Tulioingia kwenye kilimo tukaangukia pua tukutane hapa

Tulioingia kwenye kilimo tukaangukia pua tukutane hapa

Sikiliza mzee baba...wanataka cheti ulichopimia udongo wako mara water content ya shamba lako sijui zao lako..wanataka uwe na vyeti sio chini ya vinne!kuvipata sasa ndo napochoka na hii nchi...yaan hizo broccoli ziwe safi zisishikwe na finyofinyo lolote....nimesahau had majina a hayo madude wanayotaka..kifupi mie nili🙌🙌..nikaishia kuwa member wa TAHA tu nikiwamisi naenda tu wanipe moyo...!lakini ni safari ndefu usikate tamaa..! Serikali hii km huna connection hata hawana muda wa kukusaidia ..nimehenyeka sn kwenye wizara husika ila wapi..labda miaka hii
Hiyo ni plan ya baadae sana kwa sasa ngoja nipambane nitafute pesa nipate mashamba ya kumiliki kwanza
 
Ku a jamaa mmoja alinambia ng'ombe wakila shamba lako halafu wakakuzungusha unachukua asali unaenda unapakaza nyasi.Basi ng'ombe wakila huwa wanapatwa kiu balaa hata wakinywa maji haiishi hadi wanapasuka matumbo.
Mimi nililima mpunga heka kumi ukakubali kweli kweli shamba lilikua langu bwana bwana kukaa hivi napigiwa simu wasukuma wameingiza ng'ombe usiku wamekula shamba lote aisee nilidata. Alafu washenzi wale wamehonga polisi ukienda kushtaki unapigwa danadana tu nilitamani nikapige risasi ng'ombe wote. Morogoro iyo
 
Wewe ni mmoja wa wazee wa wazee wa Fursa.
Usilime kwa ushawishi fanya research ya soko kwanza. Kuna dada ninamfahamu wateja wake ni foreigners. Analima carrots, cabbage, hoho, nyanya, vitunguu. Kila siku anapeleka mzigo nyumbani kwa wateja. Ana list yao kabisa akifunga jumu shillings 10,000. Hakosi 200,000-250,000 kwa siku.
 
Ule mchele nautumiaga ni mbaya hatari. Ule wananunua watu wanachanganya na mchele bora
Kunaitwa NDUNGU mkuu unaingilia hapa mombo nimefika kote kule hadi gonja ila nimeuliza nimeambiwa ule mchele sio mtam kama wa kyela na ifakara ni mbegu za kijapan
 
Mimi nilizamia Luhangwa 2015 na milion zangu 3 kulima tikikiti eneo la Nanganga jimboni kwake Kasim Majaliwa nakumbuka wakati kwa kampeni nilikutana na majaliwa live pale relini Nanganva akimpokea mama Salma. Bora ningejua nikajitambulisha vyema labda leo ningelamba dume. Nilishushua mh. Waziri mkuu sana akaishia kuniangalia.

Sasa kilimo kilipamba moto nikalima zangu eka 3, kwa mbinde nilipambana hatari sana muda wa kuvuna tafuta soko holaaa nikaona wacha nikauze mwenyewe nikakodi gari fuso nikayaleta lindi mjini mengine mtwara. As usual madalali na msimu wa maembe ukaingilia niliambulia laki 7 kwenye milioni 3.

Nikahamia Ruvu nikalima tena eka 2 ile yanaanza kutambaa Ruvu ikafurika yakasombwa nikapoteza kama laki 8.

Nikaona wacha nipande mpunga mwezi 2, 2016 mpunga ulishamiri na kustawi nikajua hapa nitaunafuu ile unaanza kuchanua sijui nini kilitokea mpunga ukaungua na kuwa mwekundu kwenye eka 3 niliambulia gunia 7. Tangia hapo sijawahi rudi shamba.

Kabla ya hapo niliwahi kufuga kuku chotara kutoka ruvu nilianza na vifaranga 200,baada ya miezi 4 pumzi ilikata nikawauza nikapata kama 1000000 nilikuwa nimeishatumia km laki 6. Nikachukua tena vifaranga 100 nikawafuga na kufika miezi 8 walikuwa wamebaki 94 ila wakubwa sana nikaona niwauze na wengine niwachinje niuze nilipata laki 8 nikadhurumiwa laki 5.

Kusema kweli sijakata tamaa lazima nirudi shamba siku moja najipanga kwasasa.
Naanza kwa kutoa experience yangu.

