Uchaguzi 2020 Tulia Ackson ameshashindwa kabla hata kampeni hazijaanza

Wacha uwongo. Nyie ndiyo mnamshauri vibaya Tulia. Kaangalie hizo clip ndiyo uje kuandika humu
 
Vijana wanaandamana kwa amani kabisa bila shida yoyote.

Asante Robert Amsterdam, asante Vyombo vya dola kwa kuelewa watanzania wanataka nini.
Chadema bure kabisa, yaani mawakili wote waliojaa mfano Kibatala nk hamuwaoni Hadi muambiwe na Hilo beberu lenu Amsterdam.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Mwambie mbunge aliye maliza muda wake ajiandae kuendelea kuandika mashairi. Arudi kwenye taaluma yake ya utunzi wa mashairi. Juzi alipokuwa anajibishana na yuke OSS inaonesha uzoefu wake katika tabia za kihunihuni bado anao. Maana alianza kwa kumchimba afande mkwara mbuzi baadaye akalegea kama mlenda.
 
Hekima na busara inahitajika sana kwenye baadhi ya majimbo kwenye huu uchaguzi.. Maamuzi ya wananchi yaheshimiwe na si vinginevyo, kuna picha naiona si nzuri kama wazee wenye hekima na busara hawatashauri kitu..
 
Mlianza hivyo hivyo eti Chadema iko Facebook tu na nyuma ya keyboard.

Afterall mbunge aliyemaliza muda wake ni sugu hapo hapo Mbeya na alichaguliwa na hao unaoita hawapigi kura.
Mwaka 2015 Sugu alikuwa mbunge aliye chaguliwa kwa kura nyingi kuliko wabunge wote nchini.
 
Mlianza hivyo hivyo eti Chadema iko Facebook tu na nyuma ya keyboard.

Afterall mbunge aliyemaliza muda wake ni sugu hapo hapo Mbeya na alichaguliwa na hao unaoita hawapigi kura.

Huyo Sugu alibahatika kipindi kile cha CCM ronyaronya. Kipindi hiki asahau ubunge. Huyu Tulia ni among wanawake ambao ni asset kwa Tanzania, ni kichwa, msomi, anajiamini, anauelewa wa hali ya juu ni presidential material, etc. Kwa Taifa linalojielewa kama Tanzania lazima angaliwe kwa karibu huyu na kwa umakini wa hali ya juu Wengine tuligundua kipaji chake tangu bunge la katiba.
 
Hapendwi Mbeya period. Hata kwao Rungwe nako hawamtaki ndiyo wakamsukumiza Mbeya. Huku nako anagawa RUSHWA tu kwenye misiba . Hela zake wanakula na atashangaa
Tulia Akson atakuwa mbunge kwa njia haramu za kupora jimbo lakini kwa kura halali hawezi kuwa mbunge kamwe
 
ccm wajitafakari sana na kuelewa kuwa jamii ilishawachoka na waache kulazimisha mambo! ndio maana wanaojifanya ni ccm mchana usiku wako upinzani hasa chadema.
CCM wengi hasa watumishi wa umma ambao hawajapewa Nyongeza za mishahara kwa miaka 5 wamelazimishwa kuhamia Dodoma familia zipo huko Dsm wanaipenda chadema toka moyoni
 
Huyo mtoto wa kike bora atulie nyumbani ampikie chai mume wake, ule umati wa jana wa Lissu utakuwa umemmaliza nguvu kabisa, japo anasubiri kupewa ushindi wa wizi, lakini ajue fika hiyo kazi haitakuwa rahisi hata kidogo.
Mbeya wamejipanga kumsomea Albadiri kubwa endapo atampora ushindi Sugu, mbeya watamlaani hawataki mwakilishi batili
 

Maamuzi ya wananchi lazima yaheshimiwe, kama issue ni kipaji zipo namna nyingi za kumgroom sio lazima awe mbunge...otherwise tubadili katiba na ubunge uwe ni matakwa ya dola kuamua nani awe mbunge na sio maamuzi ya wananchi..Hekima na busara ni muhimu sana..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…