Tukumbushane: Wimbo bora wenye jina la kike...

Tukumbushane: Wimbo bora wenye jina la kike...

Patrick Balisidya, Owen, Jacky, Monte na Shebby Mbotoni na Afro 70 'Wana Afrosa' na Kibao cha HARUSI:

Kuoana ni jambo la sifa,
Na tena ni jambo la fahari kubwa,
Katika historia ya binadamu,


Ni shangwe isiyo kifani,
Kwa watu wawili waliopendana,
kuoana katika ndoa kamili,


Hivi leo Ndyanao na Saibaa mnaona,
Kumbukeni wazi mmetimiza ahadi yenu kwa mungu,\


Harusi mliyofanya ni kiapo kitakachowahukumu,
mara mtakapo jaribu kutengana,

Katika hali yoyote kaeni kwa amani nawausia,
Mpaka kifo kije kuwatenganisha x 2


(chorus)


Jaribuni kuwaepuka marafiki wabaya,
kwani huenda wakaipotosha ndoa yenu,
mkatenganaa, wakawadharau,


Wakumbukeni wazazi wenu wa pande zote,
watapopatwa na shida yoyote ile,
wasaidieni, mtapata baraka,


Kuweni na moyo wa mapenzi kwa mtu,
tena muwe wacheshi kwa kila mtu,
ni sifa kubwaa, mtaheshimiwa,


Kuweni wakarimu wakubwa nyumbani mwenu,
mzaapo watoto wenu muwatunze vyema,
wawe na adabuu, na heshima nyingii,
ndivyo walivyoishi wazazi wetu x 2




Patrick Balisidy aliutunga na kuuimba huu wimbo kwa ajili ya harusi ya dada yake Ndyanao kwa Saibaa kama anayowataja kwenye ubeti wa tatu.

Na huyu Ndyanao ndiye mtunzi wa kitabu cha SHIDA, ambapo wahusika wakuu ni Matika "Shida" na Sefu "Chonya of Chilonwa me"
 
Maria Nyerere Mama mpendwa kwaheri mama Maaria
Pokea shukrani zetu za dhati Maria Nyerere mamaa x2

Kwaaheri Maria Nyerere Mama
Yoyooyooo Poole Mama
Twakutakieni mapumziko mazuri
Pamoja na maisha marefu Mama x2

Mama Maria twakutakia kila la kheri Mama
mama Maria nyerere pole mama mpendwa kwaheri
Pumzika kwa amani mama Butiama kijijini x2
 
Maria Nyerere Mama mpendwa kwaheri mama Maaria
Pokea shukrani zetu za dhati Maria Nyerere mamaa x2

Kwaaheri Maria Nyerere Mama
Yoyooyooo Poole Mama
Twakutakieni mapumziko mazuri
Pamoja na maisha marefu Mama x2

Mama Maria twakutakia kila la kheri Mama
mama Maria nyerere pole mama mpendwa kwaheri
Pumzika kwa amani mama Butiama kijijini x2

duh umenikumbusha 1985 Marehemu Ndala Kasheba alipohama kutoka OSS kwenda kwa mahasimu wake Maquis alikotunga wimbo huu.
 
Mimi Kumi Bora yangu Ni:

1. Selina - Muhidin Mwalimu Gurumo/Mlimani park Orchestre
2. Georgina - Marijani Rajab/Safari Trippers/wanaSokomoko
3. Mariam Cleopatra - Zahir Ally Zorro/Orcherstre Sambulumaa
4. Maumivu Makali - Kasongo Mpinda 'Clayton'/Issa nundu/MK Group (japo haukuwa na jina la kike!)
5. Dada Lidya - Patrick Balisidya/Montgomery Makangila/ Afro 70 band wana Afrosa
6. Christina Bundala - Muhidin Maalim Gurumo/Mlimani Park Orchestre
7. Christina - Marijani Rajab/David Mussa/Safari Trippers wana Sokomoko
8. Hanifa - " " " " " " "
9. Nzowa - Chinyama Chiyaza/Motombo Lufungulo 'Audax'/Orchestre Marquiz Du Zaire Wana kamanyola.
10. Betty - Mbaraka Mwishehe Mwaruka/Morogoro Jazz Band

Selina ulitungwa na Joseph Mulenga ingawa Gurumo ndiye muimbaji
 
Ooh selina piga konde moyo ooh selina ooh selina tutafanikiwa ooh selina aah


Sent from my Nokia 8310 using Tapatalk
 
Ziada- (Kabeya Badu) IOSS


Sent from my Nokia 8310 using Tapatalk
 
......Old is Gold, kila nyimbo inanirudisha sehemu mbali mbali na kumbukumbu za miaka mingi nyuma!
 
Back
Top Bottom