clubs n.k, mkija DSM ushamba wenu wa mikoani kwenu muuache, fuateni kilichowaleta. Unaonekana hukujua kuwa baada ya chuo utakuwa peke yako.Maliza kwanza chuo dogo ndio uje kunitolea shombo. Hizo ni akili za boom zinakusumbua
Unanipa tabu sana kukujibu dogo, kwani kielimu nimekuzidi mbali sana. Halafu pili wewe sio udsm member sababu ya ufaulu mdogo uliokuwa nao.Unajuaje kama nina boom? Je kama sina? Huo ndio uhalisia, wengi mnajisahau na kuishi maisha yasiyo yenu, unaonekana tu kuwa ulikuwa mzee wa sosho, makundi kwa sana, clubs n.k, mkija DSM ushamba wenu wa mikoani kwenu muuache, fuateni kilichowaleta. Unaonekana hukujua kuwa baada ya chuo utakuwa peke yako.
Nani kakuambia kila asiyesoma UD ana ufaulu mdogo kaka? Unakosea sana, sasa kam mpaka div 3 wapo wanaosoma UD, sasa mimi nikihitaji kwa nini nishindwe? Hoja dhaifu hiyo bro, pia hujui nasomea kozi gani na hujui kama hapo UD ipo au haipo.Unanipa tabu sana kukujibu dogo, kwani kielimu nimekuzidi mbali sana. Halafu pili wewe sio udsm member sababu ya ufaulu mdogo uliokuwa nao.
Ndio maana nakwambia maliza kwanza chuo ndio uje kunipa ushauri.
Jibu hoja bro[emoji115][emoji115]Ni aibu huu uzi tunakumbushana mambo tuliopitia udsm members. Mtu anasoma sijui teifilo kisanji anakuja kujifanya mshauri humu
Naomba uniambie bro, kwa nia njema tu. Ulisoma kozi gani na ni mwaka gani?Ni aibu huu uzi tunakumbushana mambo tuliopitia udsm members. Mtu anasoma sijui teifilo kisanji anakuja kujifanya mshauri humu
Mie sitosahau vyoo vya hall5..nyaa nje nje nawee unaenda jazia lakoo...Haabari wadau..!
Maisha ya UDSM enzi hizo yalikuwa powa sana sijajua kwa sasa.
Tuanzie wapi ,ngoja tuanze na Boom enzi hizo lilikuwa 4000/= kwa siku ila tulivyoingia chuo ikabidi tufanye mgomo Boom liongezwe watoto wa mama hawataelewa.
Maandamano yalianzia Revo Square sijuhi kama watoto wa leo wanaijua Revo Square watu wakatolewa lecture room wajoin movement watoto wa mama wakakimbia ila watoto wa mbwa tukaingia mtaani tulivyofika Mlimani City mabomu yalipigwa kama yote vile tukapoteana.
Kipindi hicho kuna wale wajamaa ndio wakuu wa vyuo wanajiita Tripple M yaani Mkandala,Mgaya na Maboko.
Mgomo ulipoisha chuo kizima tulirudishwa nyumbani kwa mda usiojulikana,baada ya kurudishwa tena sisi waanzilishi wa mgomo tukafukuzwa ila mm nikafanya harakati sikufukuzwa.
Mwaka wa kwanza nilipata room mabibo hostel pale maisha yalikuwa powa sana wale wa mwaka wa pili na kuendelea tukawa tunawabeba yaani kitanda chembamba mnalala wawili kana mpo lupango vile ,usiombe umbebe mtu mrefu.
Mwaka wa pili inabidi huwai chuo kabla akijafunguliwa ukatafute mtu wa kukubeba (kushare naye kitanda).
Ukiwa mwaka wa kwanza ni ngumu sana kupata demu wengi wanadharau mwaka wa kwanza,ila mwaka wa pili ndio mwaka wa kupata demu inabidi uliwahi konteana jipya (first year),asikwambie mtu hapa watoto wa mwaka wa kwanza wanamegeka kiurahini sana .
Boom likiingia safari za mlimani City ,Survey ,Ambiace n.k ila boom likikata tunaanza kupiga pasi ndefu kama hatuna akili nzuri hata lectures hazipandi kipindi hiki mademu wasio na msimamo wanaanza kujiuza ili wapate pesa za kujikimu,yaani kama una demu anaweza kukusaliti boom likikata.
Kipindi cha boom likikata wahuni tunaanza kugonga RB (Rice Beens) wali maharage ambao bei yake ilikuwa 600/=Boom likikata watu wanaanza kusifia wali mahatagr wa Cafe 1 na Coet ndio mtamu.Wazee wa bibo wanapiga tu shato pori mwendo wa kutembea kwa mguu toka main campus aibu washikaji wakikuona wanajua umefua.
Kuishi mabibo ni mateso hakukuwa na Kijazi Flyover foleni mtindo mmoja usishangae kutoka bibo mpk campus ukamaliza masaa zaidi ya matatu ubungo mataa.kukosa lecture au kuchelewa test kawaida kisa foleni ya ubungo mataa.