Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Tulichomfanya yule mchawi hatakuja kusahau kamwe

Yeah Wengine ili ufanikiwe kwenye mambo yako pesa n.k pia lazima uue ! utoe sadaka/ kafara!
Yani kuna tukio la kichawi liliomtokea ndugu yangu wa damu sina hamu nahawa viumbe na mpaka waleo naendelea kukiri Mungu anatupenda sana na anamakusudi nami! sijui ndio niseme mizimu ya kwetu ni mikali sana mi sijuiiii ilaa Asante yesu!🙏
mmash upoo ☺️??
Bado nakufatilia kwa makini sana,naona Leo anga limetulia,Makono Leo haji,anajua shughuli ya Jana😂😂
 
Oya umughaka una msala huku
Screenshot_20221013-035415_Instagram.jpg
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 22.




Baada ya kufika senta niliendelea na biashara yangu ya uuzaji wa miwa kama kawaida!,sasa ilipofika jioni muda ambao wanafunzi walikuwa wametoka shule,nilimuona Mwise siku hiyo tena akiwa na marafiki zake wakiwa wanakuja hapo senta,safari hii sikutaka kabisa mazoea na mtoto wa mtu,niliamua kuuchuna na sikuwa na shobo nae kabisa!.Sasa yeye alidhani uenda ningemuita ila mwanaune niliamua kula buyu la hatari!,alikuwa anajiangalisha kwangu lakini kila nikimcheki kwa jicho la kuibia najifanya kupiga stori na jamaa yangu aliyekuwa akiuza kata mbuga.

Walipo maliza kufanya kilichokuwa kimewapeleka hapo senta waliondoka huku mimi nikijifanya niko bize kipiga stori na jamaa lakini kiukweli moyo wangu ulikuwa unauma sana!.Siku hiyo mama mdogo hakuka kabisa hapo senta na sikufahamu sababu ni nini!.

Ilipofika jioni mida ya saa 12 nilirudisha ile miwa iliyokuwa imebaki kwa yule mama na mimi kuianza safari ya kurejea nyumbani.Nilifika nyumbani mida ya saa 1 usiku kuelekea saa 2,niliingia jikoni nikachukua dumu la maji nikaondoka zangu kuelekea lamboni kuchota maji ili nije kuoga nijiweke safi kwasababu Monica alikuwa ameniambia angekuja kunichukua!.

Sasa wakati napandisha nyumbani nikakutana na Ema akiwa bado amevaa nguo za shule akiwa na Deborah,mimi napandisha na wao wakiteremsha!.

Deborah "Mambo umughaka"

Mimi "Poa,vp?"

Deborah "poa!,aya baadae!"

Nilipata mashaka kidogo kwasababu haikuwaga tabia ya Deborah nikionana nae kuacha kupiga stori na mimi,sikuumiza kichwa sana maana niliamini mpumbavu Ema atakuwa amenikandia sana kwa demu wake!,kwasababu hata wakati Deborah ananisalimia jamaa alikuwa anajitembeza taratibu huku akinikaushia!.Basi nilibeba zangu dumu nikanyoosha zangu nyumbani!.
Nilipomaliza kuoga niliingia jikoni fasta kupika ili atakapokuja Monica akute nikiwa nimemaliza kila kitu!.Kama nilivyosema hapo awali ya kwamba,kule kwenye kile kijiji kutembea usiku haikuwa shida,shida ilikuwa ni wachawi tu,lakini mambo ya wezi na majambazi hayakuwepo kabisa,kuna matukio machache sana yaliwahi kufanyika kule senta yaliyohusu wezi lakini yalikuwa yakuhesabika na hayakujirudia tena!.

Nilipomaliza kupika nilichukua sinia nikafunika ugali nikauweka mezani,kisha nikachukua mabakuli ya mboga nikapakua mboga kisha nazo nikapeleka sebuleni,sasa niliendelea kuona ndani kwa Headmaster kuko kimya hata mwanga wa taa au tochi haukuonekana!.Nilisogea karibu nikaanza kugonga ule mlango kuwakaribisha kwa ajili ya chakula lakini nikaona kimya!,nilipoangalia vizuri mlangoni nikakuta kuna kofuli,basi niliamini watakuwa wametoka.

