Tukumbushane: Wimbo bora wenye jina la kike...

Tukumbushane: Wimbo bora wenye jina la kike...

Jamani jana nilikuwa naiona thread hii na kuipita lakini leo imenikumbusha mbali sana hongera Balantanda nimekuvulia kofia......

kuna wimbo mmoja sijui kama mmeutaja... Kosa la mesenja....sijui uliimbwa na nani.....
messenger alipotoka posta ofisi ikawa imefungwa akaipeleka barua nyumbani kwa bosi ila bosi hakuwepo akaipokea wife... alipoifungua maandishi yakawa yamelalia kushoto... ikawa kasheshe sijui mnaukumbuka, Balantanda, Sikonge nisaidie beti zake.
 
Kuna Chrstina ulioimbwa na Bushoke(Niliichezea kamari roho yangu....),na mwingine Christina Moshi ulioimbwa na OSS wana Ndekule

Balantanda x-tina bundala la nginde ndio soo...
Humo Gurumo kaingia akisema...

Kwa kweli mpenzi x-tina leo naomba unisamehe...
Niite uniongoze kwenye penzi letu la hakii..

Chorus:
Niliichezea kamali roho yangu
Na kuuza utu wangu
Kwa wasio thamini penzi wala kujua maana ya kupenda...

Gulumo
Nilihadaikaa na anasa za dunia
Nilihangaikaaa na anasa za dunia
Binadamu hujifunza kutokana na makosaa
 
mama nipe naulii
Nikamfate monica
Amekimbia zambia
Na treni ya mizigo...

Kisa cha kukimbia
Madeni yamemzidi
Doti kumi za kanga
alizokopa hajalipa eeeh...
 
Daudi Kabaka...

Msichana wa sura nzuri
Kitu gani kinakufanya usiolewe
Elimu unayo ya kutosha
Hata ng'ambo ukaenda ukarudi

Ooh baby Ona vijana wa rika lako
Wameolewa wamekuacha ukihangaika...
 
salaam nimpe nani
Mpenzi salaama eeeh
Hata zikufikieee popote ulipo dada
Sina wa kumuamini nachoka kuhangaika eeh,
Naomba tukuane mimi nawe salama eeh...

salama anayeimbwa hapa sio huyu chizi ooohooo msichanganye wadau
 
Amisa eeeh eeeeeh
Amisa ooooh ooooh oooooh...

Nimetokea kumpenda mpenzi wangu amiisaa....

Hah hah hah haaaaa jamani huyu ni Dr alifall kwa mkagulu aliyeukana ugogo
 
Msomdo walikuwa na ngoma yao Jack...

Mtotoo Jack eeh mpenzi wangu, najaribu kukusahau lakini nashindwa, labda ni kwa ile ndoto inayonisumbua, naota unaniletea kifuko cha zambaru...

Sauti yako nyororo inaniuwa sana, na mwendo wako wa maringo unanikondesha mammamaaa
Kama sio kampara ni Tanzania Mamaa Jack yeh yeh yeh ooooh mamaaa....
 
Jamani jana nilikuwa naiona thread hii na kuipita lakini leo imenikumbusha mbali sana hongera Balantanda nimekuvulia kofia......

kuna wimbo mmoja sijui kama mmeutaja... Kosa la mesenja....sijui uliimbwa na nani.....
messenger alipotoka posta ofisi ikawa imefungwa akaipeleka barua nyumbani kwa bosi ila bosi hakuwepo akaipokea wife... alipoifungua maandishi yakawa yamelalia kushoto... ikawa kasheshe sijui mnaukumbuka, Balantanda, Sikonge nisaidie beti zake.


Wimbo huu uliimbwa na Maxmillan Bushoke akiwa na Bima Lee Orchestra wana Magnet Tingisha,ni wimbo mzuri sana maana ulikuwa kama jamaa anwahadithia watu stori flani hivi.....

Wee Mesenjaa,hallow Sekretari(naam bosi) Mesenja yuko wapi(sijui bosi)
Mara Mesenja anaitika naaam bosi nilikuwa uani tumbo linaniletea matatizo mimi
Nae bosi anasema nenda Post office kachuke barua za ofisini na za nyumbani,za ofisini leta ofisini na za nyumbani peleka nyumbani

Kama inavyoeleweka kazi ya Mesenja ni kutumwa Posta au ofisi za nje na shughuli nyingine zinazohusu kutumwana kiofisi(rudia tena)

Mesenja kaleta balaa nyumbni kwa Meneja bila kufahamu(Mesenja kaleta balaa nyumbani kwa Meneja bila kufahamu)

Wakati anakwenda Post office anawaza moyoni mzee mie darasa la 3 la mkoloni nyumbani mke wangu na watoto wangu wamelalia ugali wa muhogo na sunga la kuchemsha jana,kutoka Post office kapitia Kariakoo,kaingia mitaaani anaikimbiza mia wakati siku hizi mia imeota matairi Mesenja hajatahamaki ni saa 7 na nusu wakati osisi zinafungwa saa 6 na nusu mchana

