Tukumbushane: Ulishawahi kuanzisha vagi au kuanzishiwa vagi Mtaani?

Tukumbushane: Ulishawahi kuanzisha vagi au kuanzishiwa vagi Mtaani?

Mmmh, hivi niliwahi kupigwa kweli mm sidhani, lbd mambo ya fumanizi fumanizi ndiyo nimebobea sana [emoji12] [emoji12]
(Joking)
 
Kuna siku nilikuw nimeenda club bn..
Nikatumia bapa za kutosha mpk akili akiwa sio yangu tena. Pembeni angu kulikuw na mrembo , kama kawaida yetu nikamfata bana. Kumbe alikuw na jamaa ake
Yule jamaa ake akanikazia kidg, nikaona isiwe tabu bn nikamtia kitasa
Kumbe jamaa alikue na kundi lake kam la watu 12 iv. Wakanivamia, nahic nilikula scale kubwa zaid ambayo cjawahi kuipata tangu nianze vurugu mpk nikakata moto.
Nimekuja kustuka saa 10 alfajir nipo mtaroni tena mvua ndo ilikuw imeanza kunyesha.
Siku ile siwezi kuisahau mimi


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hahaaaaa umenikumbusha mwaka 2013 niko na Demu fulani hivii maeneo ya relini saa mbili unusu!
Niko namtomasa mtoto Zubedaa mara kaka yake akatingaa huyoo aisee nikapagawa, Jamaa akataka afosi anijue mm ni nani Demu akamkazia hataki animulike na tochi Huku na huku mara wakavaana wakaanza kutembezeana mkono wao kwa wao..
Muda wotee huo nimekaa sijui hata nifanyaje, nilishindwa kuamua wala kuingila huku moyoni najisemea ugonvi wa ndugu sipaswii kushirikii, dem naona anambinua kaka yake mara anabinuliwa na kakaka yake hadi akabaki taiti tupuuu..
Akili ikanijia nikatoka mbio nikaenda kuita watu wakaja kuamua, Alipotoka Akaja akanikumbatia akaniambia -Mond- wangu achana na hili lipuuzi Nakupenda sana huku ananinywesha juisi mbele za watu..
Toka siku hiyo nilijiona mm ni NYUMBU HASWAA huyu kama ningemuoa ningekua nimepata bodigadi wa maana..

Duuuh I miss you Zubee wangu bin cheupe
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]

sent from my iphone 7 nimeinunua SAPNA pale POSTA
 
Au Daudi na Goliathi.

Nakumbuka nilikuwa Kariakoo mwaka mmoja, dunga dunga akataka kunigeuza kitoweo....mbona nilitaka kuondoka na dhakari zake.
Afu katikati ya soko
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]

sent from my iphone 7 nimeinunua SAPNA pale POSTA
 
Mimi nakumbuka wakati bado chalii wa darasa la 6A sisahau hiyo siku tumetoka kufanya mitihani ya mwisho mwaka,

Tukamaliza vizuri wakati tunapishana pishana baada ya kumaliza mitihani bahati mbaya Mimi naingia darasani Kile kidemu kikawa kinatoka nikakitegeshea mguu kikajikwaa kikaanguka sketi ikapanda kufunika uso.
Bahati mbaya chupi imetoboka wanafunzi walivyoona tundu la chupi kelele shangwe kibao kama unavyojuwa wanafunzi tulivyokuwaga,
Nikashangaa gafla napigwa makofi na videmu kama kumi ivi akiwemo na yule chupi iliyotoboka nilikula makofi mchanganyiko alafu yanauma kinoma

