Tukumbushane vipindi vya ITV, CTN, na DTV 1994

Tukumbushane vipindi vya ITV, CTN, na DTV 1994

Hahaha we jamaa umenikumbusha nilivyokesha siku moja hadi saa 11 asubuhi nikazidiwa na usingizi nikakosa pambano la Tyson aiseee
Mi siku ile alivyodundwa na Holyfield nakumbuka tulikuwa kama wagonjwa wiki nzima kijiwe chetu chote hakukaa mtu.Kila mmoja alijifungia nyumbani anaugulia😀
 
Mwenye email au simu ya itv nataka niwashauri wamepoteza mashabiki sana zamani walikuwa super kweli sikuhizi ikiisha tu habari basi zamani walikuwa na vipindi vizuri mno wao ndo walileta tamthilia za kikorea zilipata mashabiki sana hata katuni za watoto enzi hizo kina ed edd eddy dexter powerpuf girls ben ten etc
Kweli mkuu hebu waambie warudie
 
Mwenye picha angalau ya Time Trax atuwekee hapa wadau
 
Mimekumbuka pia Tangazo la Coca cola la father krismas ITV lilikuwa la msafara mrefuu wa magari ya coca cola nilikuwa nalipenda sana wakati wa krismas
 
Tangazo la Revola da sijui kwanini walilitoa bora hata wangeliacha you tube alikua miriam odemba yule nazani
Hakuna mdau anaeweza kulisaka popote atuwekee hapa
 
enzi hizo epl iko live dtv, hakuna cha king'amuzi wala malipo labda itokee mgao wa umeme ...lakini tv inakuwa moja mtaa mzima!
Nakumbuka ilikuwa bureee kabisaa mkuu
 
Sijui jengua yupo wapi
Jengua yupo mkuu ameludi tena kwenye hizi bongo movie kuna siku nilimbahatisha nilikua kwenye basi naenda moro waliweka movie yake mi huwa sio mpenzi wa bongo movie sana kwasababu utakuta mtu anawaza miaka kumi iliyopita alafu unakuta picha ya magufuli ukutani kama rais
 
Mwenye picha angalau ya Time Trax atuwekee hapa wadau

5d60274c09a78145579eca2c5fb6d131.jpg
1eee85fd77d9e891c8b9d92e3b219c18.jpg
1b87728dd6dbd994ead275964af97114.jpg
 
Ila ITV wajitahidi warudishe Vioja mahakamani kile kipindi licha burydani kinaelimisha sana
 
Back
Top Bottom