Tulifikirie suala la Sarafu moja kati ya Tanzania na Kenya

Tulifikirie suala la Sarafu moja kati ya Tanzania na Kenya

Kwa nini hiyo EAS isiwe quoted kwenye dhahabu badala ya US$? Mfano.
EAS 1 iwe sawa na ounce 1 ya dhahabu na hivyo malipo ya madeni na manunuzi yakokotolewa kwa mtindo huo. [emoji848] [emoji848]
Tatizo na hiyo thamani ya dhahabu ipo kwa usd
 
Sioni haja ya kumtukana mleta mada....sidhani mada ya kuwa na same currency ni mada ya ovyo...labda wew mwenyew kama una matatizo binafsi.

Mleta mada ana point ya msingi sana
Umejisumbua sana kumjibu kistaarabu asiye mstaarabu.
 
Sioni haja ya kumtukana mleta mada....sidhani mada ya kuwa na same currency ni mada ya ovyo...labda wew mwenyew kama una matatizo binafsi....

Mleta mada ana point ya msingi sana
Tatizo hamsomi historia nyinyi. Mngekuwa mmesoma kwanini EAC ilivunjika zamani. Mngeona kuwa huu mnaowaza ni upuuzi. To have one currency na kenyans it’s a no! A never
 
Na central bank moja ? central bank itakaa wapi? CEO atatoka wapi? Unataka wakenya waanze Ku manipulate data za uchumi?
Kuwa na sarafu moja (Singe Currency) haimaanishi ni lazima tuwe na benki kuu moja. Maana kama nchi inaweza kuwa haina benki kuu na mambo yake mengi yakaenda vizuri, japo inabidi hiyo nchi iwe imeendelea sana na ina taasisi imara za kifedha. Kuna mbinu nyingi kisheria ambazo zinaweza zikatumika kufanikisha hili, mfano tunaweza kuanzisha Benki Kuu ya pamoja (The East African Central Bank) huku benki za nchi wanachama kama Kenya na Tanzania zikiwa na viti kwenye bodi ya wakurugenzi.

Umoja wa Ulaya (The EU) wana benki kuu ya pamoja (The European Central Banks) ambayo inasimamia sarafu ya Ulaya, pamoja na kusimamia na kuhakikisha utekelezaji mzuri wa sera za kifedha (Monetary Stability) ndani ya Ulaya. Sasa Ulaya wana mfumo uitwao The European System of Cental Bank (ESCB) ambao hujumuisha benki kuu zote za Ulaya (Central Banks) na Benki Kuu ya Ulaya (European Central Bank) zikifanya kazi pamoja katika kusimami sera za kifedha.

Kubwa zaidi hili la kuanzisha benki ya pamoja linawezekana vizuri tu maana hadi kufika mwaka 1965 nchi za Afrika Mashariki (Kenya, Tanzania na Uganda) zilikuwa na chombo kimoja kilichofanya kazi kama Benki Kuu. Chombo hicho kiliitwa The East African Currency Board (EACB) na kilianzishwa na mkoloni ili kuweza kusimamia benki za kibiashara (Commercia Banks) na utoaji wa sarafu (Issuing Legal Tender). Kilienda vizuri tu lakini haraka za kina Mzee Nyerere na Kenyatta ndiyo zilivuruga kila kitu.

NB: Jambo muhimu kufahamu ni kwamba tunaweza kuwa na benki kuu ya Afrika Mashariki (East African Central Bank), lakini tukaipa hiyo benki kazi chache tu kama kutengeneza sarafu ya pamoja (Issuing Currency/Legal Tenders), kusimamia sera za kifedha (Monetary Policies) na kudhibiti mfumuko wa bei (Control of Prices). Hayo mengine ya kusimamia benki za kibiashara, ukopeshaji mkubwa na kutengeneza sera za kiuchumi za nchi (Fiscal Policy) zinaachiwa benki kuu za mataifa husika.
 