Nimejitahidi kufurukuta huku na kule nikabahatisha kukunja ngumi nikaitupa kama kurusha jiwe gizani bahati mbaya nikampata kidemu kimoja ngumi ya ziwa nikaona wametulia kama sekunde tatu ivi naona kile kidemu kama kinalegea , kuangalia kwa mbali naona mwalimu anakuja na viranja wawili kurudisha macho kwa kile kidemu naona kimelala chini.
Nilipata wazo na kutoka mbiyo naskia sauti ya mwalimu kwa mbali mkamateni,
Hiyo mbiyo niliyo toka nayo hapo na kundi la wanafunzi waliokuwa wananikimbiza nikaona hapa naenda kusimamia nyumbani.
Kutokana hapakuwa mbali sana kama mita 400 iv nilipofika nyumbani nikaingia chumbani wanafunzi wamefika nawasikia kwa getini Odi,Odi,Odi dingi akatoka naskia wanamsalimia mzee shimoo baba mimi apa,
Walipoulizwa kuna nini naskia tumetumwa tumkamate tumrudishe shule walikuwa wanapigana, walipoulizwa kwani yuko wapi wakasema kaingia ndani, mzee akaanza kuita kaita kama mara tatu nikatoka, ananiuliza mbona umevimba na maalama ya makofi nikamwambia ukweli
Kwa mana mzee wangu alikuwa mkali kinoma. Akaniambia nikupeleke shule mimi mwenyewe au unaenda mwenyewe, nikamwambia naenda mwenyewe, nikatoka tena pale nimekabiziwa kwa wanafunzi twende nao, wale wanafunzi wananipeleka mperampera alafu kulikuwa na Majeba mawili yanataka kuninyanyuwa juu juu yaende kupata sifa .., Itaendelea

kwa mana kilichotokea kingine baada kuanza kunyanyuliwa mara unazomewa kitafata kwa sasa natakiwa nilale kesho kazini.

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]

sent from my iphone 7 nimeinunua SAPNA pale POSTA
 
Nakumbuka One time nipo kwenye sherehe ya binamu yangu kipaimara it was wayback nimekaa zangu kimya kama nimelazimishwa kukaa pale.. Kuna vijana wa mitaani walikua wanazengea msosi kama unavyojua mambo ya uswazi.. Tangu nimefika asubuhi kuna kabint nilikua nakaona kanazunguka pale Mara katumwe vocha na wageni waalikwa kalikua kapoleee na sio kabishi.. Muda umefika wa kula chakula watoto walikua ni wengi balaa wakapewa portion yao maskini wababe wakala watoto wakakosa.. Utafanyaje sasa Shea yao haikuepo.. Nipo zangu ndani maana Nyumba ilikua na uzio hata cjaanza kula nkakaona kale kabinti kanashangaa tu kwa nje midomo imekauka tumaini la kula limepotea.. Roho ikaniuma.. Japo walikua wengi kwa nje lakini wengi wao walionekana wanatokea familia za jirani.. Na walikua watundu na wabishi mno.. Basi nkaona isiwe tabu nikatoka nje ya geti na kukaita kale kabinti.. Ile nafika tu nkakutana na vivulana flani ivii kuniona tu vikaanza kunitania utani wa kikubwa haswa wezere language... Hua spend mtu ayaseme makalio yangu.. Nkaachana nao na kukachukua kale kabinti mpaka jikoni nikakapa msosi kwenye sahani kila mtu kwenye sherehe ananishangaa tu.. Nkarudi ukumbini nikakaa nako jirani.. Mgao wa vinywaji umepita nkakapa soda kakawa kanakula.. Badae nkaitwa ndani na Uncle eti hajaniona tangu nimefika.. Nikawa nimesepa like 5 min ile narudi nkakuta pale amekaa mgeni mwingine aliechelewa kufika na kale kabinti hakapo.. Kumbe kamefukuzwa na wamama wa pale kakaambiwa kakalie kule nje.. Kufika nje nakuta wale vijana wameshika sahani wanakula na soda wanagawana.. Nikawachukulia poah tu wamemaliza kula kama nguruwe wakatupa sahani wakakimbia na chupa.. Nikamchukua Dogo nikaja nae ndani akiwa analia nikampa msosi mwingine nikamwambia kaa hapo usitoke.. Kakamaliza kula kakarudisha sahani maskini kakashukuru kakaondoka.. Nikakaita na kukapa sh. 1000 then nkaendelea na Mishe zingne pale.. Badae kidogo naskia naitwa nje na mmoja wa vibinti pale... Wee Dada.. Hawa wakaka wamempokonya Lisa hela ulompa.. Nikatoka nje na hasira za ajabu kufika nawakuta wale vijana.. Kuniona wakanichukulia poaah.. Nikakamata wawili mmoja akakimbia nikashusha kerbu za maana na hivi nilikua nimevaa suruali kivumbi kilitoka pale.. Nilishusha mnyigo wa maana mpaka nakuja kuwaachilia kila mmoja alipita njia yake... Sherehe ikasimama ghafla kila aliehadithiwa kile kisa akabaki anacheka na kustaajabu.. Nikatafta bodaboda nikageuza zangu home.. Mpaka Leo cuzoo hua hasau like tukio...
Maelezo yotee hayo nmeelewa kwenye wezere tu
 
