Tulia Ackson atoa msimamo wa Bunge, asema Rais ni Mkuu wa Nchi na ana mambo yote!

Katiba ni nzuri haina tatizo lolote,, shida kubwa uliyonayo ni hauna cheo tena,,
Kwanini hata msiimbe kama kina Diamond ali kiba harmonies, ili mpate hela kwani lazima uajiriwe serikalini?
Au uwe mcheza mpira kama kina khalfan ngasa, etc,
Unapata hela zako hazina mawazo, wala ulalamishi wa kutwa mitandaoni,,
Kama muzic au mpira huwezi,, cheza hata boxing,, mbona vijana wanaishi tu?
Sio lazima upate cheo, kama vipi njoo tulime mpunga huku mpanda, no stress, no nothing... [emoji23][emoji23]

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
.... as long as uhakika wa mpunga upo sasa na baada ya kustaafu wala hawanaga shida kujitoa ufahamu!
 

[emoji23][emoji23][emoji23], Kupewa vitasa vya kina Dullah mbabe ndio uishi yataka Moyo sana.

Naamini kila mtu anapambana na hali yake, japo nafsi ikiwa inamfukuta vile wahuni wanavyochezea Kodi zetu na Kujigawia Uongozi bila ridhaa ya Waongozwaji.
 
Hii nchi yetu haina viongozi.

Walau January Makamba ameonyesha mshangao kwa matamshi hayo ya Naibu Spika ila sasa sijui kama atasalimika maana Mama nae anapenda wapiga makofi.
Wewe kuna kitu huelewi, KUNA MIHIMILI MITATU, (SERIKALI, BUNGE na MAHAKAMA) sawa haina shida, kila mhimili unafanya kazi katika kuingalia ungine sawa tumekubali. Kila mhimili una kiongozi wake ambao ni RAIS, SPIKA na JAJI MKUU tumekubali. Katika hao viongozi kuna wawili kazi zao na majukumu yao ni machache na yako na athari katika maisha yetu na katika kuamua mambo yetu ya ndani, kiongozi mmoja hapo ana majukumu zaidi ya wenzake, MKUU WA NCHI, AMIRI JESHI MKUU WA MAJESHI YA ULINZI NA USALAMA, YEYE NDIO ANAWEZA AMUA WANANCHI WALALE MUDA UPI KUENDANA NA HALI ANAYOIONA YEYE, YEYE PIA ANAJUKUMU LA KUIWAKILISHA NCHI DUNIA NZIMA, YEYE NDIO MTU WA MWISHO KATIKA MAAMUZI YA NCHI HII.
HAWAWEZI KUWA SAWA. MIHIMILI IKO SAWA, ILA VIONGOZI SIO SAWA.
MFANO MKUU WA POLISI HAWEZI KUFANANA NA CDF.
 
Mihimili haiko huru,.rais ana nafas kubwa Sana katika upatikanaji wa spika,.na pia ndie anaemteua jaji mkuu hapo usitegemee Uhuru wowote...
 
Hata huyu jicho rembuo wanaomsifia leo, kesho watakuwa wa kwanza kumnanga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

..bunge linamsaidia raisi na serikali.

..kwa mfano, wabunge wakifichua wazembe serikalini na wakaondolewa anayefaidika ni Raisi.

..wabunge wakiibua changamoto za wananchi na serikali ikazipatia ufumbuzi wanaopata sifa ni Raisi na serikali.

..Wanaowachukulia wabunge kama maadui na kuwaziba midomo ni wajinga.
 
Kama Ndugai alishambuliwa na kutakiwa kujiuzulu kwa kusema nchi itakuja kupigwa mnada, basi Tulia ndio anapaswa kujiuzulu kwa kauli hii:

View attachment 2076322

Pia tuone tofauti iliyopo kati yetu na wenzetu wakenya:

View attachment 2076324

Sio bure; huu ni uchizi. Nguvu ya Rais anayoizingumzia hapa ni ipi? Nguvu ya kuwafurusha wakuu wa mihimili mingine?

Nimemdharau sana. Hafai hata kuwa naibu speaker tu!
 
PhD ya sheria imenajisiwa na Tulia .
Ameongea mambo ya ajabu sana ambayo hayako kwenye katiba wala sheria yeyote ya nchi.

Sijui katoa wapi tafsiri ile.
 
Mnalalamika nyie mabavicha?

Wakati mnashangilia Hangaya alipolinajisi bunge ili kumkomoa ndugai mlitegemea nini?
Shida na mahangaiko yako yote huwa unasingizia CHADEMA!Hata ukivimbiwa makande utasingizia BAVICHA walikulisha?
 
Hii nchi yetu haina viongozi.

Walau January Makamba ameonyesha mshangao kwa matamshi hayo ya Naibu Spika ila sasa sijui kama atasalimika maana Mama nae anapenda wapiga makofi.
Ameonesha wqpi huo mshangao?
 
Hamieni Kenya, Kenya ni Kenya na Tanzania ni Tanzania! Kila nchi ina utaratibu wake na namna ya kuendesha nchi zao, ni nchi huru! Mbona husemi tuwaige Somalia wanavyowakata vichwa wapinzani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…