Tuliopitia maisha ya "Saidia Fundi" tukutane hapa

Tuliopitia maisha ya "Saidia Fundi" tukutane hapa

Pengine alikua anamfanya kweli, utaitwaje mke na mwanaume mwenzio halafu uchukulie poa!?
Ombea usikutane na fundi alievurugwa 😂😂 kuna saidia fundi alikuwa anaitwa "mke wangu" na fundi, yani haya maisha watu wanapitia mengi sana.
 
Picha linaanza niliambiwa pima ndoo 120 za mchanga jamaa akawasha fegi hapo bado kuchanganya na kuanza kumsogezea,nakumbuka hii siku nilivyopanda kitandani hapo hapo nikasikia jogoo anawika kwamba kumeshakucha siku nyingine inaanza.
🤣🤣🤣🤣🤣
 
haya mazingira ni unforgetable kwangu

kuna apartment ilikua inasimamishwa na boss mtasha wa pale town. Kama ilivyo kawaida watoto wa mjini hawakosi connection za madili wakanistua na mimi sikufanya kosa nikaibukia

ilikua ni ishu ya umwagaji zege tu iliyojumlisha wafanya kazi zaidi ya 50 na ndio ilikua mara yangu ya kwanza kufanya kazi na group kubwa la watu ambalo ndani yake hadi wamama na mabinti walikuwepo

Asubuhi mtasha akaja site akatangaza dau kua kila mmoja atamlipa 25k, raia wakaonekana kutoridhika mi nikawa nawashangaa kwasababu ile pesa niliiona kubwa kulingana na idadi ya watu ilivyokua niliamini ni kazi itakayo kamilishwa masaa machache tu.

zikaletwa mashine za kuchanganyia zege na mimi nikachukua chepe nikajiunga kwenye sector ya kupakia kwenye vindoo.

sasa hii zege ilikua inaenda kumiminwa kwenye floor ya pili huko juu, kwa hiyo ukatengenezwa utaratibu wa wabebaji kupanga mstari kutoka chini ambako zege inachanganywa hadi floor ya mwisho ambako zege ilikua inamiminwa

haikua rahisi kwa mmoja mmoja kubeba zege na kupanda nayo hadi juu na ndio maana uliwekwa mstari ambao mtu wa kwanza anampasia zege mtu wa pili mpaka inafika eneo inayo hitajika

Kutokana na kazi kuambatana na wanawake hasa wamama ikabidi iwekwe sheria ya kipimo cha ujazo wa zege kua ni chepe mbili tu ili kutowaumiza

baada ya masaa takribani kama saba hivi baada ya kula lunch watu wakiwa wamejipumzisha kusubiria round ya pili nikasema ngoja nipande juu nicheki tumefikia wapi maana nilikua nahesabu idadi ya mifuko 53 tuliyoitumia nikawa nishafanya estimation kua robo tatu ya kazi kivyovyote itakua imekamilika kutokana na u expert niliopata kwenye kumwaga vizege vya renta

Aisee nilipopanda kule juu nilichoka, kwani nilikuta ile foundation imesukwa kwa namna ya kipekee. Nondo zilisukwa za kutosha halafu space ya kuijaza ile zege kutoka juu mpaka chini ilikua inanifika usawa wa paja na mi nishazoea space ya renta kutoka chini ni inch 5 tu leo hii nimekutana na hii shuguli

halafu ukicheki upana wa lile eneo lilikua ni kubwa sana kiasi cha kufanya kazi tulioifanya ionekane kama ni robo kazi huku eneo kubwa likiwa tupu bila zege

Hapa nikawa nawakumbuka wale wadau waliokua wanadai pesa iongezwe nikajisema daah wale miamba walikua na jicho la tatu walifika hii angle ila kutokana na kujifanya mjuaji nikawapinga
Hiyo inaitwa raft foindation mzee... poleni sana!!
 
Uchungu wa nn mkuu 😅
mkuu kureport site tu engineer anasema saa 12 asubuhi watu wawe wamefika mazingira ya kazi yaaandaliwe
hapo cement tunatakiwa kuleta eneo la kazi kama mifuko 100 ya kuanzia
mashine ikiwaka haizimi mpaka muda wa chakula cha mchana ikiharibika mnasema alhamdulilah😀😀😀
yani ni lile zege mnamwaga kwa kasi ya ajabu mchaka mchaka ukiwa slow kulikuwa na wana wametoka mjini wanatukana vibaya sana hizi kazi haziendi bila matusi 😀😀
yani kitengo cha afadhali ni kile cha kuweka cement kwenye mashine ukitoka hapo huwezi kupita road watoto wa shule wanakimbia
tulikuwa site moja kubwa mkuu yani mashine inawaka 12;30 inazimwa 6;30 mchana muda wa kula ugali maziwa
baada ya kula watu wanapumzika kidogo kabla ya kurudi tena muda wa kulala ulimi nje kama kibudu cha mbuzi
 
kuna mafundi wanapenda umwinyi sana muda wa kazi anakupeleka kama fuso la mkaa yupo mmoja kwenye kazi nimeshakimbiza
mpaka nimechoka nimejiinamia mara kobilo imetua kichwani alafu yupo hapo juu anauliza umeumia?
nilivunja lile jukwaa fundi akalala ndani week mimi nduki😀😀
 
Hii mikazi sidhani kama kuna mtu anapenda kuifanya ila kuna stage ilitubidi wengine tufanye ili tusukume siku.

