Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 6.



Haukupita muda ba'mdogo akawa amerudi ndani na kusema amejaribu kutazama kila pembe ya lile jiko hakuona mbuzi.Sasa tukawa tunajiuliza yule mbuzi alikuwa akilia mle ndani ya jiko au alikuwa akililia nje?,mashaka na hofu viliendelea kutawala sana.

"Naona hawa wajinga wanataka tena kurudia mambo yao" Alisema ba'mdogo.

"Hizi dalili siyo nzuri kabisa za kuendelea kuishi hapa,haya mambo yalinitesa sana kipindi fulani ila yalikoma,naona sasa yanaanza kurudi" Aliendelea kusema.


Tulikaa macho kiasi kwamba mpaka kukapambazuka mida ya saa 11 alfajiri.Sasa Ema nae akawa anajigeuza geuza akiugulia maumivu ya kipigo alichokuwa amepokea usiku.Ilipofika mida ya saa 7 headmaster alielekea shuleni akisema angewahi kuja ili aelekee kwa mwenyekiti wa kijiji kutoa taarifa uenda ingesaidia kama mwanzo.
Mimi niliendelea na shughuli zangu za kawaida hapo nyumbani,sasa wakati nikiwa nje jamaa akawa ametoka anachechemea akaenda kukaa kwenye jiwe akawa anaota jua!.
Nilimsalimia lakini aliitikia kama vile hataki,sasa nikawa namdodosa ajaribu kunieleza usiku ilikuwaje mpaka kufikia kuning'inizwa kwenye makenji ya darasa,Jamaa alikuwa anasonya tu!,niliendelea kumsihi ajaribu kunieleza lakini akaendelea kukaa kimya!.

Baada ya kuona ana kiburi nilimuacha nikaendelea na mambo yangu.Ilipofika mida ya saa 5 headmaster alirudi pale nyumbani akiwa na wazee wawili ambao sikuwafahamu.
Sasa akaniita akaniambia "Hebu mwambia huyo aje hapa"

Nikatoka nje nikaenda kumuita jamaa aliyekuwa amejianika juani kama kibambala.Baada ya jamaa kuingia ndani ikabidi na mimi sasa nisogee karibu ili nisikie umbeya maana nilivyojaribu kumwambia aligoma kuniambia.

"Dogo mwenye ndo huyu hapa mwenyekiti" alisema ba'mdogo.

Aliendelea "yaani jana hatujalala kabisa"

Mwenyekiti "Eti wewe!,hebu tuambie ni nini kilikupata"

Ema "Mi sijui chochote,nilishituka nikaona nimefungwa juu ya mbao huku nikipigwa"

Mwenyekiti "Waliokuwa wanakupiga uliwaona?"

Ema "Hapana"

Ba'mdogo "Yaani ni hatari mwenyekiti,nadhani nilikueleza haya mambo ya kiendelea mi nitaondoka"

Mwenyekiti "Sasa mwalimu Wambura utaondoka halafu watoto wetu nani atawafundisha!?"

Ba'mdogo "Siwezi kuendelea kukaa hapa wakati unaona kabisa huu ni ushirikina"

Mwenyekiti "Sasa rafiki wakati wanakupiga hawakusema chochote?"

Ema "Mi wakati wananichapa nilikuwa nasikia wanacheka na nilikuwa napigwa na watu wawili,maana alipokuwa ananipiga huyu na mwingine pia ananipiga"

Mwenyekiti "Hebu toa shati nione"

Ema alivua shati alilokuwa amevaa akamgeuzia mgongo yule mwenyekiti.Ema hakuwa na majeraha lakini mgongo ulikuwa umeumuka kama andazi.

Mwenyekiti "Mwalimu hebu tuteremke na huyu kijana senta akapate dawa pale kwa Malimi"

Basi baada ya maongezi yalichokuwa takribani nusu saa waliondoka wote kuelekea huko Senta.Siku hiyo ilikuwa ngumu sana na sikutaka kabisa kuzurura hovyo,ilipofika mida ya saa 10 alasiri nilichukua zangu dumu nikaelekea lamboni kuchota maji ya kuoga.Usiku wa siku hiyo jamaa hakulala kabisa,japo alikuwa akijifanya mbishi lakini ilibidi arudi kitandani kulala maana aliona angeendelea kulala chini yangemkuta kama ya usiku ulokuwa umepita.

Sasa hali ya mambo ikawa shwari kwa siku kadhaa na yale mauzauza hatukuyaona.

