Tulifika Dar saa 9 usiku kutoka Zanzibar, kitu cha ajabu tukaambiwa kushuka ni saa 12 asubuhi

Kama alikuwa anawahi jambo asubuhi sana na amepata hiyo fursa ya saa tatu aiache aende akalale?

Issue hapa shughuli nyingi haziendi kisa tunafanya kazi masaa 12, inabidi tubadilike tuwe kama maaskari au hospitali.

Ni zamu kwa zamu hakuna kulala.
Kwanini alichelewA?
Then anaita watu maskini huku ye ni kiongozi wa Maskini.
 
We mwenyewe maskini,
umechelewa, ukapanda boti la usiku.
Umeshindwa nini kulala Hotel uondoke kesho?
Ndege hazipo kwanza?
We ni Maskini kuliko hata hao unaita Maskini
Daah ndugu yangu upo chaka gani kupanda Boat ni umasikini au kusafiri usiku aisee yaani Nchi inatumia 14 billion kuwahesabu ninyi si bora wangewakadiria tu kwa mawazo haya?
 
CRDB waliwahi kufunga mlango tukabaki mimi na wahudumu tu na muda ulikuwa umeshaisha. Walicheza na tatizo langu hadi likaisha. Akaunti ilikuwa inakubali kutoa pesa tawi moja tu tena kuna mhudumu ndio alikuwa anaipatia.
 
Kwa hiyo ndege huko Marekani mnapanda benki? Na hizo benki zina bandari kama ya Dar ya boti za Unguja?
 

Ni mambo ya kiusalama na utendaji zaidi. Wewe umefikiria upande wako wa abiria lakini hujafikiria upande wa wafanyakazi wakaokuja kukuhudumia. Wengine hiyo saa 9 usiku ndiyo wanatoka makwao ili waje kukuhudumia wewe saa 12 asubuhi.

Kifupi ni mipangilio ya kikazi tu.

Tatizo letu kubwa Tanzania ni ujinga tu, kwanini meli iondoke huko ilitoka saa ambazo wanafahamu itafika Dar saa 9 usiku na abiria watakalishwa ndani ya boti mpaka ifike 12 asubuhi?

Ni ujinga tu wa safari ilipoanzia siyo ilipoishia.
 
Kuna watu wapo bandarini bado wanawaza kijima sana, mabasi yanasafiri saa ishirini na nne, una meli inajulikana inaingia saa flani bandarini. Wao wanafunga vipi mageti na kuendelea kulala hadi asubuhi?

Je abiria wasio na mizigo wanakatazwa nini kuendelea na safari. Hadi Mhe. Rais aseme ndipo watabadilika? Nchi hii inakwama kiuchumi kwa sababu watu wanapenda sana kulala......nashauri huu utaratibu uondolewe watu kukimbizana na ratiba za mabus
 
Kama bandari inafanya kazi masaa 24 kwa nini wafanyakazi wasiwe na shift za mchana na usiku
 
Kwanza inaonyesha kisa ni cha kuhadithiwa saa 3 mpaka saa 9 mlikwenda mogadishu ndio mkarudi dar!
 
Niliwauliza wakasema ; kwanza ni usalama wa abiria, pili ni kutokuwa na wakaguzi nyakati za usiku pale bandarini
Kwahiyo vyote vinakwenda pamoja, hivyo inabidi Mamlaka zilitazame hilo kwa makini.

Maisha yamebadilika jiji limekuwa kuna maeneo sasa YANAPASWA kutoa huduma kwa masaa 24. Kikubwa WAKAGUZI waongoze muda wa kufanya kazi.

Mbona ndege zinatua wakati wowote, ukaguzi unafanyika na kila abiria anatafuta usafiri wake.

Treni linafika muda wowote na kila abiria anakadiria muda wake na usalama wa kule aendako safari inaendelea.

Kuna mazoea fulani ya kutoa huduma inabidi YABADILIKE sasa ,tuache kukariri tujaribu KUJIFIKIRISHA na kuondoa UKALE.
 
Kabisa bandari ikeshe..soko la kariakoo likeshe..etc
 
Umenikumbusha mambo ya kitambo sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…