Basi nilichukua sahani nikakata ugali wa kunitosha size yangu nikaanza kula!.Nimekula mpaka namaliza si Ba'mdogo wala Maza mdogo aliyerudi,nikakumbuka uenda kwa kuwa ilikuwa ijumaa labda watakuwa wameondoka kwenda mjini,lakini isingekuwa rahisi kwasababu niliondoka kwenda senta nikawaacha hapo nyumbani,halafu pia ile Hiace ya kuelekea mjini ilikuwaga inaondoka saa 12 asubuhi,niliamini uenda watakuwa wametoka tu na walikuwepo hayo mazingira ya kijijini.Kilicho fanya pia kujiuliza uenda wakawa wameenda mbali ni kitendo cha Ema na mpenzi wake Deborah kujiachia usiku ule bila presha!.Nilirudishia ule mlango wa sebuleni nikarudi zangu chumbani kwetu!.

Mpaka inafika mida ya saa 3 sikumuona Ema na nikajua kabisa headmaster na mkewe watakuwa wameenda mbali.Mpaka muda huo sikumuona Monica hivyo nikaamua kujilaza huku nikiwa namsikilizia.

Haukupita muda nikasikia mlango wa nje unagongwa!,nilienda kuufungua ndipo nilikuta alikuwa Monica!.

Mimi "Karibu"

Monica "Ulikuwa umelala mpenzi wangu?"

Mimi "Nimekusubiri sana"

Monica "Nilikuwa napika,nisamehe"

Mimi "Sikunyingine usiwe unagonga bhana utaniletea shida!"

Monica "Unadhani mimi mjinga?"

Aliendelea "Nimejua hawapo ndiyo maana nimegonga"

Mimi "Umejuaje?"

Monica "Twende nyumbani tunachelewa"

Basi niliingia ndani nikavaa viatu nikatoka zangu,nilifunga ule mlango wa chumbani kwetu na komeo lakini sikuweka kufuli!.Ule wa nje nilirudishia tu tukaondoka zetu na Monica.Mara ya kwanza kutembea na Monica ilikuwa ni kutuliza tu uwendawazimu wa abdala kichwa wazi lakini sikumpenda kabisa,sasa kadri siku zilivyokuwa zikienda ndivyo ulikuwa uniambii kitu kwa yule binti wa kisukuma na kiukweli kuna wakati nilikuwa naona ni kwanini nilichelewa kumfahamu maana alikuwa akinijali sana,licha ya kwamba papuchi ilikuwa ni moja ya sababu ya kumpenda lakini sura yake nzuri pia ilinivutia zaidi,alichokuwa amekosa yule binti wa kisukuma ni matako makubwa tu ambayo ndiyo ulikuwa ugonjwa wangu wakati huo,lakini kwingine kote alikuwa amekamilika binti wa watu wala nisimseme vibaya!.

Mimi "Umeambia ulijua hawapo,umejuaje"

Monica "Nishakwambia mpenzi wangu usiwe unauliza uliza maswali,utaelewa tu siku moja"

Aliendelea "Nimemuona ndugu yako wakati nakuja akiwa na mpenzi wake"

Mimi "Umekutana nao?"

Monica "Kuna mahali nimewaona wanaongozana"

Mimi "Nadhani tupite pale kwao Deborah ili nikamuulize kama headmaster ametoka anarudi au harudi maana muda umeenda"

Monica "Ningekwambia lakini unaweza usiniamini,twende ukamuulize!".

Basi tulichepuka na kuacha ile njia kubwa na tukashika njia ya kuelekea kwao Deborah,basi tulipofika Monica alisimama kwa mbali kidogo hakutaka kuongozana na mimi!.

Monica "Nenda utanikuta nakusuniri hapa"

Nilipofika kwenye boma la ile nyumba kwa mbali nikaona taa ikiwa inawaka kwenye kile kinyumba alichokuwa akilala Deborah na nikaelewa watakuwa bado macho!.Basi nilipofika nikasikia watu wakiongea kwa sauti za chini lakini cha ajabu niligonga sana ule mlango bila mtu kutoka wala kuitikia!.Sikutaka kupoteza muda niliondoka zangu kimya kimya kama mtu aliyetengwa na wazazi wake,nilikuwa najiuliza maswali mengi sana nikawa nakosa majibu!.Nilifahamu kabisa Ema atakuwa amemlisha sumu mbaya Deborah kwasababu haikuwa kawaida ya Deborah kunidharau kiasi kile.

Monica "Umemkuta"

Mimi "Nimewasikia kabisa wanaongea lakini wamekataa kuniitikia"

Monica "Huyo ndugu yako anakiburi sana,wewe subiri ajifanye mjanja"

Aliendelea "Baba yako na mama yako mdogo kuna mahali wameenda na wangekuwa wanajua wanajisumbua wangebaki wakatulia"

Mimi "Kwani unajua walipoenda?"