Nakumbuka siku moja mida ya saa 11 jioni headmaster akiwa amerudi nyumbani,alinituma niende Senta nikanunue betri za redio,sasa wakati naondoka sikutaka kabisa kupita njia ya ile miembe kwasababu nilianza kuingiwa na hofu,ilinibidi nizungukie njia ya kwenye lambo japo ilikuwa ya mzunguko lakini ilikuwa salama kabisa.Sasa wakati nikiwa napita kando kando mwa lambo nikama nilimuona yule binti aliyekuwa na Ema pale kwa rafiki yake Jackson ule usiku wa varangati la yeye na Deborah.
Wakati namtazama alikuwa anachuma yale majani marefu huwa yanaota kando kando mwa maji yanayotumikaga kutengenezea majanvi.
Sasa wakati navuta taswira huku nikigeuka nyuma kumtazama ili nimpe hai!,ghafla sikumuona,nikashituka ikabidi nisimame nitazame vizuri,kweli hakuwepo.Sasa ile nageuka zangu mbele niendelee na safari ya kuelekea senta nikakutana naye uso kwa uso akiwa amejitwisha yale majani kichwani!,kiukweli niliogopa sana na nikajikuta nimepiga kelele "Mamaaaaaaa".

Ili kuondoa aibu ya kiume,nikajifanya "Umenishitua".

Yule binti akaanza kucheka huku akiniambia "kumbe na wewe shemeji yangu ni muoga hivo eeenh".

Mimi "vipi lakini"

Yeye "freshi"

Mimi "Huonekani"

Yeye "Mi nipo,ndugu yako hajambo?"

Mimi "Yeye mzima"

Yeye "Wapi mbona upo spidi?"

Mimi "Naelekea senta mara moja"

Yeye " sawa shemeji tutaonana,ngoja niwahi nyumbani kupika"

Niliondoka nikiwa namtazama yule binti lakini sikummaliza hata kidogo,nilijiuliza maswali mengi sana ambayo kiukweli sikupata majibu.
Basi nilifika Senta nikachukua nilichokuwa nimekifuata na kurudi zangu nyumbani.

Nilipofika nyumbani baada ya kukabidhi zile betri kwa Headmaster nilirudi kule kwenye chumba chetu,sasa safari hii jamaa akaanza kuongea na mimi kwa furaha sana,sikujua ile furaha alikuwa ameitoa wapi maana kwa siku kadhaa alikuwa ameninunia kama mwanamke.

Ema "Baadae nataka unisindikize kwa debo kaka"

Mimi "Kuna nini?"

Ema "Tulipo onana shule aliniambia niende kwao baadae"

Mimi "Mlishayamaliza?"

Ema "Tuliyaongea yakaisha kaka"

Mimi "Sasa baadae ya saa ngapi?"

Ema "Tusubiri kwanza headmaster akilala tuondoke"

Mimi "Haitakuwa noma?"

Ema "Hapana,huwa akiingia kulala ni mpaka asubuhi"

Mimi "Sawa nitakusindikiza".

Kweli,baada ya kupata msosi wa usiku,tuliingia ndani kwenye chumba chetu na headmaster alifunga mlango wa sebuleni akaingia chumbani kwake.

Sasa ilipofika mida ya saa 3 ikabidi jamaa anaimbie tusepe.Kule kijijini kutembea usiku ilikuwa ni kitu cha kawaida sana,kulikuwa hakuna majambazi wala vibaka,changamoto ya kule ilikuwa hayo mambo ya kishirikina.
Tukiwa njiani tuelekea kwao debo,nikamwambia jamaa nilikutana na demu wake alikuwa anamsalimia.

Mimi "Hivi huwa mnasoma nae?"

Ema "Kale kademu nilionana nako pale mashineni siku moja nikienda kusaga"

Mimi "Ooh sawa,nikajua labda ni kanafunzi"

Ema "Halafu siku ile nilikaambia kaondoke kakawa kanang'ang'ania kulala kaka"

Mimi "Kwahiyo baada sisi kuondoka ulilala nako mpaka asubuhi?"

Ema " Niliamua kulala nako kaka,yaani huwezi amini siku ile Deborah nilikuwa namuona kama mavi pamoja na uzuri wake wote"

Mimi "Inaonekana kalikupa vitu ambavyo debo hajawahi kukupa"

Baada ya kumwambia hivyo jamaa akaanza kucheka sana huku akiniambia "Hamna kaka ni kawaida tu"

Mimi " Huwa anakaa wapi?"

Ema "Anakaa kule Masairo"

Sasa baada ya jamaa kuniambia hiyo sehemu inayoitwa masairo na nikipiga umbali niliomkuta yule binti pale lamboni nilibaki nimechoka,hiyo Masairo aliyoniambia jamaa kutoka tu hapo senta mpaka hapo masairo si chini ya kilometa 7,sasa vuta picha kutoka pale lamboni ambapo ilikuwa jirani na shule mpaka huko masairo,kiukweli ilikua ni mbali mno kikawaida tena kwa mtoto wa kike ndipo nikabaki najiuliza maswali yasiyokuwa na idadi.

Sikutaka kumwambia jamaa kile nilichokuwa nimekiona pale lamboni wakati ule,ilibidi nikaushe ili niendelee kujifanya bwege stori zinoge.
Endelea mkuu stori imenoga
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 6.



Haukupita muda ba'mdogo akawa amerudi ndani na kusema amejaribu kutazama kila pembe ya lile jiko hakuona mbuzi.Sasa tukawa tunajiuliza yule mbuzi alikuwa akilia mle ndani ya jiko au alikuwa akililia nje?,mashaka na hofu viliendelea kutawala sana.

