Tulioingia kwenye kilimo tukaangukia pua tukutane hapa

Tulioingia kwenye kilimo tukaangukia pua tukutane hapa

Sasa faida ya Gunia kumi afadhali ingekufuta machungu mzee wa watu ukute aliuacha mpaka ukaaribika
Huenda vibarua walikua wana mdai kwa hiyo hata angeuza bado pesa ingerudi kule kule tu.
 
Mkuu kuna mbinu moja hiyo ya soda hasa koka na Pepsi msukuma akigundua umefanya ivyo hapeleki ng'ombe hata karibu na shamba. Ni washenzi sana wanawaingiza wengi hasara.
Tupe ujuzi mkuu,ng'ombe wana sumbua sana aisee,halafu tatizo kubwa ni kwamba ng'ombe huwa wanapitishwa mchana kwa kuchungwa karibu na shamba ili hawaingii shambani ila baadae wanavyo enda kulala wana vunja zizi la kufuata harufu shamba lilipo hapo ndipo unapokua msala
 
Kwann uliziterekeza
Nimewahi kuwekezs kwenye kilimo cha ufuta mkoa wa Pwani ekari 10, nikaajiri wasimamizi tena wanakijiji wa pale. Kila weekend asubuhiii nipo shamba kucheck mradi kuanzia kupanda, palizi etc..... anyway to cut the story short yaliyotokea sikutaka hata kusimulia washkaji. Nlivuna gunia 12 tu sikuzibeba hata nkaziacha hapo hapo kijijini kwa mzee wa shamba nikasepa na sijawahi kurudi tena.

Kilimo ni full time job like any other job. Watu wa mjini tunakuwa na hype sana kwny stori ila uhalisia sio.
 
Tupe ujuzi mkuu,ng'ombe wana sumbua sana aisee,halafu tatizo kubwa ni kwamba ng'ombe huwa wanapitishwa mchana kwa kuchungwa karibu na shamba ili hawaingii shambani ila baadae wanavyo enda kulala wana vunja zizi la kufuata harufu shamba lilipo hapo ndipo unapokua msala
Kuna watu waliwahi niambia unachukua soda unachanganya na asali then mwaga pembeni ya shamba kwenye majani ng'ombe akijaribu kula tu hawezi kutembea zaidi ya nusu kilometa lazima aanguke tumbo linamjaa gesi.
 
Hakuna aliyefanikiwa kwa kilimo cha cm make sure 90% ya muda wako upo shamba na ujikane na anasa zote za dunia. Inafikia kipindi hata kwenda shamban ukiwa umebeba mkononi maji ya kunywa makubwa unaonekana kama unafanya anasa hahahaha
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Maji makubwa yakunywa!!! Mimi nilikuwa nikienda shamba nalala guest halafu asubuhi napelekwa na bodaboda shambani,kilichonikuta thiri yangu (sio Siri)
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Maji makubwa yakunywa!!! Mimi nilikuwa nikienda shamba nalala guest halafu asubuhi napelekwa na bodaboda shambani,kilichonikuta thiri yangu (sio Siri)
Bora hata wewe. Kuna jamaa alikua anatoka na Landcruiser single cabin ya petrol Dar analima vitunguu Ruaha mbuyuni. Kila wkend yupo pale jion bia sana na kuchoma mbuzi, mademu wengine alikua anatoka nao Dar. Kilichompata nahisi atakua ameuza hata hiyo gari yenyewe
 
Kilimo kina changamoto sana, unaweza ukalima vizuri ila likidukuliwa ni shida, hasa mazao ya chini, kitunguu nk
 