Wapo ambao zimewatoa, na tupo ambao hazikututoa.

Niliacha hii mikazi kipindi hicho napambana life baada ya braza mmoja aliyekuwa ameshika kazi, akishachukua mpunga kwa bosi basi anasema tumfuate mpaka kilabuni huko ndiko anaenda kutupea hela. Ili wamama wa kilabuni wajue yeye ndio bosi.

Kiufupi ni kazi ambayo inachangamoto zake hasa zikikukuta sio mtu wa kujichanganya sana kwa watu.

Ukiona mtu miaka nenda rudi anafanya saidia fundi ameshindwa hata kujiongeza na yeye kuwa fundi basi jua ana matatizo ya kiakili.

Nawaoneaga huruma vijana wanaotoka chuo na kuanza kupiga hii kazi.
Dah aisee nakumbuka miaka ya 2013 na 14 hivi nikiwa zangu kusini pande za mtwara huko.

Kwa siku nilikuwa nalipwa alfu saba alafu ikitokea kazi ya kuchimba msingi ni hela mbali na ya saidia,kuna siku nikawa narudi na 10 mpaka 15K alhamdulillaah

Ila bhana kuna siku hiyo maeneo flani hivi tulienda kupiga kazi sasa kulikuwa na ishu ya kujaza zege kama vyumba viwili hivi aisee japokuwa kila chumba ilikuwa tunachukua 15k lakini mziki wake haukuwa wa kitoto aisee.

Nakumbuka narudi nyumbani siku hiyo kudadeki nalala tu naanza kuota ndoto kila tukio la pale site mpaka naamka asubuhi najikuta nimechoka kishenzi mpaka natamani kulala tena ili nipumzike yani nilliona kama ule usiku nimerudi tena site hivi.

Nilipofanya kazi ya usaidia kwa miezi kadhaa nikaenda zangu nyumbani kuna bro wangu alitaka nisimamie nyumba yake,basi nimefika site kwa bro fundi akawa anatafuta saidia wake watatu,nikamuambia fundi tafuta saidia wawili wa tatu ni mie fundi kashangaa wewe safuher si msimamizi ? Nikamuambia nitaplay part mbili hapa usijali.

Nikawa napiga two ndegez at once,ile kazi imwnifunza mambo mengi sana aisee.
 
Mkuu hapo nimesimulia nusu tu hii kazi ilikua na shughuli sio ya kitoto

Ilifika wakati ukaanza mzozo kati ya wanaume na wanawake kua kazi haiendi kutokana na kipimo cha zege kua kidogo hivyo round ya pili baada ya lunch tutakua tunajaza

Wamama wakawa wabishi kua hawawezi kubeba huo ujazo so ikatubidi tuongeze kipimo kidogo tukaweka koleo tatu ila sio kwa level ya kujaa

Basi kazi ikaendelea na dakika zilizokua zikijongea ndivyo nilivyoanza kuyaona mateso. Pale katikati kwenye uchanganyaji zege hatukupewa zile plastic boots kwa ajili ya kukinga cement isidhuru miguu so hapa miguu yote ilikua tayari imeshika cement na kama ujuavyo ratio ya cement ya zege inavyokuaga kali

Nikaona bora ni switch niende kitengo kingine, nikataka niende kwenye msululu kupasiana ndoo za zege lakini nikamuona mwanangu mmoja naye anataka aje kwenye kitengo changu maana zile ndoo za zege zilikua zimelowa zege kwenye mishkio kiasi cha kufanya mikono ya jamaa kuanza kuuma.