"Naona hawa wajinga wanataka tena kurudia mambo yao" Alisema ba'mdogo.

"Hizi dalili siyo nzuri kabisa za kuendelea kuishi hapa,haya mambo yalinitesa sana kipindi fulani ila yalikoma,naona sasa yanaanza kurudi" Aliendelea kusema.


Tulikaa macho kiasi kwamba mpaka kukapambazuka mida ya saa 11 alfajiri.Sasa Ema nae akawa anajigeuza geuza akiugulia maumivu ya kipigo alichokuwa amepokea usiku.Ilipofika mida ya saa 1 asubuhi headmaster alielekea shuleni akisema angewahi kuja ili aelekee kwa mwenyekiti wa kijiji kutoa taarifa uenda ingesaidia kama mwanzo.
Mimi niliendelea na shughuli zangu za kawaida hapo nyumbani,sasa wakati nikiwa nje jamaa akawa ametoka anachechemea akaenda kukaa kwenye jiwe akawa anaota jua!.
Nilimsalimia lakini aliitikia kama vile hataki,sasa nikawa namdodosa ajaribu kunieleza usiku ilikuwaje mpaka kufikia kuning'inizwa kwenye makenji ya darasa,Jamaa alikuwa anasonya tu!,niliendelea kumsihi ajaribu kunieleza lakini akaendelea kukaa kimya!.

Baada ya kuona ana kiburi nilimuacha nikaendelea na mambo yangu.Ilipofika mida ya saa 5 headmaster alirudi pale nyumbani akiwa na wazee wawili ambao sikuwafahamu.
Sasa akaniita akaniambia "Hebu mwambia huyo aje hapa"

Nikatoka nje nikaenda kumuita jamaa aliyekuwa amejianika juani kama kibambala.Baada ya jamaa kuingia ndani ikabidi na mimi sasa nisogee karibu ili nisikie umbeya maana nilivyojaribu kumwambia aligoma kuniambia.

"Dogo mwenye ndo huyu hapa mwenyekiti" alisema ba'mdogo.

Aliendelea "yaani jana hatujalala kabisa"

Mwenyekiti "Eti wewe!,hebu tuambie ni nini kilikupata"

Ema "Mi sijui chochote,nilishituka nikaona nimefungwa juu ya mbao huku nikipigwa"

Mwenyekiti "Waliokuwa wanakupiga uliwaona?"

Ema "Hapana"

Ba'mdogo "Yaani ni hatari mwenyekiti,nadhani nilikueleza haya mambo ya kiendelea mi nitaondoka"

Mwenyekiti "Sasa mwalimu Wambura utaondoka halafu watoto wetu nani atawafundisha!?"

Ba'mdogo "Siwezi kuendelea kukaa hapa wakati unaona kabisa huu ni ushirikina"

Mwenyekiti "Sasa rafiki wakati wanakupiga hawakusema chochote?"

Ema "Mi wakati wananichapa nilikuwa nasikia wanacheka na nilikuwa napigwa na watu wawili,maana alipokuwa ananipiga huyu na mwingine pia ananipiga"

Mwenyekiti "Hebu toa shati nione"

Ema alivua shati alilokuwa amevaa akamgeuzia mgongo yule mwenyekiti.Ema hakuwa na majeraha lakini mgongo ulikuwa umeumuka kama andazi.

Mwenyekiti "Mwalimu hebu tuteremke na huyu kijana senta akapate dawa pale kwa Malimi"

Basi baada ya maongezi yalichokuwa takribani nusu saa waliondoka wote kuelekea huko Senta.Siku hiyo ilikuwa ngumu sana na sikutaka kabisa kuzurura hovyo,ilipofika mida ya saa 10 alasiri nilichukua zangu dumu nikaelekea lamboni kuchota maji ya kuoga.Usiku wa siku hiyo jamaa hakulala kabisa,japo alikuwa akijifanya mbishi lakini ilibidi arudi kitandani kulala maana aliona angeendelea kulala chini yangemkuta kama ya usiku ulokuwa umepita.

Sasa hali ya mambo ikawa shwari kwa siku kadhaa na yale mauzauza hatukuyaona.

Nakumbuka siku moja mida ya saa 11 jioni headmaster akiwa amerudi nyumbani,alinituma niende Senta nikanunue betri za redio,sasa wakati naondoka sikutaka kabisa kupita njia ya ile miembe kwasababu nilianza kuingiwa na hofu,ilinibidi nizungukie njia ya kwenye lambo japo ilikuwa ya mzunguko lakini ilikuwa salama kabisa.Sasa wakati nikiwa napita kando kando mwa lambo nikama nilimuona yule binti aliyekuwa na Ema pale kwa rafiki yake Jackson ule usiku wa varangati la yeye na Deborah.
Wakati namtazama alikuwa anachuma yale majani marefu huwa yanaota kando kando mwa maji yanayotumikaga kutengenezea majanvi.
Sasa wakati navuta taswira huku nikigeuka nyuma kumtazama ili nimpe hai!,ghafla sikumuona,nikashituka ikabidi nisimame nitazame vizuri,kweli hakuwepo.Sasa ile nageuka zangu mbele niendelee na safari ya kuelekea senta nikakutana naye uso kwa uso akiwa amejitwisha yale majani kichwani!,kiukweli niliogopa sana na nikajikuta nimepiga kelele "Mamaaaaaaa".