Niliingia kwenye kilimo baada ya kushawishika na vipindi vya Clouds Media kuhusiana na fursa. Presenters walishawishi sana kuwa vijana hatujitumi na hatutumii brain zetu vizuri.

Nikajitosa kwenye kilimo cha tikiti Migoli Iringa na milioni zangu 2. Nikaingia front mwenyewe sikutaka kilimo cha simu. Nilikutana na changamoto katika kulima nikapambana nazo nilikuwa nalala shamba kwenye vibanda vya nyasi, vibarua wanazingua balaa na changamoto ya madawa. Baadae nikafanikiwa kuvuna na yalikubali sana.

Mziki ukaja kwenye soko sasa. Unatoka mjini na mfanyabiashara kuja shamba kununua mzigo, mjini umeacha bei ya tikiti 1 ni elfu 4. Mfanyabiashara shamba anataka kununua tikiti 1 sh 500, nikaamua kwenda nayo mwenyewe sokoni Dodoma. Kufika pale, dah! washaambizana wafanyabiashara wao hawanunui direct kutoka kwa mkulima; wananunua kupitia madalali, ikanibidi niwakabidhi madalali mzigo. Hapo nilichoka nilirudi nyumbani na laki 4.

Nikaingia kwenye kilimo cha vitunguu Ruaha Mbuyuni. Nikapambana nacho; jani lilikubali balaa kila siku nikawa napiga picha narusha social media. Wakati wa kuvuna kuja kuchimba chini chenga tu nikaishia kuuza reja reja nikatoka na laki 7.

Nikaja kulima mahindi ya kuchoma maarufu kama Gobo. Nilipambana nayo mpaka mwisho kwenye soko tena changamoto. Mfanyabiashara anakuja kuchagua mahindi shamba anataka kununua muhindi mmoja kwa sh 120 ilihali mjini muhindi mmoja sh 500, nikaghairi kuuza nikasubiri yakauke bahati nzuri bei ya mahindi nzuri.

My take: Katika kilimo madalali na wafanyabiashara ndiyo wanaonufaika sana kuliko wakulima.
 
Mimi nilizamia Luhangwa 2015 na milion zangu 3 kulima tikikiti eneo la Nanganga jimboni kwake Kasim Majaliwa nakumbuka wakati kwa kampeni nilikutana na majaliwa live pale relini Nanganva akimpokea mama Salma. Bora ningejua nikajitambulisha vyema labda leo ningelamba dume. Nilishushua mh. Waziri mkuu sana akaishia kuniangalia.

Sasa kilimo kilipamba moto nikalima zangu eka 3, kwa mbinde nilipambana hatari sana muda wa kuvuna tafuta soko holaaa nikaona wacha nikauze mwenyewe nikakodi gari fuso nikayaleta lindi mjini mengine mtwara. As usual madalali na msimu wa maembe ukaingilia niliambulia laki 7 kwenye milioni 3.

Nikahamia Ruvu nikalima tena eka 2 ile yanaanza kutambaa Ruvu ikafurika yakasombwa nikapoteza kama laki 8.

Nikaona wacha nipande mpunga mwezi 2, 2016 mpunga ulishamiri na kustawi nikajua hapa nitaunafuu ile unaanza kuchanua sijui nini kilitokea mpunga ukaungua na kuwa mwekundu kwenye eka 3 niliambulia gunia 7. Tangia hapo sijawahi rudi shamba.

Kabla ya hapo niliwahi kufuga kuku chotara kutoka ruvu nilianza na vifaranga 200,baada ya miezi 4 pumzi ilikata nikawauza nikapata kama 1000000 nilikuwa nimeishatumia km laki 6. Nikachukua tena vifaranga 100 nikawafuga na kufika miezi 8 walikuwa wamebaki 94 ila wakubwa sana nikaona niwauze na wengine niwachinje niuze nilipata laki 8 nikadhurumiwa laki 5.