Mambo huanza hivi
Unawasikiliza Motivational speaker au wazee wa fursa za PDF wanakuvutia sana utawasikia "Ekari moja ya shamba la mpunga inatoa gunia 30 mpaka 40. Ukapata gunia 30 tu na kila gunia ukauza 120,000 unapata 3,600,000. Gharama za kuhudumia ekari 1 mpaka kuvuna ni sh laki 9 tu. Ukilima ekari 10 unapata milion 36 na unakua umetumia gharama za kuzalisha milion 9 tu". Basi mzee ukikaa chini unaona ah mbona simple tu maana ofisini ukikaa vimichongo vya laki 5 mpaka 7 vipo kibao unavipiga ukichangia na salary na pia unaona ah mbona mara kibao tu nakata laki na washkaji kwa mambo ya kipumbavu kwa nn nisizamishe kwenye kilimo nitoke faster.
Basi unaona ngoja ulime ekari 40 ili uje kupiga milion 144. Hapo ushahamasika unazama faster Ifakara tafuta mashamba kwa fujo hutaki poteza muda unaiwazia milion 144. kule ifakara unakutana na matapeli wa shamba nao ndo wanakupa muwasho unaona muda wote ulikua unapoteza bure twn na unaona kama vijana wengine wamelala sana twn kwa nn wasije huku watoke mapema. Unatafuta ekari 40 unapata yule tapeli uliyekutana nae ifakara ndo anageuka msimamizi wako ww unarudi twn mnakua mnawasiliana nae kwa cm
Changamoto zinaanza
1. unakodishiwa shamba ambalo either lina maji mengi sana, au maji kufika huko ni shida sana mpaka usimamie na mtutu wa bunduki. pia unaweza pata shamba lisilo na rutuba nk
2. Kulima. Pesa ipo lakini kwa kipindi hicho trekta za kusubiria kwa foleni zinalima sehemu zingine. tayari unapoteza timing
3. Vibarua wa kuwapata kusimamia ekari 40 huwapati wanapatikana wachache, wazinguaji, pesa mbele. Vibarua wazuri wamewahiwa na wazoefu ( Hapa pia pesa unayo lakini wafanyakazi hakuna na mazao yanazidi kuharibika shambani)
4. Wasimamizi uliowaamini waliopo shamba kila siku wanakupiga hela lakini kazi haiendi inavyotakiwa.
5. Unaweza pata mbegu isiyo bora kwa kukosa uzoefu
6. Ukiagiza mbolea na madawa wasimamizi wanakupiga wanawauzia wenye mashamba ya jirani kwako wanapulizia mapovu. Pia kipindi ambacho ww haupo vibarua wanapiga dei waka mashamba ya jirani
7. Gharama za uzalishaji zinazidi ile laki 9 uliyoambiwa kwa ekari. WW mwenyewe wkend unawasha Harrier lexus kutoka Dar mpaka Ifakara ukifika kule unalala Lodge, kula, kunywa, bado utavuta na kamchepuko hahahahahahaahahahahah
8. Unapatwa na majanga either Ng"ombe wanaingia shamba au mwaka huo mvua zikawa chache au nyingi sana mafuriko yakasomba kila kitu

Baada ya hapo kama uliinvest milion 36 ili upate milion 144 utajikuta umeambulia laki 7
ha ha ha ha ha ha umeandika ukweli kabisa kuna jamaa yangu aliwekeza milioni 100 nikawa nikienda ofisini kwake anawasha lapton anaanza kunionesha projections ha ha ha ha ha zinavutia balaa baada ya mavuno nilimfuata akasema hataki tena kilimo ha ha ha ha ha jamaa aliweka hadi wamama shambani anawalisha na chakula cha bure kilimo cha kizungu
 
ha ha ha ha ha ha umeandika ukweli kabisa kuna jamaa yangu aliwekeza milioni 100 nikawa nikienda ofisini kwake anawasha lapton anaanza kunionesha projections ha ha ha ha ha zinavutia balaa baada ya mavuno nilimfuata akasema hataki tena kilimo ha ha ha ha ha jamaa aliweka hadi wamama shambani anawalisha na chakula cha bure kilimo cha kizungu
Kipindi hicho watu wanakuaga wamehamasika yaani huwaambii kitu na ndo wanapopigwa. Jamaa yangu alienda kutafuta shamba alime vitunguu saumu hapo ashaambiwa gunia moja laki 7 na ekari moja inatoa gunia 30. Alipokosa shamba akakuta ekari 3 za gobo inakaribia kuchumwa akainunua akapitisha panga yote akaichoma ili alime kitunguu hahahahaha
 
Back
Top Bottom