Ili kuondoa aibu ya kiume,nikajifanya "Umenishitua".

Yule binti akaanza kucheka huku akiniambia "kumbe na wewe shemeji yangu ni muoga hivo eeenh".

Mimi "vipi lakini"

Yeye "freshi"

Mimi "Huonekani"

Yeye "Mi nipo,ndugu yako hajambo?"

Mimi "Yeye mzima"

Yeye "Wapi mbona upo spidi?"

Mimi "Naelekea senta mara moja"

Yeye " sawa shemeji tutaonana,ngoja niwahi nyumbani kupika"

Niliondoka nikiwa namtazama yule binti lakini sikummaliza hata kidogo,nilijiuliza maswali mengi sana ambayo kiukweli sikupata majibu.
Basi nilifika Senta nikachukua nilichokuwa nimekifuata na kurudi zangu nyumbani.

Nilipofika nyumbani baada ya kukabidhi zile betri kwa Headmaster nilirudi kule kwenye chumba chetu,sasa safari hii jamaa akaanza kuongea na mimi kwa furaha sana,sikujua ile furaha alikuwa ameitoa wapi maana kwa siku kadhaa alikuwa ameninunia kama mwanamke.

Ema "Baadae nataka unisindikize kwa debo kaka"

Mimi "Kuna nini?"

Ema "Tulipo onana shule aliniambia niende kwao baadae"

Mimi "Mlishayamaliza?"

Ema "Tuliyaongea yakaisha kaka"

Mimi "Sasa baadae ya saa ngapi?"

Ema "Tusubiri kwanza headmaster akilala tuondoke"

Mimi "Haitakuwa noma?"

Ema "Hapana,huwa akiingia kulala ni mpaka asubuhi"

Mimi "Sawa nitakusindikiza".

Kweli,baada ya kupata msosi wa usiku,tuliingia ndani kwenye chumba chetu na headmaster alifunga mlango wa sebuleni akaingia chumbani kwake.

Sasa ilipofika mida ya saa 3 ikabidi jamaa anaimbie tusepe.Kule kijijini kutembea usiku ilikuwa ni kitu cha kawaida sana,kulikuwa hakuna majambazi wala vibaka,changamoto ya kule ilikuwa hayo mambo ya kishirikina.
Tukiwa njiani tuelekea kwao debo,nikamwambia jamaa nilikutana na demu wake alikuwa anamsalimia.

Mimi "Hivi huwa mnasoma nae?"

Ema "Kale kademu nilionana nako pale mashineni siku moja nikienda kusaga"

Mimi "Ooh sawa,nikajua labda ni kanafunzi"

Ema "Halafu siku ile nilikaambia kaondoke kakawa kanang'ang'ania kulala kaka"

Mimi "Kwahiyo baada sisi kuondoka ulilala nako mpaka asubuhi?"

Ema " Niliamua kulala nako kaka,yaani huwezi amini siku ile Deborah nilikuwa namuona kama mavi pamoja na uzuri wake wote"

Mimi "Inaonekana kalikupa vitu ambavyo debo hajawahi kukupa"

Baada ya kumwambia hivyo jamaa akaanza kucheka sana huku akiniambia "Hamna kaka ni kawaida tu"

Mimi " Huwa anakaa wapi?"

Ema "Anakaa kule Masairo"

Sasa baada ya jamaa kuniambia hiyo sehemu inayoitwa masairo na nikipiga umbali niliomkuta yule binti pale lamboni nilibaki nimechoka,hiyo Masairo aliyoniambia jamaa kutoka tu hapo senta mpaka hapo masairo si chini ya kilometa 7,sasa vuta picha kutoka pale lamboni ambapo ilikuwa jirani na shule mpaka huko masairo,kiukweli ilikua ni mbali mno kikawaida tena kwa mtoto wa kike ndipo nikabaki najiuliza maswali yasiyokuwa na idadi.

Sikutaka kumwambia jamaa kile nilichokuwa nimekiona pale lamboni wakati ule,ilibidi nikaushe ili niendelee kujifanya bwege stori zinoge.
Depal
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 7.




Tulitembea kwa muda kidogo hatimaye tukawa tumefika kwao Deborah,sasa tulipofika mbwa walianza kubweka sana,kwakuwa jamaa alikuwa akifahamika pale,aliwapigia wale mbwa mruzi hatimaye wakawa wanamfuata wakitikisa mikia.

Tulisonga mpaka kwenye kile kinyumba alichokuwa anakaa debora na mdogo wake,sasa kwa muda ule alikuwa debora mwenyewe na yule mdogo wake nadhani alilala nyumba kubwa.Ema alianza kugonga mlango hatimaye binti wa watu alifungua!.

Ema "Ulikuwa umelala?"