Mesenja kaleta balaa nyumbni kwa Meneja bila kufahamu(Mesenja kaleta balaa nyumbani kwa Meneja bila kufahamu)

Kakimbilia ofisini kakuta ofisi imefungwa na mlangoni yupo mlinzi kajaribu kumbembeleza zile barua akakataa akaamua kuzipeleka nyumbani kwa bosi wake alimkuta mkewe bosi na kumpa zile barua za ofisini na za nyumbani,mkewe bosi kapokea zile barua akaamua azitazame zile za ofisini kwa kuwa si desturi barua za ofisini kufika nyumbani katazama kaweka kando,katazama barua nyingine anuani maandishi yamelalia kushoto,hati kama ya kike akaamua aifungue na akakumbana na neno Darling kama kichwa cha habari na baada ya kuisoma akazimia nusu saa maskini

Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu(Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu)

Alipozinduka akamkuta mwanae mdogo amamuegemea analia mama nasikia njaa,alimjibu subiri baba ako aje apike,mimi leo sipiki sipakui,analia akisema mimi Baba Kulwa nimemtendea nini mie jamani eee,haya kamjengea nyumba ya ghorofa na gari kamnunulia huyu Darling jamani

Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu(Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu)

Bosi siku hiyo karudi saa 6 na nusu za usiku kichwani ana moja moto moja baridi,kubisha hodi aanza kushambuliwa na maneno,kalale huko huko kwa hao unaowajengea majumba na kuwanunulia magari,ilibidi bosi abembeleze alipoingia ndani kataka tu kumgusa mkewe kidogo,alipigwa kibao na zogo kubwa likaanza,mara maneno,mara kavutwa koti,mara kachaniwa shati...Mesenja kaleta aibu jama

Siri imefichuka siri imefichuka(imefichukaaa) kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu(Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu) kaleta aibuuuu
 
  • Thanks
Reactions: Iza
Hapa zangu ni hizi:

Georgina - Marijani
Christina Moshi - Ndekule
Zuwena - Marijani
Maria - Vijana
Neema - Sikinde
Sauda (MV Mapenzi) - Sikinde
 
Clara- Sikinde. Wimbo huu Kitwana amelazwa na anamtuma mwenzake ambaye yu karibu kutoka Hospitali.

Ubeti wa 1
Unajua mwenzangu karibuni utatoka hospitalini,
Utokapo tafadhali, fika mjini umtafute mpaka umuonee mchumba wangu Clara, Mchumba wangu Crara!

Ubeti 2
Nyumbani anapoishi ni Msimbazi Kota
Ukimuona mpe salamu nyingi sana
Mueleze Mchumba wako Kitwana, anakusalimu...

Kiitikio:
Tafadhali, ukimuona muulize kama kweli Clara yuko radhi niteseke hospitalini

Nyimbo nyingine nazokumbuka ni

1. Colleta- Marquiz
2. Nia- Mlimani Park, huu wimbo ukipigwa hata leo utafurahi
 
Sawa wakuu.. nadhani zile nyimbo zilizovuma sana wakati ule zenye majina ya kike karibu zote tumezitaja nyingine ni nyongeza tu; sasa naomba kila mtu aje na kumi bora ya nyimbo hizo... halafu tutazishindanisha ili hatimaye tupate 5 bora na hatimaye the best Tanzanian female named love song of all times!
 
Vipi malaika iliyokuwa copied na kuleta kasheshe?
 
Sawa wakuu.. nadhani zile nyimbo zilizovuma sana wakati ule zenye majina ya kike karibu zote tumezitaja nyingine ni nyongeza tu; sasa naomba kila mtu aje na kumi bora ya nyimbo hizo... halafu tutazishindanisha ili hatimaye tupate 5 bora na hatimaye the best Tanzanian female named love song of all times!

Kwangu mimi 10 bora ni hizi(hakuna ya kwanza wala ya mwisho)..Nimepata tabu sana kuchuja nyimbo nyingi zilizopo hapa jamvini na nyingine nilizonazo maana karibu kila nyimbo ninayoiona ni BORA...Hata hivyo baadaye nikaja kufikia muafaka kwamba hizi hapa chini ndizo nyimbo zangu bora 10 zenye majina ya kike;

1.Christina Moshi-OSS wana Ndekule

2.Pamela-Less Wanyika

3.Clara-DDC Mlimani Park Orch

4.Asha mwana Seif-Juwata Jazz Band

5.Maria-Vijana Jazz Pambamoto

6.Jacky- Nico Zengekala na Les Cuban

7.Neema-DDC Mlimani Park Orch

8.Georgina-Marijani Rajab

9.Queen Case(Cathy?)-Juwata Jazz Band

10.Vicky-The Bantu Group Band
 
Paulina, sijui umeimbwa na nani - Marijani Rajabu? una maneno haya... Paulina mamaa shemeji naleta mashitaka ee sielewi lengo la nduguyo ooh... kiitikio... Paulina mimi ninakwita, nimeshayakubali makosa, njoo mama tulee watoto... mimi naapa sitarudia tena...