Hahahahaha hii noma sana umenikumbusha time fulani kitambo tulikuwa na mechi za kitaa
Day moja hiyo tukajichanganya kuna watoto wa kota waliomba tucheze nao game tukazama kambini kwao kukisanua.
Game tulianza vizuri tu sasa tulivyo wapiga goal tu mpira ukaanza vurugu game ikawa na boot kinoma hapo unaombea game iishe tu maana boot zaidi ya league ya bundasliga ka kipindi kile.
Kumbe watoto wa kota game inaendelea wengine wafata faru na mikanda majumbani kwao mzee ilikuwa noma.
Game imeisha hivi ilibidi kila mtu ajue njia ipo wapi maana tupo kambini ila ilibidi tuanze kushughulika nao mmoja mmoja wakipita mtaani maana kambini walileta ubabe
Nasi tukawa tunawawinda kitaani tu.


Mtoto wa kambini kila akipita kitaani kazi alikuwa nayo ni kichapo tu.
 
Me hua nakinukisha tu kuliko vyoo vya baa hasa mtu anaponizingua na najua kabisa sina kosa ila anataka kuniletea za kinyonge sijui niwahadithie ipi?? Ila poa acha nianze na hii :

Ilikua shule ya msingi na ilikua kila siku naandikwa kwenye majina ya wapiga kelele kuna siku hiyo sasa nikasema nikae kimya siku nzima nione itakuwaje cha kushangaza bado nikawepo kwenye list ya noise maker japo sijawah kukanyaga arusha(joking) na kama kawa nikachezea kichapo cha mwalimu huyo anapiga kama kakufumania na mkewe basi kichwani nikajisemea leo mda wa kutoka mguu wa shingo mguu wa roho lazima huyu monitor anijue vizuri kama mimi mwenzake chekechea china

Itaendelea...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilipewa pass ya kwenda kung'oa jino Mawenzi hospital, ilikuwa Ijumaa niliamua kuingia disco kbla ya kurudi shule J'mosi. Sasa kulikuwa na wavulana wawili wananifukuzia kheri si nikawakuta wote ndani, kila mtu anataka kuwa na mimi ugomvi disco lilifungwa.

Moshi si kuwa ninajulikana vijana walitaka sana kumjua manzi aliyesababisha disco kufungwa na police kuingilia, wakati huo nilishachukua tax na kutokomea.
 
Hahahaha
Umenikumbusha nilipoanzishiwa vagi pale Blue bird hotel Sinza, kisa walihisi niko na mume wake ndani (mwanamke alikuja na shoga zake)
Huku na huku meneja akaja, mlango ukafunguliwa, tupsi likaingia, kuangalia sio mume wao.
Wakaomba radhi, wakasepa.....
Baada ya wiki 2 nikakutana na yule dada MK bar Kinondoni (aliyekuja Sinza kumtafuta mumewe chumbani kwetu) nilimuanzishia vagi, mpaka nikalala Oysterbay maana yule bwana alinimwaga kwa kujua eti ile varangati nilipanga mimi na yule mwanamke ili kumchomoa pesa.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] we ni kiboko ya uchafu; mi cjawahi kugombana jmn afu nikikasirika cwez kuongea nalia tyu mpka Leo!!ila nilikuwa na best yngu hyo ngumi mkononi c anajua mi muoga MTU akinichokoza tu ananunua ugomvi wee hakubali kushindwa wakawa wanamuita ngumi jiwe [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12]
 
Nishaanzisha mavagi mengi saaana mana utata upo damuni ila sitasahau matukio matatu.
MOJA
Nikiwa darasa la tano tulikua na mobb tunazamia shughuli za watu hatar. Sasa siku moja form four kwny shule ya wilaya nlokuwepo walikua na graduation mm na mobb yangu tulifanya kila tuwezalo kuzamia ukumbini tukashindwa basi tukaamua tuvuruge ukumbi ulikua na fensi ya tofali ila juu wazi tukatafuta mayai viza tukayarusha ukumbini yakawapata watu kadhaa. Ebana nakumbuka ilikua jioni km saa moja ivi sasa walivotoka kutafuta walorusha mm nikajishtukia nikakimbia baba ili toka troop kunikimbiza nakumbuka enzi hizo nilikua kadogodogo nachomoka hatar ila ilitokea njemba moja mbele yangu ikanirukia km swala. Nilichezea kichapo hicho km mtu mzima nikiwa hoi full damu wakanipeleka kituoni. Sasa wasijue OCS ni mother angu na kipindi hicho bro wangu wa kwanza sahv marehemu alikua likizo ni mjeda na muda huo wananipeleka kituoni alikua huko na maza. Kufika kituoni watu km sita ndo wameniweka mtu kati mara ghafla bro hyu kwanza akajua nimepata ajali kumbe kichapo si wale jamaa wakajichanganya kusema wamenipiga kisa nimeharibu sherehe wakat huo na mother akatoka nje ananiona navuja damu ebana kibao kikawageukia walikula kichapo heavy na vichura na kugharaghara sana tu. Sema nilivyorudi home dingi alivyopewa udaku akanipa tena kipigo nilimind sana siku hyo.