Debo "mmh" aliitikia huku akipiga miayo.

Basi nilimwambia Deborah aniletee kiti mie nikae kwa nje kama wao walikuwa na mazungumzo marefu,Debo akanitaka niingie tu ndani!.Basi niliingia ndani hatimaye taa ya chemri ikawashwa,sasa kwakuwa hakukuwa na mazungumzo yeyote ya maana,mimi ilibidi nijiongeze nitoke nje ili jamaa achakate papuchi.

Nilitoka nje nikakaa kwa muda kama saa nzima.Walipotoka ili kupotezea nikajifanya kama najipigisha mruzi wa uongo na kweli ili kupotezea.Nilimuona jamaa ni mshamba sana kwasababu hawezi kunitembeza usiku wote huo kisa tu yeye anakwenda kuchakata papuchi kwa demu wake,nilichukia sana lakini ikabidi nivunge tu.Mimi nilidhani wanakwenda kuzungumza vitu vya maana ambavyo ilinipasa niwepo ili nitoe ushauri kumbe ilikuwa ni uchakataji wa papuchi.

Basi bana hatukumaliza muda debo akawa anatusindikiza,sasa tulipotoka nje ya fensi ya miti ya boma lao ilibidi nimgusie kuhusu yule binti ambaye nilimuona lamboni akiwa anafua.Sasa baada ya kuwa nimempa specifications za namna yule binti alivyo,debo alicheka sana.

Debo "Jamani shem,mwanamke gani yule sasa"

Ema akadakia "Kwani ni nani?"

Debo "Si yule Mwise!"

Ema "Wewe umejuaje ni Mwise?"

Debo "Sasa ni nani Pale shuleni mwenye matako makubwa kama siyo Mwise?"

Basi kwa namna nilivyomuelezea Debora namna yule binti alivyo alikuwa ameshamfahamu kabisa.Sasa mimi kiukweli yule binti nilitokea kumtamani sana kulingana na umbo lake namna lilivyokuwa,kiukweli sura ilikuwa ya baba yake(mbaya) lakini umbo lilikuwa la mama yake(zuri),Kuhusu sura kwangu haikuwa tatizo,mimi nilichotaka ni kuchakata papuchi tu!.

Debo "Shem yule hata hakufai,hata hamuendani!"

Mimi "Shem mbona yupo freshi tu!"

Debo "Yaani ulivyo smati hivyo utembee na yule binti?,hapana kwa kweli"

Debo "Wewe usijali shem mimi nitakupa rafiki yangu,ni mzuri kweli nahisi utampenda"

Basi kiukweli yale maneno ya Debo ni kama yalitaka kunikata stimu lakini moyoni bado tamanio langu ni kuwa na mtoto Mwise matako makubwa maana ndivyo vitu nilivyokuwa nikivipenda kwa miaka hiyo!.Kweli,baada ya yale mazungumzo tuliondoka kurejea nyumbani kama kawaida,hiyo ilikuwa yapata saa 5 usiku.

Sasa kuna siku mwanakijiji mmoja alileta Jogoo mkubwa pale nyumbani,kama nilivyosena hapo awali ya kwamba,pale kwa Headmaster wakati ule kila siku alikuwa analetewa kidumu cha maziwa fresh cha lita tano na kila wikiendi alikuwa akiletewa kuku na wanakijiji tofauti tofauti,hii ilikuwa ni kama bonasi ya Mwalimu mkuu kwasababu ile shule ilikuwa ikifanya vizuri kimasomo.Sasa wikiendi hiyo headmaster hakwenda mjini kama kawaida yake,nilimchinja yule Kuku na hatimaye mchana tukawa tume mla tukabakiza mboga ya usiku.

Baadae mida ya mchana saa 8 ba'mdogo akasema anashuka senta na baadae angerudi na mama mdogo kwasababu walikuwa wanatokea mjini kuja hapo kijijini,hivyo akasema angekaa huko mpaka mida atakayompokea mke wake waje nae.Pale kijijini kulikuwaga na gari aina ya Hiace ambayo ilikuwa ikitoka mjini inalala hapo na kesho yake inaondoka,hivyo kama ulikuwa unakwenda mjini na hiyo gari ikikuacha basi inakubidi uhairishe safari.

Ba'mdogo "Hiyo mboga muiche kwa ajili ya wageni,nyie chambueni dagaa ambazo mtalia ugali usiku"

Mimi "Sawa baba"

Basi bana huo mchana nikaingia zangu kupumzika,Ema yeye alikuwa ameenda madarasani huko kusoma na wanafunzi wenzie.Ilipofika saa kumi na moja nikaanza kutengeneza dagaa kwa ajili ya kitoweo cha usiku.
Ilipofika saa 12 niliwasha jiko ili sasa nipashe yule kuku tuliyemla mchana halafu baada ya hapo nipike wale dagaa.

