Tukumbushane ukoloni uliowahi fanyiwa na wazee wako

[emoji23][emoji23][emoji23] tukiwa shule ya msingi, alikuwa akitoka kuangalia mechi ya simba na Yanga, halafu Yanga ikitoka imefungwa hasira zote zinaishia kwetu asee. Bi mkubwa alikuwa akijua tu simba na Yanga zinacheza alikuwa anatuwahisha kulala
 
Ni story nilipewa na jamaa yangu
Ilikuwa siku ya jumamosi wanakwenda kukogesha mbwa mbele ukapita msafara wa mwenye kitI wa mkoa wa chama kwa miaka hiyo chama kimeshika hatamu kweli kweli mambo ya utoto kuwinda ndege na nini basi jiwe likatua penye kioo cha 109 ya chama vijana wakatoka mbio wakajaribu kuwafukuza bila mafanikio ila wakawajua ni watoto wa nani mbaya zaidi baba yao alikuwa na cheo katika chama eneo hilo.
Jioni wapo nyumbani mzee katokea na kuanza kutoa kichapo anahadithia "tulipigwa nyinyi tulipigwa! yaani tulipigwa! mpaka leo huwa nahisi labda yule jamaa sio dingi yetu.
 
ahahahahaha noma sana
 
Hamna kunywa chai bila kuoga
Sa kumi na mbili geti limefungwa...
Alileta ukoloni zaidi pale alipoanza kukusanya simu zetu sa mbili usiku na kuzizima mpaka asubuhi anapoenda kazini.
 
Hamna kunywa chai bila kuoga
Sa kumi na mbili geti limefungwa...
Alileta ukoloni zaidi pale alipoanza kukusanya simu zetu sa mbili usiku na kuzizima mpaka asubuhi anapoenda kazini.
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]
Hawa wazee bhana kukusanya simu tena
 
duh nimecheka saaanaaaa!!!!!
 
Wangu mimi ilikuwa mkimaliza kula hakuna kunawa mikono lazima usubiri kwanza yeye amalize kunawa ndio na nyie mnawe.Ilikuwa inaniboa sana hii kitu,ukikuta chakula ni ugali utakomaa akili maana mpaka mkono haukunjuki jinsi ulivyo ganda.
 
Umenikumbusha mbali.... Mzee alikuwa anaulizia Kama mifugo imekula hata Kama nyie mtalala njaa shauri yenu.
umenikumbusha mzee alikua anatwambia kama cc tunavyokula mara tatu ma mifugo ilishw hivyo.kwa hyo akija akakuta haina chakula lazima kiwlewek tu
 
Mkoloni alikuwa nuksi sana ukichelewa kufungulia kuku muda wa jioni, kuna siku alinifata kituo cha maji akanikata flying kick ya maana kabla hajanchapa makofi mazito mazito. anapotoka kilabuni lazima apitie shambani kuangalia kama mumemwagilia miti ya ulanzi
R.I.P Jemedari/mkoloni/Joslin/Mshua
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]pole sana mkuu
 
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
Huyo alikuwa zaidi ya mkoloni
 
Nakumbuka siku ya ckukuu nipo na madogo tushapanga kwenda zetu swimming na wana mtaani tushavaa tunaaga tu ili tupewe pocket money Mzee akasema haya chukua madaftari mezani kusoma hamna kutoka..dah full Kuchek tukamvizia kalala tukatoroka,kwenda swimming tukakutana na janga mtu kazama kafia ndani ya kina na aliyegundua ni mdgo wangu bas ikabidi aende peleka maelezo kituoni.daah na tulitoroka..kurudi tumekuja chukuliwa kituoni nyumbani tulichapwa na mbao sio fimbo [emoji23][emoji23][emoji23]..ukoloni kweli yan ckukuu mchana usome kitaingia kweli.
 
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]
 
Nimekulia Lugalo ndani. Dad NI mjeda mstaafu kwa sasa. Nilipewa amri nikitoka shuleni SAA saba hakuna kwenda kutembea. Kazi NI kufungulia vifaranga vya kuku na bata na kuanza kuvichunga kunguru wasivichukue. Kikichukuliwa kifarana kazi NI kumfukuza kunguru kwa mawe mpaka nimnyang'anye hata kama kimekufa. Nakwenda kukilaza bandani. Akivihesabu vikipungua anaangalia bandani akikikuta kimekufa anakwambia KATOE KIFARANGA KIMEFIA BANDANI. akiambiwa kilichukuliwa na kunguru, viboko vya kulala mezani. Nampenda BABA yangu kwani alinifundisha kutokuwa mzururaji kama mwanafunzi wa mbeya
 
Daaa vimbwanga vya wazee wangu vingi xn ,,mojawapo anakununulia nguo over size lengo usimsumbue eti unakuwa nazo ,unajkuta upo class 3 lakini shati adi magotini ka kanzu ,kaputula adi kwenye visigino ,,pia bibi yangu anakzingua hapiki ka hujafanya anavotaka na akienda ulabuni kwenye kindoo chenye unga anachora lipicha lolote ju ya unga complex ili ukchota unga upke lazima aje atambue so nilkuwa nachora pembeni lipicha lake nachota unga then naichora tena picha ju ya unga
 
Hyo ya kuchora unga duuu nimenyoosha mikono juu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…