PILI
Tulikua field ya mwaka wa kwanza Dodoma tumekula pombe saaana pale carribean bar karibu na bunge mida ya saa tisa tukakubaliana twende mnadani kula mbuzi. Tukapanda coaster sasa kutokana na nilikua maji nilikua nazingua kinoma ndani ya gari baada ya muda kidogo nikaanza msumbua dereva asimamishe gari nichimbe dawa raia wakawa wanadai asimamishe toka lini daladala ikasimamishwa kuchimba dawa nikatishia ntakojoa humohumo dereva ikabidi asimame wakat huo nitema lugha ya malkia tu sasa wakat nafika mlangoni kuna jamaa yanki tu akaniwekea mkono kifuani akidai siwez shuka dereva aondoe gari sasa mm nikiwa maji enzi hizo sifikirii Mara mbili nikampa BONGE ya ndoo kuna ni vile vijeda vilivyopo depo makotopora bana na vipo km sita mule nilichezea kipigo kitakatifu km niko arena vile na wakasema gari break ya kwanza kambini wakanionyeshe uanaume ulivyo dah pombe zilikata. Pona pona ni kuna bibi mmoja alikua amekaa siti moja na mm wakat huo nipo siti ya dirishani akaanza waambia anataka shukia kituo kinachofuata haiwezekan wampitishe na hana hela ya kurudi si ndo kosa lililofanyika hilo nikafungua dirisha huku gari linaelekea kusimama nilivojirusha nje hata wanajeshi wenyewe walisema kwel mm kamanda kila mtu alifumba macho basi speed nlotoka nayo hapo Mungu ndo anajua.

TATU
Nikiwa likizo home ndo ya kwanza tokea niajiriwe sasa nilijipanga kwel kwel kwenda kula likizo tulikua na braza angu na ndugu yangu mmoja tulikua tunakula bia 24/7 mana nilipanga kukaa wk mbili na niliandaa laki ya kila siku kula bia siunajua wilayan hakuna mambo mengi so ilitosha mno. Sasa mm sijulikani sana huko wilayan kwetu na kuna wanajeshi wengi na walikua wameshushwa km 600 kwny operation maalum so kumbe tule tuanajeshi vijana tulikua tunamind sana rohoni navyokula monde wakat vyenyewe ndo talk of the town. Siku moja km saa tano usiku ivi braza na yule ndugu yangu wakiwa chakari wakazinguana nikawa nawasuluhisha vile vijeda si ndo vikapatia upenyo wa kurevenge vikidai nawapiga ndugu zangu ambao ni rafiki zao vilinipa vinu vya hatar sema safar hii nami nilimuachia mmoja alama nilimpiga kichwa hicho nikatoka na jino lake kwny paji la USO hfu mi nduki asubuh nikaamkia barabarani hyoo Dar.
Baada ya matukio hayo yote nlitafakar pombe siwez acha ila nliamua kutokua nakunywa nagrp la watu especially kunywa na warembo, pili sinywi kwny bar za ushenzini na nikaanza kula bia expensive tu ambazo siwez kunywa nyingi sasa nastaarabika na mchumba ninae mwaka keshokutwa naoa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jirani,

huyo alijiharibua mwenyewe kwa kuandika jina mwishoni.
.............................................................................

Hii nyingine ndo ilifanya mpka leo kuwa makini na hasira zang.utoto raha sana.
Siku moja niko zangu mitaa ya kwa jirani ila ni karibu na home niko nausuka mpira wangu wa makaratasina na hii mifuko ya plastic,,jirani najua utakuwa unaijua hii mipira..nilipomaliza nikaanza kijipigisha danadana kumbe kuna mkaka alikuwa akiangalia kila kitu ninachokifanya (nilishawahigi kumtia kinazi (ndoo) ndg yake.kumbe aliniweka kiporo)

Sina hili wa lile jamaa akauchukua mpira wangu halafu akaniambia sikupi (jamaa alikuwa mkubwa kwangu nisingweza kumpiga) nilimuangalia kwa hasira nikajikuta nalia.ebwana nikajikuta natetemeka mwili mzima.kuangalia kushoto kuna tofali la udongo mbele yangu kuna jiwe.