Nimeenda kuchukua sufuria ile ili niweke kwenye jiko nakuta ni nyepesi mno,kufungua mfuniko na kutazama ndani nakuta mboga hamna,ni mifupa tu inanikodorea macho!,yaani hata mchuzi tu ulikuwa ulambwa wote!.Nilishituka sana na nikajiuliza hiyo mboga ni nani atakuwa amekula?
Nilitoka nje ili niende pale darasani kumshitua Ema kumuuliza yawezekana yeye ndiye aliyekula ile mboga ili headmaster atakaporudi aweze kujibu.
Sasa wakati nakwenda kule madarasani nikamuona na yeye akiwa anakuja.

Mimi "Ndo mnatoka?"

Ema "eeenh ndo tumemaliza pindi"

Mimi "Yule kuku ulimla wewe?"

Ema "Kuku?,kuku yupi?"

Mimi "Si ile mboga tuliyokula mchana"

Ema "Kwani imekuwaje?"

Mimi "Aiseee twende ukajionee mwenyewe".

Basi tulipofika ndani moja kwa moja jikoni.

Ema "Daaaah sa nani kala?"

Mimi "mimi sijui,nimelala mchana nikaamka ili niipashe ndo kama unavyoona".

Mimi "Na dingi alisema anakuja na mama mdogo,sasa sijui itakuaje maana alisema kuku tuache kwa ajili ya mgeni na sisi tupike dagaa"

Tuliendelea kutazamana pale tusijue cha kufanya.Nilimwambia Ema tutamwambia dingi kilichotokea lakini Ema ni kama alisita sana.

Ema "Wewe headmaster humjui vizuri,usione anakuchekea hapa ukamfanyia utani,niulize mimi"

Mimi "Yule ni baba yangu mdogo na nina mfahamu vema,sasa kama hatujala sisi tufanyeje?

Ema "Yule hawezi kuamini kaka"

Ema "Sikiliza,mimi ngoja nikimbie kwao Debo nimwambie anikamatie kuku tuje kuchinja,vinginevyo itakuwa hatari"

Mimi "Mbona kama muda umeenda sana,na wao nadhani wanaweza kuwahi kurudi"

Ema "Headmaster namjua,hawezi kurudi saa hizi,hapo mpaka ngoma tatu ndo unamuona hapa na mkewe"

Basi jamaa ilibidi aondoke anakimbia kwenda kwa demu wake kufata kuku wakuja ku-replace.Kiukweli ile hali haikuwa ya kawaida kabisa,pamoja na vile vitisho lakini wanaume bado tuliendelea kukomaa!.Ilipofika mida ya saa moja usiku nilikuwa nikismubiri jamaa lakini sikuona,sasa baada ya kupika wale dagaa na jamaa alikuwa haonekani,niliona nikimbie nimfuate,nilisema yawezekana alipofika kwa demu wake uchakataji ukaanza akasahau mambo ya kuku.

Nikafunga mlango nikaondoka zangu,nimetembea sana bila kukutana na jamaa njiani,nilikuwa nimekasirika sana na hakuna siku niliyomuona jamaa ni mpumbavu kama siku hiyo,sasa nimefika kwao Deborah nakuta jamaa amekaa kwenye kiti tena amekunja kabisa nne.

Mimi " Sasa ema umefika tena umekaa?"

Ema " Hapana kaka sijakaa kama unavyodhani,Deborah amesema anampika kabisa ili tukifika sisi ni kusonga ugali tu kaka"

Basi ikabidi nikae tusubiri huyo kukua aive,kiukweli nilikuwa nimechukia sana kwa namna jamaa ambavyo alikuwa hachukulii vitu serious!.
Sasa tumekaa pale mpaka mida ya saa tatu usiku ndipo kuku akawa ameiva,nilikuwa nawaza tukimkuta dingi kafika tutamueleza tulikuwa wapi!.

Baada ya Deborah kutukabidhi yule kuku kwenye hotpot tukaanza mwendo wa kutembea haraka kuwahi nyumbani,sasa cha ajabu tulitembea sana lakini tukawa hatufiki,Aisee kiukweli wasukuma nawanyooshea mikono.

Yaani fikiria tunatembea lakini kila tukiangalia hatufiki,sasa nikamwambia jamaa "hebu tusimame kwanza".

Mimi "Isije kuwa hii njia tumeichanganya Ema".

Ema " Kaka njia ndiyo hii".

Mimi "Mbona sasa tumetumia muda mrefu sana?"

Jamaa akaniambia "twende nzetu tutafika kaka,najua una kimuhe muhe cha dingi yako".

Jamaa alikuwa anafanya masihara lakini kiukweli tulipiga sana makitaimu.

Sasa wakati tunatembea hatuna hili wala lile,tukasikia sauti nyuma yetu ikiita "Emaaa mpenziiii".

Aiseee sitakuja kuisahau ile siku,kila mtu alipita chocho lake na tulikutana nyumbani asubuhi.
Nimecheka kama mazuri.
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 7.




Tulitembea kwa muda kidogo hatimaye tukawa tumefika kwao Deborah,sasa tulipofika mbwa walianza kubweka sana,kwakuwa jamaa alikuwa akifahamika pale,aliwapigia wale mbwa mruzi hatimaye wakawa wanamfuata wakitikisa mikia.