Monica "Tuondoke tunachelewa"

Basi tulitembea kwa haraka kuelekea kwao Monica,jambo lilikuwa ni lilelile la kufika mapema ingawa palikuwa mbali.Sasa nilipofika niliwakuta watu kadhaa wakiwa pale nje wakiwa wamekaa wakipiga stori huku wakiwa wameshaa taa ikiwa juu ya jamvi.

Mama Monica "Karibu mwanangu"

Mimi "Shikamoo mama"

Mama Monica "Marhaba mwanangu,karibu"

Mama yake Monica alinyanyuka kwenye kiti alichokuwa amekaa akawa amenikabidhi nikalie.Basi haukupita muda nikaona Monica anebeba kimeza kidogo anakileta mahali nilipokuwa nimekaa!.Baada ya kuileta ile meza na kuiweka vizuri akawa ameingia ndani ndipo akaja na vyungu akawa ameviweka chini ya meza,alirudi tena akaja na mabakuli akaanza kupakua mboga,kisha akaendea ugali wa udaga na kuukarisha juu ya meza,alinikaribisha kwa kupiga magoti hadi chini!.

Mwanaume nikaanza kula,kumbe nilikuwa nimeachiwa bata ambaye alipikwa kwa ajili ya bibi yake aliyekuwa amekuja kuwatembelea,kwakweli nilikula sana japo nilikuwa nimeshiba maana nilimisi sana nyama ya bata!.Baada ya kumaliza kula mama yake Monica alianza kuongea kisukuma na yule mwanamke mzee ambaye nilifahamu kabisa ni bibi yake Monica kwasababu alikuwa amekwisha kunitonya!.

Mama Monica "Mwanangu,huyu ni mama yangu"

Mimi "Ooh sawa"

Baada ya kuongea na mimi kisha akawa anaongea na bibi yake Monica!.

Monica "Bibi hajui kiswahili ndiyo maana unaona mama anaongea nae kilugha"

Basi tuliendelea kupiga stori za hapa na pale na Monica, sasa muda ulivyozidi kwenda bibi yake Monica akasimana akawa ameingia ndani,nadhani aliingia kulala!.Baada ya kuingia ndani,mama yake Monica alisogeza kiti mahali nilipokuwa nimekaa na Monica.

Mama Monica "Mwanangu kwanza nikupe Pole kwa uliyayaona jana"

Mimi "Aaah mama wala usijali"

Mama Monica "Sasa mwanangu nisikilize kwa makini"

Aliendelea "Niliwahi kukwambia haya yote nayafanya kwa ajili ya binti yangu,nakuomba usije kumuacha mwenzako"

Mimi "Siwezi kumuacha mama"

Mama Monica "Sawa"

Aliendelea "Sasa ila mwalimu anachokifanya si jambo jema,angetulia ningemsaidia"

Mimi "Amefanya nini mama?"

Mama Monica "Maalimu anaenda kwa waganga akitaka kufahamu wanaomuaharibu"

Aliendelea "Mmmmh ngoja tumuone"

Mimi "Mama kwanini usimsaidie tu ba mdogo?"

Mama Monica "Yule mwalimu aliwahi kunitukana mwanangu,wewe hujui tu!,na hata niliposikia unaishi kwa mwalimu nilikujaribu ukanibebea kuni zangu,nilipoona wewe ni kijana mzuri na mwanangu kukupenda nikaona nikusaidie wewe!"

Aliponiambia ya kwamba nimewahi kumbebea kuni nilishituka sana lakini sikutaka kuonyesha!,niliendelea kujipa moyo nikiamini kwasasa hawezi kunifanyia jambo baya kwasababu nilikuwa kwenye mahusiano na binti yake,nilifahamu kabisa ile familia niya kishirikina lakini kwakuwa walikuwa wakinilinda sikuwa na namna!.

Mama Monica "Hata huko walipoenda wameenda kupoteza muda tu mwanangu"

Mimi "Kwani wameenda kwa mganga"

Monica "Wewe nilikwambia nikikuambia hutoniamini,ngoja mama akueleze sasa"

Mama Monica "kwani hujui mwanangu?"

Mimi "Nimetoka senta sijakuta mtu nyumbani mama"

Mama Monica "Hawawezi kukwambia mwanangu"

Aliendelea "Sasa kesho kuna vitu nitakupatia uende navyo nyumbani na nitakuja mwenyewe baadae kukuelekeza namna ya kufanya!"