Annina

Ni Less Wanyika walioimba wimbo huu
 
Sawa wakuu.. nadhani zile nyimbo zilizovuma sana wakati ule zenye majina ya kike karibu zote tumezitaja nyingine ni nyongeza tu; sasa naomba kila mtu aje na kumi bora ya nyimbo hizo... halafu tutazishindanisha ili hatimaye tupate 5 bora na hatimaye the best Tanzanian female named love song of all times!

Kumi bora za Ibra ni hizi:-
1. Neema- Mlimani Park
2. Celina-Mlimani Park
3. Nia- Mlimani Park
4. Hiba- Mlimani Park
5. Salama- Dar International
6. Siwema- Dar International
7.Solemba- JUWATA/OTTU
8. Julie- Washirika Tanzania Stars
9. Fatuma- JUWATA
10. Editha- Mlimani Park
 
Wimbo huu uliimbwa na Maxmillan Bushoke akiwa na Bima Lee Orchestra wana Magnet Tingisha,ni wimbo mzuri sana maana ulikuwa kama jamaa anwahadithia watu stori flani hivi.....

Wee Mesenjaa,hallow Sekretari(naam bosi) Mesenja yuko wapi(sijui bosi)
Mara Mesenja anaitika naaam bosi nilikuwa uani tumbo linaniletea matatizo mimi
Nae bosi anasema nenda Post office kachuke barua za ofisini na za nyumbani,za ofisini leta ofisini na za nyumbani peleka nyumbani

Kama inavyoeleweka kazi ya Mesenja ni kutumwa Posta au ofisi za nje na shughuli nyingine zinazohusu kutumwana kiofisi(rudia tena)

Mesenja kaleta balaa nyumbni kwa Meneja bila kufahamu(Mesenja kaleta balaa nyumbani kwa Meneja bila kufahamu)

Wakati anakwenda Post office anawaza moyoni mzee mie darasa la 3 la mkoloni nyumbani mke wangu na watoto wangu wamelalia ugali wa muhogo na sunga la kuchemsha jana,kutoka Post office kapitia Kariakoo,kaingia mitaaani anaikimbiza mia wakati siku hizi mia imeota matairi Mesenja hajatahamaki ni saa 7 na nusu wakati osisi zinafungwa saa 6 na nusu mchana

Mesenja kaleta balaa nyumbni kwa Meneja bila kufahamu(Mesenja kaleta balaa nyumbani kwa Meneja bila kufahamu)

Kakimbilia ofisini kakuta ofisi imefungwa na mlangoni yupo mlinzi kajaribu kumbembeleza zile barua akakataa akaamua kuzipeleka nyumbani kwa bosi wake alimkuta mkewe bosi na kumpa zile barua za ofisini na za nyumbani,mkewe bosi kapokea zile barua akaamua azitazame zile za ofisini kwa kuwa si desturi barua za ofisini kufika nyumbani katazama kaweka kando,katazama barua nyingine anuani maandishi yamelalia kushoto,hati kama ya kike akaamua aifungue na akakumbana na neno Darling kama kichwa cha habari na baada ya kuisoma akazimia nusu saa maskini

Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu(Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu)

Alipozinduka akamkuta mwanae mdogo amamuegemea analia mama nasikia njaa,alimjibu subiri baba ako aje apike,mimi leo sipiki sipakui,analia akisema mimi Baba Kulwa nimemtendea nini mie jamani eee,haya kamjengea nyumba ya ghorofa na gari kamnunulia huyu Darling jamani

Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu(Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu)

Bosi siku hiyo karudi saa 6 na nusu za usiku kichwani ana moja moto moja baridi,kubisha hodi aanza kushambuliwa na maneno,kalale huko huko kwa hao unaowajengea majumba na kuwanunulia magari,ilibidi bosi abembeleze alipoingia ndani kataka tu kumgusa mkewe kidogo,alipigwa kibao na zogo kubwa likaanza,mara maneno,mara kavutwa koti,mara kachaniwa shati...Mesenja kaleta aibu jama

Siri imefichuka siri imefichuka(imefichukaaa) kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu(Siri imefichuka siri imefichuka kosa la Mesenja kaleta balaa kosa la Mesenja kaleta aibu) kaleta aibuuuu


Asante sana Balantanda huu wimbo nafikiri wa miaka ya 80s niliupenda sana na ujumbe wake ulikuwa wazi kabisa enzi tunazamia disko Bwiru Girls Sec safi sana mkuu.
 
Back
Top Bottom