Tulia Ackson: Gazeti la mwananchi, JamiiForums tunawategemea kuwapelekea taarifa sahihi, tusipeleke za upotoshaji

Tulia Ackson: Gazeti la mwananchi, JamiiForums tunawategemea kuwapelekea taarifa sahihi, tusipeleke za upotoshaji

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Spika wa Bunge, Tulia Ackson ameongelea vyombo vya habari na kuwaomba waandishi hawapendezwi na habari za upotoshaji kuhusu Bunge kwasababu liko wazi.

Tulia kasema wanawategemea Mwananchi, JamiiForums kuwapelekea wananchi taarifa sahihi na si za upotoshaji, amesema haipendezi hasa kama waandishi hawajanyimwa taarifa.

 
Hakika JF inazidi kupaa!

Alianza Rais Samia, kwenye kongamano la Chadema, akiitaja JF, na hivi leo nimemsikia mwenyewe Spika wa Bunge, Tulia Ackson, akiitaja JF, kuwa ndiyo kinara wa kutoa habari hapa nchini👏👏
 
Mh Spika Tulia Ackson amesema anategemea kipindi hiki cha vikao vya muda mrefu Bungeni, Jamiiforums na Gazeti la Mwananchi mnategemewa kupeleka taarifa sahihi kwa wananchi

Je kwa nini mh Spika ataje hivi vyombo viwili?
 
Wanabodi,

Hii ni Breaking News kutoka Bungeni Dodoma!. Baada ya Rais Samia kusema huwa anaingiaga JF, kutusoma na kubaki akicheka. Leo kwa mara ya kwanza mtandao numero Uno Tanzania, Jamiiforums, leo imetajwa rasmi Bungeni na Spika wa Bunge Dr. Tulia Ackson " Vyombo vya Habari Mwananchi na Jamiiforums, Tunawategemea" Kutusaidia Kuihabarisha Jamii taarifa sahihi za Bunge"

clip kwa hisani ya Mkuu Replica
Tulia kasema wanawategemea Mwananchi, JamiiForums kuwapelekea wananchi taarifa
Mimi ni member wa JF kwa muda wa miaka 15 sasa, if imekuwa ikifanya mengi makubwa mazuri kuisaidia serikali na viongozi wake but was barely or hardly recognised, hivyo hii mention ya Spika, it's good kwa JF.

Sisi members wa jf tuwe makini zaidi, kama Mkuu wa Mhimili Mkuu, Rais wa JMT amesema anasoma JF, leo Mkuu wa Mhimili wa Bunge ametutaja, bado Mkuu wa Mhimili mmoja tuu wa Mahakama, of which its just a matter of time.

Mimi kwa niaba yangu binafsi kama mwana JF, nakiri kuwa niko very proud to be a JF member.
AA8A6372.jpg


AA8A6376.jpg
AA8A6360.jpg

Nichukue fursa hii kumpongeza Mkuu Maxence Melo na timu yake ya JF kwa kazi kubwa na nzuri ya uhabarishwaji wa jamii, upashanaji habari, na kutupatia fursa adhimu na adimu ya kutupatia mawanda ya Freedom of Speech and Expression kwa sisi members.

Pia natoa shukrani zangu kwa JF kutu recognizes baadhi yetu na kutupatia zawadi na bahasha nene ya chochote kitu!.

Thanks JF,
God Bless Mkuu Maxence Melo
God Bless JF Staff
God Bless JF Members
Mungu Ibariki Tanzania

Paskali
 
Back
Top Bottom