Mama Monica "Kwakuwa hata hivyo yule mbwa anataka kuniulia nyinyi wanangu nitamshikisha adabu halafu baada ya hapo nitapandishwa cheo"
Unazidi kula shule tu mzee UMUGHAKA 😂
 
Tulichomfanya Yule Mchawi hatokuja kusahau kamwe! - 22.




Baada ya kufika senta niliendelea na biashara yangu ya uuzaji wa miwa kama kawaida!,sasa ilipofika jioni muda ambao wanafunzi walikuwa wametoka shule,nilimuona Mwise siku hiyo tena akiwa na marafiki zake wakiwa wanakuja hapo senta,safari hii sikutaka kabisa mazoea na mtoto wa mtu,niliamua kuuchuna na sikuwa na shobo nae kabisa!.Sasa yeye alidhani uenda ningemuita ila mwanaune niliamua kula buyu la hatari!,alikuwa anajiangalisha kwangu lakini kila nikimcheki kwa jicho la kuibia najifanya kupiga stori na jamaa yangu aliyekuwa akiuza kata mbuga.

Walipo maliza kufanya kilichokuwa kimewapeleka hapo senta waliondoka huku mimi nikijifanya niko bize kipiga stori na jamaa lakini kiukweli moyo wangu ulikuwa unauma sana!.Siku hiyo mama mdogo hakuka kabisa hapo senta na sikufahamu sababu ni nini!.

Ilipofika jioni mida ya saa 12 nilirudisha ile miwa iliyokuwa imebaki kwa yule mama na mimi kuianza safari ya kurejea nyumbani.Nilifika nyumbani mida ya saa 1 usiku kuelekea saa 2,niliingia jikoni nikachukua dumu la maji nikaondoka zangu kuelekea lamboni kuchota maji ili nije kuoga nijiweke safi kwasababu Monica alikuwa ameniambia angekuja kunichukua!.

Sasa wakati napandisha nyumbani nikakutana na Ema akiwa bado amevaa nguo za shule akiwa na Deborah,mimi napandisha na wao wakiteremsha!.

Deborah "Mambo umughaka"

Mimi "Poa,vp?"

Deborah "poa!,aya baadae!"

Nilipata mashaka kidogo kwasababu haikuwaga tabia ya Deborah nikionana nae kuacha kupiga stori na mimi,sikuumiza kichwa sana maana niliamini mpumbavu Ema atakuwa amenikandia sana kwa demu wake!,kwasababu hata wakati Deborah ananisalimia jamaa alikuwa anajitembeza taratibu huku akinikaushia!.Basi nilibeba zangu dumu nikanyoosha zangu nyumbani!.
Nilipomaliza kuoga niliingia jikoni fasta kupika ili atakapokuja Monica akute nikiwa nimemaliza kila kitu!.Kama nilivyosema hapo awali ya kwamba,kule kwenye kile kijiji kutembea usiku haikuwa shida,shida ilikuwa ni wachawi tu,lakini mambo ya wezi na majambazi hayakuwepo kabisa,kuna matukio machache sana yaliwahi kufanyika kule senta yaliyohusu wezi lakini yalikuwa yakuhesabika na hayakujirudia tena!.

Nilipomaliza kupika nilichukua sinia nikafunika ugali nikauweka mezani,kisha nikachukua mabakuli ya mboga nikapakua mboga kisha nazo nikapeleka sebuleni,sasa niliendelea kuona ndani kwa Headmaster kuko kimya hata mwanga wa taa au tochi haukuonekana!.Nilisogea karibu nikaanza kugonga ule mlango kuwakaribisha kwa ajili ya chakula lakini nikaona kimya!,nilipoangalia vizuri mlangoni nikakuta kuna kofuli,basi niliamini watakuwa wametoka.

Basi nilichukua sahani nikakata ugali wa kunitosha size yangu nikaanza kula!.Nimekula mpaka namaliza si Ba'mdogo wala Maza mdogo aliyerudi,nikakumbuka uenda kwa kuwa ilikuwa ijumaa labda watakuwa wameondoka kwenda mjini,lakini isingekuwa rahisi kwasababu niliondoka kwenda senta nikawaacha hapo nyumbani,halafu pia ile Hiace ya kuelekea mjini ilikuwaga inaondoka saa 12 asubuhi,niliamini uenda watakuwa wametoka tu na walikuwepo hayo mazingira ya kijijini.Kilicho fanya pia kujiuliza uenda wakawa wameenda mbali ni kitendo cha Ema na mpenzi wake Deborah kujiachia usiku ule bila presha!.Nilirudishia ule mlango wa sebuleni nikarudi zangu chumbani kwetu!.