Kuwa na sarafu moja (Singe Currency) haimaanishi ni lazima tuwe na benki kuu moja. Maana kama nchi inaweza kuwa haina benki kuu na mambo yake mengi yakaenda vizuri, japo inabidi hiyo nchi iwe imeendelea sana na ina taasisi imara za kifedha. Kuna mbinu nyingi kisheria ambazo zinaweza zikatumika kufanikisha hili, mfano tunaweza kuanzisha Benki Kuu ya pamoja (The East African Central Bank) huku benki za nchi wanachama kama Kenya na Tanzania zikiwa na viti kwenye bodi ya wakurugenzi.
Hivi South Africa wamewezaje ku control fedha zao na bank kuu ni binafsi na sio ya serikali?
 
Tatizo hamsomi historia nyinyi. Mngekuwa mmesoma kwanini EAC ilivunjika zamani. Mngeona kuwa huu mnaowaza ni upuuzi. To have one currency na kenyans it’s a no! A never
Sasa kama hata wewe umechangia unauitaje upuuzi mkuu! Au na wewe umekubali uwe mpuuzi kama sisi??
 
Kuwa na sarafu moja (Singe Currency) haimaanishi ni lazima tuwe na benki kuu moja. Maana kama nchi inaweza kuwa haina benki kuu na mambo yake mengi yakaenda vizuri, japo inabidi hiyo nchi iwe imeendelea sana na ina taasisi imara za kifedha. Kuna mbinu nyingi kisheria ambazo zinaweza zikatumika kufanikisha hili, mfano tunaweza kuanzisha Benki Kuu ya pamoja (The East African Central Bank) huku benki za nchi wanachama kama Kenya na Tanzania zikiwa na viti kwenye bodi ya wakurugenzi.

Umoja wa Ulaya (The EU) wana benki kuu ya pamoja (The European Central Banks) ambayo inasimamia sarafu ya Ulaya, pamoja na kusimamia na kuhakikisha utekelezaji mzuri wa sera za kifedha (Monetary Stability) ndani ya Ulaya. Sasa Ulaya wana mfumo uitwao The European System of Cental Bank (ESCB) ambao hujumuisha benki kuu zote za Ulaya (Central Banks) na Benki Kuu ya Ulaya (European Central Bank) zikifanya kazi pamoja katika kusimami sera za kifedha.

Kubwa zaidi hili la kuanzisha benki ya pamoja linawezekana vizuri tu maana hadi kufika mwaka 1965 nchi za Afrika Mashariki (Kenya, Tanzania na Uganda) zilikuwa na chombo kimoja kilichofanya kazi kama Benki Kuu. Chombo hicho kiliitwa The East African Currency Board (EACB) na kilianzishwa na mkoloni ili kuweza kusimamia benki za kibiashara (Commercia Banks) na utoaji wa sarafu (Issuing Legal Tender). Kilienda vizuri tu lakini haraka za kina Mzee Nyerere na Kenyatta ndiyo zilivuruga kila kitu.

NB: Jambo muhimu kufahamu ni kwamba tunaweza kuwa na benki kuu ya Afrika Mashariki (East African Central Bank), lakini tukaipa hiyo benki kazi chache tu kama kutengeneza sarafu ya pamoja (Issuing Currency/Legal Tenders), kusimamia sera za kifedha (Monetary Policies) na kudhibiti mfumuko wa bei (Control of Prices). Hayo mengine ya kusimamia benki za kibiashara, ukopeshaji mkubwa na kutengeneza sera za kiuchumi za nchi (Fiscal Policy) zinaachiwa benki kuu za mataifa husika.
Shukrani sana mkuu kwa kutuongezea maarifa... Ubarikiwe
 
Sio rahisi hivyo. Kwanza lazime kuwe na makubaliona ya economic policy "Fiscal & Monetary" pia lzn kuwe na EA-Central Bank ya ku monitor hizo policy.