Sikujua ni saa ngapi nililishika jiwe ila nilichokishuhudia ni yule kaka katupa mpira wangu chini analia na damu zikimtoka.ohoooo kuona hivyo mbio mpka kwa rafiki wa mama yangu wa kimasai nikampa mkanda mzima.akanambia kaa jion nitakupeleka nyumbn

Uko nyuma sasa mkaka wa watu kapelekwa hospital kashonwa nyuzi kama sio nane basi ni sita na ilibaki kidogo lile jiwe limlenge jichoni.

Jion nakuja kurudishwa kila kitu kimeshakaa sawa kule nilikoharibu kimbembe ni kwangu sasa..jmn baba aliniandalia mikwaju ya maana.mwisho wa siku maongezi yakafanyika hali ikwa shwar.

Tangu siku hiyo hadi leo marufuku hasira kuniongoza.

Na nashukuru huyo kaka mpka leo tumarafiki sana.
Jirani wewe ni mtata... hata ukiniita pm siji naogopa vaaagi
 
Unajua kuna baadhi ya wanaume wanadhani wanawake wote ni maboya.
Mie sipendi dharau....
Yaani mie ukinichokoza jua nikitibiwa na kupona,
lazima nikutafute tuanze A.
Niliwahi pigwa stop Masai club, Waungwana bar na pale Igo Sinza....cheza vizuri, ukinibambia tu, kiboya nina wewe.
Halafu virampasi vyako vya sehemu za vilaji... wewe muumini mwenzetu tena dhehebu moja
 
Aisee nakumbuka kipindi cha nyuma kidogo enzi hizo olevel nipo boarding sasa kuna jamaa alikua mwizi kishenz alikuwa katokea Tanga jina lake tukawa tunamwita "mtanga" sasa akawa anaiba nguo, mashuka, soksi,
Watu waka kaa kikao kumsaka mwizi siku ya siku ukaguzi ukaanza kwa wale wanao hisiwa daah kwenye dranka la mtanga tulikuta hadi sabuni, mashuka, nguo, soksi watu wakataka kumshushia kipigo dom leader akaamuru tumpe adhabu akavuliwa nguo, zote akabak
uchi kama alivozaliwa akapewa kipigo kwel mpaka akavimba uso baada ya hapo akatolewa nje daah ilikua aibu
Sasa kimbembe kavimba na anahitaji dawa alivimba usoni jichoni basi siku anaenda kuchukua dawa akamkuta
Matron, matron akamuuliza vip mbona umevimba mtanga akajibu "nimeng'atwa na nyuki" matroni watu walio kuwa karibu nae walicheka sana ila wizi aliacha kabisa
Duuuh..
 
Hahaaaaa umenikumbusha mwaka 2013 niko na Demu fulani hivii maeneo ya relini saa mbili unusu!
Niko namtomasa mtoto Zubedaa mara kaka yake akatingaa huyoo aisee nikapagawa, Jamaa akataka afosi anijue mm ni nani Demu akamkazia hataki animulike na tochi Huku na huku mara wakavaana wakaanza kutembezeana mkono wao kwa wao..
Muda wotee huo nimekaa sijui hata nifanyaje, nilishindwa kuamua wala kuingila huku moyoni najisemea ugonvi wa ndugu sipaswii kushirikii, dem naona anambinua kaka yake mara anabinuliwa na kakaka yake hadi akabaki taiti tupuuu..
Akili ikanijia nikatoka mbio nikaenda kuita watu wakaja kuamua, Alipotoka Akaja akanikumbatia akaniambia -Mond- wangu achana na hili lipuuzi Nakupenda sana huku ananinywesha juisi mbele za watu..
Toka siku hiyo nilijiona mm ni NYUMBU HASWAA huyu kama ningemuoa ningekua nimepata bodigadi wa maana..

Duuuh I miss you Zubee wangu bin cheupe
haha..! NYUMBU kweli wewe!
 