Mpaka inafika mida ya saa 3 sikumuona Ema na nikajua kabisa headmaster na mkewe watakuwa wameenda mbali.Mpaka muda huo sikumuona Monica hivyo nikaamua kujilaza huku nikiwa namsikilizia.

Haukupita muda nikasikia mlango wa nje unagongwa!,nilienda kuufungua ndipo nilikuta alikuwa Monica!.

Mimi "Karibu"

Monica "Ulikuwa umelala mpenzi wangu?"

Mimi "Nimekusubiri sana"

Monica "Nilikuwa napika,nisamehe"

Mimi "Sikunyingine usiwe unagonga bhana utaniletea shida!"

Monica "Unadhani mimi mjinga?"

Aliendelea "Nimejua hawapo ndiyo maana nimegonga"

Mimi "Umejuaje?"

Monica "Twende nyumbani tunachelewa"

Basi niliingia ndani nikavaa viatu nikatoka zangu,nilifunga ule mlango wa chumbani kwetu na komeo lakini sikuweka kufuli!.Ule wa nje nilirudishia tu tukaondoka zetu na Monica.Mara ya kwanza kutembea na Monica ilikuwa ni kutuliza tu uwendawazimu wa abdala kichwa wazi lakini sikumpenda kabisa,sasa kadri siku zilivyokuwa zikienda ndivyo ulikuwa uniambii kitu kwa yule binti wa kisukuma na kiukweli kuna wakati nilikuwa naona ni kwanini nilichelewa kumfahamu maana alikuwa akinijali sana,licha ya kwamba papuchi ilikuwa ni moja ya sababu ya kumpenda lakini sura yake nzuri pia ilinivutia zaidi,alichokuwa amekosa yule binti wa kisukuma ni matako makubwa tu ambayo ndiyo ulikuwa ugonjwa wangu wakati huo,lakini kwingine kote alikuwa amekamilika binti wa watu wala nisimseme vibaya!.

Mimi "Umeambia ulijua hawapo,umejuaje"

Monica "Nishakwambia mpenzi wangu usiwe unauliza uliza maswali,utaelewa tu siku moja"

Aliendelea "Nimemuona ndugu yako wakati nakuja akiwa na mpenzi wake"

Mimi "Umekutana nao?"

Monica "Kuna mahali nimewaona wanaongozana"

Mimi "Nadhani tupite pale kwao Deborah ili nikamuulize kama headmaster ametoka anarudi au harudi maana muda umeenda"

Monica "Ningekwambia lakini unaweza usiniamini,twende ukamuulize!".

Basi tulichepuka na kuacha ile njia kubwa na tukashika njia ya kuelekea kwao Deborah,basi tulipofika Monica alisimama kwa mbali kidogo hakutaka kuongozana na mimi!.

Monica "Nenda utanikuta nakusuniri hapa"

Nilipofika kwenye boma la ile nyumba kwa mbali nikaona taa ikiwa inawaka kwenye kile kinyumba alichokuwa akilala Deborah na nikaelewa watakuwa bado macho!.Basi nilipofika nikasikia watu wakiongea kwa sauti za chini lakini cha ajabu niligonga sana ule mlango bila mtu kutoka wala kuitikia!.Sikutaka kupoteza muda niliondoka zangu kimya kimya kama mtu aliyetengwa na wazazi wake,nilikuwa najiuliza maswali mengi sana nikawa nakosa majibu!.Nilifahamu kabisa Ema atakuwa amemlisha sumu mbaya Deborah kwasababu haikuwa kawaida ya Deborah kunidharau kiasi kile.

Monica "Umemkuta"

Mimi "Nimewasikia kabisa wanaongea lakini wamekataa kuniitikia"

Monica "Huyo ndugu yako anakiburi sana,wewe subiri ajifanye mjanja"

Aliendelea "Baba yako na mama yako mdogo kuna mahali wameenda na wangekuwa wanajua wanajisumbua wangebaki wakatulia"

Mimi "Kwani unajua walipoenda?"

Monica "Tuondoke tunachelewa"

Basi tulitembea kwa haraka kuelekea kwao Monica,jambo lilikuwa ni lilelile la kufika mapema ingawa palikuwa mbali.Sasa nilipofika niliwakuta watu kadhaa wakiwa pale nje wakiwa wamekaa wakipiga stori huku wakiwa wameshaa taa ikiwa juu ya jamvi.