Mfano. Tusema currency mpya inaitwa EA-Shilling (EAS). hii currency tunipa value labda EAS 1 = USD 1. tunachofanya ni ku convert madeni yote kwenda kwenye hii USD na kenda kwenye EAS lbda TZ tuna daiwa 37B USD, Kenya labda 16B USD na uganda 12B USD haya madeni yote tunatapeleka kwenye EAS kama shilling yetu mpya sasa TZ inakua inadaiwa 37B EAS hivyo hivyo kwa madeni ya nchi nyingine. Baada yapo ndo ela inaingia kwenye circulation

Changamoto ni kwamba sera ya fedha kwenye nchi moja ikibadilika ina affected dhani ya fedha kwenye jumiiya nzima. Alfu pia tutashea inflation ikitokea bei zimepanda Sudani hivyo hiyo bei itakuja kupanda tanzania. Haita weze kama bei ya bidhaa au mafuta ipande sudani halafu bei za hizo bidhaa sizipande sehemu nyingine, hii itasababisha speculation kwenye uchumi.

Kwa sasa common currency haiwezekani
Mkuu, siyo rahisi japo inawezekana vizuri kabisa endapo tutaamua,
 
Hivi South Africa wamewezaje ku control fedha zao na bank kuu ni binafsi na sio ya serikali?
Hata Marekani benki kuu ni binafsi lakini wanawezaje ???
Hata Uingereza benki kuu ilikuwa binafsi hadi kufika mwaka 1946 ilipotaifishwa, lakini waliwezaje ???

Hapa ndiyo tunarudi kwenye majukumu muhimu za benki kuu, ambapo ni kusimamia uchumi kupitia Macroeconomic and Microeconomic Functions. Hilo la kwanza benki kuu inasimamia sera za kiuchumi na kifedha (Fiscal and Monetary Policies), kama mambo ye kudhibiti mfumuko wa bei, uingiza wa fedha kwenye uchumi, kutengeza mikopo ya umma kupitia dhamana ili kufidia bajeti endapo makusanyo ya kodi ni madogo kuliko matumizi (Incase of deficit) na kufanya matumizi mazito endapo biashara zitakuwa zimedorora.

Kwenye hilo la pili sasa (Microeconomic Function), hapa benki kuu kazi yake huwa ni kuzisimamia benki za kibiashara pamoja na taasisi nyingine za kiuchumi (Commercial Banks and Financial Institutions). Hapa jukumu kubwa ni kuhakikisha benki kuu inazisaidia benki za kibiashara kufanya kazi vizuri kwa kuweza kuzipa mikopo ili ziweze kujiendesha na kutoa huduma (A Lender of Last Resort). Ndiyo maana wachumi na wanasheria huwa tunaita Benki Kuu kama benki ya mabenki (Central Banks are Bankers of Commercial Banks).

Ndiyo maana sasa hata hapa Tanzania, kuna ulazima kwamba kila benki ya kibiashara iwe na akaunti ya fedha kwenye Benki ya Tanzania ambayo itaendana na uwezo wa benki hiyo kukopesha. Huu mfumo kitaalamu huwa tunauita Fractional Reserve Banking. Kuna siku benki inaweza ikawa imepata wateja wengi lakini haina fedha nyingi za kuwahudumia hao wateja kwa kuwapa mikopo, kwasababu inakuwa imetumbukiza fedha yote ndani ya mzunguko, huu mfumo wa Fractional Reserve Banking huruhusu mabenki ya kibiashara yaende benki kuu kukopa fedha zaidi.

Ukisoma The Bank of Tanzania Act na kanuni zake, inasema kwamba endapo benki ya kibiashara itaenda kufilisika au kushindwa kujiendesha kwa kukosa mtaji, Benki Kuu lazima iingilie kati kwa kuichukua hiyo benki na kuiendesha. Hili kisheria huwa tunaitwa Central Bank Receivership, na hili hufanywa ili kuzuia kusababisha madhara kwenye uchumi kwasababu huathiri wateja na biashara zao. Kama unakumbuka mwaka 2016, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilivunja bodi ya Wakurugenzi wa benki ya Twiga Bancorp na kuiweka chini yake ili kuzuia madhara kwenye sekta ya uchumi na biashara.