Hahaaaaa umenikumbusha mwaka 2013 niko na Demu fulani hivii maeneo ya relini saa mbili unusu!
Niko namtomasa mtoto Zubedaa mara kaka yake akatingaa huyoo aisee nikapagawa, Jamaa akataka afosi anijue mm ni nani Demu akamkazia hataki animulike na tochi Huku na huku mara wakavaana wakaanza kutembezeana mkono wao kwa wao..
Muda wotee huo nimekaa sijui hata nifanyaje, nilishindwa kuamua wala kuingila huku moyoni najisemea ugonvi wa ndugu sipaswii kushirikii, dem naona anambinua kaka yake mara anabinuliwa na kakaka yake hadi akabaki taiti tupuuu..
Akili ikanijia nikatoka mbio nikaenda kuita watu wakaja kuamua, Alipotoka Akaja akanikumbatia akaniambia -Mond- wangu achana na hili lipuuzi Nakupenda sana huku ananinywesha juisi mbele za watu..
Toka siku hiyo nilijiona mm ni NYUMBU HASWAA huyu kama ningemuoa ningekua nimepata bodigadi wa maana..

Duuuh I miss you Zubee wangu bin cheupe
Mwanangu una-talent ya kuandka Shigongo aende course

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakumbuka One time nipo kwenye sherehe ya binamu yangu kipaimara it was wayback nimekaa zangu kimya kama nimelazimishwa kukaa pale.. Kuna vijana wa mitaani walikua wanazengea msosi kama unavyojua mambo ya uswazi.. Tangu nimefika asubuhi kuna kabint nilikua nakaona kanazunguka pale Mara katumwe vocha na wageni waalikwa kalikua kapoleee na sio kabishi.. Muda umefika wa kula chakula watoto walikua ni wengi balaa wakapewa portion yao maskini wababe wakala watoto wakakosa.. Utafanyaje sasa Shea yao haikuepo.. Nipo zangu ndani maana Nyumba ilikua na uzio hata cjaanza kula nkakaona kale kabinti kanashangaa tu kwa nje midomo imekauka tumaini la kula limepotea.. Roho ikaniuma.. Japo walikua wengi kwa nje lakini wengi wao walionekana wanatokea familia za jirani.. Na walikua watundu na wabishi mno.. Basi nkaona isiwe tabu nikatoka nje ya geti na kukaita kale kabinti.. Ile nafika tu nkakutana na vivulana flani ivii kuniona tu vikaanza kunitania utani wa kikubwa haswa wezere language... Hua spend mtu ayaseme makalio yangu.. Nkaachana nao na kukachukua kale kabinti mpaka jikoni nikakapa msosi kwenye sahani kila mtu kwenye sherehe ananishangaa tu.. Nkarudi ukumbini nikakaa nako jirani.. Mgao wa vinywaji umepita nkakapa soda kakawa kanakula.. Badae nkaitwa ndani na Uncle eti hajaniona tangu nimefika.. Nikawa nimesepa like 5 min ile narudi nkakuta pale amekaa mgeni mwingine aliechelewa kufika na kale kabinti hakapo.. Kumbe kamefukuzwa na wamama wa pale kakaambiwa kakalie kule nje.. Kufika nje nakuta wale vijana wameshika sahani wanakula na soda wanagawana.. Nikawachukulia poah tu wamemaliza kula kama nguruwe wakatupa sahani wakakimbia na chupa.. Nikamchukua Dogo nikaja nae ndani akiwa analia nikampa msosi mwingine nikamwambia kaa hapo usitoke.. Kakamaliza kula kakarudisha sahani maskini kakashukuru kakaondoka.. Nikakaita na kukapa sh. 1000 then nkaendelea na Mishe zingne pale.. Badae kidogo naskia naitwa nje na mmoja wa vibinti pale... Wee Dada.. Hawa wakaka wamempokonya Lisa hela ulompa.. Nikatoka nje na hasira za ajabu kufika nawakuta wale vijana.. Kuniona wakanichukulia poaah.. Nikakamata wawili mmoja akakimbia nikashusha kerbu za maana na hivi nilikua nimevaa suruali kivumbi kilitoka pale.. Nilishusha mnyigo wa maana mpaka nakuja kuwaachilia kila mmoja alipita njia yake... Sherehe ikasimama ghafla kila aliehadithiwa kile kisa akabaki anacheka na kustaajabu.. Nikatafta bodaboda nikageuza zangu home.. Mpaka Leo cuzoo hua hasau like tukio...
Wewe nooma aseeh
 
Back
Top Bottom