Wamama walifunga kanga mikononi kama gloves ili waweze kubeba ndoo bila kudhurika na ile cement iliyoko kwenye vishikizo vya ndoo

Nikaamua niende kitengo kimoja cha kudaka ndoo kutoka floor ya juu mbazo zimesha miminwa hivyo zinatakiwa zirejeshwe chini ili zipakiwe zege nyingine. Kwahiyo mmiminaji wa zege pembeni yake kulikua na mdau mwingine ambaye alikua na kazi ya kuchukua zile ndoo na kuzirusha chini ambapo huko zinatakiwa zidakwe na mtu ili kuzuia zisipasuke

Basi nikajitusu kwenye kitengo cha udakaji ndoo kisha site manager akaagiza kazi ifanyike kwa speed ili tuwahi kumaliza mapema. Hapo ndipo mchaka mchaka ulipoanza kwanza baada ya lisaa limoja ukatokea ukimya huku ikisikika misonyo ya ghadhabu kwa wafanyakazi hasa wamama

mmoja akasema anaenda kunywa maji akazunguka nyuma ya kibaraza akasepa mazima, wawili walisema wanaenda chooni kwa muda tofauti tofauti wote nao hawa hawakurudi so nguvu kazi ikawa imepungua

Huku namimi shughuli ikaanza kuambatana na mvua maana yule mdau kule juu alielemewa na wingi wa ndoo hivyo akawa anazitupa roughly bila kuangalia hali ya mdakaji chini mpaka ikafika muda nikawa nazikwepa zinadondoka nyingine zinapasuka.

Site manager akasikika akitoa sauti ya mamlaka akinikemea kua nisikwepe ndoo badala yake nidake vinginevyo pesa yangu itakatwa kufidia hasara ya uvunjifu wa ndoo

Zile ndoo zilikua zimeshikamana na zege kiasi cha kufanya ziwe nzito pasipo hatazege ndani yake, nikajikuta mikono imechubuka damu zinatoka nikaamua kusepa fasta kwenye hicho kitengo

kwa ufupi

Ile kazi tulitoka mida kama hii majira haya haya ya saa 2 kuelekea saa 3 usiku na bado haikua imeisha so mtasha akasema tutaendelea kesho

pamoja na hayo Boss mtata akasema siongezi pesa niko tayari nilipe pesa ya kukodi hizi machine za kuchanganyia zege zukae hata wiki mbili

nilivyofika geto nilishindwa kuoga bafuni maana mikono yote ilijaa vidonda vibichi vilivyosababisha nishindwe kuvua nguo. Kwa jinsi mikono ilivyokua damaged nilishindwa unauma nilishindwa kula hata ugali kwa mikono nilitumia kijiko napo kwa shida sana

Nlienda kuoga mtoni kwenye kibwawa cha kuzuga nilijitupa kwenye maji hivyo hivyo nikiwa niko complete nguo hadi viatu. Na nilienda kulala hivyo hivyo na viatu

kesho yake tulifanikisha kumaliza kazi majira ya saa nane tukapewa mpunga wetu bila usumbufu nakumbuka nusu ya ile hela nili spend kununua madawa ya kujiuguza
😂😂 Kupokezana zege ilikuwa upuuzi wa hali ya juu. Ni afadhali mgebeba hata kama kidogo kidogo.
 
kuna siku bwana kuna kazi ilitoke homee ya ufundi mimi ndo nkawa saidia fundi fundi nlimpiga udongo mpaka alikimbia kazi akurudi tena na vifaa akaachaa vipo mpaka leoo kibegi chake chenye vifaa mkono bao,pima maji tukamba kamba na kijikoo hahaaaaa

Hii Chai ya rangi. Alafu haina sukari

Ipo kama vile dawa ya Madagascar
 
mkuu kureport site tu engineer anasema saa 12 asubuhi watu wawe wamefika mazingira ya kazi yaaandaliwe
hapo cement tunatakiwa kuleta eneo la kazi kama mifuko 100 ya kuanzia
mashine ikiwaka haizimi mpaka muda wa chakula cha mchana ikiharibika mnasema alhamdulilah😀😀😀
yani ni lile zege mnamwaga kwa kasi ya ajabu mchaka mchaka ukiwa slow kulikuwa na wana wametoka mjini wanatukana vibaya sana hizi kazi haziendi bila matusi 😀😀
yani kitengo cha afadhali ni kile cha kuweka cement kwenye mashine ukitoka hapo huwezi kupita road watoto wa shule wanakimbia
tulikuwa site moja kubwa mkuu yani mashine inawaka 12;30 inazimwa 6;30 mchana muda wa kula ugali maziwa
baada ya kula watu wanapumzika kidogo kabla ya kurudi tena muda wa kulala ulimi nje kama kibudu cha mbuzi
Pole mkuu.
Nilidhulumiwa 70k na fundi mkuu tangu hapo nikasema sifanyi tena kazi ya kusaidia kwenye ujenzi.
 
Pole mkuu.
Nilidhulumiwa 70k na fundi mkuu tangu hapo nikasema sifanyi tena kazi ya kusaidia kwenye ujenzi.
shukrani sana mkuu bora yako 70k mimi nilipigwa 150k na nikatelekezwa site maana tulipiga kambi kambi pale
nikarudi home na fuso la pumba😀😀
 
Back
Top Bottom