Nimecheka Sana aisee [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Daaah watu wanapitia magumu Kuna mdau kanichekesha hapo alivyopata kazi nyingine[emoji1787]
Pole mkuu...maisha lazima yaendeleeHadi leo sijui sababu witnessj. Nafikir kuna mjinga mmoja alikuwa ananichawia. Maana sikuwa na kosa lolote kabisa.
Bahati mbaya na hiyo taasisi yao ilishakufa , iliniuma sana kusikia wamefilisika, kwa sababu pamoja na kwamba walinifukuza bila kosa lolote lakini ni ukweli kwamba walinisaidia kupata pa kuanzia.
Gudi tu umeadimika sana.Safi vip Mzee!
Na forex wewe ni billionaire.Mi sikufukuzwa kazi.
Nilipiga chini tu hiyo kazi.
Mshahara mdogo sana. Unatoka tar 25 ikifika tar 1 ushaisha wote.
Nikarudi home kuanza moja.
Kama zile ofisi za almashauri [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Kuna viofisi ukifika wafanyakazi wana hali mbaya sana.
Wenye afadhali ukiachana na boss utakuta ni Accountants na watu wa Procurement.
Hawa no Wala rushwa wazuri hasa kwa wahindi ..hawafai kabisa mkuu. Mimi wakati bado sijatoka bongo niliwahi peleka mashtaka sehemu nlokuwa napiga kazi. Aise hamna kitu hapo watakupiga danadana maana boss no muhindi so anawatoa tu basi hamuna kitu watafanyaWana ofisi mikoa yote ndani ya Tanzania kulingana na ulipo.
Cheki hii link Home | Commission for Mediation and Arbitration uangalie address na namba za simu za maofisa wa CMA kulingana na mkoa uliopo. Unaweza kuanza kwa kumpigia simu ofisa wa CMA wa ofisi ya mkoa uliopo kwa kadri ya namba walizoziweka, kwa kuanzia anaweza kukupa ushauri murua sana wa nini cha kufanya juu ya ishu yako, mimi binafsi hawa jamaa waliwahi kunisaidia sana nikapata haki zangu kutoka kwa muajiri ambae alinizingua, hadi leo nawaheshimu sana. Rcrusso Jr
Duh 2005 shkamoo faza ..min Niko dasaa la tatu apoNilifukuzwa kazi mwaka 2005 october.Wiki nzima nilijikuta naongea peke yangu barabarani
Hawa no Wala rushwa wazuri hasa kwa wahindi ..hawafai kabisa mkuu. Mimi wakati bado sijatoka bongo niliwahi peleka mashtaka sehemu nlokuwa napiga kazi. Aise hamna kitu hapo watakupiga danadana maana boss no muhindi so anawatoa tu basi hamuna kitu watafanya
Kipindi Mkapa anaingia madarakani mabeberu walimshauri apunguze wafanyakazi wa serikali naye akakubali. Pale ofisini kulikua na watu wa IDM Mzumbe, IFM na sisi wa Mlimani (UDSM).
Kulikua na uhasama wa chini chini Kati yetu kwa upande mmoja na wale wa advanced diploma za IFM na IDM.
Waraka wa Chenkapa ukaja idarani kwamba baadhi ya watu wapunguzwe.
Aisee, aliye pewa kazi ya ku earmark watu wa kupunguzwa alikua mtu wa IDM. Hakufanya kosa, barua ya kwanza, ya pili ya tatu Ni yangu. Kipindi kile bar zinauza beer kuanzia saa mbili asubuhi, Basi nilizama bar moja kule mjini karibu na benki ya NMB.