Hizi ndiyo kazi muhumi kabisa za benki kuu, iwe benki binafsi au ile ya serikali. Ukienda kila nchi utakutana na hili suala, na ukifuatilia zaidi utafahamu kwamba Benki Kuu siku hizi huwa zinafanya kazi kuu tatu tu ambazo nyingi ni nyuma ya pazia na zina madhara makubwa kiuchumi: Mosi, Fractional Reserve Banking. Pili, Quantitative Easing na Tatu, Tax Collection Through Artificial Inflation.

NB: Siku hizi benki kuu zimegundua mbinu mpya ya kihuni ya kukusanya kodi bila kwenda bungeni na kutunga sheria ya bunge kama ambayo kanuni za bunge zinataka. Benki Kuu nyingi huamua kutengeneza mfumuko wa bei usio na kichwa wala miguu (Artificial Inflation) ili kukuibia wewe fedha zako. Mfano, bidhaa kama mchele gunia ulikuwa unauzwa Tsh 50,000, ghafla unafika Tsh 80,000 halafu wanasingizia vita.

Kumbe ile Tsh 30,000 iliyoongezeka ni kodi ya nyuma ya pazia ambayo bungeni isingeweza kukubalika kupitia kikokotoo cha The Finance Act na ingeleta minong'ono na makelele mengi kwa wakina kajamba-nani. Hivyo mtapigwa sana na atasingiziwa Putin.
 
mpaka Family de Rothschild waamue na wakubali......weledi watanielewa
Umeongea kitu kizito mno, lakini sidhani kama watakuelewa....
Nchi za Afrika zikianzisha mfumo wa sarafu ya pamoja ndiyo kwaheri Dollar, Euro, Yuan n.k
Nadhani ndiyo itakuwa sarafu yenye thamani zaidi dunia kwasababu haitakuwa Fiat Currency....
 
Hata Marekani benki kuu ni binafsi lakini wanawezaje ???
Hata Uingereza benki kuu ilikuwa binafsi hadi kufika mwaka 1946 ilipotaifishwa, lakini waliwezaje ???

Hapa ndiyo tunarudi kwenye majukumu muhimu za benki kuu, ambapo ni kusimamia uchumi kupitia Macroeconomic and Microeconomic Functions. Hilo la kwanza benki kuu inasimamia sera za kiuchumi na kifedha (Fiscal and Monetary Policies), kama mambo ye kudhibiti mfumuko wa bei, uingiza wa fedha kwenye uchumi, kutengeza mikopo ya umma kupitia dhamana ili kufidia bajeti endapo makusanyo ya kodi ni madogo kuliko matumizi (Incase of deficit) na kufanya matumizi mazito endapo biashara zitakuwa zimedorora.

Kwenye hilo la pili sasa (Microeconomic Function), hapa benki kuu kazi yake huwa ni kuzisimamia benki za kibiashara pamoja na taasisi nyingine za kiuchumi (Commercial Banks and Financial Institutions). Hapa jukumu kubwa ni kuhakikisha benki kuu inazisaidia benki za kibiashara kufanya kazi vizuri kwa kuweza kuzipa mikopo ili ziweze kujiendesha na kutoa huduma (A Banker of Last Resort). Ndiyo maana wachumi na wanasheria huwa tunaita Benki Kuu kama benki ya mabenki (Central Banks are Bankers of Commercial Banks).

Ndiyo maana sasa hata hapa Tanzania, kuna ulazima kwamba kila benki ya kibiashara iwe na akaunti ya fedha kwenye Benki ya Tanzania ambayo itaendana na uwezo wa benki hiyo kukopesha. Huu mfumo kitaalamu huwa tunauita Fractional Reserve Banking. Kuna siku benki inaweza ikawa imepata wateja wengi lakini haina fedha nyingi za kuwahudumia hao wateja kwa kuwapa mikopo, kwasababu inakuwa imetumbukiza fedha yote ndani ya mzunguko, huu mfumo wa Fractional Reserve Banking huruhusu mabenki ya kibiashara yaende benki kuu kukopa fedha zaidi.

Ukisoma The Bank of Tanzania Act na kanuni zake, inasema kwamba endapo benki ya kibiashara itaenda kufilisika au kushindwa kujiendesha kwa kukosa mtaji, Benki Kuu lazima iingilie kati kwa kuichukua hiyo benki na kuiendesha. Hili kisheria huwa tunaitwa Central Bank Receivership, na hili hufanywa ili kuzuia kusababisha madhara kwenye uchumi kwasababu huathiri wateja na biashara zao. Kama unakumbuka mwaka 2016, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilivunja bodi ya Wakurugenzi wa benki ya Twiga Bancorp na kuiweka chini yake ili kuzuia madhara kwenye sekta ya uchumi na biashara.

Hizi ndiyo kazi muhumi kabisa za benki kuu, iwe benki binafsi au ile ya serikali. Ukienda kila nchi utakutana na hili suala, na ukifuatilia zaidi utafahamu kwamba Benki Kuu siku hizi huwa zinafanya kazi kuu tatu tu ambazo nyingi ni nyuma ya pazia na zina madhara makubwa kiuchumi: Mosi, Fractional Reserve Banking. Pili, Quantitative Easing na Tatu, Tax Collection Through Artificial Inflation.

NB: Siku hizi benki kuu zimegundua mbinu mpya ya kihuni ya kukusanya kodi bila kwenda bungeni na kutunga sheria ya bunge kama ambayo kanuni za bunge zinataka. Benki Kuu nyingi huamua kutengeneza mfumuko wa bei usio na kichwa wala miguu (Artificial Inflation) ili kukuibia wewe fedha zako. Mfano, bidhaa kama mchele gunia ulikuwa unauzwa Tsh 50,000, ghafla unafika Tsh 80,000 halafu wanasingizia vita.

Kumbe ile Tsh 30,000 iliyoongezeka ni kodi ya nyuma ya pazia ambayo bungeni isingeweza kukubalika kupitia kikokotoo cha The Finance Act na ingeleta minong'ono na makelele mengi kwa wakina kajamba-nani. Hivyo mtapigwa sana na atasingiziwa Putin.
Hahahahaaa hatiamye umefikia lengo ulilolikusudia... hiyo aya ya mwisho..!!
 
Kenya na Tanzania mambo mengine kila mmoja afanye kivyake, lakini hili la shilingi moja tulifikirie. Tuwe na shilingi moja jamani, itatufaa sana..!!

Hoja Binafsi.
Hiyo ni hatari sana ...maana nchi moja inaweza kuchapa pesa haramu na kujinufaisha ni kama dola ya marekani kwa sasa ni pesa ya dunia hivyo marekani inapata utajiri kwa kuchapa tu pesa
 
Sio rahisi hivyo. Kwanza lazime kuwe na makubaliona ya economic policy "Fiscal & Monetary" pia lzn kuwe na EA-Central Bank ya ku monitor hizo policy.

Mfano. Tusema currency mpya inaitwa EA-Shilling (EAS). hii currency tunipa value labda EAS 1 = USD 1. tunachofanya ni ku convert madeni yote kwenda kwenye hii USD na kenda kwenye EAS lbda TZ tuna daiwa 37B USD, Kenya labda 16B USD na uganda 12B USD haya madeni yote tunatapeleka kwenye EAS kama shilling yetu mpya sasa TZ inakua inadaiwa 37B EAS hivyo hivyo kwa madeni ya nchi nyingine. Baada yapo ndo ela inaingia kwenye circulation

Changamoto ni kwamba sera ya fedha kwenye nchi moja ikibadilika ina affected dhani ya fedha kwenye jumiiya nzima. Alfu pia tutashea inflation ikitokea bei zimepanda Sudani hivyo hiyo bei itakuja kupanda tanzania. Haita weze kama bei ya bidhaa au mafuta ipande sudani halafu bei za hizo bidhaa sizipande sehemu nyingine, hii itasababisha speculation kwenye uchumi.

Kwa sasa common currency haiwezekani
Nikweli ila kuna wajinga wanawaza positive things tu bila kuwaza negative things kwenye pesa ya pamoja kunamambo mengi sana yanaweza kutumika kihalifu kama nchi moja kufanikiwa kuchapa hiyo pesa kifisadi na kuhujumu nchi zingine
 
Umeongea kitu kizito mno, lakini sidhani kama watakuelewa....
Nchi za Afrika zikianzisha mfumo wa sarafu ya pamoja ndiyo kwaheri Dollar, Euro, Yuan n.k
Nadhani ndiyo itakuwa sarafu yenye thamani zaidi dunia kwasababu haitakuwa Fiat Currency....
siyo rahisi mkuu....hiyo familia ina umiliki wa hisa katika central banks zote duniani isipokuwa chache kama north korea, cuba na iran. hamuwezi mkajitoa. Hata hao wachina wanawapigia magoti maana ukijifanya jeuri wanakuondoa kwenye mfumo wa SWIFT, biashara za kimataifa hufanyi.
 
Hiyo ni hatari sana ...maana nchi moja inaweza kuchapa pesa haramu na kujinufaisha ni kama dola ya marekani kwa sasa ni pesa ya dunia hivyo marekani inapata utajiri kwa kuchapa tu pesa
Marekani anachapisha pesa kwasababu ana kitu kiitwacho The Exorbitant Privilege. Fedha yake ndiyo inatumika kwa asilimia zaidi ya 70% kwenye biashara ya dunia (A Global Reserve Currency). Marekani hata achapishe pesa mwisho wa siku hakumbani na matatizo ya uwino wa malipo (Balance of Payment) kama nchi nyingine za duniani.

Sasa leo hii Tanzania na Kenya tuwe na sarafu moja halafu Kenya au Tanzania achape pesa feki, ina maana yeye hatakumbwa na kadhia ya mfumuko wa bei ???
 
Hiyo ni hatari sana ...maana nchi moja inaweza kuchapa pesa haramu na kujinufaisha ni kama dola ya marekani kwa sasa ni pesa ya dunia hivyo marekani inapata utajiri kwa kuchapa tu pesa
Sasa hapo huoni tutanufaika wote, maana itakua ni pesa yetu wote.


Kiufupi ni kwamba haya mambo yanawezekana kama tutaamua tatizo ni ile familia iliyosemwa hapo juu, itakubali?
 
siyo rahisi mkuu....hiyo familia ina umiliki wa hisa katika central banks zote duniani isipokuwa chache kama north korea, cuba na iran. hamuwezi mkajitoa. Hata hao wachina wanawapigia magoti maana ukijifanya jeuri wanakuondoa kwenye mfumo wa SWIFT, biashara za kimataifa hufanyi.
Nakubali lakini inawezekana kabisa endapo waafrika wataamua. Hata hiyo SWIFT siku hizi inaweza kukwepeka vizuri na mataifa makubwa kama Uchina, japo kuna maumivu nchi lazima iyapate. Kuna mbinu mpya inatumika siku hizi inaitwa CURRENCY SWAP, ambapo Benki Kuu ya nchi moja inasaini mkataba na Benki Kuu ya nchi nyingine na kukubaliana kuweza kutumia fedha zao moja kwa moja na kulipana kiasi cha utofauti wa thamani......

Hii haina haja ya kupitia SWIFT tena, na Uchina ashaanza kufanya hizi itikadi maana mpaka kufika mwezi wa January alikuwa na CURRENCY SWAP AGREMEENT sitini (60) yani. Uzuri ni kwamba mfumo wa kifedha (Finance Economy) una mianya mingi na mno na unaweza kuangushwa kwa haraka kwasababu ni lazima uendeshwe na uchumi wa bidhaa (Commodity Economy). Leo hii tukisema nchi zirudishe The Gold Standard au Afrika tuanze kutumia The Gold Standard, dunia nzima itabomoka......

Hili hata wakubwa wa dunia wanalifahamu vizuri.....
 
Back
Top Bottom