Tulisonga mpaka kwenye kile kinyumba alichokuwa anakaa debora na mdogo wake,sasa kwa muda ule alikuwa debora mwenyewe na yule mdogo wake nadhani alilala nyumba kubwa.Ema alianza kugonga mlango hatimaye binti wa watu alifungua!.

Ema "Ulikuwa umelala?"

Debo "mmh" aliitikia huku akipiga miayo.

Basi nilimwambia Deborah aniletee kiti mie nikae kwa nje kama wao walikuwa na mazungumzo marefu,Debo akanitaka niingie tu ndani!.Basi niliingia ndani hatimaye taa ya chemri ikawashwa,sasa kwakuwa hakukuwa na mazungumzo yeyote ya maana,mimi ilibidi nijiongeze nitoke nje ili jamaa achakate papuchi.

Nilitoka nje nikakaa kwa muda kama saa nzima.Walipotoka ili kupotezea nikajifanya kama najipigisha mruzi wa uongo na kweli ili kupotezea.Nilimuona jamaa ni mshamba sana kwasababu hawezi kunitembeza usiku wote huo kisa tu yeye anakwenda kuchakata papuchi kwa demu wake,nilichukia sana lakini ikabidi nivunge tu.Mimi nilidhani wanakwenda kuzungumza vitu vya maana ambavyo ilinipasa niwepo ili nitoe ushauri kumbe ilikuwa ni uchakataji wa papuchi.

Basi bana hatukumaliza muda debo akawa anatusindikiza,sasa tulipotoka nje ya fensi ya miti ya boma lao ilibidi nimgusie kuhusu yule binti ambaye nilimuona lamboni akiwa anafua.Sasa baada ya kuwa nimempa specifications za namna yule binti alivyo,debo alicheka sana.

Debo "Jamani shem,mwanamke gani yule sasa"

Ema akadakia "Kwani ni nani?"

Debo "Si yule Mwise!"

Ema "Wewe umejuaje ni Mwise?"

Debo "Sasa ni nani Pale shuleni mwenye matako makubwa kama siyo Mwise?"

Basi kwa namna nilivyomuelezea Debora namna yule binti alivyo alikuwa ameshamfahamu kabisa.Sasa mimi kiukweli yule binti nilitokea kumtamani sana kulingana na umbo lake namna lilivyokuwa,kiukweli sura ilikuwa ya baba yake(mbaya) lakini umbo lilikuwa la mama yake(zuri),Kuhusu sura kwangu haikuwa tatizo,mimi nilichotaka ni kuchakata papuchi tu!.

Debo "Shem yule hata hakufai,hata hamuendani!"

Mimi "Shem mbona yupo freshi tu!"

Debo "Yaani ulivyo smati hivyo utembee na yule binti?,hapana kwa kweli"

Debo "Wewe usijali shem mimi nitakupa rafiki yangu,ni mzuri kweli nahisi utampenda"

Basi kiukweli yale maneno ya Debo ni kama yalitaka kunikata stimu lakini moyoni bado tamanio langu ni kuwa na mtoto Mwise matako makubwa maana ndivyo vitu nilivyokuwa nikivipenda kwa miaka hiyo!.Kweli,baada ya yale mazungumzo tuliondoka kurejea nyumbani kama kawaida,hiyo ilikuwa yapata saa 5 usiku.

Sasa kuna siku mwanakijiji mmoja alileta Jogoo mkubwa pale nyumbani,kama nilivyosena hapo awali ya kwamba,pale kwa Headmaster wakati ule kila siku alikuwa analetewa kidumu cha maziwa fresh cha lita tano na kila wikiendi alikuwa akiletewa kuku na wanakijiji tofauti tofauti,hii ilikuwa ni kama bonasi ya Mwalimu mkuu kwasababu ile shule ilikuwa ikifanya vizuri kimasomo.Sasa wikiendi hiyo headmaster hakwenda mjini kama kawaida yake,nilimchinja yule Kuku na hatimaye mchana tukawa tume mla tukabakiza mboga ya usiku.

Baadae mida ya mchana saa 8 ba'mdogo akasema anashuka senta na baadae angerudi na mama mdogo kwasababu walikuwa wanatokea mjini kuja hapo kijijini,hivyo akasema angekaa huko mpaka mida atakayompokea mke wake waje nae.Pale kijijini kulikuwaga na gari aina ya Hiace ambayo ilikuwa ikitoka mjini inalala hapo na kesho yake inaondoka,hivyo kama ulikuwa unakwenda mjini na hiyo gari ikikuacha basi inakubidi uhairishe safari.

Ba'mdogo "Hiyo mboga muiche kwa ajili ya wageni,nyie chambueni dagaa ambazo mtalia ugali usiku"

Mimi "Sawa baba"

Basi bana huo mchana nikaingia zangu kupumzika,Ema yeye alikuwa ameenda madarasani huko kusoma na wanafunzi wenzie.Ilipofika saa kumi na moja nikaanza kutengeneza dagaa kwa ajili ya kitoweo cha usiku.
Ilipofika saa 12 niliwasha jiko ili sasa nipashe yule kuku tuliyemla mchana halafu baada ya hapo nipike wale dagaa.