Hakika Mkuu. Ahsante! Barua ilisema;Pole mkuu...maisha lazima yaendelee
then ikawaje mkuu/ uliachaje kazi?Kuna siku nilipata kazi kwenye kampuni kubwa sana hapa nchini, hii kampuni Ina makao makuu mjini na branch moja Chang'ombe Dar. Basi baada ya kupata Ile kazi nikaambiwa kituo changu Cha kazi itakua branch. Mimi nikachukua taxi mpaka branch kuripoti. Kufika nakuta meneja wa branch Ni jamaa tulisoma nae form five na six, pale nilitakiwa kua assistant wake. Jamaa wa IT Ni mshamba mmoja nilisoma nae UDSM course tofauti yeye computer science. Aisee mnajua fitna, hata Rage Ile fitna haifikii.
Kwanza meneja aliniambia sitapewa gari wakati magari pale yako mawili moja lake jingine la assistant.
Pili kaniambia ngoja akaongee na makaburu halafu atanipigia simu.
Sijui aliwaambia Nini makaburu mwisho wa siku hakunipigia na Mimi sikuhangaika nae. Kipindi kile kazi zinatafuta watu.
Binadamu wana mambo.Kuna mfanyakazi mmoja ameachishwa kazi baada ya kupata msiba watu wameenda kumpa pole kufika wakakuta mjengo wa maana
Alivyorudi kazini anaulizwa hela ya kujenga nyumba kama hii kaipata wapi
Watendaji Kazi wa shetani furaha yao ni kuona wengi wakiumiaDuu huo muda mpaka wa kuhesabiana nguo hadi ujue leo huyu kavaa nguo mpya watu huwa wanatoa wapi?
Pole sana mkuu. Hope umekaa vizuri now.Kiongozi hii thread yako imenikumbusha machungu Makubwa sana.
Nilivomaliza chuo nikapata sehemu ya kujishikiza bn, nikapiga kazi miezi mitatu tu nikapandishwa hadhi kidogo bana. Kazi ikaendelea, baada ya Mwaka mmoja kuisha, Kiongozi mmojawapo katika ofisi yetu akapa nafasi ya kuajiriwa serikalini, kampuni ikanipa nafasi yake. Kumbe ile hali wenzangu ambao tulikuwa tunafanya nao kazi walichukia sana. Why me?
Sijawa na hili wale like, mdogo wangu akauugua, wadogo zangu wengine walikuwa wanasoma bado secondary, so ikabidi nichukue likizo ya siku 14 kwanza nikamuuguze, bahati mbaya haikuwa riziki akafariki. Baada ya kumaliza matanga, nilirejea kazini, lakn haikuisha hata mwezi mama akaugua.
Akapelekwa hospital, akawa anakaa na dada yangu, kila wikend lazima niwe huko, nikalazimika kumhamishia kwangu (getho) pamoja na sista, afu Mimi nikawa nalala kwa mpangaji mwezangu msela. Uguza weee, hadi hela ikakata. Kazi nikiwa naendelea nayo lakini.
Basi bana nakumbuka ilikuwa Tarehe 1/10 tukaenda kuchukua mshahara, nilivyofika kwa mhasibu akanipa mshahara wangu na barua. Kuifungua, eti nimeachishwa kazi!
Kosa silijui. Basi ile hela yote nikamtibia mama, lakini haikufua dafu. Nikauza kabati la nguo laki 100,000/, nikauza sofa langu elfu 70, latop hp, 150,000,, uza king'amzi na TV, na dish lake 170,00, friji 70,000 nikaendelea kumtibia mama. Nilivyoishiwa kabisa, mama akapona!
Basi tukarejea kijijini, nikaanza kulima nyanya. Nikipeleka maombi ya ualimu hata shule za kata nakataliwa! Naambiwa nitaitwa lakn siitwi. Nyanya hakuna wanunuzi. Ikabidi nianze kuvua samaki, lkn wapi.
Wale watumishi wenzangu hata hawapokei simu yangu, kila surauali sasa hainitoshi, mwonekano umeshazidi umri wangu halisi. Nimezeeka balaa.
Sema ndo hivo siku hazifanani, nilikuja kupata pa kujishikiza na maisha yanaendelea. Lakn ukweli kuamka bila kujua pa kwenda ni shida.