Mama Monica "Karibu mwanangu"

Mimi "Shikamoo mama"

Mama Monica "Marhaba mwanangu,karibu"

Mama yake Monica alinyanyuka kwenye kiti alichokuwa amekaa akawa amenikabidhi nikalie.Basi haukupita muda nikaona Monica anebeba kimeza kidogo anakileta mahali nilipokuwa nimekaa!.Baada ya kuileta ile meza na kuiweka vizuri akawa ameingia ndani ndipo akaja na vyungu akawa ameviweka chini ya meza,alirudi tena akaja na mabakuli akaanza kupakua mboga,kisha akaendea ugali wa udaga na kuukarisha juu ya meza,alinikaribisha kwa kupiga magoti hadi chini!.

Mwanaume nikaanza kula,kumbe nilikuwa nimeachiwa bata ambaye alipikwa kwa ajili ya bibi yake aliyekuwa amekuja kuwatembelea,kwakweli nilikula sana japo nilikuwa nimeshiba maana nilimisi sana nyama ya bata!.Baada ya kumaliza kula mama yake Monica alianza kuongea kisukuma na yule mwanamke mzee ambaye nilifahamu kabisa ni bibi yake Monica kwasababu alikuwa amekwisha kunitonya!.

Mama Monica "Mwanangu,huyu ni mama yangu"

Mimi "Ooh sawa"

Baada ya kuongea na mimi kisha akawa anaongea na bibi yake Monica!.

Monica "Bibi hajui kiswahili ndiyo maana unaona mama anaongea nae kilugha"

Basi tuliendelea kupiga stori za hapa na pale na Monica, sasa muda ulivyozidi kwenda bibi yake Monica akasimana akawa ameingia ndani,nadhani aliingia kulala!.Baada ya kuingia ndani,mama yake Monica alisogeza kiti mahali nilipokuwa nimekaa na Monica.

Mama Monica "Mwanangu kwanza nikupe Pole kwa uliyayaona jana"

Mimi "Aaah mama wala usijali"

Mama Monica "Sasa mwanangu nisikilize kwa makini"

Aliendelea "Niliwahi kukwambia haya yote nayafanya kwa ajili ya binti yangu,nakuomba usije kumuacha mwenzako"

Mimi "Siwezi kumuacha mama"

Mama Monica "Sawa"

Aliendelea "Sasa ila mwalimu anachokifanya si jambo jema,angetulia ningemsaidia"

Mimi "Amefanya nini mama?"

Mama Monica "Maalimu anaenda kwa waganga akitaka kufahamu wanaomuaharibu"

Aliendelea "Mmmmh ngoja tumuone"

Mimi "Mama kwanini usimsaidie tu ba mdogo?"

Mama Monica "Yule mwalimu aliwahi kunitukana mwanangu,wewe hujui tu!,na hata niliposikia unaishi kwa mwalimu nilikujaribu ukanibebea kuni zangu,nilipoona wewe ni kijana mzuri na mwanangu kukupenda nikaona nikusaidie wewe!"

Aliponiambia ya kwamba nimewahi kumbebea kuni nilishituka sana lakini sikutaka kuonyesha!,niliendelea kujipa moyo nikiamini kwasasa hawezi kunifanyia jambo baya kwasababu nilikuwa kwenye mahusiano na binti yake,nilifahamu kabisa ile familia niya kishirikina lakini kwakuwa walikuwa wakinilinda sikuwa na namna!.

Mama Monica "Hata huko walipoenda wameenda kupoteza muda tu mwanangu"

Mimi "Kwani wameenda kwa mganga"

Monica "Wewe nilikwambia nikikuambia hutoniamini,ngoja mama akueleze sasa"

Mama Monica "kwani hujui mwanangu?"

Mimi "Nimetoka senta sijakuta mtu nyumbani mama"

Mama Monica "Hawawezi kukwambia mwanangu"

Aliendelea "Sasa kesho kuna vitu nitakupatia uende navyo nyumbani na nitakuja mwenyewe baadae kukuelekeza namna ya kufanya!"

Mama Monica "Kwakuwa hata hivyo yule mbwa anataka kuniulia nyinyi wanangu nitamshikisha adabu halafu baada ya hapo nitapandishwa cheo"
Kwa hii michakato inamaana wachawi Hawanaga OFF DAYS Kila siku ni mbilinge tu.
 
Back
Top Bottom