Nimeenda kuchukua sufuria ile ili niweke kwenye jiko nakuta ni nyepesi mno,kufungua mfuniko na kutazama ndani nakuta mboga hamna,ni mifupa tu inanikodorea macho!,yaani hata mchuzi tu ulikuwa ulambwa wote!.Nilishituka sana na nikajiuliza hiyo mboga ni nani atakuwa amekula?
Nilitoka nje ili niende pale darasani kumshitua Ema kumuuliza yawezekana yeye ndiye aliyekula ile mboga ili headmaster atakaporudi aweze kujibu.
Sasa wakati nakwenda kule madarasani nikamuona na yeye akiwa anakuja.

Mimi "Ndo mnatoka?"

Ema "eeenh ndo tumemaliza pindi"

Mimi "Yule kuku ulimla wewe?"

Ema "Kuku?,kuku yupi?"

Mimi "Si ile mboga tuliyokula mchana"

Ema "Kwani imekuwaje?"

Mimi "Aiseee twende ukajionee mwenyewe".

Basi tulipofika ndani moja kwa moja jikoni.

Ema "Daaaah sa nani kala?"

Mimi "mimi sijui,nimelala mchana nikaamka ili niipashe ndo kama unavyoona".

Mimi "Na dingi alisema anakuja na mama mdogo,sasa sijui itakuaje maana alisema kuku tuache kwa ajili ya mgeni na sisi tupike dagaa"

Tuliendelea kutazamana pale tusijue cha kufanya.Nilimwambia Ema tutamwambia dingi kilichotokea lakini Ema ni kama alisita sana.

Ema "Wewe headmaster humjui vizuri,usione anakuchekea hapa ukamfanyia utani,niulize mimi"

Mimi "Yule ni baba yangu mdogo na nina mfahamu vema,sasa kama hatujala sisi tufanyeje?

Ema "Yule hawezi kuamini kaka"

Ema "Sikiliza,mimi ngoja nikimbie kwao Debo nimwambie anikamatie kuku tuje kuchinja,vinginevyo itakuwa hatari"

Mimi "Mbona kama muda umeenda sana,na wao nadhani wanaweza kuwahi kurudi"

Ema "Headmaster namjua,hawezi kurudi saa hizi,hapo mpaka ngoma tatu ndo unamuona hapa na mkewe"

Basi jamaa ilibidi aondoke anakimbia kwenda kwa demu wake kufata kuku wakuja ku-replace.Kiukweli ile hali haikuwa ya kawaida kabisa,pamoja na vile vitisho lakini wanaume bado tuliendelea kukomaa!.Ilipofika mida ya saa moja usiku nilikuwa nikismubiri jamaa lakini sikuona,sasa baada ya kupika wale dagaa na jamaa alikuwa haonekani,niliona nikimbie nimfuate,nilisema yawezekana alipofika kwa demu wake uchakataji ukaanza akasahau mambo ya kuku.

Nikafunga mlango nikaondoka zangu,nimetembea sana bila kukutana na jamaa njiani,nilikuwa nimekasirika sana na hakuna siku niliyomuona jamaa ni mpumbavu kama siku hiyo,sasa nimefika kwao Deborah nakuta jamaa amekaa kwenye kiti tena amekunja kabisa nne.

Mimi " Sasa ema umefika tena umekaa?"

Ema " Hapana kaka sijakaa kama unavyodhani,Deborah amesema anampika kabisa ili tukifika sisi ni kusonga ugali tu kaka"

Basi ikabidi nikae tusubiri huyo kukua aive,kiukweli nilikuwa nimechukia sana kwa namna jamaa ambavyo alikuwa hachukulii vitu serious!.
Sasa tumekaa pale mpaka mida ya saa tatu usiku ndipo kuku akawa ameiva,nilikuwa nawaza tukimkuta dingi kafika tutamueleza tulikuwa wapi!.

Baada ya Deborah kutukabidhi yule kuku kwenye hotpot tukaanza mwendo wa kutembea haraka kuwahi nyumbani,sasa cha ajabu tulitembea sana lakini tukawa hatufiki,Aisee kiukweli wasukuma nawanyooshea mikono.

Yaani fikiria tunatembea lakini kila tukiangalia hatufiki,sasa nikamwambia jamaa "hebu tusimame kwanza".

Mimi "Isije kuwa hii njia tumeichanganya Ema".

Ema " Kaka njia ndiyo hii".

Mimi "Mbona sasa tumetumia muda mrefu sana?"

Jamaa akaniambia "twende nzetu tutafika kaka,najua una kimuhe muhe cha dingi yako".

Jamaa alikuwa anafanya masihara lakini kiukweli tulipiga sana makitaimu.

Sasa wakati tunatembea hatuna hili wala lile,tukasikia sauti nyuma yetu ikiita "Emaaa mpenziiii".

Aiseee sitakuja kuisahau ile siku,kila mtu alipita chocho lake na tulikutana nyumbani asubuhi.
Noma sana[emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom