The Hurricane
JF-Expert Member
- Sep 19, 2012
- 760
- 1,048
Nlilima kilimo cha umwagiliaji maji yakakauka kisimaniNyanya nasikia inasoko mwezi december na january kipindi cha mvua sema huko shambani ndio changamoto manake kila mtu anakua amekimbia inabidi uwe kama komandoo huko porini ndio utoboe
Pole sanaMimi nililima mpunga heka kumi ukakubali kweli kweli shamba lilikua langu bwana bwana kukaa hivi napigiwa simu wasukuma wameingiza ng'ombe usiku wamekula shamba lote aisee nilidata. Alafu washenzi wale wamehonga polisi ukienda kushtaki unapigwa danadana tu nilitamani nikapige risasi ng'ombe wote. Morogoro iyo
okMashamba yako milimani
HahahahahahaHiki ndo kilimo cha online,kinashawishi kinoma
Mimi nashangaa wanaolalamia soko..mm mpka ss napigiwaga simu wanataka berries nawaambia sihusiki nazo tena..but mm nilijitangaza vilivyo!
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]ZINGINALI wenyewe wanapaita
Hapo kwenye kuku je uliwapa chanjo zote muhimuNilipiga heka za Mahindi 30.za.mahindi karibu 8m. huko Morogoro.kabla ya kuvuna Ngombe wakapita nikaambulia gunia 30.maana yake kila eka gunia moja.
nikarudia tena mvua ikazingua ktk eka 20 nikapata gunia 3.nikarudisha home.tumekula ugali mwaka mzima.
Nikajaribu matikiti eka 4 .kabla ya kuiva yakawa yanapasuka pasuka.sikuuza kabisa .sema tulikula matunda home na wanangu.
Nikajaribu matango. eka 2.hayo yakakubali.na yanakomaa ndani ya mida mgupi sana .nikachelewa kuvuna.nilikiwa safari ya kikazi.nikawambia madogo wasubiri nirudi wasivune nilihofia kupigwa.hivyo yakaiva yakawa na mekundu hivi .kumpeleka bos shamba ilil akanunue,akaishia kuniitukana eti nimemsumbua na kumpotezea muda wake wakati.mzigo wenyeqe hauuzilki
Nilijaribu kufuga kuku chotara.hao walikubali sana.sema wakiwa na miezi mitano wakapata ugonjwa wa ajabu ghafla.asubuhi tunaamka tinaona wanasinzia na kukohoa. walikufa kwa wingi ndani ya muda mfupi.ndani siku 4 kuku300 walikufa nikabaki na kama kuku 33.ndiyo naokota mayai ya kula na familia.
Hilo shamba linalimwa vitunguu kila mwaka na wanavuna sana. Nahisi wenyeji walidukua vitunguu changu. Hata mambo ya udukuzi yapo pia ktk kilimoKwenye vitunguu kitu kimoja hukufaham kilikuanfisha ni shamba halikuwa zuri pamoja na matumizi ya pembejeo. Hata Mimi nililima ila kwa sim nilirudisha peaa yangu tu.
Mzee muhindi mmoja kuuza 120 mbona ilikuwa bei fair kabisa? Ulitaka uuze sh ngapi sasa 300? Ingekuwa hasara kwakeNaanza kwa kutoa experience yangu.
Niliingia kwenye kilimo baada ya kushawishika na vipindi vya Clouds Media kuhusiana na fursa. Presenters walishawishi sana kuwa vijana hatujitumi na hatutumii brain zetu vizuri.
Nikajitosa kwenye kilimo cha tikiti Migoli Iringa na milioni zangu 2. Nikaingia front mwenyewe sikutaka kilimo cha simu. Nilikutana na changamoto katika kulima nikapambana nazo nilikuwa nalala shamba kwenye vibanda vya nyasi, vibarua wanazingua balaa na changamoto ya madawa. Baadae nikafanikiwa kuvuna na yalikubali sana.
Mziki ukaja kwenye soko sasa. Unatoka mjini na mfanyabiashara kuja shamba kununua mzigo, mjini umeacha bei ya tikiti 1 ni elfu 4. Mfanyabiashara shamba anataka kununua tikiti 1 sh 500, nikaamua kwenda nayo mwenyewe sokoni Dodoma. Kufika pale, dah! washaambizana wafanyabiashara wao hawanunui direct kutoka kwa mkulima; wananunua kupitia madalali, ikanibidi niwakabidhi madalali mzigo. Hapo nilichoka nilirudi nyumbani na laki 4.
Nikaingia kwenye kilimo cha vitunguu Ruaha Mbuyuni. Nikapambana nacho; jani lilikubali balaa kila siku nikawa napiga picha narusha social media. Wakati wa kuvuna kuja kuchimba chini chenga tu nikaishia kuuza reja reja nikatoka na laki 7.
Nikaja kulima mahindi ya kuchoma maarufu kama Gobo. Nilipambana nayo mpaka mwisho kwenye soko tena changamoto. Mfanyabiashara anakuja kuchagua mahindi shamba anataka kununua muhindi mmoja kwa sh 120 ilihali mjini muhindi mmoja sh 500, nikaghairi kuuza nikasubiri yakauke bahati nzuri bei ya mahindi nzuri.
My take: Katika kilimo madalali na wafanyabiashara ndiyo wanaonufaika sana kuliko wakulima.
Aisee, kumbe..unaweza kulima kwenye hali ya hewa na udongo kama ya huku Dar au Pwani?Yap kupitia nayemuuzia changamoto kubwa nje wanataka mazao yenye high quality na pia wanataka msign contract ujicomit kua kila mwezi utaoeleka minimum tani ngapi. Hapo lazima uhakikishe una mashamba yako mwenyewe si chini ya ekar 20 ambayo utayapanda ktk vipindi tofauti kuhakikisha unakua na uhakika wa kusupply mzigo mwaka mzima. Hivi vi ekari 2 tatu tunavyokodi mwenye shamba hachelewi kukuzingua akachukua shamba lake
wapogoro walishindwa kusema signal wakaamua kuita zinginali kama ilivyo cow way ya KAWE[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Walah leo ndio nimejua zinginali ni signal!!![emoji134][emoji134][emoji134]
Kuna jamaa yangu aliishawai kuzikimbia fuso mbili za tikiti sokoni akawaachia msala wenye fuso manake hata hela ya kufikishia pale sokoni isingetosha alafu yakaanza kupasukaTikiti halijawahi kumuacha mtu salama![emoji16][emoji16][emoji16]
na waliolima na wakafaidika je wafuate ushauri wako?
Same sehemu gani na gharama za kukodi shamba ni kiasi ganiNendeni Same kuna kilimo cha mpunga cha umwagiliaji uhakika wa mazao mkubwa na mpunga hauharibiki unaweka stoo unasubiria bei ipande
Rebeca, hayo Ni ya kweli usemayo?usikate tamaa mwaya,Kilimo hakithaminiwi sababu serikali haijagundua potential ya kuwekeza kwenye kilimo,siku zitakuja ambapo serikali ita invest kwenye kilimo na kila mlimaji atanufaika nacho..