Kusema kweli sijakata tamaa lazima nirudi shamba siku moja najipanga kwasasa.
Mpaka kufika kwenye mavuno unakua umepambana balaa ndo maana wanaolima kwa simu hata kwenye mavuno hua hawafiki
 
Kilimo Cha bangi hakijawai kunipa majuto ni timing tu na usiri ndio mafanikio yake,Kuna zao lingine miraa inapesa ya hatari sema serikali ilitakiwa kuhalalisha hizi mambo.wewe ukilima heka kumi za mahindi Mimi heka moja ya bangi ninapata faida kuliko wewe hivyo hivyo kwa miraa square meter chache pesa nyingi.karibuni meru na makanya
Kilimo na Ufugaji ni vitu ambavyo nitavikwepa daily. Bora kuwa mtu wa kati hapo faida lazima uipate tu.
Kilimo cha bangi hakiwezi kukuangusha
 
Nilipiga heka za Mahindi 30.za.mahindi karibu 8m. huko Morogoro.kabla ya kuvuna Ngombe wakapita nikaambulia gunia 30.maana yake kila eka gunia moja.

nikarudia tena mvua ikazingua ktk eka 20 nikapata gunia 3.nikarudisha home.tumekula ugali mwaka mzima.

Nikajaribu matikiti eka 4 .kabla ya kuiva yakawa yanapasuka pasuka.sikuuza kabisa .sema tulikula matunda home na wanangu.

Nikajaribu matango. eka 2.hayo yakakubali.na yanakomaa ndani ya mida mgupi sana .nikachelewa kuvuna.nilikiwa safari ya kikazi.nikawambia madogo wasubiri nirudi wasivune nilihofia kupigwa.hivyo yakaiva yakawa na mekundu hivi .kumpeleka bos shamba ilil akanunue,akaishia kuniitukana eti nimemsumbua na kumpotezea muda wake wakati.mzigo wenyeqe hauuzilki

Nilijaribu kufuga kuku chotara.hao walikubali sana.sema wakiwa na miezi mitano wakapata ugonjwa wa ajabu ghafla.asubuhi tunaamka tinaona wanasinzia na kukohoa. walikufa kwa wingi ndani ya muda mfupi.ndani siku 4 kuku300 walikufa nikabaki na kama kuku 33.ndiyo naokota mayai ya kula na familia.
 
Mie pia nilianza kilimo serious mwaka 2015...!nililima mchicha nusu eka..nikanogewa....nikalima tena na trna ..awamu ya 4kumbe chuo nachopeleka mchicha kimefungwa..nikala hasara nikauzs shamba zima kw shilingi 20000!
Nikahamia kwa tikiti..mara ya kwanza nilipata faida...ss nilikuja angukia pua kupitia hao the so called madalali.... Nijajifanya mm mjanja niwazunguke niuze mwenyew... Nilisumbuka mwez mzima nauza tikiti....
Nikaja gundua ishu ya 🍓🍓..naamini nilikua wa kwanza kbs kufanya hii mishe kiutalam zaidi hzi nikastick nazo km miaka mi3...nadhan kilimo ambacho hakina chngamoto sn ni matunda tu..nikapata ajali mbaya nikachefukwa kbs kuskia kuna strawberries...nikawa nasema naacha lakini daily unapata oda...kiukwel it pays..ila inachosha sn kupanda milimani!...nimewaachia watu waendeleze tu ...!kilimo cha Tz ni changamoto sna sna!...

Nyie ndio mnalima strawberry Sumbawanga? Hizi nasikia soko ni changamoto sana
 
Nilipiga heka za Mahindi 30.za.mahindi karibu 8m. huko Morogoro.kabla ya kuvuna Ngombe wakapita nikaambulia gunia 30.maana yake kila eka gunia moja.

nikarudia tena mvua ikazingua ktk eka 20 nikapata gunia 3.nikarudisha home.tumekula ugali mwaka mzima.

Nikajaribu matikiti eka 4 .kabla ya kuiva yakawa yanapasuka pasuka.sikuuza kabisa .sema tulikula matunda home na wanangu.

Nikajaribu matango. eka 2.hayo yakakubali.na yanakomaa ndani ya mida mgupi sana .nikachelewa kuvuna.nilikiwa safari ya kikazi.nikawambia madogo wasubiri nirudi wasivune nilihofia kupigwa.hivyo yakaiva yakawa na mekundu hivi .kumpeleka bos shamba ilil akanunue,akaishia kuniitukana eti nimemsumbua na kumpotezea muda wake wakati.mzigo wenyeqe hauuzilki

Nilijaribu kufuga kuku chotara.hao walikubali sana.sema wakiwa na miezi mitano wakapata ugonjwa wa ajabu ghafla.asubuhi tunaamka tinaona wanasinzia na kukohoa. walikufa kwa wingi ndani ya muda mfupi.ndani siku 4 kuku300 walikufa nikabaki na kama kuku 33.ndiyo naokota mayai ya kula na familia.

ha ha ha ha mzee wewe kila kitu tee!!! pole sana arifu
 
Back
Top Bottom